< 1 Corinthians 1 >

1 Paul called apostle Christ Jesus through/because of will/desire God and Sosthenes the/this/who brother
Paulo, aliyeitwa na Kristo Yesu kuwa mtume kwa mapenzi ya Mungu, na Sosthene ndugu yetu,
2 the/this/who assembly the/this/who God the/this/who to be in/on/among Corinth to sanctify in/on/among Christ Jesus called holy: saint with all the/this/who to call (on)/name the/this/who name the/this/who lord: God me Jesus Christ in/on/among all place it/s/he (and/both *k) and me
kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, kwa wale ambao wamewekwa wakfu katika Yesu Kristo, ambao wameitwa kuwa watu watakatifu. Tunawaandikia pia wale wote wanaoliitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo katika mahali pote, Bwana wao na wetu.
3 grace you and peace away from God father me and lord: God Jesus Christ
Neema na amani iwe kwenu kutoka kwa Mungu baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
4 to thank the/this/who God me always about you upon/to/against the/this/who grace the/this/who God the/this/who to give you in/on/among Christ Jesus
Siku zote namshukru Mungu wangu kwa ajili yenu, kwa sababu ya neema ya Mungu ambayo Kristo Yesu aliwapa.
5 that/since: since in/on/among all to enrich in/on/among it/s/he in/on/among all word and all knowledge
Amewafanya kuwa matajiri katika kila njia, katika usemi na pamoja maarifa yote.
6 as/just as the/this/who testimony the/this/who Christ to confirm in/on/among you
Amewafanya matajiri, kama ushuhuda kuhusu Kristo ya kwamba amethibitishwa kuwa kweli miongoni mwenu.
7 so you not to lack in/on/among nothing gift to expect the/this/who revelation the/this/who lord: God me Jesus Christ
Kwa hiyo hampungukiwi karama za kiroho, kama mlivyo na hamu ya kusubiri ufunuo wa Bwana wetu Yesu Kristo.
8 which and to confirm you until goal/tax irreproachable in/on/among the/this/who day the/this/who lord: God me Jesus Christ
Atawaimarisha ninyi pia hadi mwisho, ili msilaumiwe siku ya Bwana wetu Yesu Kristo.
9 faithful the/this/who God through/because of which to call: call toward participation the/this/who son it/s/he Jesus Christ the/this/who lord: God me
Mungu ni mwaminifu ambaye aliwaita ninyi katika ushirika wa mwana wake, Yesu Kristo Bwana wetu.
10 to plead/comfort then you brother through/because of the/this/who name the/this/who lord: God me Jesus Christ in order that/to the/this/who it/s/he to say all and not to be in/on/among you split to be then to complete in/on/among the/this/who it/s/he mind and in/on/among the/this/who it/s/he resolution
Sasa nawasihi kaka na dada zangu, kupitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba wote mkubali, na kwamba kusiwe na migawanyiko miongoni mwenu. Nawasihi kwamba muungane pamoja katika nia moja na katika kusudi moja.
11 to make clear for me about you brother me by/under: by the/this/who Chloe that/since: that quarrel in/on/among you to be
Kwani watu wa nyumba ya Kloe wamenitaarifu kuwa kuna mgawanyiko unaoendelea miongoni mwenu.
12 to say then this/he/she/it that/since: that each you to say I/we on the other hand to be Paul I/we then Apollos I/we then Cephas I/we then Christ
Nina maana hii: Kila mmoja wenu husema, “Mimi ni wa Paulo,” au “Mimi ni wa Apolo”, au “Mimi ni wa Kefa” au “Mimi ni wa Kristo”.
13 to divide the/this/who Christ not Paul to crucify above/for you or toward the/this/who name Paul to baptize
Je! Kristo amegawanyika? Je! Paulo alisulubiwa kwa ajili yenu? Je! Mlibatizwa kwa jina la Paulo?
14 to thank the/this/who God that/since: that none you to baptize if: not not Crispus and Gaius
Namshukuru Mungu kuwa sikumbatiza yeyote, isipokuwa Krispo na Gayo.
15 in order that/to not one to say that/since: that toward the/this/who I/we name (to baptize *N+KO)
Hii ilikuwa kwamba hakuna yeyote angesema mlibatizwa kwa jina langu.
16 to baptize then and the/this/who Stephanas house: household henceforth no to know if one another to baptize
(Pia niliwabatiza wa nyumba ya Stephania. Zaidi ya hapo, sijui kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote).
17 no for to send me Christ to baptize but to speak good news no in/on/among wisdom word in order that/to not to empty the/this/who cross the/this/who Christ
Kwa kuwa, Kristo hakunituma kubatiza bali kuhubiri injili. Hakunituma kuhubiri kwa maneno ya hekima ya kibinadamu, ili kwamba nguvu ya msalaba wa Kristo isiondolewe.
18 the/this/who word for the/this/who the/this/who cross the/this/who on the other hand to destroy foolishness to be the/this/who then to save me power God to be
Kwa kuwa ujumbe wa msalaba ni upuuzi kwa wale wanaokufa. Lakini kwa wale ambao Mungu anawaokoa, ni nguvu ya Mungu.
19 to write for to destroy the/this/who wisdom the/this/who wise and the/this/who understanding the/this/who intelligent to reject
Kwa kuwa imeandikwa, “Nitaiharibu hekima ya wenye busara. Nitauharibu ufahamu wa wenye akili.”
20 where? wise where? scribe where? debater the/this/who an age: age this/he/she/it not! be foolish the/this/who God the/this/who wisdom the/this/who world (this/he/she/it *k) (aiōn g165)
Yuko wapi mtu mwenye busara? Yuko wapi mwenye elimu? Yuko wapi msemaji mshawishi wa dunia hii? Je, Mungu hakuigeuza hekima ya dunia hii kuwa ujinga? (aiōn g165)
21 since for in/on/among the/this/who wisdom the/this/who God no to know the/this/who world through/because of the/this/who wisdom the/this/who God to delight the/this/who God through/because of the/this/who foolishness the/this/who preaching to save the/this/who to trust (in)
Tangu dunia imekuwa katika hekima yake haikumjua Mungu, ilimpendeza Mungu katika ujinga wao wa kuhubiri ili kuokoa wale wanaoamini.
22 since and Jew (sign *N+KO) to ask and Greek, Gentile wisdom to seek
Kwa Wayahudi huuliza ishara za miujiza na kwa Wayunani hutafuta hekima.
23 me then to preach Christ to crucify Jew on the other hand stumbling block (Gentiles *N+KO) then foolishness
Lakini tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa, aliye kikwazo kwa Wayahudi na ni ujinga kwa Wayunani.
24 it/s/he then the/this/who called Jew and/both and Greek, Gentile Christ God power and God wisdom
Lakini kwa wale ambao waliitwa na Mungu, Wayahudi na Wayunani, tunamhubiri Kristo kama nguvu na hekima ya Mungu.
25 that/since: since the/this/who foolish the/this/who God wise the/this/who a human to be and the/this/who weak the/this/who God strong the/this/who a human (to be *k)
Kwa kuwa ujinga wa Mungu una hekima kuliko ya wanadamu, na udhaifu wa Mungu una nguvu zaidi ya wanadamu.
26 to see for the/this/who calling you brother that/since: that no much wise according to flesh no much able no much of noble birth
Angalia wito wa Mungu juu yenu, kaka na dada zangu. Si wengi wenu mlikuwa na hekima katika viwango vya kibinadamu. Si wengi wenu mlikuwa na nguvu. Si wengi wenu mlizaliwa katika ukuu.
27 but the/this/who foolish the/this/who world to select the/this/who God in order that/to to dishonor the/this/who wise and the/this/who weak the/this/who world to select the/this/who God in order that/to to dishonor the/this/who strong
Lakini Mungu alichagua vitu vijinga vya dunia ili kuviaibisha vyenye hekima. Mungu alichagua kilicho dhaifu katika dunia kukiaibisha chenye nguvu.
28 and the/this/who lowly the/this/who world and the/this/who to reject to select the/this/who God (and *ko) the/this/who not to be in order that/to the/this/who to be to abate
Mungu alichagua kile kilicho cha hali ya chini na kilichodharauliwa katika dunia. Alichagua hata vitu ambavyo havikuhesabiwa kuwa kitu, kwa kuvifanya si kitu vitu vilivyo na thamani.
29 that not to boast all flesh before the/this/who (God *N+KO)
Alifanya hivi ili asiwepo yeyote aliye na sababu ya kujivuna mbele zake.
30 out from it/s/he then you to be in/on/among Christ Jesus which to be wisdom me away from God righteousness and/both and holiness and redemption
Kwa sababu ya kile Mungu alichofanya, sasa mko ndani ya Kristo Yesu, ambaye amefanyika hekima kwa ajili yetu kutoka kwa Mungu. Alikuwa haki yetu, utakatifu na ukombozi.
31 in order that/to as/just as to write the/this/who to boast in/on/among lord: God to boast
Kama matokeo, kama andiko lisemavyo, “Anayejisifu, ajisifu katika Bwana.”

< 1 Corinthians 1 >