< Psalms 113 >

1 Praise ye Yah! Praise, O ye servants of Yahweh, Praise the Name of Yahweh;
Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
2 Be the Name of Yahweh blessed, henceforth, even to times age-abiding.
Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
3 From the rising of the sun unto the going in thereof, Worthy to be praised, is the Name of Yahweh:
Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
4 High above all nations, is Yahweh, Above the heavens, his glory.
Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
5 Who is like Yahweh our God? that goeth on high to dwell,
Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
6 That cometh down low to look, through the heavens and through the earth;
ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
7 That raiseth, out of the dust, the poor, From the dunghill, uplifteth the needy;
Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
8 To give a seat with nobles, with the nobles of his people!
huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
9 Causing the barren woman to dwell in a household, A mother of sons in her joy! Praise ye Yah.
Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.

< Psalms 113 >