< Joshua 13 >

1 And Joshua he was old he had come in days and he said Yahweh to him you you are old you have come in days and the land it remains much very to take possession of it.
Sasa Yoshua alikuwa mzee wakati Yahweh alipomwambia, “Umekuwa mzee, lakini bado kuna nchi kubwa ya kuteka.
2 This [is] the land which remains all [the] territories of the Philistines and all the Geshurite[s].
Nchi iliyosalia ndio hii: mikoa yote ya Wafilisti, na mikoa ile ya Wageshuri,
3 From the Shihor which - [is] on [the] face of Egypt and to [the] border of Ekron north-ward to the Canaanite[s] it is reckoned [the] five - [the] rulers of [the] Philistines the Gazite[s] and the Ashdodite[s] the Ashkelonite[s] the Gittite[s] and the Ekronite[s] and the Avvite[s].
(tangu Shihori, iliyoko mashariki mwa Misri, na upande wa kaskazini kuelekea mpaka wa Ekroni, inayofikiriwa kuwa ni mali ya Wakanaani; wafalme watano wa Wafilisti, wale wafalme wa Gaza, Ashidodi, Ashikeloni, Gathi na Ekroni - miliki ya Waavi.
4 From [the] south all [the] land of the Canaanite[s] and Mearah which [belongs] to the Sidonians to Aphek towards to [the] border of the Amorite[s].
Katika upande wa kusini, kulisalia nchi yote ya Wakanaani, na Meara ambayo ni miliki ya Wasidoni, hadi Afeki, hata mpaka wa Waamori;
5 And the land of the Gebalite[s] and all Lebanon [the] rising of the sun from Baal Gad under [the] mountain of Hermon to Lebo Hamath.
nchi ya Wagebali, Lebanoni kuelekea upande wa mapambazuko ya jua, kutoka Baali- Gadi chini ya Mlima Hermoni mpaka Lebo Hamathi.
6 All [the] inhabitants of the hill country from Lebanon to Misrephoth Maim all [the] Sidonians I I will dispossess them from before [the] people of Israel only make fall it to Israel an inheritance just as I have commanded you.
Pia, wenyeji wote wa nchi ya milima kutoka Lebanoni hadi Misrefothi - Maimu, pamoja na watu wa Sidoni. Nitawafukuza mbele ya jeshi la Israeli. Uwe na uhakika wa kuwapa Waisraeli nchi kama urithi, kama nilivyokuagiza.
7 And therefore apportion the land this an inheritance to [the] nine the tribes and [the] half of the tribe Manasseh.
Igawanye nchi hii kama urithi kwa makabila tisa na kwa nusu ya kabila la Manase.
8 With it the Reubenite[s] and the Gadite[s] they had received inheritance their which he had given to them Moses on [the] other side of the Jordan east-ward just as he had given to them Moses [the] servant of Yahweh.
Pamoja na nusu nyingine ya kabila la Manase, Wareubeni na Wagadi wamekwisha kupokea urithi wao ambao Musa aliwapa katika upande wa mashariki wa Yordani,
9 From Aroer which [is] on [the] edge of [the] wadi of Arnon and the city which [is] in [the] middle of the wadi and all the plain Medeba to Dibon.
kutoka Aroeri, iliyo katika ukingo wa bonde la mto Arnoni (kujumuisha na mji ambao uko katikati ya bonde), kwa nyanda zote za Medeba hadi Diboni;
10 And all [the] cities of Sihon [the] king of the Amorite[s] who he reigned in Heshbon to [the] border of [the] people of Ammon.
miji yote ya Sihoni, mfalme wa Waamori, ambaye alitawala katika Heshiboni, hata mpaka wa Waamori,
11 And Gilead and [the] territory of the Geshurite[s] and the Maacathite[s] and all [the] mountain of Hermon and all Bashan to Salecah.
Gileadi na mkoa wa Wageshuri na Maakathi, mlima wote wa Hermoni, Bashani yote mpaka Saleka;
12 All [the] kingdom of Og in Bashan who he reigned in Ashtaroth and in Edrei he he was left one of [the] remnant of the Rephaites and he had defeated them Moses and he had dispossessed them.
ufalme wote wa Ogu katika Bashani, aliyetawala katika Ashitarothi na Edrei - hawa ni wale waliosalia katika Refaimu - ambao Musa aliwapiga na kuwafukuzia mbali.
13 And not they dispossessed [the] people of Israel the Geshurite[s] and the Maacathite[s] and it has dwelt Geshur and Maacah in [the] midst of Israel until the day this.
Lakini watu wa Israeli hawakuwafukuza Wageshuri wala Wamakathi. Badala yake, Wageshuri na Wamakathi wanaishi miongoni mwa Waisraeli hadi leo.
14 Only to [the] tribe of the Levite[s] not he gave an inheritance [the] fire offerings of Yahweh [the] God of Israel that [was] inheritance its just as he had spoken to it.
Kabila la Lawi pekee halikupewa urithi na Musa. Urithi wao ni sadaka za Yahweh, Mungu wa Israeli, zilizotolewa kwa moto, kama Mungu alivyomwagiza Musa.
15 And he gave Moses to [the] tribe of [the] descendants of Reuben to clans their.
Musa aliwapa urithi kabila la Rubeni, ukoo kwa ukoo.
16 And it belonged to them the territory from Aroer which [is] on [the] edge of [the] wadi of Arnon and the city which [is] in [the] middle of the wadi and all the plain at Medeba.
Miliki yao ilikuwa kutoka Aroeri, juu ya ukingo wa bonde la Mto Arnoni, na mji ulio katikati ya bonde, na nyanda zote za Medeba.
17 Heshbon and all cities its which [are] in the plain Dibon and Bamoth Baal and Beth Baal Meon.
Wareubeni walipata pia Heshiboni, na miji yake yote zilizo katika uwanda, Diboni, na Bamathi Baali, na Bethi Baalimeoni,
18 And Jahaz and Kedemoth and Mephaath.
na Yahazi, na Kedemothi, na Mefaathi,
19 And Kiriathaim and Sibmah and Zereth Shahar on [the] hill of the valley.
na Kiriathaimu, na Sibuma, na Zerethishahari juu ya kilima cha bonde.
20 And Beth Peor and [the] slopes of Pisgah and Beth Jeshimoth.
Wareubeni walipata pia Bethi Peori, miteremko ya Pisiga, Bethi Yeshimothi,
21 And all [the] cities of the plain and all [the] kingdom of Sihon [the] king of the Amorite[s] who he reigned in Heshbon whom he had defeated Moses him - and [the] leaders of Midian Evi and Rekem and Zur and Hur and Reba [the] princes of Sihon [who] dwelt of the land.
miji yote ya uwanda, na ufalme wote wa Sihoni, mfalme wa Waamori, ambaye alikuwa ametawala katika Heshiboni, ambaye Musa alikuwa amemshinda pamoja na viongozi wa Midiani, Evi, Rekemu, Zuri, Huri na Reba, wana wa mfalme wa Sihoni, ambao walikuwa wameishi katika nchi.
22 And Balaam [the] son of Beor the diviner they killed [the] people of Israel with the sword to slain [ones] their.
Pia, watu wa Israeli walimwua kwa upanga Baalam mwana wa Beori, ambaye alifanya mambo ya uaguzi, miongoni mwa wale waliowaua.
23 And it was [the] border of [the] descendants of Reuben the Jordan and a territory this [was] [the] inheritance of [the] descendants of Reuben to clans their the cities and villages their.
Mpaka wa kabila la Rubeni ni Mto Yordani; huu ndio mpaka wao. Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Rubeni, uliotolewa kwa kila ukoo, pamoja na miji na vijiji vyao.
24 And he gave Moses to [the] tribe of Gad to [the] descendants of Gad to clans their.
Hiki ndicho Musa alilipa kabila la Gadi, ukoo kwa ukoo:
25 And it belonged to them the territory Jazer and all [the] cities of Gilead and [the] half of [the] land of [the] people of Ammon to Aroer which [is] on [the] face of Rabbah.
Himaya yao ilikuwa Yazeri, miji yote ya Gileadi na nusu ya nchi ya Waamoni, hadi Aroeri, iliyo mashariki mwa Raba,
26 And from Heshbon to Ramath Mizpah and Betonim and from Mahanaim to [the] territory of Lo Debar.
kutoka Heshiboni hadi Ramathi - Mizipe na Betonimu, kutoka Mahanaimu mpaka himaya ya Debiri.
27 And in the valley Beth Haram and Beth Nimrah and Succoth and Zaphon [the] remainder of [the] kingdom of Sihon [the] king of Heshbon the Jordan and a border to [the] end of [the] sea of Kinnereth [the] other side of the Jordan east-ward.
Katika bonde, Musa aliwapa Bethi -Haramu, Bethi - Nimra, Sukothi, na Zafoni, ufalme uliobakia wa Sihoni mfalme wa Heshiboni, pamoja na Yordani kama mpaka, katika sehemu za chini za mwisho wa Bahari ya Kinerethi, upande wa mashariki ng'ambo ya Yordani.
28 This [was] [the] inheritance of [the] descendants of Gad to clans their the cities and villages their.
Huu ni urithi wa kabila la Gadi, ukoo kwa ukoo, pamoja na miji na vijiji vyao.
29 And he gave Moses to [the] half of [the] tribe of Manasseh and it belonged to [the] half of [the] tribe of [the] descendants of Manasseh to clans their.
Musa aliwapa urithi nusu ya kabila la Manase. Urithi uligawiwa kwa nusu ya kabila la watu wa Manase kutokana na kabila zao.
30 And it was territory their from Mahanaim all Bashan all [the] kingdom of - Og [the] king of Bashan and all [the] villages of Jair which [are] in Bashan sixty citi[es].
Miliki yao ilikuwa kutoka Mahanaimu, Bashani yote, ufalme wote wa mfalme Ogu wa Bashani, na miji yote ya Yairi, iliyo katika Bashani, miji sitini;
31 And [the] half of Gilead and Ashtaroth and Edrei [the] cities of [the] kingdom of Og in Bashan [belong] to [the] descendants of Makir [the] son of Manasseh to [the] half of [the] descendants of Makir to clans their.
nusu ya Gileadi, na Ashitarothi na Edrei (miji ya kifalme ya Ogu katika Bashani). Miji hii iligawanywa kwa ukoo wa Makiri mwana wa Manase -nusu ya watu wa Makiri, walipewa kwa kila familia zao.
32 These [are that] which he gave as a possession Moses in [the] plains of Moab from [the] other side of [the] Jordan of Jericho east-ward.
Huu ndio urithi ambao Musa aliowagawia katika nyanda za Moabu, ng'ambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko.
33 And to [the] tribe of the Levite[s] not he gave Moses an inheritance Yahweh [the] God of Israel he [was] inheritance their just as he had spoken to them.
Musa hakulipa urithi kabila la Lawi. kwa kuwa Yahweh, Mungu wa israeli, ni urithi wao, kama vile alivyowaambia.

< Joshua 13 >