< Hebrews 10 >

1 A shadow for having the law of the coming good things, not themselves the form of the things, each year with the same sacrifices which they offer to the continuous never (is able *NK+o) those drawing near to perfect;
Sheria ni kivuli tu cha mambo mema yajayo, wala si uhalisi wa mambo yenyewe. Kwa sababu hii, haiwezekani kamwe kwa njia ya dhabihu zitolewazo mwaka hadi mwaka kuwakamilisha wale wanaokaribia ili kuabudu.
2 Otherwise not would they have ceased being offered because of none having any longer conscience of sins those serving once (cleansed! *N+KO)
Kama dhabihu hizo zingeweza kuwakamilisha, hazingeendelea kutolewa tena. Kwa kuwa hao waabuduo wangekuwa wametakaswa mara moja tu, wala wasingejiona tena kuwa na dhambi.
3 But in these [there is] a reminder of sins every year;
Lakini zile dhabihu zilikuwa ukumbusho wa dhambi kila mwaka,
4 Impossible [it is] indeed [for the] blood of bulls and of goats to take away sins.
kwa sababu haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.
5 Therefore coming into the world He says: Sacrifice and offering not You have desired, a body however You have prepared me;
Kwa hiyo, Kristo alipokuja duniani, alisema: “Dhabihu na sadaka hukuzitaka, bali mwili uliniandalia;
6 Burnt offerings and [offerings] for sin not You have delighted in;
sadaka za kuteketezwa na za dhambi hukupendezwa nazo.
7 Then I said; Behold I have come — in [the] scroll of [the] book it has been written of Me — to do, O God, the will of You.
Ndipo niliposema, ‘Mimi hapa, nimekuja, imeandikwa kunihusu katika kitabu: Nimekuja kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu.’”
8 Above saying that (sacrifices *N+KO) and (offerings *N+KO) and burnt offerings and [offerings] for sin not You have desired nor You delighted in, which according to (the *k) Law are offered,
Kwanza alisema, “Dhabihu na sadaka, sadaka za kuteketezwa na za dhambi hukuzitaka, wala hukupendezwa nazo” (ingawa sheria iliagiza zitolewe).
9 then He has said; Behold I have come to do (of the God *K) the will of You. He takes away the first that the second He may establish;
Kisha akasema “Mimi hapa, nimekuja kuyafanya mapenzi yako.” Aondoa lile Agano la kwanza ili kuimarisha la pili.
10 By that will sanctified we are through the offering of the body of Jesus Christ once for all.
Katika mapenzi hayo sisi tumetakaswa na kufanywa watakatifu kwa njia ya sadaka ya mwili wa Yesu Kristo alioutoa mara moja tu.
11 And every indeed priest has stood every day ministering and the same repeatedly offering sacrifices, which never are able to take away sins;
Kila kuhani husimama siku kwa siku akifanya huduma yake ya ibada, na kutoa tena na tena dhabihu zile zile ambazo haziwezi kamwe kuondoa dhambi.
12 (This [One] *N+kO) however one for sins having offered sacrifice in perpetuity sat down at [the] right hand of God,
Lakini huyu kuhani akiisha kutoa dhabihu moja kwa ajili ya dhambi kwa wakati wote, aliketi mkono wa kuume wa Mungu.
13 the henceforth awaiting until may be placed the enemies of Him [as] a footstool for the feet of Him.
Tangu wakati huo anangoja mpaka adui zake wawekwe chini ya miguu yake,
14 By one for offering He has perfected for all time those being sanctified.
kwa sababu kwa dhabihu moja amewafanya kuwa wakamilifu milele wale wote wanaotakaswa.
15 Bears witness now to us also the Spirit Holy; after for (to have said: *N+KO)
Pia Roho Mtakatifu anatushuhudia kuhusu jambo hili. Kwanza anasema:
16 This [is] the covenant that I will make with them after the days those, says [the] Lord, putting [the] laws of Mine into [the] hearts of them and into (the mind *N+kO) of them I will inscribe them;
“Hili ndilo Agano nitakalofanya nao baada ya siku hizo, asema Bwana. Nitaziweka sheria zangu mioyoni mwao, na kuziandika katika nia zao.”
17 and The sins of them and the lawless acts of them certainly not (will I remember *N+kO) any more.
Kisha aongeza kusema: “Dhambi zao na kutokutii kwao sitakumbuka tena.”
18 Where now forgiveness of these [is], no longer no longer an offering for sin.
Basi haya yakiisha kusamehewa, hakuna tena dhabihu yoyote inayotolewa kwa ajili ya dhambi.
19 Having therefore, brothers, confidence for the entering to the Holy [Places] by the blood of Jesus,
Kwa hiyo, ndugu zangu, kwa kuwa tunao ujasiri wa kupaingia Patakatifu pa Patakatifu kwa damu ya Yesu,
20 which He dedicated for us a way new and living through the veil, That is through the flesh of Him,
kwa njia mpya iliyo hai tuliyofunguliwa kwa ajili yetu kupitia kwenye lile pazia, yaani, mwili wake,
21 and [having] a priest great over the house of God,
basi kwa kuwa tunaye Kuhani Mkuu juu ya nyumba ya Mungu,
22 we may draw near with a sincere heart in full assurance of faith sprinkled clean [our] hearts from a conscience evil and (having ourselves washed *N+kO) [our] body with water pure.
sisi na tumkaribie Mungu kwa moyo mnyofu kwa imani timilifu, mioyo yetu ikiwa imenyunyizwa damu ya Kristo na kuwa safi kutokana na dhamiri mbaya nayo miili yetu ikiwa imeoshwa kwa maji safi.
23 We may hold fast to the confession of [our] hope firmly, faithful for [is] the [One] having promised,
Tushike kwa uthabiti lile tumaini la ukiri wetu bila kuyumbayumba, kwa maana yeye aliyeahidi ni mwaminifu.
24 And we may think one another toward stirring up to love and to good works
Tuangaliane na kuhimizana sisi kwa sisi katika upendo na katika kutenda mema.
25 not forsaking the assembling together of ourselves even as [is the] custom with some, but encouraging [one another], and so much more as much as you see drawing near the Day.
Wala tusiache kukutana pamoja, kama wengine walivyo na desturi, bali tuhimizane sisi kwa sisi kadiri tuonavyo Siku ile inakaribia.
26 [If] willingly for sin we after [we are] to receive the knowledge of the truth no longer no longer for sins remains a sacrifice,
Kama tukiendelea kutenda dhambi kwa makusudi baada ya kupokea ufahamu wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi.
27 terrifying however a certain expectation of judgment and of fire fury to devour being about the adversaries.
Lakini kinachobaki ni kungoja kwa hofu hukumu ya moto uwakao, utakaowaangamiza adui za Mungu.
28 Having set aside anyone [the] law of Moses without mercies on the basis of two or three witnesses he dies;
Yeyote aliyeikataa sheria ya Mose alikufa pasipo huruma kwa ushahidi wa watu wawili au watatu.
29 How much think you worse will he deserve punishment the [one] the Son of God having trampled upon and the blood of the covenant ordinary having esteemed by which he was sanctified and the Spirit of grace having insulted?
Je, mnadhani ni adhabu kali kiasi gani anayostahili kupewa mtu aliyemkanyaga Mwana wa Mungu chini ya nyayo zake, yeye aliyeifanya damu ya Agano iliyomtakasa kuwa kitu najisi na kumtendea maovu Roho wa neema?
30 We know for the [One] having said; Mine [is] vengeance, I myself will repay (says Lord; *K) and again: Will judge [the] Lord the people of Him.
Kwa kuwa tunamjua yeye aliyesema, “Ni juu yangu kulipiza kisasi; nitalipiza.” Tena asema, “Bwana atawahukumu watu wake.”
31 [It is] a fearful thing to fall into [the] hands of God [the] living.
Ni jambo la kutisha kuanguka mikononi mwa Mungu aliye hai.
32 do remember however the former days in which having been enlightened a great conflict you endured of sufferings,
Kumbukeni siku zile za kwanza, ambazo mkiisha kutiwa nuru mlistahimili mashindano makali ya maumivu.
33 this indeed by revilings both and by tribulations being made a spectacle, this however partners of those thus passing through [them] having become;
Wakati mwingine mlitukanwa na kuteswa hadharani; wakati mwingine mlikuwa radhi kuungana na wale waliofanyiwa hivyo.
34 Both for with the (prisoners *N+KO) you sympathized and the plundering of the possessions of you with joy you accepted knowing to have (in *k) (yourselves *N+kO) (a better *NK+o) possession (in heavens *K) and abiding.
Mliwahurumia wale waliokuwa kifungoni, mkikubali kwa furaha kunyangʼanywa mali zenu kwa maana mlijua kwamba mnayo mali iliyo bora zaidi idumuyo.
35 Not may throw away therefore the boldness of you, which has a great reward.
Kwa hiyo msiutupe ujasiri wenu, kwa maana una thawabu kubwa mno.
36 Of endurance for You have need, so that the will of God having done you may receive the promise.
Inawapasa kuvumilia ili mkiisha kufanya mapenzi ya Mungu mpate kile alichoahidi.
37 Yet for A little very while, the [One] who is coming will come and not will delay.
Kwa kuwa bado kitambo kidogo tu, “Yeye ajaye atakuja wala hatakawia.
38 The one however righteous (of Mine *NO) by faith will live; and if he shall shrink back, not takes pleasure the soul of Mine in him.
Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani. Naye kama akisitasita, sina furaha naye.”
39 We ourselves however not are of [those] drawing back to destruction but of faith to [the] preserving [of the] soul.
Lakini sisi hatumo miongoni mwa hao wanaositasita na kuangamia, bali tuko miongoni mwa hao wenye imani na hivyo tunaokolewa.

< Hebrews 10 >