< Luke 5 >

1 And it occurred, that a multitude gathered about him, to hear the word of God. And he was standing by the side of the sea of Gennesaret,
Siku moja Yesu alikuwa amesimama kando ya ziwa Genesareti, na watu wengi walikuwa wamemzunguka wakisongana wanalisikiliza neno la Mungu.
2 and he saw two ships standing near the sea, and the fishermen were gone out of them, and were washing their nets.
Akaona mashua mbili ukingoni mwa ziwa; wavuvi wenyewe walikuwa wametoka, wanaosha nyavu zao.
3 And one of them belonged to Simon Cephas: and Jesus entered and sat in it. And he told them to draw off a little from the shore, into the sea: and he seated himself, and taught the multitude from the ship.
Baada ya Yesu kuingia katika mashua moja, iliyokuwa ya Simoni, alimtaka Simoni aisogeze majini, mbali kidogo na ukingo wa ziwa. Akaketi, akafundisha umati wa watu akiwa ndani ya mashua.
4 And when he ceased from speaking, he said to Simon: Launch out into the deep, and cast your net for a draught.
Alipomaliza kufundisha, akamwambia Simoni, “Peleka mashua mpaka kilindini, mkatupe nyavu zenu mpate kuvua samaki.”
5 Simon answered, and said to him: Rabbi, all the night we have toiled, and have caught nothing: but, at thy bidding, I will cast the net.
Simoni akamjibu, “Bwana, tumejitahidi kuvua samaki usiku kucha bila kupata kitu, lakini kwa kuwa umesema, nitatupa nyavu.”
6 And when they had done so, they inclosed very many fishes, so that the net was rent.
Baada ya kufanya hivyo, wakavua samaki wengi, hata nyavu zao zikaanza kukatika.
7 And they made signs to their associates, in the other ship, to come and help them. And when they came, they filled both the ships, so that they were near to sinking.
Wakawaita wenzao waliokuwa katika mashua nyingine waje kuwasaidia. Wakaja, wakazijaza mashua zote mbili samaki, hata karibu zingezama.
8 And when Simon Cephas saw it, he fell before the feet of Jesus, and said to him: I beseech thee, my Lord, that thou leave me, for I am a sinful man.
Simoni Petro alipoona hayo, akapiga magoti mbele ya Yesu akisema, “Ondoka mbele yangu, ee Bwana, kwa kuwa mimi ni mwenye dhambi!”
9 For astonishment had seized him, and all that were with him, at the draught of fishes which they had caught:
Simoni pamoja na wenzake wote walishangaa kwa kupata samaki wengi vile.
10 and in like manner also James and John, the sons of Zebedee, who were partners of Simon. But Jesus said: Fear thou not; henceforth thou shalt catch men unto life.
Hali kadhalika Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo, waliokuwa wavuvi wenzake Simoni. Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope; tangu sasa utakuwa ukivua watu.”
11 And they brought the vessels to the land: and they left all and followed him.
Basi, baada ya kuzileta zile mashua ukingoni mwa ziwa, wakaacha yote, wakamfuata.
12 And when Jesus was in one of the cities, a man came all full of leprosy and seeing Jesus, he fell upon his face, and besought him, and said to him: My Lord, if thou wilt, thou canst cleanse me.
Ikawa, Yesu alipokuwa katika mmojawapo wa miji ya huko, mtu mmoja mwenye ukoma mwili mzima akamwona. Basi, mtu huyo akaanguka kifudifudi akamwomba Yesu: “Mheshimiwa, ukitaka, waweza kunitakasa.”
13 And Jesus put forth his hand, and touched him, and said to him: I will it; be thou clean. And immediately his leprosy went from him.
Yesu akaunyosha mkono wake, akamgusa na kusema, “Nataka, takasika!” Mara ule ukoma ukamwacha.
14 And he charged him: Speak to no one; but go and show thyself to the priests, and offer the oblation for thy purification, as Moses hath commanded, for a testimony to them.
Yesu akamwamuru: “Usimwambie mtu yeyote; bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani, ukatoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama inavyotakiwa na Sheria ya Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona.”
15 And his fame spread abroad still more: and much people assembled to hear him, and to be cured of their diseases.
Lakini habari za Yesu zilizidi kuenea kila mahali. Watu makundi mengi wakakusanyika ili kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao.
16 And he retired into a desert, and prayed.
Lakini yeye alikwenda zake mahali pasipo na watu, akawa anasali huko.
17 And it occurred, on one of the days when Jesus was teaching, that Pharisees and Doctors of the law were sitting by, who had come from all the villages of Galilee and of Judaea, and Jerusalem: and the power of the Lord was present to heal them.
Siku moja Yesu alikuwa akifundisha. Mafarisayo na walimu wa Sheria kutoka katika kila kijiji cha Galilaya, Yudea na Yerusalemu, walikuwa wameketi hapo. Nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye kwa ajili ya kuponyea wagonjwa.
18 And some persons brought a paralytic man, on a couch, and sought to bring him in, and to place him before him.
Mara watu wakaja wamemchukua mtu mmoja aliyepooza maungo, amelala kitandani; wakajaribu kumwingiza ndani wamweke mbele ya Yesu.
19 And when they could not thus introduce him, because of the multitude of the people, they ascended to the roof, and let him down with the couch, from the covering, into the midst, before Jesus.
Lakini kwa sababu ya wingi wa watu, hawakuweza kuingia ndani. Basi, wakapanda juu ya dari, wakaondoa vigae, wakamshusha huyo aliyepooza pamoja na kitanda chake, wakamweka mbele ya Yesu.
20 And when Jesus saw their faith, he said to the paralytic: Man, thy sins are forgiven thee.
Yesu alipoona jinsi walivyokuwa na imani kubwa, akamwambia huyo mtu, “Rafiki, umesamehewa dhambi zako.”
21 And the Scribes and Pharisees began to reason, and to say: Who is this that speaketh blasphemy? Who can forgive sins, but God only?
Walimu wa Sheria na Mafarisayo wakaanza kujiuliza: “Nani huyu anayemkufuru Mungu kwa maneno yake? Hakuna mtu awezaye kusamehe dhambi ila Mungu peke yake!”
22 And Jesus knew their thoughts, and said to them: What think ye in your heart?
Yesu alitambua mawazo yao, akawauliza, “Mnawaza nini mioyoni mwenu?
23 Which is the easier, to say, Thy sins are forgiven thee, or to say, Arise and walk?
Ni lipi lililo rahisi zaidi: kusema, Umesamehewa dhambi, au kusema, Simama utembee?
24 But that ye may know, that the Son of man is competent to forgive sins on the earth, he said to the paralytic: I say to thee, Arise, take up thy couch, and go to thy home.
Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anao uwezo wa kusamehe dhambi duniani.” Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza, “Simama, chukua kitanda chako uende zako nyumbani.”
25 And instantly, he rose up before their eyes, and took up his couch, and went home, glorifying God.
Mara, huyo mtu aliyepooza akasimama mbele yao wote, akachukua kitanda chake akaenda zake nyumbani huku akimtukuza Mungu.
26 And astonishment seized every one; and they Praised God; and they were filled with awe, and said: We have seen wonders today.
Wote wakashangaa na kushikwa na hofu; wakamtukuza Mungu wakisema: “Tumeona maajabu leo.”
27 And after these things, Jesus went out and saw a publican, named Levi, sitting among the publicans; and he said to him: Come after me.
Baada ya hayo, Yesu akatoka nje, akamwona mtoza ushuru mmoja aitwaye Lawi, ameketi ofisini. Yesu akamwambia, “Nifuate!”
28 And he left every thing, and arose, and went after him.
Lawi akaacha yote, akamfuata.
29 And Levi made a great entertainment for him at his house; and there was a numerous company of publicans and others who reclined with them.
Kisha Lawi akamwandalia Yesu karamu kubwa nyumbani mwake; na kundi kubwa la watoza ushuru na watu wengine walikuwa wameketi pamoja nao.
30 And the Scribes and Pharisees murmured, and said to his disciples: Why do ye eat and drink with publicans and sinners?
Mafarisayo na walimu wa Sheria wakawanung'unikia wafuasi wake wakisema: “Mbona mnakula na kunywa pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?”
31 And Jesus answered and said to them: A physician is not sought after for the well, but for those very sick.
Yesu akawajibu, “Wenye afya hawahitaji daktari, lakini wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa.
32 I came not to call the righteous, but sinners, to repentance.
Sikuja kuwaita watu wema, bali wenye dhambi, ili wapate kutubu.”
33 And they said to him: Why do the disciples of John fast often, and pray, and also those of the Pharisees; but thine eat and drink?
Watu wengine wakamwambia Yesu, “Wafuasi wa Yohane mbatizaji hufunga mara nyingi na kusali; hata wafuasi wa Mafarisayo hufanya vivyo hivyo. Lakini wafuasi wako hula na kunywa.”
34 And he said to them: Ye cannot make the guests of the nuptial chamber fast, while the bridegroom is with them.
Yesu akawajibu, “Je, mnaweza kuwataka wale walioalikwa arusini wafunge hali bwana arusi yuko pamoja nao?
35 But the days will come, when the bridegroom will be taken up from them, and then will they fast, in those days.
Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kati yao, na wakati huo ndipo watakapofunga.”
36 And he spoke a similitude to them: No one teareth a patch from a new garment, and putteth it to an old garment; lest he tear the new, and the patch from the new cease to make the old garment whole.
Yesu akawaambia mfano huu: “Hakuna mtu akataye kiraka cha nguo mpya na kukitia katika vazi kuukuu; kama akifanya hivyo, atakuwa amelikata hilo vazi jipya, na hicho kiraka hakitachukuana na hilo vazi kuukuu.
37 And no one putteth new wine into old sacks; otherwise, the new wine will burst the sacks, and the wine will run out, and the sacks be ruined.
Wala hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu; kwani hiyo divai mpya itavipasua hivyo viriba, divai itamwagika, na viriba vitaharibika.
38 But they put new wine into new sacks, and both are preserved.
Divai mpya hutiwa katika viriba vipya!
39 And no one drinketh old wine, and immediately calleth for new; for he saith, The old is the delicious.
Wala hakuna mtu ambaye hutamani kunywa divai mpya baada ya kunywa ya zamani, kwani husema: Ile ya zamani ni nzuri zaidi.”

< Luke 5 >