< Exodus 1 >

1 and these name son: child Israel [the] to come (in): come Egypt [to] with Jacob man: anyone and house: household his to come (in): come
Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli waliokuja Misri pamoja na Yakobo kila moja na familia yake:
2 Reuben Simeon Levi and Judah
Rubeni, Simioni, Lawi, na Yuda,
3 Issachar Zebulun and Benjamin
Isakari, Zebuluni, na Benjamini,
4 Dan and Naphtali Gad and Asher
Dani, Naftali, Gadi, na Asheri.
5 and to be all soul: person to come out: produce thigh Jacob seventy soul: person and Joseph to be in/on/with Egypt
Jumla ya watu wa ukoo wa Yakobo walikuwa sabini. Yusufu alikuwa Misri tayari.
6 and to die Joseph and all brother: male-sibling his and all [the] generation [the] he/she/it
Ndipo Yusufu, pamoja na kaka zake wote, na kizazi chote wakafa.
7 and son: descendant/people Israel be fruitful and to swarm and to multiply and be vast in/on/with much much and to fill [the] land: country/planet with them
Waisraeli walifanikiwa sana, wakaongezeka sana idadi yao, na wakawa na nguvu maana nchi ilijazwa na wao.
8 and to arise: rise king new upon Egypt which not to know [obj] Joseph
Wakati huu sasa mfalme mpya asiyemjua Yusufu aliinuka katika Misri.
9 and to say to(wards) people his behold people son: descendant/people Israel many and mighty from us
Akawaambia watu wake, “Tazama, hawa Waisraeli ni wengi na wenye nguvu kuliko sisi.
10 to give [emph?] be wise to/for him lest to multiply and to be for to encounter: chanced battle and to add also he/she/it upon to hate us and to fight in/on/with us and to ascend: rise from [the] land: country/planet
Njooni na tukae nao kwa akili, ama sivyo wataendelea kuongezeka na kama vita ikiibuka, wataungana na adui zetu, watapigana nasi, na kisha wataondoka.”
11 and to set: appoint upon him ruler taskworker because to afflict him in/on/with burden their and to build city storage to/for Pharaoh [obj] Pithom and [obj] Raamses
Hivyo wakawekea walinzi ambao waliwatesa kwa kuwatumikisha kazi ngumu. Waisraeli walijenga maghala ya miji kwa ajili ya Farao: Pishoni na Ramsei.
12 and like/as as which to afflict [obj] him so to multiply and so to break through and to loathe from face: because son: descendant/people Israel
Lakini kadiri Wamisri walivyowatesa, ndivyo Waisraeli waliendelea kuongezeka na kusambaa. Hivyo Wamisri wakaanza kuwaogopa Waisraeli.
13 and to serve Egyptian [obj] son: descendant/people Israel in/on/with severity
Wamisri waliwafanya Waisraeli wafanye kazi kwa nguvu nyingi.
14 and to provoke [obj] life their in/on/with service severe in/on/with clay and in/on/with brick and in/on/with all service: work in/on/with land: country [obj] all service: work their which to serve in/on/with them in/on/with severity
Waliyafanya maisha yao kuwa machungu kwa kuwafanyisha kazi ngumu kwa vinu na matofali na kwa kila aina ya kazi za shambani. Kazi zao zote zilikuwa ngumu.
15 and to say king Egypt to/for to beget [the] Hebrew which name [the] one Shiphrah and name [the] second Puah
Kisha mfalme wa Misri akawaambia wakunga wa Kiebrania; mmoja wao aliitwa jina lake Shifra, na mwingine aliitwa Puha.
16 and to say in/on/with to beget you [obj] [the] Hebrew and to see: see upon [the] wheel if son: child he/she/it and to die [obj] him and if daughter he/she/it and to live
Akasema, “Wakati mnapowasaidia wanawake wa Kiebrania wanapojifungua, chunguzeni wanapozaa. Ikiwa ni mtoto wa kiume, basi muueni; bali ikiwa ni mtoto wa kike, basi mwacheni aishi.”
17 and to fear: revere [the] to beget [obj] [the] God and not to make: do like/as as which to speak: speak to(wards) them king Egypt and to live [obj] [the] youth
Lakini wale Wakunga walimwogopa Mungu na hawakufanya kama mfalme wa Misri alivyowaagiza; badala yake waliwaacha watoto wa kiume waishi.
18 and to call: call to king Egypt to/for to beget and to say to/for them why? to make: do [the] word: thing [the] this and to live [obj] [the] youth
Mfalme wa Misri akawaita Wakunga na kuwaambia, “Kwanini mmefanya haya, na kuwaacha watoto wa kiume wakaishi?”
19 and to say [the] to beget to(wards) Pharaoh for not like/as woman [the] Egyptian [the] Hebrew for vigorous they(fem.) in/on/with before to come (in): come to(wards) them [the] to beget and to beget
Wale Wakunga wakamjibu Farao, “Hawa wanawake wa Kiebrania siyo kama wanawake wa Kimisri. Hawa wana nguvu na jasiri sana maana wao humaliza kuzaa kabla hata mkunga hajafika.”
20 and be good God to/for to beget and to multiply [the] people and be vast much
Mungu aliwalinda hawa Wakunga. Watu waliongezeka kwa idadi na kuwa na nguvu sana.
21 and to be for to fear: revere [the] to beget [obj] [the] God and to make: offer to/for them house: household
Kwa sababu wale Wakunga walimwogopa Mungu, aliwapa familia.
22 and to command Pharaoh to/for all people his to/for to say all [the] son: child [the] born [the] Nile [to] to throw him and all [the] daughter to live [emph?]
Farao akawaagiza watu wote, “Lazima mmutupe kila mtoto wa kiume anayezaliwa katika mto, lakini kila mtoto wa kike wamwache aishi.”

< Exodus 1 >