< Ephesians 1 >

1 Paul an apostle of Christ Jesus through [the] will of God To the saints who are being in Ephesus and faithful in Christ Jesus;
Mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, nawaandikia ninyi watu wa Mungu huko Efeso, mlio waaminifu katika kuungana na Kristo Yesu.
2 Grace to you and peace from God [the] Father of us and [the] Lord Jesus Christ.
Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
3 Blessed [be] the God and Father of the Lord of us Jesus Christ, the [One] having blessed us with every blessing spiritual in the heavenly realms in Christ,
Atukuzwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Maana, katika kuungana na Kristo ametubariki kwa kutujalia zawadi zote za kiroho mbinguni.
4 even as He chose us in Him before [the] foundation of [the] world to be for us holy and blameless before Him in love
Kabla ya kuumbwa ulimwengu, Mungu alituteua tuwe wake katika kuungana na Kristo ili tuwe watakatifu na bila hitilafu mbele yake. Kwa sababu ya upendo wake,
5 having predestined us for divine adoption as sons through Jesus Christ to Himself according to the good pleasure of the will of Him
Mungu alikuwa ameazimia tangu zamani kutuleta kwake kama watoto wake kwa njia ya Yesu Kristo. Ndivyo alivyopenda na kunuia.
6 to [the] praise of [the] glory of the of grace of Him, (in *K) (which *N+kO) He has freely given us in the Beloved [One],
Basi, tumsifu Mungu kwa sababu ya neema yake tukufu katika Mwanae mpenzi!
7 in whom we have redemption through the blood of Him, the forgiveness of trespasses, according to (the riches *N+kO) of the grace of Him,
Maana kwa damu yake Kristo sisi tunakombolewa, yaani dhambi zetu zinaondolewa. Ndivyo ulivyo ukuu wa neema yake
8 which He lavished upon us in all wisdom and in understanding
aliotukirimia bila kipimo! Kwa hekima na ujuzi wake wote
9 having made known to us the mystery of the will of Him according to the pleasure of Him, which He purposed in Him
Mungu alitekeleza kile alichonuia, akatujulisha mpango wake uliofichika, ambao alikuwa ameazimia kuutekeleza kwa njia ya Kristo.
10 for [the] administration of the fullness of the times, to bring together the all things in Christ, the [things] (then *k) (in *N+kO) the heavens and the [things] upon the earth, in Him,
Mpango huo ambao angeutimiza wakati utimiapo ni kukusanya pamoja viumbe vyote, kila kitu mbinguni na duniani, chini ya Kristo.
11 in whom also we have obtained an inheritance having been predestined according to [the] purpose of the [One] all things working according to the counsel of the will of Him
Kila kitu hufanywa kufuatana na mpango na uamuzi wa Mungu; naye Mungu ametuteua sisi tuwe watu wake kwa mapenzi yake katika kuungana na Kristo, kufuatana na azimio alilofanya tangu mwanzo.
12 for to be us to [the] praise (of the *k) glory of Him, the [ones] having first trusted in Christ;
Basi, sisi tuliotangulia kumtumainia Kristo tunapaswa kuusifu utukufu wa Mungu!
13 in whom also you yourselves having heard the word of truth, the gospel of the salvation of you, in whom also having believed you were sealed with the Spirit of promise Holy
Nanyi pia watu wa mataifa mengine, mliusikia ujumbe wa kweli yaani Habari Njema iliyowaletea wokovu, mkamwamini Kristo; naye Mungu, ili kuonyesha kuwa ninyi ni wake, akawapiga mhuri kwa kuwapeni yule Roho Mtakatifu aliyetuahidia.
14 (who *N+kO) is [the] guarantee of the inheritance of us to [the] redemption of the acquired [possession] to [the] praise of the glory of Him.
Huyu Roho ni dhamana ya kurithi yote yale Mungu aliyowaahidia watu wake, na jambo hili latuhakikishia kwamba Mungu atawakomboa kabisa wote walio wake. Tuusifu utukufu wake!
15 Because of this I myself also I myself also having heard of the among you faith in the Lord Jesus and the love toward all the saints
Kwa sababu hiyo, tangu niliposikia juu ya imani yenu kwa Bwana Yesu na mapendo yenu kwa watu wa Mungu,
16 not do cease giving thanks for you mention (of you *k) making in the prayers of mine
sijaacha kamwe kumshukuru Mungu kwa ajili yenu. Ninawakumbuka katika sala zangu
17 that the God of the Lord of us Jesus Christ, the Father of glory, (may give *NK+o) to you [a] spirit of wisdom and revelation in [the] knowledge of Him,
ili Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo Baba mtukufu, awajalieni Roho wake atakayewapa hekima na kuwafunulieni Mungu mpate kumjua.
18 enlightened [are] the eyes of the (heart *N+KO) of you in order for to know you what is the hope of the calling of Him, (and *k) what [are] the riches of the glory of the inheritance of Him in the saints,
Namwomba Mungu aifunue mioyo yenu iweze kuuona mwanga wake, mpate kutambua lile tumaini alilowaitieni na utukufu mkuu wa zawadi alizowawekea watu wake,
19 and what [is] the surpassing greatness of the power of Him toward us those believing according to the working of the might of the strength of Him,
mpate kutambua jinsi uwezo wake ulivyo mkuu mno kwa ajili yetu sisi tunaoamini. Uwezo huo unaofanya kazi ndani yetu, ni sawa na nguvu ile kuu mno
20 which (He worked *NK+o) in Christ having raised Him out from (the *o) dead and (having sat *N+kO) (him *O) at [the] right hand of Him in the heavenly realms
aliyomfufua nayo Kristo kutoka wafu, akamketisha kulia kwake mbinguni.
21 above every principality and authority and power and dominion and every name being named not only in age this but also in the [one] coming, (aiōn g165)
Huko, Kristo anatawala juu ya kila tawala, mamlaka, enzi na ukuu; anatawala juu ya kila cheo kiwezacho kutajwa katika ulimwengu huu na katika ulimwengu ujao. (aiōn g165)
22 And all things He put under the feet of Him and Him gave [to be] head over all things to the church
Mungu ameweka vitu vyote chini ya miguu yake, akamkabidhi kwa kanisa akiwa mkuu wa vitu vyote.
23 which is the body of Him, the fullness of the [One] all in all filling.
Kanisa ni mwili wa Kristo, na ukamilifu wake yeye anayekamilisha vitu vyote kila mahali.

< Ephesians 1 >