< Luke 19 >

1 And as Jeshu entered and passed through Jirichu,
Yesu aliingia na kupita katikati ya Yeriko.
2 there was a certain man whose name was Zakai; he was rich and chief of the publicans:
Na hapo palikuwa na mtu mmoja aitwaye Zakayo. Ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3 and he wished to see Jeshu, who he was, and could not for the crowd, because in his stature Zakai was small.
Alikuwa anajaribu kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, lakini hakuweza kuona kwa sababu ya umati wa watu, kwa kuwa alikuwa mfupi wa kimo.
4 And he ran before Jeshu, and ascended a wild fig-tree to see him, because so he was about to pass.
Hivyo, alitangulia mbio mbele za watu, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona, kwa sababu Yesu alikaribia kupita njia hiyo.
5 And when Jeshu came to that place, he saw him, and said to him, Be in haste, descend, Zakai; for to-day I must be at thy house.
Wakati Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, 'Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.'
6 And he was in haste, and descended, and received him rejoicing.
Akafanya haraka, akashuka na kumkaribisha kwa furaha.
7 But when they all saw (this), they murmured, and said that with a man a sinner he hath gone in to abide.
Watu wote walipoona hayo, wakalalamika, wakisema, 'Amekwenda kumtembelea mtu mwenye dhambi.'
8 But Zakai stood, and said to Jeshu, Behold, my Lord, the dividing of my wealth give I to the poor; and to every man, whatever I have wrongfully taken, fourfold I restore.
Zakayo akasimama akamwambia Bwana, Tazama Bwana nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimemnyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne. '
9 Jeshu saith to him, To-day is there salvation to this house, because this (man) also (is a) son of Abraham.
Yesu akamwambia, 'Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa sababu yeye pia ni mwana wa Ibrahimu.
10 For the Son of man came to save that which was lost.
Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa watu waliopotea. '
11 And when they had heard these things, he added to speak a parable; because he had drawn nigh to Urishlem, and they expected that in that hour would be revealed the kingdom of Aloha.
Waliposikia hayo, aliendelea kuongea na alitoa mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalemu, na wao walidhani ya kuwa ufalme wa Mungu ulikuwa karibu kuonekana mara moja.
12 And he said, A certain man of a noble house went into a distant country, to receive for himself a kingdom, and to return.
Hivyo akawaambia, 'Ofisa mmoja alikwenda nchi ya mbali ili apokee ufalme na kisha aurudi.
13 And he called his ten servants, and gave to them ten minin, and said to them, Trade till I come.
Aliwaita watumishi wake kumi, akawapa mafungu kumi, akawaambia, 'fanyeni biashara mpaka nitakaporudi.'
14 But his citizens hated him, and sent messengers after him, saying, We are not willing that this should reign over us.
Lakini wananchi wake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende kumfuata na kusema, 'Hatutaki mtu huyu atutawale.'
15 And having received the kingdom and returned, he spake to call to him those servants to whom he had given the silver, that he might know how every one of them had traded.
Ikawa aliporudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, akaamuru wale watumishi aliokuwa amewaachia fedha waitwe kwake, apate kujua faida gani waliyoipata kwa kufanya biashara.
16 And the first came and said, My lord, thy mani ten minin hath gained.
Wa kwanza akaja, akasema, `Bwana, fungu lako limefanya mafungu kumi zaidi. '
17 He saith to him, Well, good servant: because in a little thou art found faithful, thou shalt have rule over ten towns.
Huyo Ofisa akamwambia, Vema, mtumishi mwema. Kwa sababu ulikuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi. '
18 And the second came and said, My lord, thy mani five minin hath made.
Wa pili akaja, akasema, 'Bwana, fungu lako limefanya mafungu matano.'
19 He saith also to this, Thou also shalt have rule over five towns.
Huyo Afisa akamwambia, 'Chukua mamlaka juu ya miji mitano.'
20 And the other came and said, My lord, behold thy mani which I have had with me, laid up in a napkin.
Na mwingine akaja, akasema, `Bwana hii hapa fedha yako, ambayo niliihifadhi salama katika kitambaa,
21 For I feared thee, because thou art a hard man, taking up what thou hadst not laid down, and reaping what thou sowedst not.
kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Unaondoa kile usichokiweka na kuvuna usichopanda. '
22 He said to him, From thy own mouth I will judge thee, evil servant: thou didst know that I was a hard man, taking up what I had not laid down, and reaping what I sowed not:
Huyo Ofisa akamwambia, 'Kwa maneno yako mwenyewe, nitakuhukumu, ewe mtumishi mbaya. Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, nachukua nisichokiweka na kuvuna ambacho sikupanda.
23 why (then) gavest thou not my silver upon the table, that when I came I might require it with its increase?
Basi, mbona hukuweka fedha yangu katika benki, ili nikirudi niichukue pamoja na faida?
24 And to those who stood before him he said, Take from him the mani, and give to him who hath the ten minin.
Ofisa akawaambia watu waliokuwa wamesimama hapo, 'Mnyang'anyeni hilo fungu na kumpa yule mwenye mafungu kumi.'
25 They say to him, Our lord, he hath ten minin.
Wakamwambia, `Bwana, yeye ana mafungu kumi. '
26 He saith to them, I tell you, that to every one who hath (it) shall be given; and from him who hath not, that also which he hath shall be taken.
'Nawaambia, kila mtu ambaye anacho atapewa zaidi, lakini ambaye hana, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27 But those adversaries who would not that I should reign over them, bring them, and slay them before me.
Lakini hawa maadui zangu, ambao hawakutaka niwe Mfalme wao, waleteni hapa na kuwaua mbele yangu. ''
28 AND when Jeshu had said these things, he went forward to go to Urishlem.
Baada ya kusema hayo, aliendelea mbele akipanda kwenda Yerusalemu.
29 And when he came to Bethphage and Beth-ania, at the mount that is called the Place of Olives, he sent two from his disciples,
Ikawa alipokaribia Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30 and said to them, Go to the village over against us; and as you enter, behold, you will find a colt tied, whereon no man hath ridden: loose and bring him.
akisema: `Nendeni katika kijiji cha jirani. Mkiingia, mtakuta mwana-punda hajapandwa bado. Mfungueni, mkamlete kwangu.
31 And if any man demand why you loose him, thus say: It is requested by our Lord.
Kama mtu akiwauliza, `Mbona mnamfungua? ' Semeni, “Bwana anamhitaji. ''
32 And they who were sent went and found as he had told them.
Wale waliotumwa wakaenda wakamwona mwana-punda kama Yesu alivyokuwa amewaambia.
33 And as they were loosing the colt, the owners of him said to them, Why loose you the colt?
Walipokuwa wanamfungua mwana punda wamiliki wakawaambia, 'Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?'
34 And they said to them, Because by our Lord it is requested.
Wakasema, `Bwana anamhitaji. '
35 And they brought him to Jeshu; and they cast upon the colt their garments, and Jeshu rode upon him.
Basi, wakampelekea Yesu, wakatandika nguo zao juu ya mwana punda na wakampandisha Yesu juu yake.
36 And as they went, they spread their clothes in the way.
Alipokuwa akienda watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37 And when he had come nigh to the declivity of the Mount of Olives, the whole assembly of the disciples began to rejoice, and praise Aloha with a high voice, for all the mighty acts which they had seen:
Alipokuwa anateremka mlima wa Mizeituni, jumuiya yote ya wanafunzi wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona,
38 and they said, Blessed be the King who cometh in the name of the Lord! Peace in the heavens, and glory in the highest!
wakisema, 'Ndiye mbarikiwa Mfalme ajaye kwa jina la Bwana! Amani mbinguni, na utukufu juu!'
39 But some of the Pharishee from among the multitudes say to him, Rabi, rebuke thy disciples.
Baadhi ya Mafarisayo katika mkutano wakamwambia, Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako. '
40 He saith to them, I tell you, if these should be silent, the stones would cry out.
Yesu akajibu, akasema, `Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapaza sauti. '
41 AND when he approached, and saw the city, he wept over her, saying,
Yesu alipoukaribia mji aliulilia,
42 If thou hadst known these things which are for thy peace, and in this thy day! But now they are hidden from thine eyes.
akisema, laiti ungelijua hata wewe, katika siku hii mambo ambayo yanayokuletea amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43 But the days will come to thee when thine enemies shall encompass thee and straiten thee on every side,
Kwa kuwa siku zinakuja ambapo adui zako watajenga boma karibu na wewe, na kukuzunguka na kukukandamiza kutoka kila upande.
44 and they shall overthrow thee, and thy children within thee, and not leave in thee one stone upon another, because thou knewest not the time of thy visitation.
Watakuangusha chini wewe na watoto wako. Hawatakuachia hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuwa anajaribu kukuokoa'.
45 And as he went into the temple, he began to cast out those who bought in it and sold,
Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza,
46 and said to them, It is written that my house is the house of prayer; but you have made it a den of thieves.
akiwaambia, “Imeandikwa, 'Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,' lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi”.
47 And he taught every day in the temple; but the chief priests and the scribes and the elders of the people sought to destroy him,
Kwa hiyo, Yesu alikuwa akifundisha kila siku hekaluni. Makuhani wakuu na walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumuua,
48 but could not find what they might do to him; for all the people hung upon him to hear him.
lakini hawakuweza kupata njia ya kufanya hivyo, kwa sababu watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini.

< Luke 19 >