< Luke 19 >

1 And as Jeshu entered and passed through Jirichu,
Yesu aliingia mjini Yeriko, akawa anapita katika njia za mji huo.
2 there was a certain man whose name was Zakai; he was rich and chief of the publicans:
Kulikuwa na mtu mmoja mjini, jina lake Zakayo ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3 and he wished to see Jeshu, who he was, and could not for the crowd, because in his stature Zakai was small.
Alitaka kuona Yesu alikuwa nani, lakini kwa sababu ya umati wa watu, na kwa vile alikuwa mfupi, hakufaulu.
4 And he ran before Jeshu, and ascended a wild fig-tree to see him, because so he was about to pass.
Hivyo, alitangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona Yesu, kwa maana alikuwa apitie hapo.
5 And when Jeshu came to that place, he saw him, and said to him, Be in haste, descend, Zakai; for to-day I must be at thy house.
Basi, Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.”
6 And he was in haste, and descended, and received him rejoicing.
Zakayo akashuka haraka, akamkaribisha kwa furaha.
7 But when they all saw (this), they murmured, and said that with a man a sinner he hath gone in to abide.
Watu wote walipoona hayo, wakaanza kunung'unika wakisema, “Amekwenda kukaa kwa mtu mwenye dhambi.”
8 But Zakai stood, and said to Jeshu, Behold, my Lord, the dividing of my wealth give I to the poor; and to every man, whatever I have wrongfully taken, fourfold I restore.
Lakini Zakayo akasimama akamwambia Yesu, “Sikiliza Bwana! Mimi nitawapa maskini nusu ya mali yangu, na kama nimenyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne.”
9 Jeshu saith to him, To-day is there salvation to this house, because this (man) also (is a) son of Abraham.
Yesu akamwambia, “Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa vile huyu pia ni wa ukoo wa Abrahamu.
10 For the Son of man came to save that which was lost.
Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa waliopotea.”
11 And when they had heard these things, he added to speak a parable; because he had drawn nigh to Urishlem, and they expected that in that hour would be revealed the kingdom of Aloha.
Wakati watu walipokuwa bado wanasikiliza hayo, Yesu akawaambia mfano. (Hapo alikuwa anakaribia Yerusalemu, na watu wale walidhani kwamba muda si muda, Ufalme wa Mungu ungefika.)
12 And he said, A certain man of a noble house went into a distant country, to receive for himself a kingdom, and to return.
Hivyo akawaambia, “Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa kifalme aliyefanya safari kwenda nchi ya mbali ili apokee madaraka ya ufalme, halafu arudi.
13 And he called his ten servants, and gave to them ten minin, and said to them, Trade till I come.
Basi, kabla ya kuondoka aliwaita watumishi wake kumi, akawapa kiasi cha fedha kila mmoja na kumwambia: Fanyeni nazo biashara mpaka nitakaporudi.
14 But his citizens hated him, and sent messengers after him, saying, We are not willing that this should reign over us.
Lakini wananchi wenzake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende wakaseme: Hatumtaki huyu atutawale.
15 And having received the kingdom and returned, he spake to call to him those servants to whom he had given the silver, that he might know how every one of them had traded.
“Huyo mtu mashuhuri alirudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, na mara akaamuru wale watumishi aliowapa zile fedha waitwe ili aweze kujua kila mmoja amepata faida gani.
16 And the first came and said, My lord, thy mani ten minin hath gained.
Mtumishi wa kwanza akatokea, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara kumi ya zile fedha ulizonipa.
17 He saith to him, Well, good servant: because in a little thou art found faithful, thou shalt have rule over ten towns.
Naye akamwambia: Vema; wewe ni mtumishi mwema. Kwa kuwa umekuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi!
18 And the second came and said, My lord, thy mani five minin hath made.
Mtumishi wa pili akaja, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara tano ya zile fedha ulizonipa.
19 He saith also to this, Thou also shalt have rule over five towns.
Naye akamwambia pia: Nawe utakuwa na madaraka juu ya miji mitano.
20 And the other came and said, My lord, behold thy mani which I have had with me, laid up in a napkin.
“Mtumishi mwingine akaja, akasema: Chukua fedha yako; niliificha salama katika kitambaa,
21 For I feared thee, because thou art a hard man, taking up what thou hadst not laid down, and reaping what thou sowedst not.
kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Wewe ni mtu ambaye huchukua yasiyo yako, na huchuma ambacho hukupanda.
22 He said to him, From thy own mouth I will judge thee, evil servant: thou didst know that I was a hard man, taking up what I had not laid down, and reaping what I sowed not:
Naye akamwambia: Nakuhukumu kutokana na msemo wako, ewe mtumishi mbaya! Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, ambaye huchukua yasiyo yangu na kuchuma nisichopanda.
23 why (then) gavest thou not my silver upon the table, that when I came I might require it with its increase?
Kwa nini basi, hukuiweka fedha yangu benki, nami ningeichukua pamoja na faida baada ya kurudi kwangu?
24 And to those who stood before him he said, Take from him the mani, and give to him who hath the ten minin.
Hapo akawaambia wale waliokuwa pale: Mnyang'anyeni hizo fedha, mkampe yule aliyepata faida mara kumi.
25 They say to him, Our lord, he hath ten minin.
Nao wakamwambia: Lakini Mheshimiwa, huyo ana faida ya kiasi hicho mara kumi!
26 He saith to them, I tell you, that to every one who hath (it) shall be given; and from him who hath not, that also which he hath shall be taken.
Naye akawajibu: Kila aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27 But those adversaries who would not that I should reign over them, bring them, and slay them before me.
Na sasa, kuhusu hao maadui wangu ambao hawapendi niwe mfalme wao, waleteni hapa, mkawaue papa hapa mbele yangu.”
28 AND when Jeshu had said these things, he went forward to go to Urishlem.
Yesu alisema hayo, kisha akatangulia mbele yao kuelekea Yerusalemu.
29 And when he came to Bethphage and Beth-ania, at the mount that is called the Place of Olives, he sent two from his disciples,
Alipokaribia kufika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30 and said to them, Go to the village over against us; and as you enter, behold, you will find a colt tied, whereon no man hath ridden: loose and bring him.
akawaambia: “Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana punda amefungwa ambaye hajatumiwa na mtu. Mfungeni, mkamlete hapa.
31 And if any man demand why you loose him, thus say: It is requested by our Lord.
Kama mtu akiwauliza, kwa nini mnamfungua, mwambieni, Bwana ana haja naye.”
32 And they who were sent went and found as he had told them.
Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.
33 And as they were loosing the colt, the owners of him said to them, Why loose you the colt?
Walipokuwa wanamfungua yule mwana punda, wenyewe wakawauliza, “Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?”
34 And they said to them, Because by our Lord it is requested.
Nao wakawajibu, “Bwana anamhitaji.”
35 And they brought him to Jeshu; and they cast upon the colt their garments, and Jeshu rode upon him.
Basi, wakampelekea Yesu yule mwana punda. Kisha wakatandika mavazi yao juu yake wakampandisha Yesu.
36 And as they went, they spread their clothes in the way.
Yesu akaendelea na safari, na watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37 And when he had come nigh to the declivity of the Mount of Olives, the whole assembly of the disciples began to rejoice, and praise Aloha with a high voice, for all the mighty acts which they had seen:
Alipofika karibu na Yerusalemu, katika mteremko wa mlima wa Mizeituni, umati wote na wanafunzi wake, wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona;
38 and they said, Blessed be the King who cometh in the name of the Lord! Peace in the heavens, and glory in the highest!
wakawa wanasema: “Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!”
39 But some of the Pharishee from among the multitudes say to him, Rabi, rebuke thy disciples.
Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu, wakamwambia Yesu, “Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!”
40 He saith to them, I tell you, if these should be silent, the stones would cry out.
Yesu akawajibu, “Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, hakika hayo mawe yatapaza sauti.”
41 AND when he approached, and saw the city, he wept over her, saying,
Alipokaribia zaidi na kuuona ule mji, Yesu aliulilia
42 If thou hadst known these things which are for thy peace, and in this thy day! But now they are hidden from thine eyes.
akisema: “Laiti ungelijua leo hii yale yaletayo amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43 But the days will come to thee when thine enemies shall encompass thee and straiten thee on every side,
Maana siku zaja ambapo adui zako watakuzungushia maboma, watakuzingira na kukusonga pande zote.
44 and they shall overthrow thee, and thy children within thee, and not leave in thee one stone upon another, because thou knewest not the time of thy visitation.
Watakupondaponda wewe pamoja na watoto wako ndani ya kuta zako; hawatakuachia hata jiwe moja juu jingine, kwa sababu hukuutambua wakati Mungu alipokujia kukuokoa.”
45 And as he went into the temple, he began to cast out those who bought in it and sold,
Kisha, Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuzia nje wafanyabiashara
46 and said to them, It is written that my house is the house of prayer; but you have made it a den of thieves.
akisema, “Imeandikwa: Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi.”
47 And he taught every day in the temple; but the chief priests and the scribes and the elders of the people sought to destroy him,
Yesu akawa anafundisha kila siku Hekaluni. Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumwangamiza,
48 but could not find what they might do to him; for all the people hung upon him to hear him.
lakini hawakuwa na la kufanya, maana watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini kabisa.

< Luke 19 >