< Proverbs 10 >

1 The Proverbs of Solomon: A wise son, maketh a glad father, but, a foolish son, is the grief of his mother.
Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
2 The treasures of lawlessness, do not profit, but, righteousness, delivereth from death.
Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
3 Yahweh, suffereth not to famish, the soul of the righteous, but, the desire of the lawless, he thrusteth away.
Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
4 He becometh poor, who dealeth with a slack hand, but, the hand of the diligent, maketh rich.
Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
5 He that gathereth in summer, is a prudent son, he that sleepeth long in harvest, is a son causing shame.
Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
6 Blessings, are for the head of the righteous man, but, the mouth of the lawless, covereth up wrong.
Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
7 The memory of the righteous, yieldeth blessing, but, the name of the lawless, dieth out.
Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
8 The wise in heart, will accept commandments, but, he that is foolish with his lips, shall be thrust away.
Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
9 He that walketh uprightly, may walk securely, but, he that maketh crooked his ways, shall be found out.
Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
10 He that winketh with the eye, causeth sorrow, and, he that is foolish with his lips, shall be thrust aside.
Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
11 A well-spring of life, is the mouth of the righteous, but, the mouth of the lawless, covereth wrong.
Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
12 Hatred, stirreth up strifes, but, over all transgressions, love throweth a covering.
Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
13 In the lips of the intelligent, is found wisdom, but, a rod, is for the back of him that lacketh sense.
Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
14 Wise men, treasure up knowledge, but, the mouth of the foolish, is a terror near at hand.
Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
15 The substance of the rich, is his strong city, the terror of the poor, is their poverty.
Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
16 The labour of the righteous, [leadeth] to life, the increase of the lawless, to sin.
Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
17 On the way to life, is he that heedeth correction, but, he that hateth reproof, is going astray.
Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
18 He that concealeth hatred, hath false lips, and he that sendeth forth slander, the same, is a dullard.
Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
19 In the multitude of words, there wanteth not transgression, but, he that restraineth his lips, sheweth prudence.
Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
20 Choice silver, is the tongue of the righteous, but, the sense of the lawless, is very small.
Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
21 The lips of the righteous, feed multitudes, but, the foolish, for lack of sense, shall die.
Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
22 The blessing of Yahweh, itself maketh rich, and he addeth no grievance therewith.
Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
23 It is, mere sport to a stupid man, to commit lewdness, but, wisdom, pertaineth to a man of understanding.
Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
24 The dread of the lawless one, the same, shall overtake him, but, the desire of the righteous, shall he granted.
Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
25 Like the passing away of a tempest, so the lawless one is not, but, the righteous, [hath] an age-abiding foundation.
Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
26 As vinegar to the teeth, and as smoke to the eyes, so, is the sluggard, to them who send him.
Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
27 The reverence of Yahweh, addeth days, but, the years of the lawless, shall be shortened.
Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
28 The hope of the righteous, shall be gladness, but, the expectation of the lawless, shall vanish.
Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
29 A refuge for the blameless, is the path of Yahweh, but, destruction, [awaiteth] the workers of iniquity.
Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
30 The righteous, to times age-abiding, shall remain unshaken, but, the lawless, shall not inhabit the earth.
Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
31 The mouth of the righteous, beareth the fruit of wisdom, but, a perverse tongue, shall be cut off.
Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
32 The lips of the righteous, know what is pleasing, but, the mouth of the lawless, [speaketh] perversities.
Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.

< Proverbs 10 >