< Nehemiah 11 >

1 And the rulers of the people dwelt in Jerusalem, —and, the rest of the people, cast lots, to bring in one out of ten to dwell in Jerusalem, the holy city, and nine parts in [other] cities.
Basi viongozi wa watu walikaa Yerusalemu, nao watu wale wengine walipiga kura ili kuleta mtu mmoja kati ya watu kumi aje kuishi Yerusalemu, mji mtakatifu, nao wengine tisa waliobaki wakae katika miji yao wenyewe.
2 And the people bestowed a blessing on all the men, who willingly offered themselves to dwell in Jerusalem.
Watu waliwasifu wale wote waliojitolea kuishi Yerusalemu.
3 Now, these, are the chiefs of the province, who dwelt in Jerusalem, but, in the cities of Judah, dwelt every man in his possession throughout their cities, Israel, the priests, and the Levites and the Nethinim, and the Sons of the Servants of Solomon.
Hawa ndio viongozi wa majimbo waliokuja kuishi Yerusalemu (baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi, watumishi wa Hekalu, na wazao wa watumishi wa Solomoni waliendelea kuishi katika miji ya Yuda, kila mmoja katika milki yake mwenyewe katika miji mbalimbali,
4 And, in Jerusalem, dwelt certain of the sons of Judah and of the sons of Benjamin, —Of the sons of Judah, Athaiah son of Uzziah, son of Zechariah, son of Amariah, son of Shephatiah, son of Mahalalel, of the sons of Perez;
ambapo watu wengine kutoka Yuda na Benyamini waliishi Yerusalemu). Kutoka wazao wa Yuda: Athaya mwana wa Uzia, mwana wa Zekaria, mwana wa Amaria, mwana wa Shefatia, mwana wa Mahalaleli, mzao wa Peresi.
5 and Maaseiah son of Baruch, son of Col-hozeh, son of Hazaiah, son of Adaiah, son of Joiarib, son of Zechariah, son of the Shilonite.
Naye Maaseya mwana wa Baruku, mwana wa Kolhoze, mwana wa Hazaya, mwana wa Adaya, mwana wa Yoyaribu, mwana wa Zekaria, mzao wa Mshiloni.
6 All the sons of Perez who were dwelling in Jerusalem, four hundred and sixty-eight, men of ability.
Wazao wa Peresi walioishi Yerusalemu walikuwa 468, watu wenye uwezo.
7 And, these, are the sons of Benjamin, —Sallu son of Meshullam, son of Joed, son of Pedaiah, son of Kolaiah, son of Maaseiah, son of Ithiel, son of Jeshaiah;
Kutoka wazao wa Benyamini: Salu mwana wa Meshulamu, mwana wa Yoedi, mwana wa Pedaya, mwana wa Kolaya, mwana wa Maaseya, mwana wa Ithieli, mwana wa Yeshaya
8 and, after him, Gabbai, Sallai, —nine hundred and twenty-eight.
na wafuasi wake, Gabai na Salai watu 928.
9 And, Joel son of Zichri, was in charge over them, —and, Judah son of Hassenuah, was over the city, as second.
Yoeli mwana wa Zikri alikuwa afisa wao mkuu, naye Yuda mwana wa Hasenua alikuwa msimamizi juu ya Mtaa wa Pili katika mji.
10 Of the priests, Jedaiah son of Joiarib, Jachin;
Kutoka makuhani: Yedaya, mwana wa Yoyaribu, Yakini,
11 Seraiah son of Hilkiah, son of Meshullam, son of Zadok, son of Meraioth, son of Ahitub, chief ruler of the house of God;
Seraya mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu, msimamizi katika nyumba ya Mungu,
12 and their brethren who were doing the work of the house, eight hundred and twenty-two, —and Adaiah son of Jeroham, son of Pelaliah, son of Amzi, son of Zechariah, son of Pashhur, son of Malchijah;
pamoja na wenzao waliofanya kazi hekaluni: watu 822. Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pelalia, mwana wa Amsi, mwana wa Zekaria, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya,
13 and his brethren, ancestral chiefs, two hundred and forty-two, —and Amashsai son of Azarel, son of Ahzai, son of Meshillemoth, son of Immer;
na wenzao, waliokuwa viongozi wa jamaa: watu 242. Amashisai mwana wa Azareli, mwana wa Azai, mwana wa Meshilemothi, mwana wa Imeri,
14 and their brethren, strong men of ability, a hundred and twenty-eight, —and, he who was in charge of them, was Zabdiel, son of Haggedolim.
na wenzao waliokuwa wenye uwezo: watu 128. Afisa wao mkuu alikuwa Zabdieli mwana wa Hagedolimu.
15 And, of the Levites, Shemaiah son of Hasshub, son of Azrikam, son of Hashabiah, son of Bunni;
Kutoka Walawi: Shemaya mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, mwana wa Buni;
16 and Shabbethai and Jozabad, over the outside business of the house of God, of the chiefs of the Levites;
Shabethai na Yozabadi, viongozi wawili wa Walawi, ambao walisimamia kazi za nje za nyumba ya Mungu;
17 and Mattaniah son of Mica, son of Zabdi, son of Asaph, leader of the praise who giveth thanks, in prayer, and Bakbukiah the second among his brethren, —and Obadiah son of Shemaiah, son of Galal, son of Jeduthun.
Matania mwana wa Mika, mwana wa Zabdi, mwana wa Asafu, kiongozi aliyeongoza kutoa shukrani na maombi; Bakbukia aliyekuwa msaidizi wake kati ya wenzake; na Abda mwana wa Shamua, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni.
18 All the Levites in the holy city, were two hundred and eighty-four.
Jumla ya Walawi waliokaa katika mji mtakatifu walikuwa watu 284.
19 And, the door-keepers—Akkub, Talmon, and their brethren who were keeping watch in the gates, were a hundred and seventy-two.
Mabawabu: Akubu, Talmoni na wenzao, waliolinda malango: watu 172.
20 But, the residue of Israel, the priests, the Levites, were in all the cities of Judah, every one in his inheritance.
Waisraeli waliosalia, pamoja na makuhani na Walawi, walikuwa katika miji yote ya Yuda, kila mmoja katika urithi wa baba yake.
21 Howbeit, the Nethinim, were dwelling in Ophel, —and, Ziha and Gishpa, were over the Nethinim.
Watumishi wa Hekalu waliishi katika kilima cha Ofeli. Siha na Gishpa walikuwa wasimamizi wao.
22 And, the overseer of the Levites in Jerusalem, was Uzzi son of Bani, son of Hashabiah, son of Mattaniah, son of Mica, —of the sons of Asaph the singers, to take lead in the business of the house of God.
Afisa mkuu wa Walawi huko Yerusalemu alikuwa Uzi mwana wa Bani, mwana wa Hashabia, mwana wa Matania, mwana wa Mika. Uzi alikuwa mmoja wa wazao wa Asafu, waliokuwa waimbaji wenye kuwajibika kwa ajili ya huduma ya nyumba ya Mungu.
23 For, the commandment of the king, was upon them, —as to a fixed provision for the singers, the need of a day upon its day.
Waimbaji walikuwa chini ya amri za mfalme, ambazo pia ziliratibu shughuli zao za kila siku.
24 And, Pethahiah son of Meshezabel, of the sons of Zerah, son of Judah, was at the hand of the king, in every matter pertaining to the people.
Pethahia mwana wa Meshezabeli, mmoja wa wazao wa Zera mwana wa Yuda, alikuwa mwakilishi wa mfalme katika mambo yote kuhusu mahusiano na watu.
25 And, as for the villages in their fields, some of the sons of Judah, dwelt in Kiriath-arba, and the hamlets thereof, and in Dibon, and the hamlets thereof, and in Jekabzeel, and the villages thereof;
Kuhusu vijiji na mashamba yake, baadhi ya watu wa Yuda waliishi Kiriath-Arba na makazi yaliyokizunguka, katika Diboni na makazi yake, katika Yekabzeeli na vijiji vyake,
26 and in Jeshua, and in Moladah, and in Beth-pelet;
katika Yeshua, katika Molada, katika Beth-Peleti,
27 and in Hazar-shual, and in Beer-sheba, and the hamlets thereof;
katika Hasar-Shuali, katika Beer-Sheba na makazi yake,
28 and in Ziklag, and in Meconah, and in the hamlets thereof,
katika Siklagi, katika Mekona na makazi yake,
29 and in En-rimmmon, and in Zorah, and in Jarmuth;
katika En-Rimoni, katika Sora, katika Yarmuthi,
30 Zanoah, Adullam and their villages, Lachish, and the fields thereof, Azekah, and the hamlets thereof, —so they encamped from Beer-sheba, unto the valley of Hinnom.
Zanoa, Adulamu na vijiji vyake, katika Lakishi na mashamba yake, na katika Azeka na makazi yake. Hivyo walikuwa wakiishi kuanzia Beer-Sheba mpaka Bonde la Hinomu.
31 And, the sons of Benjamin, [dwelt] from Geba, to Michmas and Aija, and Bethel, and the hamlets thereof:
Wazao wa Wabenyamini kutoka Geba waliishi Mikmashi, Aiya, Betheli na makazi yake,
32 Anathoth, Nob, Ananiah;
katika Anathothi, Nobu na Anania,
33 Hazor, Ramah, Gittaim;
katika Hazori, Rama na Gitaimu,
34 Hadid, Zeboim, Neballat;
katika Hadidi, Seboimu na Nebalati,
35 Lod and Ono, the valley of craftsmen.
katika Lodi na Ono, na katika Bonde la Mafundi.
36 Howbeit, of the Levites, certain courses of Judah, pertained unto Benjamin.
Baadhi ya makundi ya Walawi wa Yuda waliishi huko Benyamini.

< Nehemiah 11 >