< Psalms 75 >

1 To the Chief Musician. "Do not Destroy." A Melody of Asaph, a Song. We have given thanks unto thee, O God, we have given thanks, And, in calling upon thy Name, men have recounted thy wonders.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
2 Surely I will take a set time, —I, with equity, will judge:
Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
3 Earth was melting away with all its inhabitants, I, have fixed the pillars thereof. (Selah)
Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
4 I have said to the boasters, Do not boast, And to the lawless, Do not lift up a horn;
Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
5 Do not lift up on high your horn, Nor speak of the Rock, with arrogance;
Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
6 For neither from east nor west, Nor from the wilderness of the mountains [cometh exaltation];
Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
7 For, God himself, is about to judge, One, he will cast down, Another, he will lift up;
Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
8 For, a cup, is in the hand of Yahweh, Whose wine is foaming, It is full of spiced wine, Which he hath caused to flow from one to another, —Surely, the dregs thereof, they shall drain out—they shall drink, Even all the lawless ones of the earth.
Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
9 But, I, will exult unto times age-abiding, I will sing praises unto the God of Jacob;
Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
10 But, all the horns of the lawless, will I hew off, —Exalted shall be the horns of the Righteous One.
Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.

< Psalms 75 >