< 1 Kings 16 >

1 During the time that Baasha [was king of Israel], [the prophet] Jehu, Hanani’s son, gave Baasha this message that he had received from Yahweh:
Ndipo neno la Bwana likamjia Yehu mwana wa Hanani dhidi ya Baasha, kusema:
2 “You were very insignificant/unimportant [IDM] when I caused you to become the ruler of my Israeli people. But you have caused me to become very angry by doing [IDM] the kinds of evil things that King Jeroboam did. You have also caused me to become angry by causing my people to sin.
“Nilikuinua kutoka mavumbini na kukufanya kiongozi wa watu wangu Israeli, lakini ukaenenda katika njia za Yeroboamu na kusababisha watu wangu Israeli kutenda dhambi na kunikasirisha kwa dhambi zao.
3 So now I will get rid of you and your family [MTY]. I will do to you just like I did to Jeroboam and his family.
Basi nitamwangamiza Baasha pamoja na nyumba yake, nami nitaifanya nyumba yako kama ile ya Yeroboamu mwanawe Nebati.
4 [The bodies of] those in your family who die in this city [will not be buried; they] will be eaten by dogs; and [the corpses of] those who die in the fields will be eaten by vultures.”
Mbwa watawala watu wa Baasha watakaofia mjini na ndege wa angani watajilisha kwa wale watakaofia mashambani.”
5 The other things that happened during the time that Baasha ruled Israel, and the things that he did, are written [RHQ] in the scroll called ‘The History of the Kings of Israel’.
Kwa matukio mengine ya utawala wa Baasha, aliyoyafanya na mafanikio yake, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
6 When Baasha died, he was buried in Tirzah, [the capital city]. Then his son Elah became king.
Baasha akalala na baba zake naye akazikwa huko Tirsa. Naye Ela mwanawe akawa mfalme baada yake.
7 Yahweh gave that message about Baasha and his family to the prophet Jehu. Baasha had done many things that Yahweh considered to be evil, which caused Yahweh to become angry. Baasha did the same kind of things that King Jeroboam and his family had done previously. Yahweh was also angry with Baasha because he had killed all of Jeroboam’s family.
Zaidi ya hayo, neno la Bwana likamjia Baasha pamoja na nyumba yake kupitia kwa nabii Yehu mwana wa Hanani, kwa sababu ya maovu yote aliyokuwa ametenda machoni pa Bwana, akamkasirisha kwa mambo aliyotenda, na kuwa kama nyumba ya Yeroboamu, na pia kwa sababu aliiangamiza.
8 After Asa had been the king of Judah for almost 26 years, Elah became the king of Israel. Elah ruled in Tirzah for [only] two years.
Katika mwaka wa ishirini na sita wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Ela mwana wa Baasha akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala huko Tirsa kwa miaka miwili.
9 [A man named] Zimri was one of Elah’s army officers. He commanded the drivers of half of Elah’s army’s (chariots/two-wheeled vehicles pulled by horses). He made plans to kill Elah while Elah was in Tirzah, getting drunk at the house of [a man named] Arza. Arza was the man who took care of the things in the king’s palace.
Zimri, mmoja wa maafisa wake, aliyekuwa na amri juu ya nusu ya magari yake ya vita, akafanya hila mbaya dhidi ya Ela. Wakati huo Ela alikuwa Tirsa, akilewa katika nyumba ya Arsa, mtu aliyekuwa msimamizi wa jumba la kifalme huko Tirsa.
10 Zimri went into Arza’s house and killed Elah. Then Zimri became the king of Israel. That was when Asa had been the king of Judah for 27 years.
Zimri akaingia, akampiga na kumuua katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda. Kisha Zimri akaingia mahali pake kuwa mfalme.
11 As soon as Zimri became king [MTY], he killed all of Baasha’s family [MTY]. That included every male [IDM] in Baasha’s family and all of Baasha’s male friends.
Mara tu alipoanza kutawala na kuketi juu ya kiti cha ufalme, aliua jamaa yote ya Baasha. Hakumwacha mwanaume hata mmoja, akiwa ni ndugu au rafiki.
12 That was just what Yahweh told the prophet Jehu would happen.
Hivyo Zimri akaangamiza jamaa yote ya Baasha, kulingana na neno la Bwana lililonenwa dhidi ya Baasha kupitia nabii Yehu:
13 Baasha and his son Elah had sinned and led the Israeli people to sin. They caused Yahweh, the God whom the Israeli people worshiped, to become angry, because they both urged the people [to worship] worthless idols.
kwa sababu ya dhambi zote Baasha na mwanawe Ela walizokuwa wametenda na wakasababisha Israeli kuzitenda, basi wakamkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli kwa sanamu zao zisizofaa.
14 Everything else that Elah did is written in the scroll called ‘The History of the Kings of Israel’.
Kwa matukio mengine ya utawala wa Ela, na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
15 So Zimri became the king of Israel after Asa had been king of Judah for 27 years. But Zimri ruled in Tirzah for only seven days. The Israeli army was beseiging/surrounding Gibeah, a town which belonged to the Philistine people-group.
Katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Zimri akatawala huko Tirsa siku saba. Jeshi lilikuwa limepiga kambi karibu na Gibethoni, mji wa Wafilisti.
16 The men in the Israeli army camp heard that Zimri had secretly planned to kill King Elah, and then had killed him. So on that day the soldiers chose Omri, the commander of their army, to become the king of Israel.
Wakati Waisraeli waliokuwa kambini waliposikia kuwa Zimri alikuwa amefanya hila mbaya dhidi ya mfalme na kumuua, wakamtangaza Omri, jemadari wa jeshi, kuwa mfalme wa Israeli siku iyo hiyo huko kambini.
17 The Israeli army was camped near Gibbethon [city]. When they heard what Zimri had done, they left there and went to Tirzah, and surrounded the city.
Ndipo Omri na Waisraeli wote pamoja naye wakaondoka Gibethoni na kuizingira Tirsa.
18 When Zimri realized that the city was [about to be] captured, he went into his palace and set it on fire. So the palace burned down, and he died [in the fire].
Wakati Zimri alipoona kuwa mji umechukuliwa, alikwenda ndani ya ngome ya jumba la kifalme na kulichoma moto jumba la kifalme na kujiteketeza ndani yake. Kwa hiyo akafa,
19 He died because he had sinned by doing the things that Yahweh considered to be evil. Jeroboam had led the Israeli people to sin, and Zimri sinned just like Jeroboam had sinned.
kwa sababu ya dhambi alizofanya, akitenda maovu machoni pa Bwana na kuenenda katika njia za Yeroboamu na katika dhambi alizofanya na kusababisha Israeli kuzifanya.
20 All the other things that Zimri did, and the record of how he rebelled [against King Elah], are written in the scroll called ‘The History of the Kings of Israel’.
Kwa matukio mengine ya utawala wa Zimri, na uasi alioutenda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
21 After Zimri died, the Israeli people were divided. One group wanted Tibni, the son of Ginath, to be their king. The other group wanted Omri [to be the king].
Ndipo watu wa Israeli wakagawanyika katika makundi mawili, nusu wakamuunga mkono Tibni mwana wa Ginathi ili awe mfalme na nusu nyingine wakamuunga mkono Omri.
22 Those who supported Omri (were stronger than/defeated) those who supported Tibni. So Tibni was killed, and Omri became king.
Lakini wafuasi wa Omri wakajionyesha wenye nguvu kuliko wale wa Tibni mwana wa Ginathi. Hivyo Tibni akafa na Omri akawa mfalme.
23 Omri became king when Asa had been king of Judah for almost 31 years. Omri ruled Israel for 12 years. For the first six years he ruled in Tirzah.
Katika mwaka wa thelathini na moja wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Omri akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala kwa miaka kumi na miwili, sita kati ya hiyo katika Tirsa.
24 Then he bought a hill from [a man named] Shemer and paid him about (150 pounds/70 kg.) of silver for it. Then Omri ordered his men to build a city on that hill, and he called it Samaria, to honor Shemer, the man who owned it previously.
Alinunua kilima cha Samaria kutoka kwa Shemeri kwa talanta mbili za fedha na akajenga mji juu ya hicho kilima, akiuita Samaria, kutokana na Shemeri, jina la mmiliki wa kwanza wa kilima hicho.
25 But Omri did many things that Yahweh considered to be evil. He did more evil deeds than any of the kings who ruled Israel before he did.
Lakini Omri akatenda maovu machoni pa Bwana na kutenda dhambi kuliko wote waliomtangulia.
26 [When] Jeroboam [was previously the king, he] had led the Israeli people to sin, and Omri committed the same kind of sins that Jeroboam did. The Israeli people caused Yahweh, the God the Israeli people had worshiped, to become very angry, because they worshiped worthless idols.
Akaenenda katika njia zote za Yeroboamu mwana wa Nebati na katika dhambi zake, ambazo alisababisha Israeli kutenda, hivyo basi wakamkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli kwa sanamu zao zisizofaa.
27 Everything that Omri did, and the record of the victories that his [army] won, are written in the scroll called ‘The History of the Kings of Israel’.
Kwa matukio mengine ya utawala wa Omri, yale aliyofanya na vitu alivyovifanikisha, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
28 After Omri died, he was buried in Samaria, and his son Ahab became king.
Omri akalala pamoja na baba zake na akazikwa huko Samaria. Ahabu mwanawe akatawala mahali pake.
29 Ahab became king of Israel when Asa had ruled Judah for almost 38 years. Ahab ruled in Samaria [city] for 22 years.
Katika mwaka wa thelathini na nane wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Ahabu mwana wa Omri akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala Israeli akiwa Samaria kwa miaka ishirini na miwili.
30 Ahab did many things that Yahweh considered to be evil. He did more evil things than any of the kings who ruled Israel before he did.
Ahabu mwana wa Omri akafanya maovu zaidi machoni mwa Bwana kuliko yeyote aliyewatangulia.
31 He committed the same kind of sins that Jeroboam did, but he did things that were worse than the things that Jeroboam did. He married [a woman named] Jezebel, the daughter of Ethbaal, the king of Sidon [city]. Then Ahab started to worship Baal, [the god that the Canaan people-group worshiped].
Kama vile haikutosha kuishi kama Yeroboamu mwana wa Nebati, akamwoa Yezebeli binti wa Ethbaali, mfalme wa Wasidoni, naye akaanza kumtumikia Baali na kumwabudu.
32 He built a temple in Samaria in order that the Israeli people could worship Baal there, and he put an altar there for [making sacrifices to] Baal.
Akajenga madhabahu kwa ajili ya Baali katika hekalu la Baali lile alilolijenga huko Samaria.
33 He also made an idol that represented Asherah, [Baal’s wife]. He did many more things that caused Yahweh to become angry. He did more evil things than any of the previous kings of Israel had done.
Pia Ahabu akatengeneza nguzo ya Ashera na kufanya mengi ili kumkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli, kuliko walivyofanya wafalme wote wa Israeli waliomtangulia.
34 During the years that Ahab [ruled], Hiel, a man from Bethel [city], rebuilt Jericho [city]. But when he started to rebuild the city, his oldest son Abiram died. And [when the city was finished, ] while Hiel was building the city gates, his youngest son Segub died. They died just like Yahweh had told Joshua would happen [to the sons of anyone who would rebuild Jericho].
Katika wakati wa Ahabu, Hieli, Mbetheli, akaijenga upya Yeriko. Aliweka misingi yake kwa gharama ya mzaliwa wake wa kwanza Abiramu, na kuweka malango yake kwa gharama ya mwanawe mdogo Segubu, kulingana na neno la Bwana alilosema kupitia Yoshua mwana wa Nuni.

< 1 Kings 16 >