< 1 Chronicles 9 >

1 The [names of all the] people of Israel were listed/written with the names of their clans, and that information was written in the scroll/book named ‘The Record of the Kings of Israel’. [Many of] the people of Judah were captured and forced to go to Babylon. That happened because they did not faithfully [do what was pleasing to] God.
Waisraeli wote waliorodheshwa katika koo zilizoandikwa kwenye kitabu cha wafalme wa Israeli. Watu wa Yuda walichukuliwa mateka kwenda Babeli kwa sababu ya kukosa uaminifu kwa Mungu.
2 The first people who returned [to Judah 70 years later] and lived in their own land and in their own cities and towns were some Israeli priests, other descendants of Levi, and men who worked in the temple.
Basi watu wa kwanza kurudi kukaa kwenye milki zao katika miji yao walikuwa baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi na watumishi wa Hekalu.
3 [Other] people from the tribes of Judah, Benjamin, Ephraim, and Manasseh [also returned to Judah and] lived in Jerusalem. This is a list of those people [of the tribe of Judah]:
Wale waliotoka Yuda, Benyamini, Efraimu na Manase ambao waliishi Yerusalemu walikuwa:
4 Uthai the son of Ammihud. Ammihud was the son of Omri; Omri was the son of Imri; Imri was the son of Bani; Bani was a descendant of Perez; Perez was the son of Judah.
Uthai mwana wa Amihudi, mwana wa Omri, mwana wa Imri, mwana wa Bani, wa wana wa Peresi, mwana wa Yuda.
5 Asaiah and his sons were descendants of Shelah. Asaiah was the oldest son in his family.
Wazao wa Washiloni waliorudi ni: Asaya mzaliwa wa kwanza na wanawe.
6 Jeuel and others of his relatives in Zerah’s clan. There were 690 people in this clan.
Kwa wana wa Zera: Yeueli. Watu wa Yuda jumla yao walikuwa watu 690.
7 From the tribe of Benjamin, Sallu, the son of Meshullam. Meshullam was the son of Hodaviah; Hodaviah was the son of Hassenuah.
Kwa Benyamini walikuwa: Salu mwana wa Meshulamu, mwana wa Hodavia, mwana wa Hasenua;
8 Ibneiah the son of Jeroham. Elah the son of Uzzi. Uzzi was the son of Micri. Meshullam the son of Shephatiah. Shephatiah was the son of Reuel; Reuel was the son of Ibnijah.
Ibneya mwana wa Yerohamu, Ela mwana wa Uzi, mwana wa Mikri; na Meshulamu mwana wa Shefatia, mwana wa Reueli, mwana wa Ibniya.
9 In other records of the people descended from Benjamin, there are the names of 956 people who were living in Jerusalem. All these were leaders of their clans.
Watu kutoka Benyamini kama walivyoorodheshwa katika koo zao jumla yao ni 956. Watu hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa zao.
10 Some of the priests [who returned to Judah were]: Jedaiah, Jehoiarib, Jakin,
Wa jamaa za makuhani walikuwa: Yedaya, Yehoyaribu na Yakini;
11 and Azariah who was the son of Hilkiah. Hilkiah who was the son of Meshullam; Meshullam who was the son of Zadok, Zadok who was the son of Meraioth; Meraioth who was the son of Ahitub; Ahitub who supervised the temple guards;
Azaria mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu aliyekuwa afisa kiongozi wa nyumba ya Mungu.
12 Adaiah who was the son of Jeroham; Jeroham who was the son of Pashhur; Pashhur who was the son of Malchijah; Maasai who was the son of Adiel; Adiel who was the son of Jahzerah; Jahzerah who was the son of Meshullam; Meshullam who was the son of Meshillemith; Meshillemith who was the son of Immer.
Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya; Maasai, mwana wa Adieli, mwana wa Yahzera, mwana wa Meshulamu, mwana wa Meshilemithi, mwana wa Imeri.
13 Altogether there were 1,760 priests [who returned to Judah]. They were leaders of their clans, and they all were responsible for doing work in the temple of God.
Makuhani waliokuwa viongozi wa jamaa zao walikuwa 1,760. Walikuwa watu wenye uwezo, waliowajibika kuhudumu katika nyumba ya Mungu.
14 From the descendants of Levi [who returned to Judah] there was Shemaiah the son of Hasshub. Hasshub was the son of Azrikam; Azrikam was the son of Hashabiah; Hashabiah was a descendant of [Levi’s youngest son] Merari.
Jamaa za Walawi walikuwa: Shemaya, mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, wa wana wa Merari.
15 [Other descendants of Levi who returned to Judah were] Bakbakkar, Heresh, Galal, and Mattaniah the son of Mica. Mica was the son if Zicri; Zicri was the son of Asaph.
Bakbakari, Hereshi, Galali na Matania mwana wa Mika, mwana wa Zikri, mwana wa Asafu.
16 There was also Obadiah the son of Shemaiah. Shemaiah was the son of Galal. Galal was the son of Jeduthun. There was also Berekiah the son of Asa. Asa was the son of Elkanah, who lived in one of the villages where the Netophath people-clan lived.
Obadia mwana wa Shemaya, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni. Berekia mwana wa Asa, mwana wa Elikana, ambao waliishi katika vijiji vya Wanetofathi.
17 From the [descendants of Levi who returned to Judah] who guarded the temple gates there were Shallum, Akkub, Talmon, Ahiman, and some of their relatives. Shallum was their leader.
Mabawabu katika Hekalu la Bwana waliorudi walikuwa: Shalumu, Akubu, Talmoni, Ahimani na ndugu zao. Shalumu alikuwa mlinzi wao mkuu.
18 Those gatekeepers from the tribe of Levi stood at the King’s Gate on the east side [of the temple].
Walikuwa wamewekwa katika lango la mfalme lililokuwa upande wa mashariki, mpaka wakati huu. Hawa walikuwa mabawabu wa kutoka kwenye kambi ya Walawi.
19 Shallum was the son of Kore. Kore was the son of Ebiasaph. Ebiasaph was the son of Korah. Shallum and his relatives were gatekeepers, and they were responsible to guard the gates of the Sacred Tent of Yahweh, like their ancestors had done.
Shalumu mwana wa Kore, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora, pamoja na mabawabu wenzake kutoka jamaa yake ya Kora waliwajibika kulinda malango ya Hema, kama vile baba zao walivyokuwa wamewajibika kulinda ingilio la Maskani ya Bwana.
20 Previously Phinehas, the son of Eleazar, had supervised the gatekeepers, and Yahweh (was with/helped) Phinehas.
Hapo zamani Finehasi mwana wa Eleazari alikuwa kiongozi wa mabawabu, naye Bwana alikuwa pamoja naye:
21 Zechariah the son of Meshelemiah was the gatekeeper at the entrance of the Sacred Tent.
Zekaria mwana wa Meshelemia alikuwa bawabu katika ingilio la Hema la Kukutania.
22 Altogether, there were 212 men who were chosen to guard the gates. Their names were written in the records of the clans in their villages. [King] David and the prophet Samuel appointed/chose those men because those men (were dependable/always did what they were told to do).
Jumla ya waliochaguliwa kuwa mabawabu katika sakafu za kupuria nafaka walikuwa watu 212. Waliandikishwa kwa koo zao kwenye vijiji vyao. Mabawabu hawa waliwekwa katika nafasi zao za kuaminiwa na Daudi pamoja na mwonaji Samweli.
23 The work of those gatekeepers and their descendants was to guard the entrances of the Sacred Tent of Yahweh. That was before the temple was built to replace the Sacred Tent.
Wao na wazao wao walikuwa viongozi wa kulinda malango ya nyumba ya Bwana, nyumba iliyoitwa Hema.
24 There were gatekeepers on each of the four sides of the Sacred Tent.
Mabawabu walikuwa pande zote nne: mashariki, magharibi, kaskazini na kusini.
25 Sometimes it was necessary for the relatives of the gatekeepers who lived in those villages to come and help them. Each time some of them came, they helped the gatekeepers for seven days.
Ndugu zao katika vijiji vyao walikuwa wakija mara kwa mara na kuwasaidia katika kazi zao kwa vipindi mbalimbali vya siku saba.
26 There were four descendants of Levi who [worked every day, and they] supervised the gatekeepers. They also took care of the rooms and treasures in the Sacred Tent of God.
Lakini mabawabu wanne wakuu, waliokuwa Walawi, walikabidhiwa wajibu kwa ajili ya vyumba na hazina katika nyumba ya Mungu.
27 They remained awake all during the night to guard the Sacred Tent, and each morning they opened the gates.
Walikesha mahali walipowekwa kuizunguka nyumba ya Mungu, kwa sababu iliwapasa kuilinda. Pia walitunza funguo kwa ajili ya kufungua mlango kila siku asubuhi.
28 Some of the gatekeepers took care of the articles that were used in worship. They also took care of the flour, wine, olive oil, incense, and spices [that were used in the sacrifices].
Baadhi yao walikuwa viongozi wa kutunza vifaa vilivyotumika katika huduma ndani ya Hekalu; walivihesabu kila vilipoingizwa ndani na kila vilipotolewa.
29 Other gatekeepers were appointed to take care of the other things in the Sacred Tent.
Wengine walipangiwa kutunza mapambo na vifaa vingine vya patakatifu, pamoja na unga, divai, mafuta, uvumba na vikolezo.
30 But some of the priests had the work of mixing the spices.
Lakini baadhi ya makuhani walifanya kazi ya kuchanganya vikolezo.
31 There was a descendant of Levi named Mattithiah, the oldest son of Shallum, who was a descendant of Korah. He (was very dependable/always did what he was told to do), so they gave him {he was given} the work of baking the bread that was used in the offerings [on the altar].
Mlawi aliyeitwa Matithia, mwana mzaliwa wa kwanza wa Shalumu, wa ukoo wa Kora, alikabidhiwa wajibu kwa ajili ya kuoka mikate ya sadaka.
32 Some of the gatekeepers who were descended from Kohath prepared the freshly baked loaves of sacred bread that were placed on the table [inside the Sacred Tent] every Sabbath/rest day.
Baadhi ya ndugu zao wa ukoo wa Kohathi walikuwa viongozi wa kuandaa mikate ya Wonyesho kwa ajili ya kila Sabato, mikate iliyokuwa inawekwa mezani.
33 Some of the descendants of Levi were musicians who worked in the Sacred Tent. The leaders of those families [stayed/slept] in the rooms [of the Sacred Tent]. They did not do [any other work] in the Sacred Tent because they were responsible to serve [as musicians] day and night.
Wale waliokuwa waimbaji, viongozi wa jamaa za Walawi, waliishi katika vyumba vya Hekalu, nao hawakufanya shughuli nyingine yoyote kwa sababu iliwapasa kuwajibika kwa kazi hiyo usiku na mchana.
34 Those are [the names of] the leaders of the clans descended from Levi. Their names were written in the records of the clans. They all lived in Jerusalem.
Hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa za Walawi, wakuu kama walivyoorodheshwa katika koo zao, nao waliishi Yerusalemu.
35 [One of the descendants of Benjamin, ] Jeiel, lived in Gibeon [city]. He was the city leader. His wife’s name was Maacah.
Yeieli alikuwa baba yake Gibeoni naye aliishi huko Gibeoni. Mke wake aliitwa Maaka,
36 His oldest son was Abdon. His other sons were Zur, Kish, Baal, Ner, Nadab,
mwanawe mzaliwa wa kwanza alikuwa Abdoni, akafuatiwa na Suri, Kishi, Baali, Neri, Nadabu,
37 Gedor, Ahio, Zechariah, and Mikloth.
Gedori, Ahio, Zekaria na Miklothi.
38 Mikloth was the father of Shimeam. Jeiel’s family lived near their relatives in Jerusalem.
Miklothi akamzaa Shimeamu. Wao pia waliishi karibu na jamaa zao huko Yerusalemu.
39 Ner was the father of Kish. Kish was the father of [King] Saul. Saul was the father of Jonathan, Malchishua, Abinadab, and Esh-Baal.
Neri akamzaa Kishi, Kishi akamzaa Sauli. Sauli akamzaa Yonathani, Malki-Shua, Abinadabu na Esh-Baali.
40 Jonathan’s son was Merib-Baal. Merib-Baal was the father of Micah.
Yonathani akamzaa Merib-Baali, naye Merib-Baali akamzaa Mika.
41 Micah’s sons were Pithon, Melech, Tahrea, [and Ahaz].
Wana wa Mika walikuwa: Pithoni, Meleki, Tarea, na Ahazi.
42 Ahaz was the father of Jadah (OR, Jarah). Jadah was the father of Alemeth, Azmaveth, and Zimri. Zimri was the father of Moza.
Ahazi akamzaa Yara, Yara akawazaa Alemethi, Azmawethi na Zimri, naye Zimri akamzaa Mosa.
43 Moza was the father of Binea. The son of Binea was Rephaiah. The son of Rephaiah was Eleasah. The son of Eleasah was Azel.
Mosa akamzaa Binea, Binea akamzaa Refaya, na mwanawe huyo ni Eleasa, na mwanawe huyo ni Aseli.
44 Azel had six sons: Azrikam, Bokeru, Ishmael, Sheariah, Obadiah, and Hanan.
Aseli alikuwa na wana sita, na haya ndiyo majina yao: Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia na Hanani. Hawa ndio waliokuwa wana wa Aseli.

< 1 Chronicles 9 >