< Micah 1 >

1 The word of Yahweh which came unto Micah the Morashtite, in the days of Jotham, Ahaz, Hezekiah, kings of Judah, —of which he had vision concerning Samaria, and Jerusalem: —
Neno la Bwana lilimjia Mika, Mmoreshethi, wakati wa utawala wa Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda; ufunuo aliouona kuhusu Samaria na Yerusalemu.
2 Hear ye peoples, all of you, Hearken, O earth and the fulness thereof, —and let My Lord Yahweh be among you for a witness, My Lord out of his holy temple.
Sikieni, enyi mataifa, enyi nyote, sikilizeni, ee dunia na wote mliomo ndani yake, ili Bwana Mwenyezi ashuhudie dhidi yenu, Bwana kutoka Hekalu lake takatifu.
3 For lo! Yahweh, coming forth out of his place, —that he may descend, and march along upon the high places of the earth.
Tazama! Bwana anakuja kutoka mahali pake; anashuka na kukanyaga mahali palipoinuka juu pa dunia.
4 Then shall the mountains be melted beneath him, and, the valleys, be cleft, —as wax before the fire, as waters poured out in a steep place.
Milima inayeyuka chini yake na mabonde yanagawanyika kama nta mbele ya moto, kama maji yatiririkayo kasi kwenye mteremko.
5 For the transgression of Jacob, is all this, and for the sin of the house of Israel, —Whose is the transgression of Jacob? Is it not Samaria’s? And whose is the sin of Judah? Is it not Jerusalem?
Yote haya ni kwa sababu ya kosa la Yakobo, ni kwa sababu ya dhambi za nyumba ya Israeli. Kosa la Yakobo ni lipi? Je, sio Samaria? Je, mahali pa juu pa Yuda pa kuabudia miungu ni nini? Je, sio Yerusalemu?
6 Therefore will I make of Samaria a heap in a field, the plantings in a vineyard, —and I will pour down, into the valley, her stones, and, her foundations, will I lay bare;
“Kwa hiyo nitaufanya Samaria kuwa lundo la kokoto, mahali pa kuotesha mizabibu. Nitayamwaga mawe yake katika bonde na kuacha wazi misingi yake.
7 And, all her images, shall be beaten in pieces, and, all her rewards for unchastity, shall be burned in the fire, and, all her idols, will I make a desolation, —for, out of the reward of unchastity, she gathered [them], and, unto the reward of unchastity, shall they return.
Sanamu zake zote zitavunjwa vipande vipande; zawadi zake zote za Hekalu zitachomwa kwa moto; nitaharibu vinyago vyake vyote. Kwa kuwa alikusanya zawadi zake kutokana na ujira wa kahaba, nazo zitatumika tena kulipa mishahara ya kahaba.”
8 For this cause, will I lament and howl, I will go stript and bare, —I will make a lamentation, like the wild dogs, and a mourning, like ostriches.
Kwa ajili ya hili nitalia na kuomboleza; nitatembea bila viatu na tena uchi. Nitabweka kama mbweha na kuomboleza kama bundi.
9 For dangerous are her wounds, —for she hath come as far as Judah, she hath reached as far as the gate of my people, as far as Jerusalem.
Kwa sababu jeraha lake halitibiki; limekuja Yuda. Limefika hasa kwenye lango la watu wangu, hata Yerusalemu kwenyewe.
10 In Gath, do not tell, in Accho, do not weep, —in Beth-l’aphrah, roll yourselves in dust.
Usiliseme hili huko Gathi; usilie hata kidogo. Huko Beth-le-Afra gaagaa mavumbini.
11 Pass thou over (for you), thou inhabitress of Shaphir, of disgraceful disclosure, —the inhabitress of Zaanan, hath not gone forth, at the lamentation of Beth-ezel, shall he take from you his station,
Piteni mkiwa uchi na wenye aibu, ninyi mkaao Shafiri. Wale waishio Saanani hawatatoka nje. Beth-Eseli iko katika maombolezo; kinga yake imeondolewa kwako.
12 Though the inhabitress of Maroth waited for blessing, —yet there came down calamity from Yahweh, to the gate of Jerusalem.
Wale waishio Marothi wanagaagaa kwa maumivu wakingoja msaada, kwa sababu maangamizi yamekuja kutoka kwa Bwana, hata katika lango la Yerusalemu.
13 Bind the chariot to the steed, O inhabitress of Lachish, —the beginning of sin, was she to the daughter of Zion, for, in thee, have been found the transgressions of Israel.
Enyi mkaao Lakishi, fungeni farasi kwenye magari ya vita. Mlikuwa chanzo cha dhambi kwa Binti Sayuni, kwa kuwa makosa ya Israeli yalikutwa kwako.
14 Therefore, shalt thou give a dismission, against Moresheth-gath, —The houses of Achzib, served for a deception to the kings of Israel.
Kwa hiyo utaipa Moresheth-Gathi zawadi za kuagana. Mji wa Akzibu utaonyesha wazi udanganyifu kwa wafalme wa Israeli.
15 The time shall yet be when, the heir, I will bring unto thee, O inhabitress of Mareshah, —as far as Adullam, shall enter the glory of Israel.
Nitawaleteeni atakayewashinda ninyi mnaoishi Maresha. Yeye aliye utukufu wa Israeli atakuja Adulamu.
16 Make thee bald, and cut off thy hair, for the children of thy pleasures, —enlarge thy baldness, like a vulture, for they are exiled from thee.
Nyoeni nywele zenu katika kuomboleza kwa ajili ya watoto wenu mnaowafurahia; jifanyieni upara kama tai, kwa kuwa watawaacha na kwenda uhamishoni.

< Micah 1 >