< Matthew 14 >

1 At that [very] time heard Herod the tetrarch the news of Jesus
Wakati huo, mtawala Herode alisikia sifa za Yesu.
2 and he said to the servants of him; This is John the Baptist; he himself is risen from the dead, and because of this the miraculous powers are working in him.
Basi, akawaambia watumishi wake, “Mtu huyu ni Yohane mbatizaji, amefufuka kutoka wafu; ndiyo maana nguvu za miujiza zinafanya kazi ndani yake.”
3 For Herod having seized John he bound him and in prison (put [him] aside *N+kO) on account of Herodias the wife of Philip the brother of him.
Herode ndiye aliyekuwa amemtia Yohane nguvuni, akamfunga minyororo na kumtia gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo, ndugu yake. Sababu hasa ni
4 Were saying for John to him; Not it is lawful for you to have her.
kwamba alikuwa amemwambia Herode, “Si halali kwako kuishi na huyo mwanamke!”
5 Although wishing him to kill he feared the multitude because as a prophet him they were holding.
Herode alitaka kumwua Yohane, lakini aliogopa watu kwa sababu kwao Yohane alikuwa nabii.
6 ([The] birthday *N+kO) now (having happened *N+kO) of Herod danced the daughter of Herodias in the midst and pleased Herod;
Katika sherehe za sikukuu ya kuzaliwa kwake Herode, binti ya Herodia alicheza mbele ya wageni. Herode alifurahiwa,
7 whereupon with oath he promised to her to give whatever (if *NK+o) she shall ask.
hata akaahidi kwa kiapo kumpa huyo msichana chochote atakachoomba.
8 And having been urged on by the mother of her; do give to me she says here on a platter the head of John the Baptist.
Naye, huku akichochewa na mama yake, akaomba, “Nipe papahapa katika sinia kichwa cha Yohane mbatizaji.”
9 And (being grieved *N+kO) the king on account of (now *k) the oaths and those reclining with [him] he commanded [it] to be given.
Mfalme alihuzunika, lakini kwa sababu ya kile kiapo chake na kwa sababu ya wale wageni karamuni, akaamuru apewe.
10 And he having sent beheaded John in the prison.
Basi, Herode akatuma mtu gerezani amkate kichwa Yohane.
11 And was brought the head of him on a platter and was given to the girl, and she brought [it] to the mother of her.
Kichwa chake kikaletwa katika sinia, wakampa yule msichana, naye akampelekea mama yake.
12 And having come the disciples of him took the (body *N+kO) and buried (it, *N+kO) and having come they told Jesus.
Wanafunzi wa Yohane wakaja, wakauchukua mwili wake, wakauzika. Kisha wakaenda kumpasha habari Yesu.
13 (and *k) Having heard (now *no) Jesus withdrew from there by boat to a secluded place apart [on his] own. And having heard [of it] the crowds followed Him on foot from the towns.
Yesu alipopata habari hiyo, aliondoka mahali pale kwa mashua, akaenda mahali pa faragha peke yake. Lakini watu walipata habari, wakamfuata kwa miguu toka mijini.
14 And having gone out (Jesus *k) He saw great a crowd and was moved with compassion toward (them *N+kO) and healed the sick of them.
Basi, aliposhuka pwani, aliona umati mkubwa wa watu, akawaonea huruma, akawaponya wagonjwa wao.
15 Evening now having come they came to Him the disciples (of him *k) saying; Desolate is this place, and the time already is gone by; do dismiss the crowds that having gone into the villages they may buy for themselves food.
Kulipokuwa jioni, wanafunzi wake walimwendea wakamwambia, “Mahali hapa ni nyikani, na saa zimepita. Basi, uwaage watu ili waende vijijini wakajinunulie chakula.”
16 And Jesus said to them; No need they have to go away; do give to them you yourselves to eat.
Yesu akawaambia, “Si lazima waende, wapeni ninyi chakula.”
17 And they say to Him; Not we have here only except five loaves and two fish.
Lakini wao wakamwambia, “Tunayo mikate mitano tu na samaki wawili.”
18 And He said; do bring to Me here them.
Yesu akawaambia, “Nileteeni hapa.”
19 And having commanded the crowds to sit down on (the grass, *N+kO) (and *k) having taken the five loaves and the two fish, having looked up to heaven He spoke a blessing, and having broken He gave to the disciples the loaves, and the disciples to the crowds.
Akawaamuru watu waketi katika nyasi. Kisha akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akamshukuru Mungu. Halafu akaimega hiyo mikate, akawapa wanafunzi wake, nao wakawapa watu.
20 And ate all and were satisfied; and they took up that which is remaindering of the fragments, twelve hand-baskets full.
Watu wote wakala, wakashiba. Kisha wanafunzi wakakusanya mabaki, wakajaza vikapu kumi na viwili.
21 Those then eating were men about five thousand besides women and children.
Jumla ya waliokula ilikuwa wanaume wapatao elfu tano, bila kuhesabu wanawake na watoto.
22 And immediately He compelled (Jesus *k) the disciples (of him *k) to climb into the boat and to go before Him to the other side until that He may have dismissed the crowds.
Mara, Yesu akawaamuru wanafunzi wake wapande mashua, wamtangulie ng'ambo ya ziwa wakati yeye anawaaga watu.
23 And having dismissed the crowds He went up on the mountain on [his] own to pray. Evening now having arrived alone He was there.
Baada ya kuwaaga, alipanda mlimani peke yake kusali. Ilipokuwa jioni, yeye alikuwa huko peke yake,
24 And the boat now (stadia many *NO) (from *N+KO) of the (land was fully *N+KO) being tossed by the waves; was for contrary [was] the wind.
na wakati huo ile mashua ilikwishafika karibu katikati ya ziwa, lakini ilikuwa inakwenda mrama kwa sababu upepo ulikuwa unaipinga.
25 In [the] fourth now watch of the night (he came *N+KO) to them (Jesus *k) walking on (the sea. *N+kO)
Usiku, karibu na mapambazuko, Yesu aliwaendea wanafunzi akitembea juu ya maji.
26 (and *N+kO) the disciples having seen Him on (the sea *N+kO) walking they were troubled saying that A ghost it is! And in fear they cried out.
Wanafunzi wake walipomwona akitembea juu ya maji waliingiwa na hofu, wakasema, “Ni mzimu!” Wakapiga kelele kwa hofu.
27 Immediately now spoke Jesus to them saying; Take courage! I myself it is, not do fear.
Mara, Yesu akasema nao, “Tulieni, ni mimi. Msiogope!”
28 Answering now to Him Peter said: Lord, if You yourself [it] is, do command me to come to You upon the waters.
Petro akamwambia, “Bwana, ikiwa ni wewe kweli, amuru nitembee juu ya maji nije kwako.”
29 And He said; do come. And having descended from the boat Peter walked upon the water (and *no) (came *N+kO) to Jesus.
Yesu akasema, “Haya, njoo.” Basi, Petro akashuka kutoka ile mashua, akatembea juu ya maji, akamwendea Yesu.
30 Seeing now the wind charging he was afraid, and having begun to sink he cried out saying; Lord, do save me!
Lakini alipouona ule upepo, aliogopa, akaanza kuzama; akalia kwa sauti, “Bwana, niokoe!”
31 Immediately now Jesus having stretched out the hand took hold of him and He says to him; [You] of little faith, of why did you doubt?
Hapo, Yesu akaunyosha mkono wake, akamshika na kumwambia, “Ewe mwenye imani haba! Kwa nini uliona shaka?”
32 And (when were climbing *N+kO) they into the boat ceased the wind.
Basi, wakapanda mashuani, na upepo ukatulia.
33 Those then in the boat (having come *ko) worshiped Him saying; Truly of God Son You are!
Wote waliokuwa ndani ya mashua walimsujudia, wakasema, “Hakika wewe ni Mwana wa Mungu.”
34 And having crossed over they came (into *NK+o) the land (of *no) Gennesaret.
Walivuka ziwa, wakafika nchi ya Genesareti.
35 And having recognized Him the men of the place that one sent to all surrounding region that and brought to Him all those sick being
Watu wa huko walipomtambua, wakaeneza habari pote katika sehemu hizo. Basi, wakamletea Yesu wagonjwa wote,
36 and they were begging Him that only they may touch the fringe of the garment of Him; and as many as touched were cured.
wakamwomba awaruhusu waguse tu pindo la vazi lake; wote waliomgusa walipona.

< Matthew 14 >