< 1 John 4 >

1 Beloved, not every spirit do believe but do test the spirits whether of God they are, because many false prophets have gone out into the world.
Wapendwa, msiiamini kila roho, lakini zijaribuni roho muone kama zinatokana na Mungu, kwa sababu manabii wengi wa uongo wametokea duniani.
2 By this (you know *NK+O) the Spirit of God: Every spirit that confesses Jesus Christ in [the] flesh having come of God is.
Kwa hili mtamjua Roho wa Mungu - kila roho itakayokiri kuwa Yesu Kristo amekuja katika mwili ni ya Mungu,
3 and any spirit that not confesses Jesus (Christ in flesh having come *K) from God not is; And this is that of the antichrist which you have heard that is coming and now in the world is already.
na kila roho isiyomkiri Yesu si ya Mungu. Hii ni roho ya mpinga kristo, ambayo mliyoisikia kuwa inakuja, na sasa tayari iko duniani.
4 you yourselves from God are, little children, and have overcome them, because greater is the [One] in you than the [one] in the world.
Ninyi ni wa Mungu, watoto wapendwa, na mmekwisha washinda kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika ulimwengu.
5 They themselves of the world are; because of this from out of the world they speak and the world to them listens.
Wao ni wa ulimwengu, kwa hiyo wanachokisema ni cha ulimwengu, na ulimwengu unawasikiliza.
6 We ourselves of God are; The [one] knowing God listens to us; He who not is from God not listens to us. By this we know the Spirit of truth and the spirit of falsehood.
Sisi ni wa Mungu. Yeye amjuaye Mungu hutusikiliza sisi. Yeye asiye wa Mungu hawezi kutusikiliza. Katika hili tunajua roho wa kweli na roho wa uongo.
7 Beloved, we may love one another, because love from God is and everyone who is loving from God has been born and knows God;
Wapendwa, tupendane sisi kwa sisi, kwa vile upendo ni wa Mungu, na kila mmoja apendaye amezaliwa na Mungu na kumjua Mungu.
8 The [one] not loving not has known God, because God love is.
Yeye asiyependa hamjui Mungu, kwa sababu Mungu ni upendo.
9 In this has been revealed the love of God among us, that the Son of Him the one and only has sent God into the world so that we may live through Him.
Katika hili pendo la Mungu lilifunuliwa miongoni mwetu, kwamba Mungu alimtuma Mwanae wa pekee ulimwenguni ili tuishi kupitia yeye.
10 In this is love, not that we ourselves (have loved *N+kO) God, but that He himself loved us and He sent the Son of Him [as] a propitiation for the sins of us.
Katika hili pendo, si kwamba tulimpenda Mungu, lakini yeye alitupenda, na akamtuma Mwanawe awe fidia ya dhambi zetu.
11 Beloved, if so God loved us, also we ourselves ought one another to love;
Wapendwa, ikiwa Mungu alitupenda sisi, vile vile tunapaswa kupendana sisi kwa sisi.
12 God no [one] at any time has seen; if we shall love one another, God in us abides and the love of Him in us perfected is.
Hakuna hata mmoja aliyemuona Mungu. Kama tukipendana sisi kwa sisi, Mungu anakaa ndani yetu na pendo lake limekamilika ndani yetu.
13 By this we know that in Him we abide and He in us, because from out the Spirit of Him He has given to us.
Katika hili tunajua kuwa tunakaa ndani yake na yeye ndani yetu, kwa sababu ametupa Roho wake.
14 And we ourselves have seen and testify that the Father has sent the Son [as] Savior of the world.
Na tumeona na kushuhudia kuwa Baba amemtuma Mwana kuwa mwokozi wa ulimwengu.
15 Who[ever] (maybe *N+kO) shall confess that Jesus (Christ *O) is the Son of God, God in him abides and he in God.
Kila anayekiri kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, Mungu anakaa ndani yake na yeye ndani ya Mungu.
16 And we ourselves have come to know and we have come to believe the love that has God as to us. God love is, and the [one] abiding in love in God abides, and God in him (abides. *NO)
Na tunajua na kuamini upendo alio nao Mungu ndani yetu. Mungu ni pendo, na yeye anayekaa ndani ya upendo anakaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake.
17 In this has been perfected love with us, so that confidence we may have in the day of judgment, that even as He is also we ourselves are in world this.
Katika pendo hili limekwisha kamilishwa kati yetu, ili tuwe na ujasiri siku ya hukumu, kwa sababu kama yeye alivyo, na sisi ndivyo tulivyo katika ulimwenngu huu.
18 Fear no there is in love, but perfect love out casts fear, because the fear punishment has; the [one] now fearing not has been perfected in love.
Hakuna hofu ndani ya pendo. Lakini pendo kamili huitupa hofu nje, kwa sababu hofu huhusiana na hukumu. Lakini yeye aogopaye hajakamilishwa katika pendo.
19 We ourselves love (him *K) because He himself first loved us.
Tunapenda kwa sababu Mungu alitupenda kwanza.
20 If anyone shall say that I love God and the brother of him may hate, a liar he is; The [one] for not loving the brother of him whom he has seen, God whom not he has seen (not *N+KO) is he able to love;
Ikiwa mmoja atasema, “Nampenda Mungu” lakini anamchukia ndugu yake, ni mwongo. Kwa sababu asiyempenda ndugu yake, anayemuona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hajamuona.
21 And this the commandment we have from Him, that the [one] loving God may love also the brother of him.
Na hii ndiyo amri tuliyo nayo kutoka kwake: Yeyote ampendaye Mungu, anapaswa kumpenda ndugu yake pia.

< 1 John 4 >