< Numbers 1 >

1 Then spake Yahweh unto Moses in the desert of Sinai in the tent of meeting, —on the first of the second month in the second year by their coming forth out of the land of Egypt saying:
Mungu alimwambia Musa katika hema ya kukutania walipokuwa katika jangwa la Sinai. Hii ilitokea katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili miaka miwili baadaya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Mungu alisema,
2 Reckon ye up the sum of all the assembly of the sons of Israel, by their families by their ancestral houses, —in the counting of names, every male, by their polls;
'fanya sensa ya wanaume wote wa Israel kutoka kila ukoo, katika familia za baba zao. Wahesabu kwa majina, wahesabu kila mume, kila mwanamume
3 from twenty years old and upwards, every one able to go forth to war in Israel, —ye shall number them by their hosts, thou and Aaron;
kuanzia umri a miaka ishirini na zaidi. Uwahesabu wote wanaoweza kupigana kama askari wa Israel. Wewe na Haruni mtaandika idadi ya wanaume katika makundi ya majeshi yao.
4 and with you, shall be one man for each tribe, —each man, head of his ancestral house, shall be.
Kila mwanamume kwa kila kabila, kichwa cha ukoo, lazima atumike na wewe kama kiongozi wa kabila.
5 These, then, are the names of the men who shall stand with you, —Of Reuben, Elizur, son of Shedeur;
Haya ndiyo majina ya viongozi ambao watapigana pamoja na wewe: Kutoka kabila la Reubeni, Elizuri mwana wa Shedeuri;
6 Of Simeon, Shelumiel son of Zurishaddai;
kutoka kabila la Simeoni, Shelumiel mwana wa Zurishadai
7 Of Judah, Nahshon, son of Amminadab;
Kutoka kabila la Yuda, Nashoni mwana wa Aminadabu;
8 Of Issachar, Nethanel, son of Zuar;
Ktoka kabila la Isakari, Nethaneli mwana wa Zuari;
9 Of Zebulun, Eliab, son of Helon;
kutoka kabila Zebuluni, Eliabu mwana wa Heloni
10 Of the sons of Joseph, —Of Ephraim, Elishama son of Ammihud; Of Manasseh, Gamaliel, son of Pedahzur;
kutoka kabila la Efraimu mwana wa Yusufu, Elishama mwana wa Ammihudi; kutoka kabila la Manase, Gamaliel mwan wa Pedazuri;
11 Of Benjamin, Abidan son of Gideoni;
kutoka kabila la Benjamini mwana wa Ysufu, Abidani mwan wa Gidion;
12 Of Dan, Ahiezer son of Ammishaddai;
Kutoka kabila la Dan, Ahizeri mwana wa Amishadai;
13 Of Asher, Pagiel, son of Ochran;
kutoka kabila Asheri, Pagieli mwana wa Okirani;
14 Of Gad, Eliasaph son of Deuel;
kutoka kabila la Gadi, Eliasafu mwana wa Deuli;
15 Of Naphtali, Ahira son of Enan.
na kutoka kabila la Naftali, Ahira mwana wa Enani.”
16 These, are they who had been summoned by the assembly, being princes of the tribes of their fathers, —heads of the thousands of Israel.
Hawa ndio wanaume waliochaguliwa kutoka kwa watu. Waliongoza kabila za mababu zao. Walikuwa viongozi wa koo katika Israel.
17 So then Moses and Aaron took these men, who were distinguished by name;
Musa na Haruni wakawachukua wale wanaume, waliokuwa wameandikwa kwa majina,
18 all the assembly also, called they together on the first of the second month, —and they declared their pedigree according to their families by their ancestral houses, —in the counting of names from twenty years old and upwards by their polls.
na pamoja na wanaume hao waliwakusanya wanume wote katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Kisha kila mwanume wa miaka ishirini na zaidi alitambua babu zake. Alitakiwa kutaja koo na famila kutoka katika ukoo.
19 As Yahweh commanded Moses, so he mustered them in the desert of Sinai.
Kisha Musa akaandika hesabu yao huko katika nyika ya Sinai, Kama Mungu alivyokuwa amemwamuru kufanya.
20 And they were [as followeth] —The sons of Reuben, the firstborn of Israel, in their pedigrees—by their families, by their ancestral houses, in the counting of names, by their polls, every male, from twenty years old and upwards, every one able to go forth to war;
Kutoka uzao wa Reubeni, mtoto wa kwanza wa Israel, yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini na zaidi wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka hesabu ya ukoo na familia.
21 such as were numbered of them as belonging to the tribe of Reuben, forty-six thousand and five hundred.
Waliwahesabu wanaume 46, 000 kutoka ukoo wa Reubeni.
22 Of the sons of Simeon, in their pedigrees by their families by their ancestral houses, —such as were numbered of him, in the counting of names by their polls, every male from twenty years old and upwards, every one able to go forth to war;
Kutoka uzao wa Simeoni yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini na zaidi au wenye uwezo wa kwenda vitani, kutokana na hesabu ya ukoo na familia.
23 such as were numbered of them as belonging to the tribe of Simeon, fifty-nine thousand and three hundred.
Walihesabu wanaume 59, 300 kutoka kabila la Simeoni.
24 Of the sons of Gad, in their pedigrees—by their families by their ancestral houses, in the counting of names from twenty years old and upwards, every one able to go forth to war:
Kutoka uzao wa Gadi yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
25 such as were numbered of them as belonging to the tribe of Gad, forty-five thousand and six hundred and fifty.
Walihesabu wanaume 45, 650 kutoka kabila la Gadi.
26 Of the sons of Judah, in their pedigrees by their families by their ancestral houses, —in the counting of names, from twenty years old and upwards, every one able to go forth to war;
Kutoka uzao wa Yuda yalihesabiwa majina yote ya wanaume wenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
27 such as were numbered of them as belonging to the tribe of Judah, seventy-four thousand and six hundred.
walihesabiwa wanume 74, 000 kutoka kabila la Yuda.
28 Of the sons of Issachar, in their pedigrees—by their families by their ancestral houses, —in the counting of names, from twenty year old and upwards, every one able to go forth to war;
Kutoka uzao wa Isakari yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
29 such as were numbered of them as belonging to the tribe of Issachar, fifty-four thousand and four hundred.
Walihesabiwa wanaume 54, 000 kutoka kabila la Isakari.
30 Of the sons of Zebulun, in their pedigrees—by their families by their ancestral houses, —in the counting of names from twenty years old and upwards, every one able to go forth to war;
Kutoka uzao wa Zabuloni yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
31 such as were numbered of them as belonging to the tribe of Zebulun, fifty-seven thousand and four hundred.
Walihesabiwa wanume 57, 400 kutoka kabila la Zabuloni.
32 Of the sons of Joseph—Of the sons of Ephraim, in their pedigrees—by their families by their ancestral houses, —in the counting of names, from twenty years old, and upwards, every one able to go forth to war;
Kutoka uzao wa Efraimu mwana wa Yusufu yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
33 such as were numbered of them, as belonging to the tribe of Ephraim, forty thousand and five hundred.
Walihesabiwa wanaume 40, 500 kutoka kabila la Efraimu.
34 Of the sons of Manasseh, in their pedigrees—by their families by their ancestral houses, —in the counting of names from twenty years old and upwards, every one able to go forth to war;
Kutoka uzao wa Manase mwana wa Yusufu yaliheabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu y a ukoo na familia.
35 such as were numbered of them as belonging to the tribe of Manasseh, thirty-two thousand, and two hundred.
Walihesabiwa wanaume 32, 000 kutoka kabila la Manase.
36 Of the sons of Benjamin, in their pedigrees by their families, by their ancestral houses, —in the counting of names, from twenty years old, and upwards, every one able to go forth to war;
Kutoka uzao wa Benjamini yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
37 such as were numbered of them as belonging to the tribe of Benjamin, thirty-five thousand and four hundred.
Walihesabiwa wanaume 35, 000 kutoka kabila la Benjamini.
38 Of the sons of Dan, in their pedigrees by their families by their ancestral houses, in the counting of names from twenty years old and upwards, every one able to go forth to war;
Kutoka uzao wa Dani yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, Kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
39 such as were numbered of them as belonging to the tribe of Dan, sixty-two thousand, and seven hundred.
Walihesabiwa wanaume 62, 000 kutoka kabila la Dani.
40 Of the sons of Asher, in their pedigrees—by their families by their ancestral houses, —in the counting of names, from twenty years old, and upwards, every one able to go forth to war;
Kutoka uzao wa Asheri yalihesabiwa majina yote ya kila mwanume mwenye umri wa miaka ishirini au zadi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu y a ukoo na familia.
41 such as were numbered of them as belonging to the tribe of Asher, forty-one thousand, and five hundred.
Walihesabiwa wanaume 41, 500 kutoka ukoo wa Asheri.
42 The sons of Naphtali, in their pedigrees by their families by their ancestral houses, —in the counting of names, from twenty years old, and upwards, every one able to go forth to war;
Kutoka ukoo wa Naftali yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
43 such as were numbered of them, as belonging to the tribe of Naphtali, fifty-three thousand, and four hundred.
Walihesabiwa wanaume 53, 400 kutoka kabila la Naftari
44 These, are they who were numbered, whom Moses and Aaron and the twelve princes of Israel did number, the princes acting each one for his ancestral house.
Musa na Haruni waliwahesabu wanaume wote hawa, pamoja na wale wanaume kumi na wawili waliokuwa wakiongoza yale makabila kumi na mawili ya Israeli.
45 So then all they who were numbered of the sons of Israel by their ancestral houses, from twenty years old and upwards, every one able to go forth to war in Israel;
Kwa hiyo wanaume wote wa Israeli wenye umri wa miak ishirini au zaidi, wote wenye uwezo wa kwenda vitani, walihesabiwa kutoka kwenye familia zao.
46 so then all they who were numbered were six hundred and three thousand and five hundred and fifty.
Walihesabu wanaume 603, 550.
47 But the Levites by the tribe of their fathers were not numbered in their midst.
Lakini wanaume toka uzao wa Lawi hawakuhesabiwa,
48 For Yahweh spake unto Moses saying:
Kwa sababu BWANA alimwambia Musa,
49 Only the tribe of Levi, shalt thou not number, nor the sum of them, shalt thou reckon up, in the midst of the sons of Israel.
“usiwahesabu wale wa kabila la Lawi wala kuwajumuisha kwenye jumla ya watu wa Israeli.
50 But do, thou thyself, put the Levites in charge over the habitation of the testimony, and over all the furniture thereof and over all that pertaineth thereto, they, shall bear the habitation, and all the furniture thereof, and they, shall attend thereupon; and, round about the habitation, shall they encamp.
Badala yake, waagize Walawi kuliangalia hema la amri za agano, na kuangalia mapambo ya hema na vyote vilivyomo. Walawi watalazimika kulibeba hema na lazima wayabebe mapambo ya hema. Lazima waliangalie hema na kuyatengeneza mazingira yake. Wataiangalia masikani na kuzitengeneza kambi zinazolizunguka.
51 And, when the habitation is to set forward, the Levites shall take it down, and when the habitation is to be pitched, the Levites, shall set it up, but the stranger that draweth near, shall be put to death.
Kila hema litakapotakiwa kuhamishiwa eneo jingine, Walawi ndio watakaolipeleka pale. Na kila hema litakapotakiwa kusimamishwa, Walawi ndio watakao lisimamisha. Na mgeni yeyote atakayelisogelea hema lazima auawe.
52 So then the sons of Israel shall pitch their tents, every man, near his own camp, and, every man, near his own standard, by their hosts;
Wakati watu wa Israeli watakaposimamisha hema zao, kila mwanaume lazima awe karibu na bango la jeshi lake.
53 but the Levites, shall pitch their tents round about the habitation of the testimony, that there be no wrath upon the assembly of the sons of Israel, —so shall the Levites keep the watch of the habitation of the testimony.
Hata hivyo Walawi lazima waweke hema zao kuizunguka hiyo masikani ya amri za agano ili kwamba hasira yangu isije ikawaka juu ya wana wa Israeli. Walawi lazima wailinde hiyo masikani ya amri za agano.”
54 Thus did the sons of Israel, —according to all that Yahweh commanded Moses, so, did they.
Wana wa Israeli walifanya yote haya. Walifanya yote ambayo BWANA aliagiza kupitia Musa.

< Numbers 1 >