< Luke 19 >

1 and to enter to pass through the/this/who Jericho
Yesu aliingia mjini Yeriko, akawa anapita katika njia za mji huo.
2 and look! man name to call: name Zacchaeus and it/s/he to be chief tax collector and (it/s/he *N+kO) (to be *k) rich
Kulikuwa na mtu mmoja mjini, jina lake Zakayo ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3 and to seek to perceive: see the/this/who Jesus which? to be and no be able away from the/this/who crowd that/since: since the/this/who age/height small to be
Alitaka kuona Yesu alikuwa nani, lakini kwa sababu ya umati wa watu, na kwa vile alikuwa mfupi, hakufaulu.
4 and to outrun (toward the/this/who *no) before to ascend upon/to/against sycamore tree in order that/to to perceive: see it/s/he that/since: since (through/because of *k) that to ensue to pass through
Hivyo, alitangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona Yesu, kwa maana alikuwa apitie hapo.
5 and as/when to come/go upon/to/against the/this/who place to look up/again the/this/who Jesus (to perceive: see it/s/he and *K) to say to/with it/s/he Zacchaeus to hasten to come/go down today for in/on/among the/this/who house: home you be necessary me to stay
Basi, Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.”
6 and to hasten to come/go down and to receive it/s/he to rejoice
Zakayo akashuka haraka, akamkaribisha kwa furaha.
7 and to perceive: see (all *N+kO) to murmur to say that/since: that from/with/beside sinful man to enter to destroy/lodge
Watu wote walipoona hayo, wakaanza kunung'unika wakisema, “Amekwenda kukaa kwa mtu mwenye dhambi.”
8 to stand then Zacchaeus to say to/with the/this/who lord: God look! the/this/who half me the/this/who be already lord: God the/this/who poor to give and if one one to extort to pay fourfold
Lakini Zakayo akasimama akamwambia Yesu, “Sikiliza Bwana! Mimi nitawapa maskini nusu ya mali yangu, na kama nimenyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne.”
9 to say then to/with it/s/he the/this/who Jesus that/since: that today salvation the/this/who house: home this/he/she/it to be as/just as and it/s/he son Abraham to be
Yesu akamwambia, “Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa vile huyu pia ni wa ukoo wa Abrahamu.
10 to come/go for the/this/who son the/this/who a human to seek and to save the/this/who to destroy
Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa waliopotea.”
11 to hear then it/s/he this/he/she/it to add (to) to say parable through/because of the/this/who near to exist Jerusalem it/s/he and to think it/s/he that/since: that instantly to ensue the/this/who kingdom the/this/who God to appear
Wakati watu walipokuwa bado wanasikiliza hayo, Yesu akawaambia mfano. (Hapo alikuwa anakaribia Yerusalemu, na watu wale walidhani kwamba muda si muda, Ufalme wa Mungu ungefika.)
12 to say therefore/then a human one of noble birth to travel toward country long/distant to take themself kingdom and to return
Hivyo akawaambia, “Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa kifalme aliyefanya safari kwenda nchi ya mbali ili apokee madaraka ya ufalme, halafu arudi.
13 to call: call then ten slave themself to give it/s/he ten mina and to say to/with it/s/he (to trade *NK+o) (in/on/among which *NO) (until *k) to come/go
Basi, kabla ya kuondoka aliwaita watumishi wake kumi, akawapa kiasi cha fedha kila mmoja na kumwambia: Fanyeni nazo biashara mpaka nitakaporudi.
14 the/this/who then citizen it/s/he to hate it/s/he and to send delegation after it/s/he to say no to will/desire this/he/she/it to reign upon/to/against me
Lakini wananchi wenzake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende wakaseme: Hatumtaki huyu atutawale.
15 and to be in/on/among the/this/who to return it/s/he to take the/this/who kingdom and to say to call it/s/he the/this/who slave this/he/she/it which (to give *N+kO) the/this/who money in order that/to to know (which? *k) which? (to gain in trade *N+kO)
“Huyo mtu mashuhuri alirudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, na mara akaamuru wale watumishi aliowapa zile fedha waitwe ili aweze kujua kila mmoja amepata faida gani.
16 to come then the/this/who first to say lord: master the/this/who mina you ten (to earn more *N+kO) mina
Mtumishi wa kwanza akatokea, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara kumi ya zile fedha ulizonipa.
17 and to say it/s/he (well done *N+kO) good slave that/since: since in/on/among least faithful to be to be authority to have/be above ten city
Naye akamwambia: Vema; wewe ni mtumishi mwema. Kwa kuwa umekuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi!
18 and to come/go the/this/who secondly to say the/this/who mina you lord: master to do/make: do five mina
Mtumishi wa pili akaja, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara tano ya zile fedha ulizonipa.
19 to say then and this/he/she/it and you above to be five city
Naye akamwambia pia: Nawe utakuwa na madaraka juu ya miji mitano.
20 and (the/this/who *no) other to come/go to say lord: master look! the/this/who mina you which to have/be to lay up in/on/among handkerchief
“Mtumishi mwingine akaja, akasema: Chukua fedha yako; niliificha salama katika kitambaa,
21 to fear for you that/since: since a human severe to be to take up which no to place and to reap which no to sow
kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Wewe ni mtu ambaye huchukua yasiyo yako, na huchuma ambacho hukupanda.
22 to say (then *k) it/s/he out from the/this/who mouth you to judge you evil/bad slave to perceive: know that/since: that I/we a human severe to be to take up which no to place and to reap which no to sow
Naye akamwambia: Nakuhukumu kutokana na msemo wako, ewe mtumishi mbaya! Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, ambaye huchukua yasiyo yangu na kuchuma nisichopanda.
23 and through/because of which? no to give me the/this/who money upon/to/against (the/this/who *k) table I/we and to come/go with interest if it/s/he to do/require
Kwa nini basi, hukuiweka fedha yangu benki, nami ningeichukua pamoja na faida baada ya kurudi kwangu?
24 and the/this/who to stand by to say to take up away from it/s/he the/this/who mina and to give the/this/who the/this/who ten mina to have/be
Hapo akawaambia wale waliokuwa pale: Mnyang'anyeni hizo fedha, mkampe yule aliyepata faida mara kumi.
25 and to say it/s/he lord: master to have/be ten mina
Nao wakamwambia: Lakini Mheshimiwa, huyo ana faida ya kiasi hicho mara kumi!
26 to say (for *ko) you that/since: that all the/this/who to have/be to give away from then the/this/who not to have/be and which to have/be to take up (away from it/s/he *ko)
Naye akawajibu: Kila aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27 but/however the/this/who enemy me (this/he/she/it *N+kO) the/this/who not to will/desire me to reign upon/to/against it/s/he to bring here and to slaughter it/s/he before me
Na sasa, kuhusu hao maadui wangu ambao hawapendi niwe mfalme wao, waleteni hapa, mkawaue papa hapa mbele yangu.”
28 and to say this/he/she/it to travel before to ascend toward Jerusalem
Yesu alisema hayo, kisha akatangulia mbele yao kuelekea Yerusalemu.
29 and to be as/when to come near toward Bethphage and Bethany to/with the/this/who mountain the/this/who to call: call Olivet to send two the/this/who disciple (it/s/he *ko)
Alipokaribia kufika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30 (to say *N+kO) to go toward the/this/who before village in/on/among which to enter to find/meet colt to bind upon/to/against which none ever a human to seat (and *no) to loose it/s/he to bring
akawaambia: “Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana punda amefungwa ambaye hajatumiwa na mtu. Mfungeni, mkamlete hapa.
31 and if one you to ask through/because of which? to loose thus(-ly) to say (it/s/he *k) that/since: since the/this/who lord: God it/s/he need to have/be
Kama mtu akiwauliza, kwa nini mnamfungua, mwambieni, Bwana ana haja naye.”
32 to go away then the/this/who to send to find/meet as/just as to say it/s/he
Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.
33 to loose then it/s/he the/this/who colt to say the/this/who lord: master it/s/he to/with it/s/he which? to loose the/this/who colt
Walipokuwa wanamfungua yule mwana punda, wenyewe wakawauliza, “Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?”
34 the/this/who then to say (that/since: that *no) the/this/who lord: God it/s/he need to have/be
Nao wakawajibu, “Bwana anamhitaji.”
35 and to bring it/s/he to/with the/this/who Jesus and to throw on (it/s/he *N+kO) the/this/who clothing upon/to/against the/this/who colt to mount the/this/who Jesus
Basi, wakampelekea Yesu yule mwana punda. Kisha wakatandika mavazi yao juu yake wakampandisha Yesu.
36 to travel then it/s/he to spread the/this/who clothing (it/s/he *NK+o) in/on/among the/this/who road
Yesu akaendelea na safari, na watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37 to come near then it/s/he already to/with the/this/who descent the/this/who mountain the/this/who Olivet be first all the/this/who multitude the/this/who disciple to rejoice to praise the/this/who God voice/sound: voice great about (all *NK+o) which to perceive: see power
Alipofika karibu na Yerusalemu, katika mteremko wa mlima wa Mizeituni, umati wote na wanafunzi wake, wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona;
38 to say to praise/bless the/this/who to come/go the/this/who king in/on/among name lord: God in/on/among heaven peace and glory in/on/among Highest
wakawa wanasema: “Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!”
39 and one the/this/who Pharisee away from the/this/who crowd to say to/with it/s/he teacher to rebuke the/this/who disciple you
Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu, wakamwambia Yesu, “Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!”
40 and to answer to say (it/s/he *ko) to say you (that/since: that *ko) if this/he/she/it (be quiet *N+kO) the/this/who stone (to cry *N+kO)
Yesu akawajibu, “Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, hakika hayo mawe yatapaza sauti.”
41 and as/when to come near to perceive: see the/this/who city to weep upon/to/against (it/s/he *N+kO)
Alipokaribia zaidi na kuuona ule mji, Yesu aliulilia
42 to say that/since: that if: if only to know (and indeed *k) in/on/among the/this/who day (you *k) this/he/she/it and you the/this/who to/with peace (you *ko) now then to hide away from eye you
akisema: “Laiti ungelijua leo hii yale yaletayo amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43 that/since: since to come/be present day upon/to/against you and (to encamp *N+kO) the/this/who enemy you barricade you and to surround you and to hold/oppress you from all sides
Maana siku zaja ambapo adui zako watakuzungushia maboma, watakuzingira na kukusonga pande zote.
44 and to raze you and the/this/who child you in/on/among you and no to release: leave stone upon/to/against (stone *N+kO) in/on/among you for which no to know the/this/who time/right time the/this/who oversight you
Watakupondaponda wewe pamoja na watoto wako ndani ya kuta zako; hawatakuachia hata jiwe moja juu jingine, kwa sababu hukuutambua wakati Mungu alipokujia kukuokoa.”
45 and to enter toward the/this/who temple be first to expel the/this/who to sell (in/on/among it/s/he *k) (and to buy *K)
Kisha, Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuzia nje wafanyabiashara
46 to say it/s/he to write (and *no) (to be *N+kO) the/this/who house: home me house: home prayer you then it/s/he to do/make: do cave robber/rebel
akisema, “Imeandikwa: Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi.”
47 and to be to teach the/this/who according to day in/on/among the/this/who temple the/this/who then high-priest and the/this/who scribe to seek it/s/he to destroy and the/this/who first: best the/this/who a people
Yesu akawa anafundisha kila siku Hekaluni. Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumwangamiza,
48 and no to find/meet the/this/who which? to do/make: do the/this/who a people for all to hang upon it/s/he to hear
lakini hawakuwa na la kufanya, maana watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini kabisa.

< Luke 19 >