< 1 Chronicles 21 >

1 Satan decided to cause the Israeli people to have trouble. So he incited David to find out how many men in Israel [were able to be in the army].
Shetani akainuka dhidi ya Israeli na kumshawishi Daudi ahesabu watu wa Israeli.
2 So David commanded Joab and the other army commanders, “Count all the men in Israel [who are able to be in the army]. Start at Beersheba [town in the south] and go all the way to Dan [city in the north]. Then come back and report to me, in order that I may know how many men there are.”
Kwa hiyo Daudi akamwambia Yoabu na majemadari wa jeshi, “Nendeni mkawahesabu Waisraeli kuanzia Beer-Sheba mpaka Dani. Kisha nileteeni taarifa ili kwamba niweze kufahamu wako wangapi.”
3 But Joab replied, “Your majesty, even if Yahweh allowed us to have 100 times as many soldiers as we have now, you would [RHQ] still rule all of them. So why do you want us to do this? You will surely [RHQ] cause [all the people of] Israel to be guilty of sinning.”
Yoabu akajibu, “Bwana na aongeze jeshi lake mara mia na zaidi. Mfalme bwana wangu, kwani hawa wote si raiya wa bwana wangu? Kwa nini bwana wangu unataka kufanya hivi? Kwa nini kuleta hatia juu ya Israeli?”
4 But David would not change his mind. So Joab [and his soldiers] went everywhere in Israel and in Judah, and counted the people. Then they returned to Jerusalem,
Hata hivyo, neno la mfalme likawa na nguvu juu ya Yoabu; kwa hiyo Yoabu akaondoka na kuzunguka Israeli yote kisha akarudi Yerusalemu.
5 and they reported to David that there were 1,100,000 men in Israel who could be in the army, and 470,000 in Judah.
Yoabu akampa Daudi jumla ya idadi ya watu wanaoweza kupigana. Katika Israeli kulikuwa na watu 1,100,000 ambao wangeweza kutumia upanga na katika Yuda watu 470,000.
6 Joab did not count the men from the tribes of Levi and Benjamin, because he was disgusted with what the king had commanded.
Lakini Yoabu hakuwahesabu Walawi na Wabenyamini, kwa sababu alichukizwa sana na amri ya mfalme.
7 David’s command to count the people caused God to become angry, so he [told David that he had decided to] punish [the people of] Israel.
Amri hii ilikuwa mbaya machoni pa Mungu pia; hivyo akaiadhibu Israeli.
8 Then David prayed, saying, “Yahweh, what I did was very foolish. I have sinned greatly by what I have done. So now I plead with you, please forgive me.”
Kisha Daudi akamwambia Mungu, “Nimetenda dhambi kubwa kwa kufanya jambo hili. Sasa, ninakusihi, ondoa hatia ya mtumishi wako. Nimefanya jambo la kipumbavu sana.”
9 Then Yahweh said to Gad, David’s prophet,
Bwana akamwambia Gadi, mwonaji wa Daudi,
10 “Go and tell this to David: I am allowing you to choose one of three things [to punish you]. I will do whichever one you choose.”
“Nenda ukamwambie Daudi, hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Ninakupa wewe uchaguzi wa mambo matatu. Nichagulie mojawapo nitakalotenda dhidi yako.’”
11 So Gad went to David and said to him, “This is what Yahweh says: ‘You can choose one of these [punishments]:
Kwa hiyo Gadi akamwendea Daudi akamwambia, “Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Chagua:
12 three years of famine [in Israel], or three months during which your armies will run away from their enemies [who will attack them with] swords, or three days during which I will send my angel to cause many people in the country to die because of a (plague/very serious illness).’ So, you must decide what I will say to answer [Yahweh, ] the one who sent me.”
miaka mitatu ya njaa, au miezi mitatu ya kushindwa na adui zako, ukipatwa na upanga wao, au siku tatu za upanga wa Bwana, yaani, siku tatu za tauni katika nchi na malaika wa Bwana akiangamiza kila mahali katika Israeli.’ Sasa basi, amua jinsi nitakavyomjibu yeye aliyenituma.”
13 David replied to Gad, “I am very distressed. But allow Yahweh to punish [MTY] me, because he is very merciful. Do not allow humans to punish me, [because they will not be merciful].”
Daudi akamwambia Gadi, “Ninayo mahangaiko makubwa. Mimi na nianguke mikononi mwa Bwana kwa maana rehema zake ni kuu mno, lakini usiniache niangukie mikononi mwa wanadamu.”
14 So Yahweh sent a plague on [the people of] Israel, and 70,000 of them died because of it.
Basi Bwana akatuma tauni katika Israeli, watu 70,000 wa Israeli wakafa.
15 And God sent an angel to destroy the people in Jerusalem by the plague. But when the angel was standing at the ground where Araunah, from the Jebus people-group, threshed grain, Yahweh saw all the suffering that the people had endured, and he was grieved. So he said to the angel, “Stop what you are doing [IDM]! That is enough [IDM]!”
Mungu akapeleka malaika kuangamiza Yerusalemu. Lakini malaika alipokuwa akifanya hivyo, Bwana akaona na akahuzunika kwa sababu ya maafa, akamwambia yule malaika aliyekuwa anaangamiza watu, “Yatosha! Rudisha mkono wako.” Wakati huo malaika wa Bwana alikuwa amesimama katika sakafu ya kupuria nafaka ya Arauna Myebusi.
16 David looked up and saw the angel whom Yahweh had sent, standing between the sky and the ground. The angel had a sword in his hand that was pointed toward Jerusalem. Then David and the elders [of the city], who were wearing clothes made of rough sackcloth, prostrated themselves on the ground.
Daudi akayainua macho yake akamwona huyo malaika wa Bwana akiwa amesimama katikati ya mbingu na dunia, naye ameunyoosha upanga wake juu ya Yerusalemu tayari kuangamiza. Kisha Daudi na wazee, waliokuwa wamevaa nguo za gunia, wakaanguka kifudifudi.
17 David said to God, “I am [RHQ] the one who ordered the men who could be in the army to be counted. I am the one who has sinned and done what is very wrong, but these people are [as innocent as] [MET] sheep. They have certainly not [RHQ] done anything [that is wrong]. So Yahweh my God, punish [IDM] me and my family, but do not allow this plague to continue to [cause] your people [to become sick and die].”
Daudi akamwambia Mungu, “Je, si mimi ndiye niliyeamuru watu wahesabiwe? Mimi ndiye niliyetenda dhambi na kukosa. Hawa ni kondoo tu. Wamefanya nini? Ee Bwana, Mungu wangu, mkono wako na uwe juu yangu mimi na jamaa yangu, lakini usiache tauni hii iendelee juu ya watu wako.”
18 Then the angel who was sent by Yahweh told Gad to go up to the place where Araunah threshed grain and tell David to build an altar to [worship] Yahweh there.
Kisha malaika wa Bwana akamwamuru Gadi amwambie Daudi apande na kumjengea Bwana madhabahu kwenye sakafu ya kupuria nafaka ya Arauna Myebusi.
19 So [after Gad told] David, [he] obeyed the message that Yahweh [MTY] had given to Gad, [and he went up there].
Kwa hiyo Daudi akakwea, akalitii lile neno ambalo Gadi alikuwa amelisema katika jina la Bwana.
20 While Araunah was threshing some wheat, he turned and saw the angel. His four sons who were with him [also saw the angel, and they] hid themselves.
Arauna alipokuwa akipura ngano, akageuka akamwona yule malaika. Wanawe wanne waliokuwa pamoja naye wakajificha, yeye akaendelea kupura ngano.
21 Then David approached. When Araunah saw him, he left the place where he was threshing grain and prostrated himself, with his face touching the ground.
Kisha Daudi akakaribia, Arauna alipotazama na kumwona, akaondoka kwenye uwanja wa kupuria nafaka akamsujudia Daudi akiuinamisha uso wake ardhini.
22 David said to him, “Please sell me your threshing place in order that I can build an altar here to [worship] Yahweh. Then he will stop this plague. I will pay the full price.”
Daudi akamwambia, “Nipatie huu uwanja wako wa kupuria nafaka ili niweze kujenga madhabahu ya Bwana tauni ipate kukomeshwa katika watu. Niuzie kwa bei yake kamili.”
23 Araunah replied, “Take it! Your majesty, do whatever you want to. I will give you the oxen [that thresh the grain] for an offering to be completely burned [on the altar]. And I will give you the threshing boards to use as wood [on the altar], and I will give you grain for a grain offering. I will give all those things to you.”
Arauna akamwambia Daudi, “Uchukue huo uwanja. Mfalme bwana wangu na afanye lolote analopenda. Tazama, nitatoa maksai kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, vifaa vya kupuria kuwa kuni, pamoja na ngano kwa ajili ya dhabihu ya nafaka. Natoa hivi vyote.”
24 But the king said to Araunah, “No, [I will not take these things as a gift]. I will pay you the full price for it. I will not take things that belong to you, things that have cost me nothing and offer them as sacrifices to Yahweh to be completely burned on the altar.”
Lakini Mfalme Daudi akamjibu Arauna, “La hasha! Lakini ninasisitiza kwamba nitalipa bei yake kamili. Sitachukua kilicho chako kwa ajili ya Bwana au kutoa sadaka ya kuteketezwa ambayo hainigharimu chochote.”
25 So David paid Araunah 600 pieces of gold for the whole area.
Basi Daudi akamlipa Arauna shekeli za dhahabu 600 kwa ajili ya ule uwanja.
26 David built an altar to [worship] Yahweh there, and he offered sacrifices to be completely burned [on the altar] and sacrifices to restore fellowship [with Yahweh]. David prayed to Yahweh, and Yahweh answered by sending a fire from heaven [to burn up the offerings] on the altar.
Kisha Daudi akamjengea Bwana madhabahu mahali hapo, na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Akamwita Bwana naye Bwana akajibu maombi yake kwa moto toka mbinguni juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa.
27 Then Yahweh spoke to the angel, and told him to put his sword back into its sheath. [So the angel did that].
Kisha Bwana akanena na yule malaika, naye akarudisha upanga wake katika ala yake.
28 And when David saw that Yahweh had answered him there at the place where Araunah threshed grain [and had ended the plague], he offered sacrifices there.
Wakati huo, Daudi alipoona kwamba Bwana amemjibu kule kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Arauna Myebusi, akatoa dhabihu huko.
29 Yahweh’s Sacred Tent, which Moses had commanded to be set up in the desert, and the altar for burning sacrifices completely, were at that time on a hill at Gibeon [city].
Maskani ya Bwana ambayo Mose aliitengeneza kule jangwani, pamoja na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa wakati huo vilikuwa viko mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni.
30 But David did not want to go there to request God to tell him what he wanted [him to do], because he was afraid that the angel sent from Yahweh [might strike him with] his sword.
Lakini Daudi hakuthubutu kuisogelea ili kumuuliza Mungu, kwa sababu aliuogopa upanga wa yule malaika wa Bwana.

< 1 Chronicles 21 >