< Psalms 81 >

1 To the Chief Musician. On "the Gittith." Asaph’s. Shout ye for joy, unto God our strength, Sound the note of triumph, to the God of Jacob;
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
2 Raise a melody, and strike the timbrel, The lyre so sweet, with the harp:
Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
3 Blow, at the new moon, the horn, At the full moon, for the day of our sacred festival:
Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
4 For, a statute to Israel, it is, A regulation, by the God of Jacob;
hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
5 A testimony in Joseph, he appointed it, When he went forth over the land of Egypt: A language I liked not, used I to hear;
Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
6 I took away, from the burden, his shoulder, his hands, from the clay, were set free.
Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
7 In distress, thou didst cry, and I delivered thee, —I answered thee, within a hiding-place of thunder, I proved thee by the waters of Meribah. (Selah)
Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
8 Hear, O my people, and I will adjure thee, O Israel, if thou wilt hearken unto me!
“Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
9 There shall not be, within thee, a foreign GOD, —Neither shalt thou bow down to a strange GOD:
Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
10 I, Yahweh, am thy God, Who brought thee up out of the land of Egypt, —Open wide thy mouth, that I may fill it.
Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
11 But my people, hearkened not, unto my voice, Even, Israel, inclined not unto me.
“Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
12 So then I let them go on in the stubbornness of their own heart, They might walk in their own counsels!
Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
13 If, my people, were hearkening unto me, [If, ] Israel, in my ways, would walk,
“Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
14 Right soon, their foes, would I subdue, And, against their adversaries, would I turn my hand:
ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
15 The haters of Yahweh, should come cringing unto him, Then let their own good time be age-abiding!
Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
16 Then would he feed them from the marrow of the wheat, Yea, out of the rock—with honey, would I satisfy thee.
Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”

< Psalms 81 >