< Psalms 143 >

1 melody to/for David LORD to hear: hear prayer my to listen [emph?] to(wards) supplication my in/on/with faithfulness your to answer me in/on/with righteousness your
Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, sikia sala yangu, sikiliza kilio changu unihurumie; katika uaminifu na haki yako njoo unisaidie.
2 and not to come (in): come in/on/with justice: judgement with servant/slave your for not to justify to/for face: before your all alive
Usimhukumu mtumishi wako, kwa kuwa hakuna mtu anayeishi aliye mwenye haki mbele zako.
3 for to pursue enemy soul my to crush to/for land: soil living thing my to dwell me in/on/with darkness like/as to die forever: antiquity
Adui hunifuatilia, hunipondaponda chini; hunifanya niishi gizani kama wale waliokufa zamani.
4 and to enfeeble upon me spirit my in/on/with midst me be desolate: appalled heart my
Kwa hiyo roho yangu inazimia ndani yangu, moyo wangu ndani yangu unakata tamaa.
5 to remember day from front: old to mutter in/on/with all work your in/on/with deed: work hand your to muse
Nakumbuka siku za zamani; natafakari juu ya kazi zako zote, naangalia juu ya kazi ambazo mikono yako imezifanya.
6 to spread hand my to(wards) you soul my like/as land: country/planet faint to/for you (Selah)
Nanyoosha mikono yangu kwako, nafsi yangu inakuonea kiu kama ardhi kame.
7 to hasten to answer me LORD to end: finish spirit my not to hide face your from me and to liken with to go down pit
Ee Bwana, unijibu haraka, roho yangu inazimia. Usinifiche uso wako, ama sivyo nitafanana na wale washukao shimoni.
8 to hear: hear me in/on/with morning kindness your for in/on/with you to trust to know me way: conduct this to go: went for to(wards) you to lift: kindness soul my
Asubuhi uniletee neno la upendo wako usiokoma, kwa kuwa nimeweka tumaini langu kwako. Nionyeshe njia nitakayoiendea, kwa kuwa kwako nainua nafsi yangu.
9 to rescue me from enemy my LORD to(wards) you to cover
Ee Bwana, uniokoe na adui zangu, kwa kuwa nimejificha kwako.
10 to learn: teach me to/for to make: do acceptance your for you(m. s.) God my spirit your pleasant to lead me in/on/with land: soil plain
Nifundishe kufanya mapenzi yako, kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu, Roho wako mwema na aniongoze katika nchi tambarare.
11 because name your LORD to live me in/on/with righteousness your to come out: send from distress soul my
Ee Bwana, kwa ajili ya jina lako, hifadhi maisha yangu, kwa haki yako nitoe katika taabu.
12 and in/on/with kindness your to destroy enemy my and to perish all to vex soul my for I servant/slave your
Kwa upendo wako usiokoma, nyamazisha adui zangu; waangamize watesi wangu wote, kwa kuwa mimi ni mtumishi wako.

< Psalms 143 >