< Numbers 27 >

1 Then came near the daughters of Zelophehad, son of Hepher, son of Gilead son of Machir son of Manasseh pertaining to the families of Manasseh, son of Joseph, —these being the names of his daughters, Mahlah Noah and Hoglah and Milcah, and Tirzah.
Binti za Selofehadi mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase, walikuwa wa koo za Manase mwana wa Yosefu. Majina ya hao binti yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa. Walikaribia
2 So they stood before Moses and before Eleazar the priest, and before the princes, and all the assembly, —at the entrance of the tent of meeting, saying:
ingilio la Hema la Kukutania na kusimama mbele ya Mose, kuhani Eleazari, viongozi na kusanyiko lote, wakasema,
3 Our father, died in the desert, although, he, was not among the assembly that conspired against Yahweh, in the assembly of Korah, —but, in his own sin, died he; and sons, had he none.
“Baba yetu alikufa jangwani. Hakuwa miongoni mwa wafuasi wa Kora, ambao walifungamana pamoja dhidi ya Bwana, lakini alikufa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe na hakuacha wana.
4 Wherefore should the name of our father be withdrawn out of the midst of his family, because he had no son? Give ye unto us a possession, in the midst of the brethren of our father.
Kwa nini jina la baba yetu lifutike kutoka ukoo wake kwa sababu hakuwa na mwana? Tupatie milki miongoni mwa ndugu za baba yetu.”
5 And Moses brought near their cause before Yahweh.
Kwa hiyo Mose akalileta shauri lao mbele za Bwana,
6 Then spake Yahweh unto Moses, saying:
naye Bwana akamwambia Mose,
7 A right thing, are the daughters of Zelophehad speaking: Thou shalt, surely give, them a possession for an inheritance, in the midst of the brethren of their father, —and shalt cause the inheritance of their father to pass over unto them.
“Wanachosema binti za Selofehadi ni sawa. Ni lazima kwa hakika uwape milki kama urithi miongoni mwa ndugu za baba yao, na kubadili urithi wa baba yao uwe wao.
8 And unto the sons of Israel, shalt thou speak, saying, —When, any man, shall die, having no son, then shall ye cause his inheritance to pass over to his daughter.
“Waambie Waisraeli, ‘Ikiwa mtu atakufa naye hakuacha mwana, utampa binti yake urithi wake.
9 And, if he hath no daughter, then shall ye give his inheritance unto his, brethren.
Ikiwa hana binti, wape ndugu zake wa kiume urithi wake.
10 And if he hath no brethren, then shall ye give his inheritance unto the brethren of his father.
Ikiwa hana ndugu wa kiume toa urithi wake kwa ndugu za baba yake.
11 And, if his father hath no brethren, then shall ye give his inheritance unto his blood-relation that is near unto him of his family, and he shall possess it, —So shall it serve the sons of Israel as a regulative statute, As Yahweh commanded Moses.
Ikiwa baba yake hakuwa na ndugu wa kiume, toa urithi wake kwa ndugu wa karibu katika ukoo wake, ili aumiliki. Hili litakuwa dai la sheria kwa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru Mose.’”
12 And Yahweh said unto Moses, Go up into this mount of Abarim, —and see, the land which I have given unto the sons of Israel;
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Panda juu ya mlima huu katika kilele cha Abarimu uione nchi ambayo nimewapa Waisraeli.
13 And, when thou hast seen it, then shalt thou also be withdrawn unto thy kinsfolk, —as Aaron thy brother was withdrawn;
Baada ya kuiona, wewe pia utakusanywa pamoja na watu wako kama ndugu yako Aroni alivyokusanywa,
14 because ye resisted my bidding—in the desert of Zin when the assembly contended, —that ye should hallow me regarding the waters, before their eyes, —the same, were the waters of Meribah, of Kadesh in the desert of Zin.
kwa kuwa jumuiya ilipoasi amri yangu kwenye maji katika Jangwa la Sini, wakati jumuiya ilipogombana nami, nyote wawili mliacha kuitii amri yangu ya kuniheshimu kama mtakatifu mbele ya macho yao.” (Haya yalikuwa maji ya Meriba huko Kadeshi, katika Jangwa la Sini.)
15 Then spake Moses unto Yahweh saying:
Mose akamwambia Bwana,
16 Let Yahweh, God of the spirits of all flesh, appoint a man over the assembly;
“Bwana, Mungu wa roho zote za wanadamu, na amteue mtu juu ya jumuiya hii
17 who may go out before them and who may come in before them, and who may take them out and who may bring them in, —that the assembly of Yahweh become not as sheep that have no shepherd.
ili atoke na kuingia mbele yao, atakayewaongoza katika kutoka kwao na kuingia kwao, ili watu wa Bwana wasiwe kama kondoo wasio na mchungaji.”
18 And Yahweh said unto Moses: Take thee Joshua son of Nun, a man in whom is spirit, —then shalt thou lean thy hand upon him;
Kwa hiyo Bwana akamwambia Mose, “Mchukue Yoshua mwana wa Nuni, mtu ambaye Roho yuko ndani yake, uweke mkono juu yake.
19 and shalt cause him to stand before Eleazar the priest, and before all the assembly, —and shalt charge him before their eyes;
Msimamishe mbele ya kuhani Eleazari pamoja na kusanyiko lote, umpe maagizo mbele yao.
20 and shalt put some of thine honour upon him, —that all the assembly of the sons of Israel may hearken.
Mpe sehemu ya mamlaka yako ili jumuiya yote ya Waisraeli ipate kumtii.
21 And, before Eleazar the priest, shall he stand, and shall ask by him for the decision of the Lights, before Yahweh, —at the bidding thereof, shall they go out, and at the bidding thereof, shall they come in—he, and all the sons of Israel with him, even all the assembly.
Atasimama mbele ya kuhani Eleazari, ambaye atapokea maamuzi kwa ajili yake, kwa kuuliza mbele za Bwana kwa ile Urimu. Kwa amri yake, yeye na jumuiya yote ya Waisraeli watatoka, na kwa amri yake, wataingia.”
22 And Moses did as Yahweh commanded him, —and took Joshua, and caused him to stand before Eleazar the priest, and before all the assembly;
Mose akafanya kama Bwana alivyomwagiza. Akamtwaa Yoshua na kumsimamisha mbele ya kuhani Eleazari na kusanyiko lote.
23 and leaned his hands upon him and charged him, —As Yahweh spake by the hand of Moses.
Kisha akaweka mikono yake juu ya kichwa cha Yoshua na kumpa maagizo, kama vile Bwana alivyoelekeza kupitia kwa Mose.

< Numbers 27 >