< Nehemiah 13 >

1 On that day, a portion, was read in the book of Moses, in the ears of the people, —and it was found written therein, that the Ammonite and the Moabite should not enter into the convocation of God, unto times age-abiding;
Siku hiyo walisoma Kitabu cha Musa katika masikio ya watu. Ilionekana imeandikwa ndani yake kwamba hakuna Mwamoni au Mmoabu anapaswa kuja katika kusanyiko la Mungu, milele.
2 because they met not the sons of Israel, with bread and with water, —but hired against them Balaam, to curse them, although our God turned the curse into a blessing.
Hii ilikuwa kwa sababu hawakuja kwa watu wa Israeli na mkate na maji, bali walikuwa wamemwajiri Balaamu kulaani Israeli. Hata hivyo, Mungu wetu aligeuza laana kuwa baraka.
3 So it came to pass, when they had heard the law, —that they separated all the mixed multitude from Israel.
Mara tu waliposikia sheria, waliwatenga Israeli toka kwa kila mgeni.
4 Now, before this, Eliashib the priest, who was set over a chamber of the house of God, was allied unto Tobiah;
Sasa kabla ya hapo Eliashibu kuhani akawekwa juu ya vyumba vya nyumba ya Mungu wetu. Alikuwa na uhusiano na Tobia.
5 so he prepared him a large chamber, where aforetime they used to lay the meal-offering, the frankincense, and the utensils, and the tithe of the corn, the new wine and the oil, in charge of the Levites, and the singers, and the doorkeepers, —and the heave-offerings for the priests.
Eliashibu alimuandalia Tobia chumba kikubwa, ambako hapo awali waliweka sadaka ya nafaka, uvumba, makala, na sehemu ya kumi ya nafaka, divai, na mafuta, ambazo ziliwekwa kwa ajili ya Walawi, waimbaji, walinzi wa mlango, na michango kwa makuhani.
6 But, throughout all this [time], was I not in Jerusalem, —for, in the thirty-second year of Artaxerxes king of Babylon, I came unto the king, and, at the end of certain days, obtained I leave of the king;
Lakini wakati huu wote sikuwepo Yerusalemu. Kwa mwaka wa thelathini na mbili wa Artashasta mfalme wa Babeli, nilikwenda kwa mfalme. Baada ya muda nikamwomba mfalme ruhusa ya kuondoka,
7 and came to Jerusalem, —and had intelligence of the wickedness which Eliashib had committed for Tobiah, in preparing for him a chamber, in the courts of the house of God;
na nikarudi Yerusalemu. Nikafahamu mabaya ambayo Eliashibu alikuwa amefanya kwa kumpa Tobia chumba cha kuhifadhi katika mahakama ya nyumba ya Mungu.
8 and it grieved me exceedingly, —and I cast forth all the household utensils of Tobiah, outside of the chamber.
Nilikuwa na hasira sana na nikatupa vitabu vya nyumba ya Tobia nje ya chumba cha kuhifadhi.
9 Then commanded I, and they purified the chambers, —and I put back there, the utensils of the house of God, the meal-offering and the frankincense.
Niliamuru kwamba watakase vituo vya kuhifadhi, nami nikarudisha ndani yao makala ya nyumba ya Mungu, sadaka ya nafaka, na uvumba.
10 Then came I to know, that, the portions of the Levites, had not been given [them], —so that the Levites and the singers, who had been doing the work, had fled every one to his field.
Niligundua kwamba sehemu zilizotolewa kwa ajili ya kuwapa Walawi hazikutolewa kwao, ili waweze kuondoka haraka hekaluni, kila mmoja kwenda shambani kwake, kama waimbaji waliofanya walivyoondoka.
11 Therefore contended I with the deputies, and said, Wherefore is the house of God, forsaken? So I gathered them together, and set them in their place.
Kwa hiyo nikawasiliana na maafisa na kusema, 'Kwa nini nyumba ya Mungu imeachwa?' Niliwakusanya pamoja na kuwaweka kwenye nafasi zao.
12 Then, all Judah, brought in the tithe of corn, and new wine, and oil, unto the treasuries;
Kisha Yuda wote wakaleta zaka ya nafaka, divai mpya, na mafuta kwenye vituo vya kuhifadhi.
13 and I made treasurers over the treasuries—Shelemiah the priest, and Zadok the scribe, and Pedaiah from among the Levites, and, next unto them, Hanan son of Zaccur, son of Mattaniah, —for faithful were they accounted, and it was [laid] upon them to distribute unto their brethren.
Nikawaweka kama watunza hazina juu ya hazina, Shelemia kuhani, na Sadoki mwandishi, na Walawi, Pedaya. Hanani, mwana wa Zakuri, mwana wa Matania, alikuwa na wafuasi wao, kwa sababu walihesabiwa kuwa waaminifu. Kazi yao ilikuwa kusambaza vifaa kwa washirika wao.
14 Remember me, O my God, concerning this, —and do not wipe out my lovingkindnesses, which I have done for the house of my God, and for those keeping charge thereof.
Nikumbuke, Ee Mungu wangu, juu ya hili, wala usiondoe matendo mema niliyoyatenda kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu na huduma zake.
15 In those days, saw I in Judah—some treading winepresses on the sabbath, and bringing in sheaves and lading asses, moreover also wine, grapes, and figs, and every kind of burden, which they were bringing into Jerusalem on the sabbath day, —so I protested against it, as a day for them to sell provisions.
Siku hizo nikaona watu wa Yuda waliokanyaga mvinyo siku ya Sabato, na kuleta makundi ya nafaka, na kuwapakia punda, na divai, na zabibu, na tini, na kila aina ya mizigo nzito, waliyoleta Yerusalemu siku ya Sabato. Nikashuhudia kuwa walikuwa wakiuza chakula siku hiyo.
16 And, men of Tyre, dwelt therein, who were bringing in fish—and every kind of ware for sale, —and were selling, on the sabbath, to the sons of Judah, and in Jerusalem;
Watu kutoka Tiro waliokaa Yerusalemu walileta samaki na kila aina ya bidhaa, na wakawauza siku ya Sabato kwa watu wa Yuda na katika mji!
17 so I contended with the nobles of Judah, —and said unto them, What is this wicked thing which, ye, are doing, and profaning the sabbath day?
Kisha nikawaambia viongozi wa Yuda, “Je! ni ubaya gani huu mnafanya, kuinajisi siku ya Sabato?
18 Was it not, thus, your fathers did, and our God brought upon us all this calamity, and upon this city?—and, ye, would add indignation against Israel, by profaning the sabbath!
Je! Baba zenu hawakufanya hivyo? Je, Mungu wetu hakuleta mabaya haya juu yetu na juu ya mji huu? Sasa unaleta ghadhabu zaidi juu ya Israeli kwa kudharau Sabato.”
19 And it came to pass, when the gates of Jerusalem made a shadow before the sabbath, then gave I word, and they shut the doors, and I gave word, that they should not open them, until after the sabbath, —and, some of my young men, set I near the gates, so that no burden should be brought in, on the sabbath day.
Mara ilipokuwa giza kwenye milango ya Yerusalemu kabla ya Sabato, niliamuru milango ifungwe na kwamba haifai kufunguliwa hadi baada ya Sabato. Niliwaweka baadhi ya watumishi wangu kwenye malango ili mzigo wowote usiweze kuletwa siku ya Sabato.
20 But the traders and sellers of all kinds of wares lodged outside Jerusalem once or twice.
Wafanyabiashara na wauzaji wa kila aina ya bidhaa walikimbia nje ya Yerusalemu mara moja au mbili.
21 Therefore I testified against them, and said unto them, Wherefore are ye lodging against the wall? if ye do it again, a hand, will I thrust upon you, —From that time, they came not on the sabbath.
Lakini niliwaonya, “Mbona mnakaa nje ya ukuta? Ikiwa mtafanya hivyo tena, nitakuweka mikononi!” Kutoka wakati huo hawakuja siku ya sabato.
22 And I gave word to the Levites, that they should be purifying themselves and coming in, as keepers of the gates, to hallow the sabbath day. This also, remember to me, O my God, and have pity upon me, according to the abundance of thy lovingkindness.
Nikawaamuru Walawi kujitakasa, na kuja kulinda milango, ili kutakasa siku ya Sabato. Nikumbuke kwa hili pia, Mungu wangu, na kunipatia huruma kwa sababu ya uaminifu wa agano ulilonalo kwangu.
23 Moreover, in these days, saw I the Jews who had married women of Ashdod, of Ammon, of Moab;
Katika siku hizo niliona Wayahudi waliokuwa wameoa wanawake wa Ashdodi, Amoni na Moabu.
24 and, their children, were one-half speaking the language of Ashdod, and understood not how to speak the language of the Jews, —but after the tongue of both people.
Nusu ya watoto wao walizungumza lugha ya Ashdodi, lakini hawakuweza kuzungumza lugha ya Yuda, lakini lugha ya mmoja wa watu wengine.
25 So I contended with them, and laid a curse upon them, and I smote, from among them, certain men, and pulled out their hair, —and I put them on oath by God, Ye shall not give your daughters unto their sons, nor take of their daughters, for your sons nor for yourselves.
Nami nikawasiliana nao, na mimi niliwaadhibu, na nikawapiga baadhi yao na kuvuta nywele zao. Naliwaapisha kwa Mungu, nikisema, Msiwape wana wao binti zenu, wala msiwachukue binti zao kwa ajili ya wana wenu, wala ninyi wenyewe.
26 Was it not, over these things, that Solomon king of Israel sinned—though, among many nations, there was no king such as he, and he was, beloved by his God, and so God gave him to be king over all Israel, —even him, did foreign women, cause to sin.
Je, Sulemani mfalme wa Israeli hakufanya dhambi kwa sababu ya wanawake hawa? Miongoni mwa mataifa mengi hapakuwa na mfalme kama yeye, na alipendwa na Mungu wake. Mungu akamfanya awe mfalme juu ya Israeli wote. Hata hivyo, wake zake wa kigeni walimfanya atende dhambi.
27 Unto you, then, shall we hearken, to do all this great wickedness, to act unfaithfully with our God, —by marrying foreign wives?
Je, tunapaswa kukusikiliza na kufanya uovu huu hata kumhalifu Mungu wetu na kuwaoa wanawake wageni?
28 And, one of the sons of Joiada, son of Eliashib the high priest, was son-in-law to Sanballat the Horonite, —therefore I chased him from me.
Mmoja wa wana wa Yoyada, mwana wa Eliashibu, kuhani mkuu, alikuwa mkwewe na Sanbalati Mhoroni. Kwa hiyo nilimondoa kutoka mbele yangu.
29 Remember them, O my God, —on account of the Defilings of the Priesthood, and the Covenant of the Priesthood, and of the Levites.
Wakukumbushe, Mungu wangu, kwa sababu wameunajisi ukuhani, na agano la ukuhani na Walawi.
30 So I purified them from everything foreign, —and appointed charges unto the priests and unto the Levites, every one in his work;
Kwa hiyo nimewatakasa kutoka kila kitu kigeni, na kuimarisha kazi za makuhani na Walawi, kila mmoja kwa kazi yake mwenyewe.
31 also for the offering of wood, at times appointed, and for the firstfruits. Remember me, O my God, for good!
Nilitoa sadaka za kuni wakati uliowekwa na matunda ya kwanza. Nikumbuke, Mungu wangu, kwa mema.

< Nehemiah 13 >