< Luke 5 >

1 It came to pass then in the crowd pressing on Him (also *N+KO) to hear the word of God and He himself was already standing by the lake of Gennesaret
Siku moja Yesu alipokuwa amesimama karibu na Ziwa la Genesareti, watu wengi wakiwa wanasongana kumzunguka ili wapate kusikia neno la Mungu,
2 and He saw two boats already lying by the lake. but the fishermen from them having gone out (were washing *N+kO) the nets.
akaona mashua mbili ukingoni mwa ziwa, zikiwa zimeachwa hapo na wavuvi waliokuwa wanaosha nyavu zao.
3 Having climbed then into one of the boats which was (of the *k) Simon’s, He asked him from the land to put off a little. (and *ko) Having sat down (then *no) from the boat He was teaching the crowds.
Akaingia katika mojawapo ya hizo mashua ambayo ilikuwa ya Simoni, akamwomba aisogeze ndani ya maji kidogo kutoka ufuoni. Kisha akaketi na kufundisha watu akiwa mle ndani ya mashua.
4 When then He left off speaking He said to Simon; do put off into the deep and do lower the nets of you for a catch.
Alipomaliza kunena, akamwambia Simoni, “Sasa peleka mashua hadi kilindini kisha mshushe nyavu zenu mkavue samaki.”
5 And answering Simon said (to him: *ko) Master, through whole night having toiled no [thing] have we taken, at however the declaration of You I will let down (the *N+kO) (nets. *N+KO)
Simoni akamjibu, “Bwana, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha na hatukuvua chochote. Lakini, kwa neno lako nitazishusha nyavu.”
6 And this having done they enclosed a multitude of fishes great; were breaking now (the *N+kO) (nets *N+KO) of them.
Nao walipozishusha nyavu zao, wakavua samaki wengi sana, nyavu zao zikajaa zikaanza kukatika.
7 And they beckoned to the partners (to the *k) in the other boat having come to help them. and they came and filled both the boats so that [were] sinking they.
Wakawaashiria wavuvi wenzao kwenye ile mashua nyingine ili waje kuwasaidia. Wakaja, wakajaza mashua zote mbili samaki hata zikaanza kuzama.
8 Having seen now Simon Peter fell at the knees of Jesus saying; do depart from me, for a man sinful am I, Lord.
Simoni Petro alipoona haya yaliyotukia, alianguka miguuni mwa Yesu na kumwambia, “Bwana, ondoka kwangu. Mimi ni mtu mwenye dhambi!”
9 Amazement for laid hold on him and on all those with him at the catch of the fish (which *N+kO) they had taken,
Kwa kuwa yeye na wavuvi wenzake walikuwa wameshangazwa sana na wingi wa samaki waliokuwa wamepata.
10 likewise now also James and John [the] sons of Zebedee, who were partners with Simon. And said to Simon Jesus; Not do fear; from now on men you will be catching.
Vivyo hivyo wenzake Simoni, yaani Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, walishangazwa pia. Ndipo Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope, tangu sasa utakuwa mvuvi wa watu.”
11 And having brought the boats to the land, having left (all [things] *N+kO) they followed Him.
Hivyo wakasogeza mashua zao mpaka ufuoni mwa bahari, wakaacha kila kitu na kumfuata.
12 And it came to pass in being Him in one of the cities that behold a man full of leprosy; (and *ko) having seen (then *no) Jesus, having fallen upon [his] face begged Him saying; Lord, if You shall be willing, You are able me to cleanse.
Ikawa siku moja Yesu alipokuwa katika mji fulani, mtu mmoja mwenye ukoma mwili mzima akamjia. Alipomwona Yesu, alianguka chini mpaka uso wake ukagusa ardhi, akamsihi akisema, “Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa.”
13 And having stretched out the hand He touched him (saying; *N+kO) I am willing, do be cleansed. And immediately the leprosy departed from him.
Yesu akanyoosha mkono wake, akamgusa yule mtu, akamwambia, “Nataka. Takasika!” Na mara ukoma wake ukatakasika.
14 And He himself ordered him no one to tell But having gone do show yourself to the priest and do offer for the cleansing of you even as commanded Moses for a testimony to them.
Yesu akamwagiza akisema, “Usimwambie mtu yeyote, bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani na ukatoe sadaka alizoagiza Mose kwa utakaso wako, ili kuwa ushuhuda kwao.”
15 Was spread abroad now still more the report concerning Him; and were coming crowds great to hear and to be healed (by him *K) from the sicknesses of them;
Lakini habari zake Yesu zikazidi sana kuenea kotekote kuliko wakati mwingine wowote. Makutano makubwa ya watu yalikuwa yakikusanyika ili kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao.
16 He Himself now was withdrawing into the wilderness and praying.
Lakini mara kwa mara Yesu alijitenga nao ili kwenda mahali pa faragha kuomba.
17 And it came to pass on one of the days that He himself was teaching; and there were sitting by Pharisees and teachers of the law who were already coming out of every village of Galilee and of Judea and of Jerusalem, And [the] power of [the] Lord was with to heal (Him. *N+KO)
Siku moja Yesu alipokuwa akifundisha, Mafarisayo na walimu wa sheria, waliokuwa wametoka kila kijiji cha Galilaya na kutoka Uyahudi na Yerusalemu, walikuwa wameketi huko. Nao uweza wa Bwana ulikuwa juu yake kuponya wagonjwa.
18 And behold men carrying upon a mat a man who was paralyzed, and they were seeking him to bring in and to place him before Him.
Wakaja watu wamembeba mgonjwa aliyepooza kwenye mkeka. Wakajaribu kumwingiza ndani ili wamweke mbele ya Yesu.
19 And not having found (through *k) what way they may bring in him on account of the crowd, having gone up on the housetop through the tiles they let down him with the mat into the midst before Jesus.
Walipokuwa hawawezi kufanya hivyo kwa sababu ya umati wa watu, wakapanda juu ya paa, wakaondoa baadhi ya matofali, wakamteremsha yule mgonjwa kwa mkeka wake hadi katikati ya ule umati pale mbele ya Yesu.
20 And having seen the faith of them He said (to him: *k) Man, have been forgiven you the sins of you.
Yesu alipoiona imani yao, akamwambia yule mgonjwa, “Rafiki, dhambi zako zimesamehewa.”
21 And began to reason the scribes and the Pharisees saying; Who is this who speaks blasphemies? Who is able sins (to forgive *N+kO) only except [the] sole God?
Mafarisayo na wale walimu wa sheria wakaanza kuuliza, “Ni nani mtu huyu anayesema maneno ya kukufuru? Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?”
22 Having known now Jesus the reasonings of them answering He said to them; Why reason you in the hearts of you?
Yesu akijua mawazo yao akawauliza, “Kwa nini mnawaza hivyo mioyoni mwenu?
23 Which is easier, to say; Have been forgiven you the sins of you, or to say; (do arise *N+kO) and do walk?
Je, ni lipi lililo rahisi zaidi, kumwambia, ‘Umesamehewa dhambi zako,’ au kusema, ‘Inuka, uende’?
24 That however you may know that the Son of Man authority has on the earth to forgive sins, He said to the [one] paralyzed; To you I say, (do arise *N+kO) and having taken up the mat of you, do go to the house of you.
Lakini ili mpate kujua kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani kusamehe dhambi…” Akamwambia yule aliyepooza, “Nakuambia, inuka, chukua mkeka wako, uende nyumbani kwako.”
25 And immediately having stood up before them, having taken up [that] on (which *N+kO) he was lying, he departed to the home of him glorifying God.
Mara yule mtu aliyekuwa amepooza akasimama mbele yao wote, akachukua mkeka wake, akaenda zake nyumbani, huku akimtukuza Mungu.
26 And amazement seized all, and they were glorifying God and were filled with fear saying that We have seen remarkable things today.
Kila mmoja akashangaa na kumtukuza Mungu. Wakajawa na hofu ya Mungu, wakasema, “Leo tumeona mambo ya ajabu.”
27 And after these things He went forth and He saw a tax collector named Levi sitting at the tax booth and He said to him; do follow Me.
Baada ya haya, Yesu alitoka na kumwona mtoza ushuru mmoja jina lake Lawi akiwa amekaa forodhani, mahali pake pa kutoza ushuru. Akamwambia, “Nifuate.”
28 And having left (all [things] *N+kO) having arisen (he was following *N+kO) Him.
Naye Lawi akaacha kila kitu, akaondoka, akamfuata.
29 And made a banquet great Levi for Him in the house of him, and there was a multitude great of tax collectors and others who were with them reclining.
Kisha Lawi akamfanyia Yesu karamu kubwa nyumbani kwake, nao umati mkubwa wa watoza ushuru na watu wengine walikuwa wakila pamoja nao.
30 And were grumbling the Pharisees and the scribes of them at the disciples of Him saying; Because of why with the tax collectors and sinners do you eat and drink?
Lakini Mafarisayo na walimu wa sheria waliokuwa wa dhehebu lao wakawalalamikia wanafunzi wa Yesu, wakisema, “Mbona mnakula na kunywa pamoja na watoza ushuru na ‘wenye dhambi’?”
31 And answering Jesus said to them; No need have those being well of a physician but those sick being.
Yesu akawajibu, “Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio wagonjwa.
32 Not I have come to call righteous [ones] but sinners to repentance.
Sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi wapate kutubu.”
33 And they said to Him; (through why *KO) The disciples of John fast often and prayers make, likewise also those of the Pharisees, those however of You eat and drink.
Wakamwambia Yesu, “Wanafunzi wa Yohana na wa Mafarisayo mara kwa mara hufunga na kuomba, lakini wanafunzi wako wanaendelea kula na kunywa.”
34 And (Jesus *no) said to them; Not are you able the sons of the bridechamber in which [time] the bridegroom with them is, to make (to fast? *N+kO)
Yesu akawajibu, “Je, mnaweza kuwafanya wageni wa bwana arusi kufunga wakati yuko pamoja nao?
35 Will come however days also when may be taken away from them the bridegroom, then they will fast in those days.
Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kwao. Hapo ndipo watakapofunga.”
36 He was speaking now also a parable to them that No [one] a piece (of *no) a garment new (having torn *NO) puts [it] on a garment old; lest then except indeed also the new (will tear, *N+kO) and to the old not (it will match *N+kO) (the *no) piece of the new.
Yesu akawapa mfano huu, akawaambia: “Hakuna mtu achanaye kiraka kutoka kwenye nguo mpya na kukishonea kwenye nguo iliyochakaa. Akifanya hivyo, atakuwa amechana nguo mpya, na kile kiraka hakitalingana na ile nguo iliyochakaa.
37 And no [one] puts wine new into wineskins old; lest then except indeed will burst the wine new the wineskins and it will be spilled out, and the wineskins will be destroyed;
Hakuna mtu awekaye divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Akifanya hivyo, hiyo divai mpya itavipasua hivyo viriba, nayo yote itamwagika.
38 But wine new into wineskins fresh must be put (and both are preserved. *KO)
Divai mpya lazima iwekwe kwenye viriba vipya.
39 And no [one] having drunk old [wine] (immediately *K) desires new, he says for; The old (good *N+kO) is.
Wala hakuna mtu anayependelea divai mpya baada ya kunywa divai ya zamani, bali husema, ‘Ile ya zamani ni nzuri zaidi.’”

< Luke 5 >