< Luke 21 >

1 to look up/again then to perceive: see the/this/who to throw: put toward the/this/who treasury the/this/who gift it/s/he rich
Yesu alitazama kwa makini, akawaona matajiri walivyokuwa wanatia sadaka zao katika hazina ya Hekalu,
2 to perceive: see then (and *k*) one widow poor to throw: put there coin two
akamwona pia mama mmoja mjane akitumbukiza humo sarafu mbili ndogo.
3 and to say truly to say you that/since: that the/this/who widow this/he/she/it the/this/who poor greater all to throw: put
Basi, akasema, “Nawaambieni kweli, mama huyu mjane ametia zaidi katika hazina kuliko wote.
4 (all *N(k)O*) for this/he/she/it out from the/this/who to exceed it/s/he to throw: put toward the/this/who gift (the/this/who God *KO*) this/he/she/it then out from the/this/who deficiency it/s/he (all *N(k)O*) the/this/who life which to have/be to throw: put
Kwa maana, wengine wote wametoa sadaka zao kutokana na ziada ya mali zao, lakini huyu mama, ingawa ni maskini, ametoa kila kitu alichohitaji kwa kuishi.”
5 and one to say about the/this/who temple that/since: that stone good and a vow offering to arrange to say
Baadhi ya wanafunzi walikuwa wanazungumza juu ya Hekalu, jinsi lilivyopambwa kwa mawe ya thamani, pamoja na sadaka zilizotolewa kwa Mungu. Yesu akasema,
6 this/he/she/it which to see/experience to come/go day in/on/among which no to release: leave stone upon/to/against stone (here *O*) which no to destroy/lodge
“Haya yote mnayoyaona—zitakuja siku ambapo hakuna hata jiwe moja litakalosalia juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa.”
7 to question then it/s/he to say teacher when? therefore/then this/he/she/it to be and which? the/this/who sign when(-ever) to ensue this/he/she/it to be
Basi, wakamwuliza, “Mwalimu, mambo hayo yatatokea lini? Na ni ishara gani zitakazoonyesha kwamba karibu mambo hayo yatokee?”
8 the/this/who then to say to see not to lead astray much for to come/go upon/to/against the/this/who name me to say (that/since: that *ko*) I/we to be and the/this/who time/right time to come near not (therefore/then *K*) to travel after it/s/he
Yesu akawajibu, “Jihadharini, msije mkadanganyika. Maana wengi watatokea na kulitumia jina langu wakisema: Mimi ndiye, na, Wakati ule umekaribia. Lakini ninyi msiwafuate!
9 when(-ever) then to hear war and disorder not to frighten be necessary for this/he/she/it to be first but no immediately the/this/who goal/tax
Basi, mtakaposikia habari za vita na misukosuko, msitishike; maana ni lazima hayo yatokee kwanza, lakini mwisho wa yote, bado.”
10 then to say it/s/he to arise Gentiles upon/to/against Gentiles and kingdom upon/to/against kingdom
Halafu akaendelea kusema: “Taifa moja litapigana na taifa lingine, na ufalme mmoja utapigana na ufalme mwingine.
11 earthquake and/both great and according to place hunger and pestilence to be fearful thing and/both and away from heaven sign great to be
Kila mahali kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, kutakuwa na njaa na tauni. Kutakuwa na vituko vya kutisha na ishara kubwa angani.
12 before then this/he/she/it (all *N(k)O*) to put on/seize upon/to/against you the/this/who hand it/s/he and to pursue to deliver toward (the/this/who *no*) synagogue and prison/watch: prison (to lead away *N(k)O*) upon/to/against king and ruler because of the/this/who name me
Lakini kabla ya kutokea hayo yote, watawatieni nguvuni, watawatesa na kuwapelekeni katika masunagogi na kuwatia gerezani; mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya jina langu.
13 to get out (then *ko*) you toward testimony
Hii itawapeni fursa ya kushuhudia Habari Njema.
14 (to place *N(k)O*) therefore/then (in/on/among the/this/who heart *N(k)O*) you not to premeditate to defend oneself
Muwe na msimamo huu mioyoni mwenu: hakuna kufikiria kabla ya wakati juu ya jinsi mtakavyojitetea,
15 I/we for to give you mouth and wisdom which no be able to oppose (or *N(k)O*) to contradict (all *N(k)O*) the/this/who be an opponent you
kwa sababu mimi mwenyewe nitawapeni ufasaha wa maneno na hekima, hivyo kwamba zenu hawataweza kustahimili wala kupinga.
16 to deliver then and by/under: by parent and brother and kindred and friendly/friend and to kill out from you
Wazazi wenu, ndugu, jamaa na rafiki zenu watawasaliti ninyi; na baadhi yenu mtauawa.
17 and to be to hate by/under: by all through/because of the/this/who name me
Watu wote watawachukieni kwa sababu ya jina langu.
18 and hair out from the/this/who head you no not to destroy
Lakini, hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea.
19 in/on/among the/this/who perseverance you (to posses *NK(o)*) the/this/who soul: life you
Kwa uvumilivu wenu, mtayaokoa maisha yenu.
20 when(-ever) then to perceive: see to surround by/under: by army camp (the/this/who *k*) Jerusalem then to know that/since: that to come near the/this/who devastation it/s/he
“Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, ndipo mtambue ya kwamba wakati umefika ambapo mji huo utaharibiwa.
21 then the/this/who in/on/among the/this/who Judea to flee toward the/this/who mountain and the/this/who in/on/among midst it/s/he to go out and the/this/who in/on/among the/this/who country not to enter toward it/s/he
Hapo walioko Yudea wakimbilie milimani; wale walio mjini watoke; na wale walio mashambani wasirudi mjini.
22 that/since: since day vengeance this/he/she/it to be the/this/who (to fill *N(k)O*) all the/this/who to write
Kwa maana siku hizo ni siku za adhabu, ili yote yaliyoandikwa yatimie.
23 woe! (then *k*) the/this/who in/on/among belly to have/be and the/this/who to suckle in/on/among that the/this/who day to be for necessity great upon/to/against the/this/who earth: planet and wrath (in/on/among *k*) the/this/who a people this/he/she/it
Ole wao waja wazito na wanyonyeshao siku hizo! Kwa maana kutakuwa na dhiki kubwa katika nchi, na hasira ya Mungu itawajia watu hawa.
24 and to collapse mouth sword and to capture toward the/this/who Gentiles all and Jerusalem to be to trample by/under: by Gentiles until (which *no*) to fulfill (and to be *O*) time/right time Gentiles
Wengine watauawa kwa upanga, wengine watachukuliwa mateka katika nchi zote; na mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa mataifa mengine, hadi nyakati zao zitakapotimia.
25 and (to be *N(k)O*) sign in/on/among sun and moon and star and upon/to/against the/this/who earth: planet anguish Gentiles in/on/among perplexity (sound *N(k)O*) sea and tossing
“Kutakuwa na ishara katika jua na mwezi na nyota. Mataifa duniani yatakuwa na dhiki kwa sababu ya wasiwasi kutokana na mshindo wa mawimbi ya bahari.
26 to faint a human away from fear and expectation the/this/who to arrive/invade the/this/who world the/this/who for power the/this/who heaven to shake
Watu watazirai kwa sababu ya uoga, wakitazamia mambo yatakayoupata ulimwengu; kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
27 and then to appear the/this/who son the/this/who a human to come/go in/on/among cloud with/after power and glory much
Halafu, watamwona Mwana wa Mtu akija katika wingu, mwenye nguvu na utukufu mwingi.
28 be first then this/he/she/it to be to straighten up and to lift up the/this/who head you because to come near the/this/who redemption you
Wakati mambo hayo yatakapoanza kutukia, simameni na kuinua vichwa vyenu juu, kwa maana ukombozi wenu umekaribia.”
29 and to say parable it/s/he to perceive: see the/this/who fig tree and all the/this/who tree
Kisha akawaambia mfano: “Angalieni mtini na miti mingine yote.
30 when(-ever) to put forth already to see away from themself to know that/since: that already near the/this/who summer to be
Mnapoona kwamba imeanza kuchipua majani, mwatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
31 thus(-ly) and you when(-ever) to perceive: see this/he/she/it to be to know that/since: that near to be the/this/who kingdom the/this/who God
Vivyo hivyo, mtakapoona mambo hayo yanatendeka, mtatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
32 amen to say you that/since: that no not to pass by the/this/who generation this/he/she/it until if all to be
Nawaambieni hakika, kizazi hiki cha sasa hakitapita kabla ya hayo yote kutendeka.
33 the/this/who heaven and the/this/who earth: planet (to pass by *NK(o)*) the/this/who then word me no not (to pass by *N(k)O*)
Mbingu na dunia vitapita, lakini maneno yangu hayatapita.
34 to watch out then themself not once/when (to burden *N(k)O*) you the/this/who heart in/on/among dissipation and drunkenness and concern of this life and to approach upon/to/against you sudden the/this/who day that
“Muwe macho, mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na shughuli za maisha haya. La sivyo, Siku ile itawajieni ghafla.
35 as/when trap (to enter *N(k)O*) for upon/to/against all the/this/who to sit upon/to/against face all the/this/who earth: planet
Kwa maana itawajia kama mtego, wote wanaoishi duniani pote.
36 be watchful (then *N(K)O*) in/on/among all time/right time to pray in order that/to (to prevail *N(K)O*) to escape this/he/she/it all the/this/who to ensue to be and to stand before the/this/who son the/this/who a human
Muwe waangalifu basi, na salini daima ili muweze kupata nguvu ya kupita salama katika mambo haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele ya Mwana wa Mtu.”
37 to be then the/this/who day in/on/among the/this/who temple to teach the/this/who then night to go out to spend the night toward the/this/who mountain the/this/who to call: call Olivet
Wakati wa mchana, siku hizo, Yesu alikuwa akifundisha watu Hekaluni; lakini usiku alikuwa akienda katika mlima wa Mizeituni na kukaa huko.
38 and all the/this/who a people to rise at dawn to/with it/s/he in/on/among the/this/who temple to hear it/s/he
Watu wote walikuwa wanakwenda Hekaluni asubuhi na mapema, wapate kumsikiliza.

< Luke 21 >