< 1 Corinthians 1 >

1 Paul called apostle Christ Jesus through/because of will/desire God and Sosthenes the/this/who brother
Paulo, niliyeitwa kwa mapenzi ya Mungu kuwa mtume wa Kristo Yesu, na Sosthene ndugu yetu.
2 the/this/who assembly the/this/who God the/this/who to be in/on/among Corinth to sanctify in/on/among Christ Jesus called holy: saint with all the/this/who to call (on)/name the/this/who name the/this/who lord: God me Jesus Christ in/on/among all place it/s/he (and/both *k) and me
Kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, kwa wale waliotakaswa katika Kristo Yesu na walioitwa kuwa watakatifu, pamoja na wale wote ambao kila mahali wanaliitia Jina la Kristo Yesu Bwana wetu, aliye Bwana wao na wetu pia:
3 grace you and peace away from God father me and lord: God Jesus Christ
Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.
4 to thank the/this/who God me always about you upon/to/against the/this/who grace the/this/who God the/this/who to give you in/on/among Christ Jesus
Ninamshukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu kwa sababu ya neema yake mliyopewa katika Kristo Yesu.
5 that/since: since in/on/among all to enrich in/on/among it/s/he in/on/among all word and all knowledge
Kwa kuwa katika Kristo mmetajirishwa kwa kila hali, katika kusema kwenu na katika maarifa yenu yote,
6 as/just as the/this/who testimony the/this/who Christ to confirm in/on/among you
kwa sababu ushuhuda wetu kumhusu Kristo ulithibitishwa ndani yenu.
7 so you not to lack in/on/among nothing gift to expect the/this/who revelation the/this/who lord: God me Jesus Christ
Kwa hiyo hamkupungukiwa na karama yoyote ya kiroho wakati mnangoja kwa shauku kudhihirishwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
8 which and to confirm you until goal/tax irreproachable in/on/among the/this/who day the/this/who lord: God me Jesus Christ
Atawafanya imara mpaka mwisho, ili msiwe na hatia siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo.
9 faithful the/this/who God through/because of which to call: call toward participation the/this/who son it/s/he Jesus Christ the/this/who lord: God me
Mungu ambaye mmeitwa naye ili mwe na ushirika na Mwanawe Yesu Kristo, Bwana wetu ni mwaminifu.
10 to plead/comfort then you brother through/because of the/this/who name the/this/who lord: God me Jesus Christ in order that/to the/this/who it/s/he to say all and not to be in/on/among you split to be then to complete in/on/among the/this/who it/s/he mind and in/on/among the/this/who it/s/he resolution
Nawasihi ndugu zangu, katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi, ili pasiwepo na matengano katikati yenu na kwamba mwe na umoja kikamilifu katika nia na katika kusudi.
11 to make clear for me about you brother me by/under: by the/this/who Chloe that/since: that quarrel in/on/among you to be
Ndugu zangu, nimepata habari kutoka kwa baadhi ya watu wa nyumbani mwa Kloe kwamba kuna magomvi katikati yenu.
12 to say then this/he/she/it that/since: that each you to say I/we on the other hand to be Paul I/we then Apollos I/we then Cephas I/we then Christ
Maana yangu ni kwamba: Mmoja wenu husema, “Mimi ni wa Paulo”; mwingine, “Mimi ni wa Apolo”; mwingine, “Mimi ni wa Kefa,” na mwingine, “Mimi ni wa Kristo.”
13 to divide the/this/who Christ not Paul to crucify above/for you or toward the/this/who name Paul to baptize
Je, Kristo amegawanyika? Je, Paulo ndiye alisulubishwa kwa ajili yenu? Je, mlibatizwa kwa jina la Paulo?
14 to thank the/this/who God that/since: that none you to baptize if: not not Crispus and Gaius
Nashukuru kwamba sikumbatiza mtu yeyote isipokuwa Krispo na Gayo.
15 in order that/to not one to say that/since: that toward the/this/who I/we name (to baptize *N+KO)
Kwa hiyo hakuna mtu yeyote anayeweza kusema kwamba alibatizwa kwa jina langu.
16 to baptize then and the/this/who Stephanas house: household henceforth no to know if one another to baptize
(Naam, niliwabatiza pia watu wa nyumbani mwa Stefana. Lakini zaidi ya hao sijui kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote.)
17 no for to send me Christ to baptize but to speak good news no in/on/among wisdom word in order that/to not to empty the/this/who cross the/this/who Christ
Kwa maana Kristo hakunituma ili kubatiza bali kuhubiri Injili; sio kwa maneno ya hekima ya kibinadamu, ili msalaba wa Kristo usije ukakosa nguvu yake.
18 the/this/who word for the/this/who the/this/who cross the/this/who on the other hand to destroy foolishness to be the/this/who then to save me power God to be
Kwa maana ujumbe wa msalaba kwa wale wanaopotea ni upuzi, lakini kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu.
19 to write for to destroy the/this/who wisdom the/this/who wise and the/this/who understanding the/this/who intelligent to reject
Kwa maana imeandikwa: “Nitaiharibu hekima ya wenye hekima, na kubatilisha akili ya wenye akili.”
20 where? wise where? scribe where? debater the/this/who an age: age this/he/she/it not! be foolish the/this/who God the/this/who wisdom the/this/who world (this/he/she/it *k) (aiōn g165)
Yuko wapi mwenye hekima? Yuko wapi msomi? Yuko wapi mwanafalsafa wa nyakati hizi? Je, Mungu hakufanya hekima ya ulimwengu huu kuwa upumbavu? (aiōn g165)
21 since for in/on/among the/this/who wisdom the/this/who God no to know the/this/who world through/because of the/this/who wisdom the/this/who God to delight the/this/who God through/because of the/this/who foolishness the/this/who preaching to save the/this/who to trust (in)
Kwa kuwa katika hekima ya Mungu, ulimwengu kwa hekima yake haukumjua yeye, ilimpendeza Mungu kuwaokoa wale walioamini kwa upuzi wa lile neno lililohubiriwa.
22 since and Jew (sign *N+KO) to ask and Greek, Gentile wisdom to seek
Wayahudi wanadai ishara za miujiza na Wayunani wanatafuta hekima.
23 me then to preach Christ to crucify Jew on the other hand stumbling block (Gentiles *N+KO) then foolishness
Lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa: yeye kwa Wayahudi ni kikwazo na kwa Wayunani ni upuzi.
24 it/s/he then the/this/who called Jew and/both and Greek, Gentile Christ God power and God wisdom
Lakini kwa wale ambao Mungu amewaita, Wayahudi na pia Wayunani, Kristo ndiye nguvu ya Mungu na pia hekima ya Mungu.
25 that/since: since the/this/who foolish the/this/who God wise the/this/who a human to be and the/this/who weak the/this/who God strong the/this/who a human (to be *k)
Kwa maana upumbavu wa Mungu una hekima zaidi kuliko hekima ya wanadamu, nao udhaifu wa Mungu una nguvu kuliko nguvu ya wanadamu.
26 to see for the/this/who calling you brother that/since: that no much wise according to flesh no much able no much of noble birth
Ndugu zangu, kumbukeni mlivyokuwa mlipoitwa. Kwa kipimo cha kibinadamu, si wengi wenu mliokuwa na hekima. Si wengi mliokuwa na ushawishi, si wengi mliozaliwa katika jamaa zenye vyeo.
27 but the/this/who foolish the/this/who world to select the/this/who God in order that/to to dishonor the/this/who wise and the/this/who weak the/this/who world to select the/this/who God in order that/to to dishonor the/this/who strong
Lakini Mungu alivichagua vitu vipumbavu vya ulimwengu ili awaaibishe wenye hekima, Mungu alivichagua vitu dhaifu vya ulimwengu ili awaaibishe wenye nguvu.
28 and the/this/who lowly the/this/who world and the/this/who to reject to select the/this/who God (and *ko) the/this/who not to be in order that/to the/this/who to be to abate
Alivichagua vitu vya chini na vinavyodharauliwa vya dunia hii, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko,
29 that not to boast all flesh before the/this/who (God *N+KO)
ili mtu yeyote asijisifu mbele zake.
30 out from it/s/he then you to be in/on/among Christ Jesus which to be wisdom me away from God righteousness and/both and holiness and redemption
Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanyika kwetu hekima itokayo kwa Mungu, yaani haki, na utakatifu na ukombozi.
31 in order that/to as/just as to write the/this/who to boast in/on/among lord: God to boast
Hivyo, kama ilivyoandikwa: “Yeye ajisifuye na ajisifu katika Bwana.”

< 1 Corinthians 1 >