< Luke 4 >

1 Jesus then full of [the] Spirit Holy returned from the Jordan and was led by the Spirit (into the wilderness *N+kO)
Kisha, Yesu akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Mto Jordani, na aliongozwa na Roho jangwani
2 days forty being tempted by the devil. And not He ate no [thing] in the days those, and when were ending they (afterward *K) He was hungry.
kwa siku arobaini, na huko alijaribiwa na Ibilisi. Wakati huo hakula chochote, na mwisho wa wakati huo alihisi njaa.
3 (and *k) Said (then *no) to Him the devil; If [the] Son You are of God, do speak to the stone this that it may become bread.
Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, liamru jiwe hili kuwa mkate.”
4 And answered to him Jesus (saying: *k) It has been written that Not on bread alone will live the man’ (but upon everything declaration of God. *KO)
Yesu akamjibu, “Imeandikwa; 'mtu hataishi kwa mkate pekee.”
5 And having led up Him (devil into mountain high *K) he showed to Him all the kingdoms of the world in a moment of time
Kisha Ibilisi alimwongoza juu kwenye kilele cha mlima, na akamwonyesha falme zote za dunia kwa muda mfupi.
6 And said to Him the devil; To You will I give authority this all and the glory of it, for to me myself it has been delivered and to whom (maybe *NK+o) I shall wish I give it;
Ibilisi akamwambia, “Nitakupa mamlaka ya kutawala falme hizi zote pamoja na fahari zake. Naweza kufanya hivyo kwa sababu vyote vimekabidhiwa kwangu nivitawale, na ninaweza kumpa yeyote nitakaye kumpa.
7 You yourself therefore if You shall worship before (me *N+kO) will be Yours (everything. *N+kO)
Kwahiyo, kama utaniinamia na kuniabudu, vitu hivi vyote vitakuwa vyako.”
8 And answering Jesus said to him (do go *KO) (behind me Satan; *K) It has been written: (for *k) [The] Lord the God of you you will worship and Him only you will serve.’
Lakini Yesu alijibu na kumwambia, “Imeandikwa, “lazima umwabudu Bwana Mungu wako, na lazima umtumikie Yeye peke yake.”
9 (and *k) He led (also *no) Him to Jerusalem and set (him *ko) upon the pinnacle of the temple and said to Him; If (the *k) Son You are of God, do cast Yourself from here down;
Baadaye Ibilisi alimwongoza Yesu hadi Yerusalemu na kumweka sehemu ya juu kabisa ya jengo la hekalu na kumwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa.
10 It has been written for that To the angels of Him He will give orders concerning You to guard You;
Kwa sababu imeandikwa, “Atawaagiza malaika zake wakutunze na kukulinda,
11 and that in [their] hands will they bear You, otherwise otherwise You may strike against a stone the foot of You.’
na watakuinua juu mikononi mwao ili kwamba usiumize miguu yako juu ya jiwe.”
12 And answering He said to him Jesus that It has been said; Not you will test [the] Lord the God of you.’
Yesu akijibu alimwambia, “Imenenwa, “usimjaribu Bwana Mungu wako.”
13 And having finished every temptation the devil departed from Him until an opportune time.
Ibilisi alipomaliza kumjaribu Yesu, alienda zake na kumwacha hadi wakati mwingine.
14 And returned Jesus in the power of the Spirit to Galilee, and a report went out into all the surrounding region concerning Him.
Kisha Yesu alirudi Galilaya kwa nguvu za Roho, na habari kumhusu yeye zikaenea na kusambaa katika mikoa jirani yote.
15 And He himself was teaching in the synagogues of them being glorified by all.
Alifundisha katika masinagogi yao, na kila mmoja alimsifu.
16 And He came to Nazareth where He was raised, and He entered according to the being customary to Him on the day of the Sabbaths into the synagogue and stood up to read.
Siku moja alikwenda Nazareti, mji ambao alilelewa na kukulia. Kama ilivyokuwa desturi yake aliingia kwenye sinagogi siku ya sabato, na alisimama kusoma maandiko.
17 And there was given to Him [the] scroll of the prophet Isaiah; and (having unrolled *NK+o) the scroll He found the place where it was written
Alikabidhiwa gombo la nabii Isaya, hivyo, alilifungua gombo na akatafuta sehemu iliyoandikwa,
18 [The] Spirit of [the] Lord [is] upon Me myself, of which because He has anointed Me (to evangelise *N+kO) to [the] poor, He has sent Me (to heal the bruised heart *K) to proclaim to [the] captives deliverance and to [the] blind recovery of sight, to send forth [the] oppressed in deliverance,
“Roho wa Bwana yuu juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuhubiri habari njema kwa maskini. Amenituma kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kuwafanya wasioona waweze kuona tena. Kuwaweka huru wale wanaogandamizwa,
19 to proclaim [the] year of [the] Lord’s favor.
kuutangaza mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake.”
20 And having rolled up the scroll having delivered [it] to the attendant He sat down, and of all the eyes in the synagogue were fixed upon Him.
Kisha akalifunga gombo, akamrudishia kiongozi wa sinagogi, na akaketi chini. Macho ya watu wote waliokuwa katika sinagogi yalimwangalia yeye.
21 He began then to say to them that Today has been fulfilled Scripture this in the hearing of you.
Alianza kuzungumza nao akisema, “Leo andiko hili limetimizwa masikioni mwenu.”
22 And all were bearing witness to Him and they were marveling at the words of the grace which are proceeding out of the mouth of Him and they were saying; (surely *N+kO) [the] son is of Joseph this?
Kila mmoja pale alishuhudia kile alichokisema Yesu, na wengi miongoni mwao walishangazwa na maneno ya hekima yaliyokuwa yakitoka katika kinywa chake. Walikuwa wakisema, “huyu ni kijana tu wa Yusufu, siyo hivyo?”
23 And He said to them; Surely you will say to Me proverb this; Physician do heal yourself! As much as we have heard has been done (in *N+kO) Capernaum, do perform also here in the hometown of You.
Yesu akawaambia, “hakika mtasema methali hii kwangu, “Tabibu, jiponye mwenyewe. Chochote tulichosikia ukifanya Kapernaumu, kifanye hapa pia kijijini kwako.”
24 He said then; Amen I say to you that no prophet acceptable is in the hometown of him.
Pia alisema, “hakika nawaambia ninyi, hakuna nabii anayekubalika katika nchi yake.”
25 In truth now I say to you; many widows there were in the days of Elijah in Israel when was shut up the heaven for years three and months six, when there was a famine great upon all the land;
Lakini nawaambia ninyi kweli kwamba kulikuwa na wajane wengi Israel katika kipindi cha Eliya, wakati mbingu ilipofungwa kusiwe na nvua kwa miaka mitatu na nusu, wakati kulipokuwa na njaa kubwa katika nchi yote.
26 and to none of them was sent Elijah only except to Zarephath (of Sidon *N+kO) to a woman a widow.
Lakini Eliya hakutumwa kwa yeyote mmoja wao, lakini kwa mjane mmoja tu aliyeishi Sarepta karibu na mji wa Sidoni.
27 And many lepers were in Israel in the time of Elisha the prophet; and none of them was cleansed only except Naaman the Syrian.
Pia, kulikuwa na wakoma wengi Israel katika kipindi cha Elisha nabii, lakini hakuna hatammoja wao aliyeponywa isipokuwa Naamani mtu wa Siria.
28 And were filled all with anger in the synagogue hearing these things;
Watu wote ndani ya sinagogi walijawa na gadhabu walipoyasikia haya yote.
29 and having risen up they cast Him out of the city and led Him unto (the *k) brow of the hill upon which the town had been built of them (in order *N+kO) to throw over him.
Walisimama na kumsukumizia nje ya mji, na kumwongoza mpaka kwenye ukingo wa mlima wa mji ambapo mji wao ulijengwa juu yake, ili waweze kumtupa chini.
30 He himself however having passed through [the] midst of them was going away.
Lakini alipita salama katikati yao na akaenda zake.
31 And He went down to Capernaum a city of Galilee And He was teaching them on the Sabbaths.
Kisha alitelemkia Kapernaumu, katika mji wa Galilaya. Sabato moja alikuwa akifundisha watu ndani ya sinagogi.
32 and they were astonished at the teaching of Him for with authority was the message of Him.
Walishangazwa na mafundisho yake, kwasababu alifundisha kwa mamlaka.
33 And in the synagogue was a man having a spirit of a demon unclean, and he cried out in a voice loud;
Sasa siku hiyo ndani ya sinagogi, kulikuwa na mtu aliyekuwa na roho ya pepo mchafu, na alilia kwa sauti ya juu,
34 (saying *ko) Ha! What to us and to You, Jesus of Nazareth? Are You come to destroy us? I know You who are, the Holy [One] of God.
“Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Ninajua wewe ni nani! Wewe ni mtakatifu wa Mungu!”
35 And rebuked him Jesus saying; do be silent and do come forth (out of *N+kO) him! And having thrown him the demon into the midst it came out from him in nothing having hurt him.
Yesu alimkemea pepo akisema, “Nyamaza kimya, na umtoke mtu huyu!” Pepo yule alipomtupa mtu yule chini katikati yao, alimtoka yule mtu bila ya kumsababishia maumivu yoyote.
36 And came astonishment upon all, and they were speaking to one another saying; What word [is] this for with authority and power He commands the unclean spirits, and they come out?
Watu wote walishangaa, na waliendelea kuzungumzia jambo hilo kila mmoja na mwenzake. Wakasema, “Ni maneno ya aina gani haya?” Anawaamuru roho wachafu kwa mamlaka na nguvu na watondoka.”
37 And was spreading [the] report concerning Him into every place of the surrounding region.
Hivyo, habari juu ya Yesu zilienea kila sehemu katika maeneo yanayozunguka mkoa huo.
38 Having risen up then (out of *N+kO) the synagogue He entered into the house of Simon. (The *k) mother-in-law then of Simon was oppressed with a fever great, and they appealed to Him for her.
Kisha Yesu aliondoka katika mji huo na akaingia katika nyumba ya Simoni. Sasa, mama mkwe wake na Simoni alikuwa anaumwa homa kali, na wakamsihi kwa niaba yake.
39 And having stood over her He rebuked the fever, and it left her; immediately then having arisen she was serving them.
Hivyo, Yesu alimsogelea, akaikemea ile homa na ikamwachia. Ghafla alisimama na akaanza kuwatumikia.
40 When is setting now the sun (all *N+kO) as many as had [any] ailing with diseases various brought them to Him; and on one each of them the hands (having laid He was healing *N+kO) them.
Jua lilipokuwa likizama, watu walimletea Yesu kila mmoja aliyekuwa mgonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Aliweka mikono yake juu ya kila mgonjwa na akawaponya wote.
41 Were going out now also demons from many (shouting out *N+kO) and saying that You yourself are (Christ *K) the Son of God. And rebuking [them] not was He allowing them to speak because they knew the Christ Him to be.
Mapepo pia yaliwatoka wengi wao yakilia kwa sauti na kusema, “Wewe ni mwana wa Mungu!” Yesu aliwakemea mapepo na hakuwaruhusu waongee, kwa sababu walijua kwamba yeye alikuwa ni Kristo.
42 When was arriving now daybreak having gone out He went into a solitary place, and the crowds (were sought after *N+kO) Him and they came up to Him and were detaining Him of the not to go from them.
Wakati kulipopambazuka, alienda eneo lisilokuwa na watu. Makutano ya watu walikuwa wakimtafuta na wakaja katika eneo alilokuwapo. Walijaribu kumzuia asiende mbali na wao.
43 But He said to them that Also to the other towns to evangelise Me it behooves of the kingdom of God, because (for *N+kO) this (have I been sent forth. *N+kO)
Lakini akawaambia, “Lazima pia nihubiri habari njema za ufalme wa Mungu katika miji mingine mingi, kwa kuwa hii ndiyo sababu nilitumwa hapa.”
44 And He was preaching (in the synagogues *N+kO) (of Judea. *N+KO)
Kisha aliendelea kuhubiri ndani ya masinagogi katika uyahudi wote.

< Luke 4 >