< Psalms 30 >

1 A Melody. A Song for the Dedication of the House. David’s. I will extol thee, O Yahweh, for thou hast drawn me up, —and not suffered my foes to rejoice over me.
Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi. Nitakutukuza wewe, Ee Bwana, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu.
2 O Yahweh, my God, I cried for help unto thee, and thou hast healed me.
Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya.
3 O Yahweh! thou hast lifted, out of hades, my soul, Thou hast brought me back to life, from among those who were going down to the pit. (Sheol h7585)
Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. (Sheol h7585)
4 Sweep the strings to Yahweh, ye his men of lovingkindness, and give ye praise at the mention of his holiness.
Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake; lisifuni jina lake takatifu.
5 For there is, a Moment, in his anger, a Life-time, in his good-pleasure, In the evening, cometh Weeping to lodge, But, by the morning,’tis a Shout of Triumph!
Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, bali upendo wake hudumu siku zote. Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, lakini asubuhi kukawa na furaha.
6 But, I, said, in my tranquility, I shall not be shaken to times age-abiding!
Nilipofanikiwa nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
7 O Yahweh, in thy good-pleasure, hadst thou caused my mountain to stand, strong, —Thou didst hide thy face—I was dismayed!
Ee Bwana, uliponijalia, uliuimarisha mlima wangu, lakini ulipouficha uso wako nilifadhaika.
8 Unto thee, O Yahweh, do I cry, —and, unto My Lord, do I make supplication:
Kwako wewe, Ee Bwana, niliita, kwa Bwana niliomba rehema:
9 What profit in my blood? in my going down into the pit? Can dust praise thee? Can it declare thy faithfulness?
“Kuna faida gani katika kuangamia kwangu? Katika kushuka kwangu shimoni? Je, mavumbi yatakusifu? Je, yatatangaza uaminifu wako?
10 Hear, O Yahweh, and show me favour, O Yahweh! become thou a helper unto me.
Ee Bwana, unisikie na kunihurumia, Ee Bwana, uwe msaada wangu.”
11 Thou hast turned my lamentation, into a dance for me, —Thou hast torn off my sackcloth, and girded me with gladness:
Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe,
12 To the end that mine honour should make melody unto thee, and not be silent. O Yahweh, my God! Unto times age-abiding, will I praise thee.
ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.

< Psalms 30 >