< Revelation 5 >

1 And I saw, upon the right hand of him that was sitting upon the throne, a scroll; written within, and on the back, sealed up with seven seals.
Kisha katika mkono wa kulia wa huyo aliyeketi juu ya kiti cha enzi, nikaona kitabu; nacho kilikuwa kimeandikwa ndani na nje na kufungwa na mihuri saba.
2 And I saw a mighty messenger, proclaiming with a loud voice—Who is worthy to open the scroll, and to unloose the seals thereof?
Tena nikamwona malaika mwenye nguvu akitangaza kwa sauti kubwa: “Nani anayestahili kuvunja hiyo mihuri na kukifungua kitabu hicho?”
3 And, no one, was able, in heaven, or on earth, or under the earth, to open the scroll, or, to look thereon.
Lakini hakupatikana mtu yeyote mbinguni, wala duniani, wala chini Kuzimu, aliyeweza kukifungua hicho kitabu au kukitazama ndani. (questioned)
4 And, I, began to weep much, because, no one, worthy, was found, to open the scroll, or, to look thereon.
Basi, mimi nikalia sana kwa sababu hakupatikana mtu aliyestahili kukifungua, au kukitazama ndani.
5 And, one of the elders, saith unto me—Do not weep! Lo! the lion that is of the tribe of Judah, the root of David, hath overcome, to open the scroll and the seven seals thereof.
Kisha mmoja wa wale wazee akaniambia, “Usilie! Tazama! Simba wa kabila la Yuda, mjukuu maarufu wa Daudi, ameshinda. Yeye anaweza kuivunja mihuri yake saba na kukifungua hicho kitabu.”
6 And I saw, in the midst of the throne and of the four living creatures, and in the midst of the elders, a Lamb, standing, showing that it had been slain, —having seven horns, and seven eyes, which are the [seven] Spirits of God sent forth into all the earth.
Kisha nikaona pale katikati ya kiti cha enzi Mwana kondoo amesimama, akizungukwa kila upande na vile viumbe hai vinne, na wale wazee. Huyo Mwanakondoo alionekana kana kwamba amechinjwa. Alikuwa na pembe saba na macho saba ambayo ni roho saba za Mungu zilizokuwa zimepelekwa kila mahali duniani.
7 And he came, and at once took [it] out of the right hand of him that was sitting upon the throne.
Mwanakondoo akaenda, akakitwaa hicho kitabu kutoka mkono wa kulia wa yule aliyeketi juu ya kiti cha enzi.
8 And, when he took the scroll, the four living creatures, and the four-and-twenty elders, fell down before the Lamb, having, each one, a harp, and bowls of gold full of incense, —which are the prayers of the saints;
Mara tu alipokwisha twaa hicho kitabu, vile viumbe hai vinne pamoja na wale wazee ishirini na wanne walianguka kifudifudi mbele ya Mwanakondoo. Kila mmoja, alikuwa na kinubi na bakuli za dhahabu zilizojaa ubani, ambao ni sala za watu wa Mungu.
9 and they sing a new song, saying—Worthy, art thou, to take the scroll and to open the seals thereof; because thou wast slain, and didst redeem unto God by thy blood [men] out of every tribe, and tongue, and people, and nation,
Basi, wakaimba wimbo huu mpya: “Wewe unastahili kukitwaa hicho kitabu na kuivunja mihuri yake. Kwa sababu wewe umechinjwa, na kwa damu yako umemnunulia Mungu watu kutoka katika kila kabila, lugha, jamaa na taifa.
10 And didst make them, unto our God, a kingdom and priests, —and they reign on the earth.
Wewe umewafanya wawe ufalme wa makuhani wamtumikie Mungu wetu nao watatawala duniani.”
11 And I saw, and heard a voice of many messengers, round about the throne and the living creatures and the elders, —and the number of them was myriads of myriads and thousands of thousands—
Kisha nikatazama, nikasikia sauti ya malaika wengi sana, idadi isiyohesabika, maelfu na maelfu. Walikuwa wamekaa kuzunguka kiti cha enzi, vile viumbe hai vinne na wale wazee;
12 saying with a loud voice—Worthy, is the Lamb that hath been slain, to receive the power, and riches, and wisdom, and might, and honour, and glory, and blessing.
wakasema kwa sauti kuu: “Mwanakondoo aliyechinjwa anastahili kupokea uwezo, utajiri, hekima, nguvu, utukufu na sifa.”
13 And, every created thing which was in heaven, and upon the earth, and under the earth, and upon the sea, and, all the things in them, heard I, saying—Unto him that sitteth upon the throne, and unto the Lamb, be the blessing, and the honour, and the glory, and the dominion, unto the ages of ages! (aiōn g165)
Nikasikia viumbe vyote mbinguni, duniani, chini kuzimuni na baharini—viumbe vyote ulimwenguni—vikisema: “Kwake yeye aketiye katika kiti cha enzi, na kwa Mwanakondoo, iwe sifa na heshima na utukufu na enzi milele na milele.” (aiōn g165, questioned)
14 And the four living creatures continued saying—Amen! And, the elders, fell down and did homage.
Na vile viumbe vinne hai vikasema, “Amina!” Na wale wazee wakaanguka kifudifudi, wakaabudu.

< Revelation 5 >