< Micah 2 >

1 Alas for them who devise iniquity and work wickedness upon their beds, —in the light of the morning, they will execute it, for it is in the power of their hand.
Ole kwa wale wapangao uovu, kwa wale wafanyao shauri la hila vitandani mwao! Kunapopambazuka wanalitimiza kwa sababu uko katika uwezo wao kutekeleza.
2 Thus do they covet fields and seize them, and houses and take them away, —and so they oppress the master and his household, the man and his inheritance.
Wanatamani mashamba na kuyakamata, pia nyumba na kuzichukua. Wanamlaghai mwanaume nyumba yake, mwanadamu mwenzake urithi wake.
3 Therefore, —Thus, saith Yahweh, Behold me! devising, against this family, a calamity, —from which ye shall not remove your neck, neither shall ye walk loftily, for, a time of calamity, shall it be.
Kwa hiyo, Bwana asema: “Ninapanga maangamizi dhidi ya watu hawa, ambayo hamwezi kujiokoa wenyewe. Hamtatembea tena kwa majivuno, kwa kuwa utakuwa ni wakati wa maafa.
4 In that day, shall one take up against you a by-word, and lament a lamentable lamentation, saying—we are made, utterly desolate, the portion of my people, he passeth to others, —How doth he set me aside! To an apostate, our fields, doth he apportion.
Siku hiyo watu watawadhihaki, watawafanyia mzaha kwa wimbo huu wa maombolezo: ‘Tumeangamizwa kabisa; mali ya watu wangu imegawanywa. Ameninyangʼanya! Ametoa mashamba yetu kwa wasaliti.’”
5 Therefore, shalt thou have none to throw a measuring-line by lot, —in the convocation of Yahweh.
Kwa hiyo hutakuwa na yeyote katika kusanyiko la Bwana wa kugawanya mashamba kwa kura.
6 Do not sputter—So they sputter! They must not sputter as to these things, Must he not put away reproaches?
Manabii wao husema, “Usitabiri. Usitabiri kuhusu vitu hivi; aibu haitatupata.”
7 O thou who art said to be the house of Jacob, Is the spirit of Yahweh, impatient? Or are, these, his doings? Are not, his words, pleasant to him who is upright in his walk?
Je, ingesemwa, ee nyumba ya Yakobo: “Je, Roho wa Bwana amekasirika? Je, yeye hufanya vitu kama hivyo?” “Je, maneno yangu hayamfanyii mema yeye ambaye njia zake ni nyofu?
8 But, against my people, as an enemy, he setteth himself, from off the robe, they tear away, the cloak, —from such as are passing by with confidence, as men averse from war.
Siku hizi watu wangu wameinuka kama adui. Unawavua joho la kitajiri wale wanaopita pasipo kujali, kama watu warudio kutoka vitani.
9 The wives of my people, ye do even drive out, each from the house of her darlings, —from over her children, ye do take away mine ornament, as long as life shall last.
Unawahamisha wanawake wa watu wangu kutoka kwenye nyumba zao za kupendeza. Unaondoa baraka yangu kwa watoto wao milele.
10 Arise ye and depart, for, this, is not the place of rest, —Because it is defiled, it shall make desolate with a desolation that is ruthless.
Inuka, nenda zako! Kwa maana hapa sio mahali pako pa kupumzikia, kwa sababu pametiwa unajisi, pameharibiwa, wala hapatengenezeki tena.
11 If there be a man, who goeth after wind, and, falsehood, hath woven, [saying] —I will discourse to thee, concerning wine and strong drink, then shall he become a fountain of discourse unto this people.
Ikiwa mwongo na mdanganyifu atakuja na kusema, ‘Nitawatabiria divai na pombe kwa wingi,’ angekuwa ndiye nabii anayekubalika na watu hawa!
12 I will, surely assemble, O Jacob, all of thee, I will, surely gather, the remnant of Israel, at once, will I make them like sheep in distress, —Like a flock in the midst of its pasture, shall they hum with men,
“Hakika nitawakusanya ninyi nyote, ee Yakobo, Hakika nitawaleta pamoja mabaki ya Israeli. Nitawaleta pamoja kama kondoo ndani ya zizi, kama kundi kwenye malisho yake, mahali hapa patakuwa na msongamano wa watu.
13 One making a breach, hath gone up, before them, they have broken in, and passed through, and, by the gate, have departed, —and their king, hath passed through, before them, with, Yahweh, at their head!
Yeye afunguaye njia atawatangulia; watapita kwenye lango na kutoka nje. Mfalme wao atawatangulia, Bwana atakuwa kiongozi.”

< Micah 2 >