< Mark 7 >

1 And are gathered together to Him the Pharisees and some of the scribes having come from Jerusalem.
Mafarisayo na baadhi ya waandishi ambao walikuwa wametokea Yerusalemu walikusanyika kumzunguka yeye.
2 And they had seen some of the disciples of Him (that *no) with defiled hands, That is unwashed, (are eating *N+kO) (the *no) bread (they found fault; *K)
Na waliona kuwa baadhi ya wanafunzi wake walikula mkate kwa mikono najisi; ambayo haikuoshwa.
3 For the Pharisees and all the Jews only unless with a fist they shall wash the hands, not eat holding the tradition of the elders;
(kwa Mafarisayo na Wayahudi wote hawali mpaka wameosha mikono yao vizuri; wanashikilia utamaduni wa wazee. Wakati
4 and [on coming] from [the] market (now *o) (when may come *ko) only unless (they shall wash *NK+o) not they eat; and other things many there are which they received to keep washings of cups and vessels and utensils and couches for dining.
Mafarisayo wanaporudi kutoka mahali pa soko, hawali mpaka wameoga kwanza. Na kuna sheria zingine ambazo wanazifuata kabisa, ikiwa ni pamoja na kuosha vikombe, masufuria, vyombo vya shaba, na hata viti vinavyotumika wakati wa chakula.)
5 (And *N+kO) questioned Him the Pharisees and the scribes; Because of why not walk the disciples of You according to the tradition of the elders, but (with unsanctified *N+KO) hands eat the bread?
Mafarisayo na waandishi walimuuliza Yesu, “Kwa nini wanafunzi wako hawaishi kulingana na tamaduni za wazee, kwani wanakula mkate pasipo kunawa mikono?”
6 And (answering *k) He said to them (that: *ko) Rightly prophesied Isaiah concerning you hypocrites, as it has been written (that *no) This people with the lips Me honors, but the heart of them far away is kept from Me.
Lakini yeye aliwaambia, “Isaya alitabiri vizuri kuhusu ninyi wanafiki, aliandika, 'Watu hawa wananiheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali na mimi.
7 In vain now they worship Me teaching [as] doctrines [the] precepts of men.’
Wananifanyia ibaada zisizo na maana, wakifundisha sheria za wanadamu kama mapokeo yao.'
8 Having neglected (for *k) the commandment of God you hold to the tradition of men (washings of vessels and of cups and more like things many things you do. *KO)
Mmeiacha sheria ya Mungu na kushikilia kwa wepesi tamaduni za wanadamu.”
9 And He was saying to them; Neatly do you set aside the commandment of God that the tradition of you (you may maintain. *N+kO)
Na akasema kwao, “Mmeikataa amri ya Mungu kwa urahisi ili kwamba mtunze tamaduni zenu!
10 Moses for said; do honor the Father of you and the mother of you,’ and The [one] speaking evil of father or mother in death should end.’
Kwa kuwa Musa alisema, 'mheshimu baba yako na mama yako,' na 'Yeye asemaye mabaya juu ya baba yake au mama yake hakika atakufa.'
11 You yourselves however say [that]: if may say a man to the father or to the mother; [It is] Corban, that is a gift, whatever if from me you shall be profited,
Lakini mnasema, 'kama mtu akisema kwa baba yake au mama, “Msaada wowote ambao mngepokea kutoka kwangu ni hazina ya Hekalu,”' (hiyo ni kusema kwamba, 'imetolewa kwa Mungu')
12 (and *ko) no longer no longer you do allow him no [thing] to do for the father (of him *k) or for the mother (of him *k)
hivyo haumruhusu kufanya jambo lolote kwa ajili ya baba au mama yake.
13 making void the word of God for the tradition of you which you have handed down; And like [things] such many you do.
Mnaifanya amri ya Mungu kuwa bure kwa kuleta tamaduni zenu. Na mambo mengi ya jinsi hiyo mnayoyafanya.”
14 And having called to [Him] (again *N+KO) the crowd He was saying to them; (do listen to *N+kO) Me all and (do understand. *N+kO)
Aliwaita makutano tena na kuwaambia, “Mnisikilize mimi, ninyi nyote, na mnielewe.
15 No [thing] there is outside of the man entering into him which is able to defile him but the [things] (out of the man *NO) proceeding (from of him *k) (that *ko) are those which are defiling the man.
Hakuna chochote kutoka nje ya mtu ambacho chaweza kumchafua mtu kiingiapo kwake. Bali ni kile kimtokacho mtu ndicho kimchafuacho.
16 (if anyone has ears to hear he should hear. *KO)
(Zingatia: mstari huu, “kama mtu yeyote ana masikio ya kusikia, na asikie” haumo kwenye nakala za kale).
17 And when He went into [the] house from the crowd, were asking Him the disciples of Him (concerning *k) (the parable. *N+kO)
Yesu alipowaacha makutano na kuingia nyumbani, wanafunzi wake wakamwuliza kuhusu mfano huo.
18 And He says to them; Thus also you yourselves without understanding are? Surely you understand that everything outside entering into the man not is able him to defile?
Yesu akasema, “Na ninyi pia bado hamjaelewa? Hamuoni kwamba chochote kimuingiacho mtu hakiwezi kumchafua,
19 because not it enters of him into the heart but into the belly and into the sewer goes out, (purifying *N+kO) all the food.
kwa sababu hakiwezi kwenda kwenye moyo wake, lakini kinaingia katika tumbo lake na kisha kinapita kwenda chooni.” Kwa maelezo haya Yesu alivifanya vyakula vyote kuwa safi.
20 He was saying now that That out of the man going forth, that [is what] defiles the man.
Alisema, “Ni kile ambacho kinamtoka mtu ndicho kimchafuacho.
21 Within for from the heart of men thoughts evil go forth sexual immorality thefts murders,
Kwa kuwa hutoka ndani ya mtu, nje ya moyo, hutoka mawazo maovu, zinaa, wizi, mauaji,
22 adulteries covetous desires, wickednesses, deceit, sensuality, an eye evil, slander, pride, foolishness;
uasherati, tamaa mbaya, uovu, udanganyifu, kujamiiana, wivu, kashfa, majivuno, ujinga.
23 All these evils from within go forth and it defiles the man.
Maovu haya yote yanatoka ndani, ndiyo yale yamchafuayo mtu.”
24 (and *ko) From there (also *no) having risen up He went away into the (region *N+KO) of Tyre (and Sidon. *KO) And having entered into a house no [one] He was wishing to know [it] and not He was able to be hidden.
Aliamka kutoka pale na kuondoka kwenda katika mkoa wa Tiro na Sidoni. Aliingia ndani na hakutaka mtu yeyote ajue kuwa alikuwa hapo, lakini haikuwezekana kumficha.
25 (But immediately *NO) having heard (for *k) a woman about Him of whom had the little daughter of her spirit unclean, having come she fell at the feet of Him;
Lakini ghafla mwanamke, ambaye mtoto wake mdogo alikuwa na roho mchafu, alisikia habari zake, akaja, na akaanguka miguuni pake.
26 Now the woman was Gentile Syrophoenician by race, and was asking Him that the demon (He may cast forth *N+kO) out of the daughter of her.
Mwanamke huyo alikuwa Myunani, wa kabila la Kifoeniki. Alimsihi yeye amfukuze pepo kutoka kwa binti yake.
27 (And *N+kO) (Jesus *k) (He was saying *N+kO) to her; do permit first to be satisfied the children; not for it is good to take the bread of the children and to the dogs to cast [it].
Yesu akamwambia mwanamke, “Waache watoto walishwe kwanza, kwa kuwa sio sawa kuuchukua mkate wa watoto na kuwatupia mbwa.”
28 But she answered and she says to Him; (yes *KO) Lord, even (for *k) the dogs under the table (eat *N+kO) of the crumbs of the children.
Lakini mwanamke akamjibu na kusema, “Ndiyo Bwana, hata mbwa chini ya meza hula mabaki ya chakula cha watoto.”
29 And He said to her; Because of this word do go, has gone forth out of the daughter of you the demon.
Akamwambia, “Kwa kuwa umesema hivi, uko huru kwenda. Pepo ameshamtoka binti yako.”
30 And having gone away to the home of her she found the (child *N+KO) (laid *N+kO) on (the bed *N+kO) and the demon having left.
Mwanamke alirudi nyumbani kwake na akamkuta binti yake amelala kitandani, na pepo alikuwa amemtoka.
31 And again having departed from the region of Tyre He came (through *N+KO) Sidon (to *N+kO) the Sea of Galilee through [the] midst of the region of [the] Decapolis.
Yesu alitoka tena nje ya mkoa wa Tiro na kupitia Sidoni kuelekea Bahari ya Galilaya mpaka kanda ya Dikapolisi.
32 And they bring to Him a deaf man (and *no) who spoke with difficulty and they implore Him that He may lay on him the hand.
Na wakamletea mtu aliyekuwa kiziwi na alikuwa hawezi kuzungumza vizuri, walimsihi Yesu aweke mikono juu yake.
33 And having taken away him from the crowd aside privately He put the fingers of Him to the ears of him, and having spit He touched the tongue of him,
Alimtoa nje ya kusanyiko kwa siri, na akaweka vidole vyake kwenye masikio yake, na baada ya kutema mate, aligusa ulimi wake.
34 and having looked up to heaven He sighed deeply and He says to him; Ephphatha! that is do be opened
Alitazama juu mbinguni, akahema na kumwambia, “Efata,” hiyo ni kusema “funguka!”
35 And (immediately *NK) (were opened *N+kO) his ears, and was loosed the band of the tongue of him, and he was speaking plainly.
Na muda ule ule masikio yakafunguka, na kilichokuwa kimezuia ulimi kiliharibiwa na akaweza kuongea vizuri.
36 And He instructed them that to no one (they may speak; *N+kO) As much as however (He himself *k) them was instructing, (they themselves *no) more excessive were proclaiming [it].
Na aliwaamuru wasimwambie mtu yeyote. Lakini kadri alivyowaamuru, ndivyo walivyotangaza habari hizo kwa wingi.
37 And above measure above measure they were astonished saying; Well all things He has done both the deaf He makes to hear and (the *NK) mute to speak.
Hakika walishangazwa, na kusema, “Amefanya kila kitu vizuri. Hata amewafanya viziwi kusikia na mabubu kuongea.”

< Mark 7 >