< Genesis 28 >

1 and to call: call to Isaac to(wards) Jacob and to bless [obj] him and to command him and to say to/for him not to take: marry woman: wife from daughter Canaan
Basi Isaki akamwita Yakobo, akambariki na akamwamuru, akisema, “Usioe mwanamke wa Kikanaani.
2 to arise: rise to go: went Paddan [to] (Paddan)-aram house: household [to] Bethuel father mother your and to take: take to/for you from there woman: wife from daughter Laban brother: male-sibling mother your
Nenda mara moja mpaka Padan-Aramu, kwenye nyumba ya Bethueli baba wa mama yako. Uchukue mke kati ya binti za Labani ambaye ni ndugu wa mama yako.
3 and God Almighty to bless [obj] you and be fruitful you and to multiply you and to be to/for assembly people
Mungu Mwenyezi na akubariki uwe na uzao uongezeke idadi yako upate kuwa jamii kubwa ya watu.
4 and to give: give to/for you [obj] blessing Abraham to/for you and to/for seed: children your with you to/for to possess: take you [obj] land: country/planet sojourning your which to give: give God to/for Abraham
Na akupe wewe na uzao wako baraka aliyopewa Abrahamu, upate kumiliki nchi unayoishi sasa kama mgeni, nchi ambayo Mungu alimpa Abrahamu.”
5 and to send: depart Isaac [obj] Jacob and to go: went Paddan [to] (Paddan)-aram to(wards) Laban son: child Bethuel [the] Aramean brother: male-sibling Rebekah mother Jacob and Esau
Kisha Isaki akamuaga Yakobo, naye akaenda Padan-Aramu, kwa Labani mwana wa Bethueli Mwaramu, ndugu wa Rebeka, aliyekuwa mama wa Yakobo na Esau.
6 and to see: see Esau for to bless Isaac [obj] Jacob and to send: depart [obj] him Paddan [to] (Paddan)-aram to/for to take: marry to/for him from there woman: wife in/on/with to bless he [obj] him and to command upon him to/for to say not to take: marry woman: wife from daughter Canaan
Sasa Esau akajua kuwa Isaki amembariki Yakobo na kumtuma kwenda Padan-Aramu ili achukue mke huko na kwamba alipombariki alimwamuru akisema, “Usioe mke katika binti za Wakanaani,”
7 and to hear: obey Jacob to(wards) father his and to(wards) mother his and to go: went Paddan [to] (Paddan)-aram
tena kwamba Yakobo amewatii baba yake na mama yake naye amekwenda Padan-Aramu.
8 and to see: see Esau for bad: evil daughter Canaan in/on/with eye: appearance Isaac father his
Esau akatambua jinsi ambavyo baba yake Isaki anavyowachukia binti za Wakanaani.
9 and to go: went Esau to(wards) Ishmael and to take: marry [obj] Mahalath daughter Ishmael son: child Abraham sister Nebaioth upon woman: wife his to/for him to/for woman: wife
Ndipo Esau akaenda kwa Ishmaeli, akamwoa Mahalati, ndugu wa Nebayothi na binti wa Ishmaeli mwana wa Abrahamu, kuongezea wale wake wengine aliokuwa nao.
10 and to come out: extends Jacob from Beersheba Beersheba and to go: went Haran [to]
Yakobo akatoka Beer-Sheba kwenda Harani.
11 and to fall on in/on/with place and to lodge there for to come (in): (sun)set [the] sun and to take: take from stone [the] place and to set: put head his and to lie down: sleep in/on/with place [the] he/she/it
Alipofika mahali fulani, akalala hapo kwa sababu jua lilikuwa limetua. Akachukua jiwe moja la mahali pale, akaliweka chini ya kichwa chake akajinyoosha akalala usingizi.
12 and to dream and behold ladder to stand land: country/planet [to] and head: top his to touch [the] heaven [to] and behold messenger: angel God to ascend: rise and to go down in/on/with him
Akaota ndoto ambayo aliona ngazi imesimamishwa juu ya ardhi, ncha yake ikiwa imefika mbinguni na malaika wa Mungu wakawa wakipanda na kushuka juu yake.
13 and behold LORD to stand upon him and to say I LORD God Abraham father your and God Isaac [the] land: country/planet which you(m. s.) to lie down: lay down upon her to/for you to give: give her and to/for seed: children your
Juu yake alisimama Bwana, akasema, “Mimi ni Bwana, Mungu wa baba yako Abrahamu na Mungu wa Isaki. Nchi ambayo umelala juu yake, nitakupa wewe na uzao wako.
14 and to be seed: children your like/as dust [the] land: soil and to break through sea: west [to] and east [to] and north [to] and south [to] and to bless in/on/with you all family [the] land: soil and in/on/with seed: children your
Uzao wako utakuwa kama mavumbi ya nchi, nawe utaenea upande wa magharibi na mashariki, kaskazini na kusini. Kupitia wewe na uzao wako mataifa yote ya duniani yatabarikiwa.
15 and behold I with you and to keep: guard you in/on/with all which to go: went and to return: return you to(wards) [the] land: soil [the] this for not to leave: forsake you till which if: until to make: do [obj] which to speak: promise to/for you
Niko pamoja nawe nami nitakulinda kila uendako na nitakurudisha katika nchi hii. Sitakuacha mpaka nitakapofanya hayo niliyokuahidi.”
16 and to awake Jacob from sleep his and to say surely there LORD in/on/with place [the] this and I not to know
Yakobo alipoamka kutoka usingizini, akawaza, “Hakika Bwana yuko mahali hapa, wala mimi sikujua.”
17 and to fear: revere and to say what? to fear: revere [the] place [the] this nothing this that if: except if: except house: home God and this gate [the] heaven
Kwa hiyo akaogopa, akasema, “Mahali hapa panatisha kama nini! Bila shaka hapa ndipo nyumba ya Mungu ilipo, hili ni lango la mbinguni.”
18 and to rise Jacob in/on/with morning and to take: take [obj] [the] stone which to set: put head his and to set: make [obj] her pillar and to pour: pour oil upon head: top her
Asubuhi yake na mapema, Yakobo akalichukua lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha kama nguzo na kumimina mafuta juu yake.
19 and to call: call by [obj] name [the] place [the] he/she/it Bethel Bethel and but Luz name [the] city to/for first
Mahali pale akapaita Betheli, ingawa mji ule hapo kwanza uliitwa Luzu.
20 and to vow Jacob vow to/for to say if to be God with me me and to keep: guard me in/on/with way: journey [the] this which I to go: went and to give: give to/for me food: bread to/for to eat and garment to/for to clothe
Kisha Yakobo akaweka nadhiri, akisema, “Kama Mungu akiwa pamoja nami na kunilinda katika safari niendayo, akinipa chakula nile na nguo nivae
21 and to return: return in/on/with peace to(wards) house: home father my and to be LORD to/for me to/for God
na nirudi salama nyumbani kwa baba yangu, hapo ndipo Bwana atakuwa Mungu wangu,
22 and [the] stone [the] this which to set: make pillar to be house: home God and all which to give: give to/for me to tithe to tithe him to/for you
nalo jiwe hili nililolisimamisha kama nguzo litakuwa nyumba ya Mungu na katika yote utakayonipa nitakutolea wewe sehemu ya kumi.”

< Genesis 28 >