< Matthew 8 >

1 (When was coming down *N+kO) now (He *N+kO) from the mountain followed Him crowds great.
Yesu aliposhuka kutoka mlimani, makutano makubwa ya watu yakamfuata.
2 And behold a leper (having come near *N+kO) was worshipping Him saying; Lord, if You shall be willing, You are able me to cleanse.
Mtu mmoja mwenye ukoma akaja na kupiga magoti mbele yake, akasema, “Bwana, kama ukitaka, unaweza kunitakasa.”
3 And having stretched out the hand He touched of him (Jesus *K) saying; I am willing, do be cleansed. And immediately was cleansed his leprosy.
Yesu akanyoosha mkono wake akamgusa yule mtu, akamwambia, “Nataka. Takasika!” Mara yule mtu akatakasika ukoma wake.
4 And says to him Jesus; do see that to no one may you tell, But do go yourself do show to the priest and do offer the gift that commanded Moses for a testimony to them.
Kisha Yesu akamwambia, “Hakikisha humwambii mtu yeyote. Lakini nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na utoe sadaka aliyoamuru Mose, ili kuwa ushuhuda kwao.”
5 (When was entering *N+kO) now (He *n+o) (Jesus *k) into Capernaum came to Him a centurion imploring Him
Yesu alipoingia Kapernaumu, jemadari mmoja alimjia, kumwomba msaada,
6 and saying; Lord, the servant of mine has been laid in the house paralyzed grievously being tormented.
akisema, “Bwana, mtumishi wangu amelala nyumbani na amepooza, tena ana maumivu makali ya kutisha.”
7 And He says to him (Jesus: *ko) I myself having come will heal him.
Yesu akamwambia, “Nitakuja na kumponya.”
8 And answering (now *o) the centurion was saying; Lord, not I am worthy that my under the roof You may come, but only do speak (a word, *N+kO) and will be healed the servant of mine.
Lakini yule jemadari akamwambia, “Bwana, mimi sistahili wewe kuingia chini ya dari yangu. Lakini sema neno tu, naye mtumishi wangu atapona.
9 Also for I myself a man am under authority (appointed *O) having under myself soldiers and I say to this [one]; do go, and he goes, and to another; do come, and he comes, and to the servant of mine; do enact this, and he enacts [it].
Kwa kuwa mimi mwenyewe ni mtu niliyewekwa chini ya mamlaka, nikiwa na askari chini yangu. Nikimwambia huyu, ‘Nenda,’ yeye huenda; na mwingine nikimwambia, ‘Njoo,’ yeye huja. Nikimwambia mtumishi wangu, ‘Fanya hivi,’ yeye hufanya.”
10 Having heard now Jesus marveled and He said to those following; Amen I say to you; (such *no) (no [one] *N+kO) so great faith in Israel have I found.
Yesu aliposikia maneno haya, alishangaa, akawaambia wale waliomfuata, “Amin, nawaambia, hata katika Israeli sijapata kuona yeyote mwenye imani kubwa namna hii.
11 I say now to you that many from east and west will come and they will recline with Abraham and Isaac and Jacob in the kingdom of the heavens.
Ninawaambia kwamba wengi watatoka mashariki na magharibi, nao wataketi karamuni pamoja na Abrahamu, Isaki na Yakobo katika Ufalme wa Mbinguni.
12 the however sons of the kingdom will be cast out into the darkness the outer; there will be the weeping and the gnashing of the teeth.
Lakini warithi wa Ufalme watatupwa katika giza la nje, ambako kutakuwako kilio na kusaga meno.”
13 And said Jesus to the centurion; do go, (and *ko) as you have believed it should be [done] to you. And was healed the servant of him in the hour that.
Kisha Yesu akamwambia yule jemadari, “Nenda na iwe kwako sawasawa na imani yako.” Naye yule mtumishi akapona saa ile ile.
14 And having come Jesus to the house of Peter He saw the mother-in-law of him lain down and fevering
Yesu alipoingia nyumbani kwa Petro, alimkuta mama mkwe wa Petro amelala kitandani, akiwa ana homa.
15 And He touched the hand of her, and left her the fever. and she arose and was ministering (to him. *N+KO)
Akamgusa mkono wake na homa ikamwacha, naye akainuka na kuanza kumhudumia.
16 When evening now having come they brought to Him being demonised many, and He cast out the spirits by a word, and all those sick being He healed,
Jioni ile, wakamletea watu wengi waliopagawa na pepo wachafu, naye akawatoa wale pepo wachafu kwa neno lake, na kuwaponya wagonjwa wote.
17 so that it may be fulfilled that having been spoken through Isaiah the prophet saying; Himself the infirmities of us He took and [our] diseases bore.
Haya yalifanyika ili litimie lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Isaya kwamba: “Mwenyewe alitwaa udhaifu wetu na alichukua magonjwa yetu.”
18 Having seen now Jesus (great *KO) (crowd *N+kO) around Him He commanded to depart to the other side.
Yesu alipoona makutano mengi wamemzunguka, aliwaamuru wanafunzi wake wavuke mpaka ngʼambo ya ziwa.
19 And having come to [Him] one scribe said to Him; Teacher, I will follow You wherever if You shall go.
Kisha mwalimu mmoja wa sheria akamjia Yesu na kumwambia, “Mwalimu, nitakufuata kokote uendako.”
20 And says to him Jesus; Foxes holes have and the birds of the air nests, but the Son of Man no has [place] where the head He may lay.
Naye Yesu akamjibu, “Mbweha wana mapango, nao ndege wa angani wana viota, lakini Mwana wa Adamu hana mahali pa kulaza kichwa chake.”
21 Another now of the disciples of Him said to Him; Lord, do allow me first to go and to bury the father of mine.
Mwanafunzi mwingine akamwambia, “Bwana, niruhusu kwanza nikamzike baba yangu.”
22 But Jesus (speaks *N+kO) to him; do follow Me, and do leave the dead to bury their own dead.
Lakini Yesu akamwambia, “Nifuate, uwaache wafu wawazike wafu wao.”
23 And having climbed He into the boat followed Him the disciples of Him.
Naye alipoingia kwenye mashua, wanafunzi wake wakamfuata.
24 And behold a storm great arose in the sea so that the boat being swamped by the waves; He Himself however was sleeping.
Ghafula, kukainuka dhoruba kali baharini hata mashua ikaanza kufunikwa na mawimbi, lakini Yesu alikuwa amelala usingizi.
25 And having come to [Him] (the disciples of Him *k) they awoke Him saying; Lord, do save (us *k) we are perishing!
Wanafunzi wake wakamwendea na kumwamsha, wakisema, “Bwana, tuokoe! Tunazama!”
26 And He says to them; Why fearful are you, O [you] of little faith? Then having arisen He rebuked the winds and the sea, and there was a calm great.
Naye Yesu akawaambia, “Kwa nini mnaogopa, enyi wa imani haba?” Kisha akaamka na kukemea dhoruba na mawimbi, nako kukawa shwari kabisa.
27 And the men marveled saying; What kind [of man] is this that even the winds and the sea Him obey
Wale watu wakashangaa, wakisema, “Ni mtu wa namna gani huyu? Hata upepo na mawimbi vinamtii!”
28 And (when was coming He *N+kO) to the other side to the region of the (Gadarenes *N+KO) met Him two being demonised out of the tombs coming forth, violent extremely, so that not to be able anyone to pass through the way that.
Walipofika ngʼambo katika nchi ya Wagerasi, watu wawili waliopagawa na pepo wachafu walitoka makaburini nao wakakutana naye. Watu hawa walikuwa wakali mno kiasi kwamba hakuna mtu aliyeweza kupita njia ile.
29 And behold they cried out saying; What to us and to you (Jesus *k) Son of God? Are You come here before [the] time to torment us?
Wakapiga kelele, “Una nini nasi, Mwana wa Mungu? Umekuja hapa kututesa kabla ya wakati ulioamriwa?”
30 There was now far off from them a herd of pigs many feeding.
Mbali kidogo kutoka pale walipokuwa, kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe wakilisha.
31 And the demons were begging Him saying; If You cast out us, (do allow *K) (do send away *N+KO) (us *N+kO) into the herd of pigs.
Wale pepo wachafu wakamsihi Yesu, “Ukitutoa humu, turuhusu twende kwenye lile kundi la nguruwe.”
32 And He said to them; do go. And having gone out they went away into (herd *k) (pigs, *N+kO) and behold rushed all the herd (of the of pigs *k) down the steep bank into the sea, and perished in the waters.
Akawaambia, “Nendeni!” Hivyo wakatoka na kuwaingia wale nguruwe, nalo kundi lote likateremka gengeni kwa kasi, likaingia katika ziwa na kufa ndani ya maji.
33 Those now feeding [them] fled, and having gone away into the city they related everything including the [matter] of those being demonised.
Wale watu waliokuwa wakiwachunga hao nguruwe wakakimbia wakaingia mjini, wakaeleza yote kuhusu yale yaliyowatokea wale waliokuwa wamepagawa na pepo wachafu.
34 And behold all the city went out to (meet *N+kO) Jesus, And having seen Him they begged [Him] that He may depart from the region of them.
Kisha watu wote wa mji huo wakatoka kwenda kukutana na Yesu. Nao walipomwona wakamsihi aondoke kwenye nchi yao.

< Matthew 8 >