< Psalms 104 >

1 Bless, O my soul, Yahweh, —Yahweh, my God, thou art exceedingly great, With honour and majesty, hast thou clothed thyself,
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
2 Putting on light, as a robe, Stretching out the heavens, as a curtain;
Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
3 Building, in the waters, his upper chambers, —Who maketh clouds his chariot, Who passeth along on the wings of the wind;
na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
4 Making His messengers, winds, His attendants, a flaming fire;
Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
5 He hath fixed the earth on its foundations, It is not to be shaken, to times age-abiding and beyond.
Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
6 With the resounding deep—as a garment, hast thou covered it, Above the mountains, stand the waters;
Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
7 At thy rebuke, they flee, At the voice of thy thunder, they hurry away;
Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
8 Mountains rise, Valleys sink, Unto the place which thou hast fixed for them;
yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
9 Bounds, hast thou set, which they are not to pass over, They are not to return to cover the earth.
Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
10 Who hast sent forth springs, through the torrent-beds, Between the mountains, they flow along;
Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
11 They give drink, to every wild beast of the field, The wild asses do break their thirst.
Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
12 Over them, the bird of the heavens settleth down, From amidst the foliage, they utter a voice.
Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
13 Who watereth the mountains out of his upper chambers, Out of the fruit of thy works, thou satisfiest the earth.
Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
14 Who causeth the grass to shoot forth for the cattle, And the herb, for the service of man, That he may bring forth food out of the earth;
Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
15 And, wine, may rejoice the heart of man, Making radiant his well-nourished face, —And, food, may, the heart of man, sustain.
divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
16 Satisfied are, The trees of Yahweh, The cedars of Lebanon, which he hath planted;
Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
17 Where the birds build their nests, The stork, in the fir-trees, hath her house;
Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
18 The high mountains, are for the chamois, The crags, are a refuge for the conies.
Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
19 He hath made the moon for seasons, And, the sun, knoweth his place for entering in.
Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
20 Thou causest darkness, and it becometh night, Therein, creepeth forth, Every wild beast of the forest;
Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
21 The young lions, roaring for prey, And seeking, from GOD, their food.
Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
22 The sun ariseth, they withdraw themselves, And, in their lairs, lay them down.
Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
23 Man goeth forth to his work, And to his labour, until evening.
Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
24 How thy works abound, O Yahweh! All of them—in wisdom, hast thou made, The earth is full of thy possession: —
Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
25 This sea here, is great and broad on both hands, —Wherein are creeping things, even without number, Living things, small with great;
Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
26 There, ships, sail along, This sea-monster, thou hast formed to sport therein;
Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
27 All of them, for thee, do wait, That thou mayest give them their food in its season;
Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
28 Thou givest unto them, they gather, Thou openest thy hand, they are satisfied with good.
Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
29 Thou hidest thy face, they are dismayed, Thou withdrawest their spirit, They cease to breathe, And, unto their own dust, do they return:
Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
30 Thou sendest forth thy spirit, they are created, And thou renewest the face of the ground.
Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
31 Be thy glory, O Yahweh, to times age-abiding, Let Yahweh rejoice in his own works:
Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
32 Who looketh at the earth, and it trembleth, He toucheth the mountains, and they smoke.
yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
33 I will sing to Yahweh, as long as I live! Yea I will touch the strings to my God, while I continue;
Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
34 Pleasing unto him, be my (meditation) I, will rejoice in Yahweh.
Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
35 Sinners shall be consumed out of the earth And, the lawless, no more, shall exist, —Bless, O my soul, Yahweh, Praise ye Yah!
Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.

< Psalms 104 >