< Numbers 9 >

1 And Yahweh spake unto Moses in the desert of Sinai, in the second year by their coming forth out of the land of Egypt in the first month, saying:
Bwana akasema na Mose katika Jangwa la Sinai katika mwezi wa kwanza wa mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka Misri. Akasema,
2 Let the sons of Israel therefore, keep the passover in its appointed season:
“Waamuru Waisraeli waadhimishe Pasaka katika wakati ulioamriwa.
3 on the fourteenth day of this month between the two evenings, shall ye keep it, in its appointed season, —according to all the statute thereof and according to all the regulations thereof, shall ye keep it.
Adhimisheni wakati ulioamriwa, yaani wakati wa kuzama jua siku ya kumi na nne ya mwezi huu, kufuatana na desturi zake zote na masharti yake.”
4 Then spake Moses unto the sons of Israel that they should keep the passover.
Hivyo Mose akawaambia Waisraeli waiadhimishe Pasaka,
5 So they kept the passover in the first [month], on the fourteenth day of the month between the two evenings, in the desert of Sinai, —according to all that Yahweh commanded Moses, so, did the sons of Israel.
nao wakafanya hivyo kwenye Jangwa la Sinai wakati wa kuzama jua siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza. Waisraeli wakafanya kila kitu kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
6 But so it was that there were, certain men who had become unclean by a dead person, and could not keep the passover on that day, —therefore came they near before Moses and before Aaron on that day.
Lakini baadhi yao hawakuweza kuadhimisha Pasaka siku ile kwa sababu walikuwa najisi kwa taratibu za kiibada kwa ajili ya kugusa maiti. Kwa hiyo wakamwendea Mose na Aroni siku ile ile,
7 Then said those men unto him, We, are unclean by a dead person, —wherefore should we become of less esteem for want of offering the oblation of Yahweh in its appointed season, in the midst of the sons of Israel?
wakamwambia Mose, “Tumekuwa najisi kwa sababu tumegusa maiti, lakini kwa nini tuzuiliwe kumtolea Bwana sadaka yake pamoja na Waisraeli wengine katika wakati ulioamriwa?”
8 And Moses said unto them, —Stay, and let me hear, what Yahweh shall command concerning you!
Mose akawajibu, “Ngojeni mpaka nitafute kile Bwana anachoagiza kuwahusu ninyi.”
9 Then spake Yahweh unto Moses, saying:
Ndipo Bwana akamwambia Mose,
10 Speak unto the sons of Israel, saying, —Though, any man, be unclean by a dead person or be on a journey afar off, whether in the case of yourselves or of your generations, yet shall he keep a passover unto Yahweh.
“Waambie Waisraeli: ‘Wakati mmoja wenu au wazao wenu wanapokuwa najisi kwa sababu ya maiti au wakiwa safarini, hata hivyo wanaweza kuadhimisha Pasaka ya Bwana.
11 In the second month, on the fourteenth day between the two evenings, shall they keep it, —with unleavened cakes and bitter herbs, shall they eat it.
Wataiadhimisha wakati wa kuzama jua siku ya kumi na nne ya mwezi wa pili. Watamla mwana-kondoo, pamoja na mkate usiotiwa chachu, na mboga chungu.
12 They shall not leave thereof until morning, and no bone, shall they break therein—according to all the statutes of the passover, shall they keep it.
Wasibakize chochote hadi asubuhi wala wasivunje mifupa ya mwana-kondoo. Wakati wanapoadhimisha Pasaka, hawana budi kufuata masharti yote.
13 But as for the man who is, clean, and no a journey, doth not chance to be and yet faileth to keep the passover, that person shall he cut off from among his kinsfolk, —for the oblation of Yahweh, hath he not offered in its appointed season, his own sin, shall, that man, bear.
Lakini kama mtu ni safi kwa taratibu za kiibada naye hayuko safarini, asipoadhimisha Pasaka, mtu huyo hana budi kukatiliwa mbali na watu wake kwa sababu hakutoa sadaka ya Bwana kwa wakati ulioamriwa. Mtu huyo atawajibika kubeba matokeo ya dhambi yake.
14 When moreover there may sojourn with you a sojourner, who would keep a passover unto Yahweh, according to the statute of the passover, and according to the regulation thereof, so, must he keep [it], —one statute, shall there be for you, both for the sojourner and for the native of the land.
“‘Mgeni anayeishi miongoni mwenu ambaye anataka kuadhimisha Pasaka ya Bwana, lazima afanye hivyo kwa kufuata desturi na masharti. Lazima masharti yawe sawasawa kwa mgeni na mzawa.’”
15 Now, on the day the habitation was reared, the cloud covered the habitation, even the tent of the testimony, —and in the evening, it was over the habitation, like an appearance of fire, until morning,
Katika siku hiyo ambayo Maskani, Hema la Ushuhuda, iliposimamishwa, wingu liliifunika. Kuanzia jioni mpaka asubuhi wingu lililokuwa juu ya Maskani lilionekana kama moto.
16 Thus, came it to pass continually, the cloud, covered it, —and an appearance of fire, by night;
Hivyo ndivyo lilivyoendelea kuwa; wingu liliifunika wakati wa mchana, na usiku lilionekana kama moto.
17 but at the bidding of the upgoings of the cloud from off the tent, then, after that, the sons of Israel set forward, —and in the place where the cloud abode, there the sons of Israel encamped:
Wakati wowote wingu lilipoinuka kutoka juu ya Hema, nao Waisraeli waliondoka; mahali popote wingu liliposimama, Waisraeli walipiga kambi.
18 at the bidding of Yahweh, the sons of Israel set forward, and at the bidding of Yahweh, they encamped, —all the days that the cloud abode upon the habitation, they remained encamped.
Kwa amri ya Bwana Waisraeli waliondoka, na kwa amri yake walipiga kambi. Kwa muda wote wingu liliposimama juu ya Maskani, Waisraeli walibaki wamepiga kambi.
19 And when the cloud lengthened out its stay upon the habitation, many days, then would the sons of Israel keep the watch of Yahweh, and would not set forward.
Wakati wingu lilipobaki juu ya Maskani kwa muda mrefu, Waisraeli walitii amri ya Bwana nao hawakuondoka.
20 And, so it was, when the cloud would be a few days upon the habitation, at the bidding of Yahweh, they remained encamped, and at the bidding of Yahweh, they set forward.
Wakati mwingine wingu lilikuwa juu ya Maskani kwa siku chache tu; kwa amri ya Bwana wangelipiga kambi na kisha kwa amri yake wangeliondoka.
21 And, so it was, when the cloud would be from evening until morning, as soon as the cloud went up in the morning, so soon did they set forward: whether by day or by night, as soon as the cloud went up, so soon did they set forward.
Wakati mwingine wingu lilikuwepo kuanzia jioni mpaka asubuhi tu, na lilipoinuka asubuhi, nao waliondoka. Ikiwa ni mchana au usiku, wakati wowote wingu lilipoinuka, waliondoka.
22 Whether for two days or a month or a year, the cloud lengthened out its stay upon the habitation abiding thereupon, the sons of Israel remained encamped and set not forward, —but at the upgoings thereof, they set forward.
Ikiwa wingu lilikaa juu ya Maskani kwa siku mbili au mwezi au mwaka, Waisraeli wangebaki wamepiga kambi na hawakuondoka; lakini lilipoinuka, wangeondoka.
23 At the bidding of Yahweh, they encamped, and at the bidding of Yahweh, they set forward, —the watch of Yahweh, they kept, at the bidding of Yahweh by the hand of Moses.
Kwa amri ya Bwana walipiga kambi, na kwa amri ya Bwana waliondoka. Walitii amri ya Bwana, kufuatana na agizo lake kupitia Mose.

< Numbers 9 >