< Psalms 17 >

1 A Prayer of David. Hear, O Yahweh, the right, Attend to my loud cry, Give ear unto my prayer, on lips that would not deceive:
Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
2 From before thee, let my sentence come forth, Thine eyes, behold with equity.
Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
3 Thou hast tested my heart, hast made inspection by night, hast refined me until thou couldst find nothing, Had I devised evil, my mouth should not have transgressed:
Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
4 As for the workings of men, By the word of thy lips, have, I, taken heed of the paths of the violent one.
Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
5 Thou hast held fast my goings on to thy ways, My footsteps have not been shaken:
Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
6 I, have called upon thee, for thou wilt answer me, O GOD, —Incline thine ear unto me, Hear thou my speech:
Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
7 Let thy lovingkindness be distinguished, thou Saviour of such as seek refuge from them who lift themselves up against thy right hand.
Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
8 Guard me, as the pupil of the eye, —Under the shadow of thy wings, wilt thou hide me:
Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
9 From the face of lawless ones who have treated me with violence, the foes of my soul, who come round against me:
kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
10 Their own fat [heart], have they shut up, —With their mouth, have they spoken proudly.
Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
11 As for our own goings, now, have they surrounded us, —Their eyes, they fix, bending to the earth:
Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
12 His likeness, is as a lion, that longeth to rend, and as a young lion, lurking in secret places.
Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
13 Rise, Yahweh! Confront his face, Bring him down, Deliver my soul from the lawless one [who is] thy sword:
Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
14 From men [who are] thy hand, O Yahweh, From the men of this age, whose portion, is among the living, and, with thy treasure, thou fillest their bosom, —They must be satisfied with sons, And must leave their abundance to their children: —
Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
15 I, in righteousness, shall behold thy face, Shall be satisfied when awakened by a vision of thee.
Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.

< Psalms 17 >