< Deuteronomy 18 >

1 not to be to/for priest [the] Levi all tribe Levi portion and inheritance with Israel food offering LORD and inheritance his to eat [emph?]
Makuhani ambao ni Walawi, yaani kabila lote la Lawi, hawatakuwa na mgawo wala urithi pamoja na Israeli. Wataishi kwa sadaka zitolewazo kwa ajili ya Bwana za kuteketezwa kwa moto, kwa maana huo ndio urithi wao.
2 and inheritance not to be to/for him in/on/with entrails: among brother: compatriot his LORD he/she/it inheritance his like/as as which to speak: promise to/for him
Hawatakuwa na urithi miongoni mwa ndugu zao; Bwana ndiye urithi wao, kama alivyowaahidi.
3 and this to be justice: custom [the] priest from with [the] people from with to sacrifice [the] sacrifice if cattle if sheep and to give: give to/for priest [the] arm and [the] jaw and [the] stomach
Hili ndilo fungu la makuhani kutoka kwa watu watakaotoa dhabihu ya fahali au kondoo: mguu wa mbele, mataya na matumbo.
4 first: beginning grain your new wine your and oil your and first: beginning fleece flock your to give: give to/for him
Mtawapa malimbuko ya nafaka zenu, divai mpya, mafuta na sufu ya kwanza kutoka manyoya ya kondoo zenu,
5 for in/on/with him to choose LORD God your from all tribe your to/for to stand: stand to/for to minister in/on/with name LORD he/she/it and son: descendant/people his all [the] day
kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewachagua pamoja na wazao wao kutoka makabila yenu kusimama na kuhudumu katika jina la Bwana siku zote.
6 and for to come (in): come [the] Levi from one gate: town your from all Israel which he/she/it to sojourn there and to come (in): come in/on/with all desire soul: appetite his to(wards) [the] place which to choose LORD
Ikiwa Mlawi atahama kutoka mmojawapo ya miji yenu popote katika Israeli ambapo anaishi, akaja kwa moyo wote mahali ambapo Bwana atapachagua,
7 and to minister in/on/with name LORD God his like/as all brother: compatriot his [the] Levi [the] to stand: stand there to/for face: before LORD
anaweza akahudumu katika jina la Bwana Mungu wake kama Walawi wenzake wote wanaohudumu hapo mbele za Bwana.
8 portion like/as portion to eat to/for alone: besides sale his upon [the] father
Atashiriki sawa katika mafao yao, hata kama amepokea fedha kutoka mauzo ya mali ya jamaa yake.
9 for you(m. s.) to come (in): come to(wards) [the] land: country/planet which LORD God your to give: give to/for you not to learn: learn to/for to make: do like/as abomination [the] nation [the] they(masc.)
Wakati mtakapoingia katika nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, msijifunze kuiga njia za machukizo za mataifa ya huko.
10 not to find in/on/with you to pass son: child his and daughter his in/on/with fire to divine divination to divine and to divine and to practice sorcery
Asionekane mtu yeyote miongoni mwenu ampitishaye mwanawe au binti yake katika moto, atakayefanya uaguzi, ulozi, anayetabiri nyakati, anayejishughulisha na uchawi,
11 and to unite spell and to ask medium and spiritist and to seek to(wards) [the] to die
wala arogaye kwa kupiga mafundo, wala mwaguzi au anayeabudu mizimu, wala awaombaye wafu.
12 for abomination LORD all to make: do these and in/on/with because of [the] abomination [the] these LORD God your to possess: take [obj] them from face: before your
Mtu yeyote afanyaye mambo haya ni chukizo kwa Bwana, tena ni kwa sababu ya matendo haya ya kuchukiza wayafanyayo ndiyo maana Bwana Mungu wenu atayafukuza mataifa hayo mbele yenu.
13 unblemished: blameless to be with LORD God your
Kamwe msilaumiwe mbele za Bwana Mungu wenu.
14 for [the] nation [the] these which you(m. s.) to possess: take [obj] them to(wards) to divine and to(wards) to divine to hear: hear and you(m. s.) not so to give: allow to/for you LORD God your
Mataifa mtakayowafukuza husikiliza wale wafanyao ulozi na uaguzi. Lakini kwenu ninyi, Bwana Mungu wenu hajawaruhusu kufanya hivyo.
15 prophet from entrails: among your from brother: compatriot your like me to arise: establish to/for you LORD God your to(wards) him to hear: hear [emph?]
Bwana Mungu wenu atawainulia nabii kama mimi kutoka miongoni mwa ndugu zenu wenyewe. Msikilizeni yeye.
16 like/as all which to ask from from with LORD God your in/on/with Horeb in/on/with day [the] assembly to/for to say not to add: again to/for to hear: hear [obj] voice LORD God my and [obj] [the] fire [the] great: large [the] this not to see: see still and not to die
Kwa kuwa hivi ndivyo mlivyomwomba Bwana Mungu wenu kule Horebu siku ile ya kusanyiko, wakati mliposema, “Na tusiisikie sauti ya Bwana Mungu wetu, wala kuuona moto huu mkubwa tena, ama sivyo tutakufa.”
17 and to say LORD to(wards) me be good which to speak: speak
Bwana akaniambia: “Wanachosema ni vyema.
18 prophet to arise: establish to/for them from entrails: among brother: compatriot their like you and to give: put word my in/on/with lip his and to speak: speak to(wards) them [obj] all which to command him
Nitawainulia nabii kama wewe kutoka miongoni mwa ndugu zao; nitaweka maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia kila kitu nitakachomwamuru.
19 and to be [the] man which not to hear: hear to(wards) word my which to speak: speak in/on/with name my I to seek from from with him
Kama mtu yeyote hatasikiliza maneno yangu ambayo huyo nabii atayasema kwa Jina langu, mimi mwenyewe nitamwajibisha.
20 surely [the] prophet which to boil to/for to speak: speak word in/on/with name my [obj] which not to command him to/for to speak: speak and which to speak: speak in/on/with name God another and to die [the] prophet [the] he/she/it
Lakini nabii ambaye atathubutu kusema kwa Jina langu kitu chochote ambacho sikumwamuru akiseme, au nabii ambaye husema kwa jina la miungu mingine ni lazima auawe.”
21 and for to say in/on/with heart your how? to know [obj] [the] word which not to speak: speak him LORD
Mnaweza kuulizana wenyewe, “Tutawezaje kujua wakati ujumbe haukusemwa na Bwana?”
22 which to speak: speak [the] prophet in/on/with name LORD and not to be [the] word and not to come (in): come he/she/it [the] word which not to speak: speak him LORD in/on/with arrogance to speak: speak him [the] prophet not to dread from him
Ikiwa kile nabii anachotangaza kwa jina la Bwana hakikutokea au kutimia, huo ni ujumbe ambao Bwana hakusema. Nabii huyo amesema kwa ujuaji. Msimwogope huyo.

< Deuteronomy 18 >