< Matthew 9 >

1 And, entering into a boat, he crossed over, and came into his own city.
Yesu alipanda mashua, akavuka ziwa na kufika katika mji wake.
2 And lo! they were bringing unto him a paralytic, on a couch, laid prostrate; and Jesus, seeing, their faith, said to the paralytic, —Take courage! child, forgiven are thy sins.
Hapo watu walimletea mtu mmoja aliyepooza mwili, amelazwa juu ya kitanda. Yesu alipoona imani yao, akamwambia huyo mtu aliyepooza, “Jipe moyo mwanangu! Umesamehewa dhambi zako.”
3 And lo! certain of the scribes, said within themselves, —This man, speaketh profanely!
Baadhi ya walimu wa Sheria wakaanza kufikiri, “Mtu huyu anamkufuru Mungu!”
4 And Jesus, knowing, their inward thoughts, said, —To what end are ye cherishing evil thoughts within your hearts?
Yesu aliyajua mawazo yao, akasema, “Kwa nini mnawaza mabaya mioyoni mwenu?
5 For which is easier—To say, Forgiven are thy sins, —or to say, Rise and be walking!
Ni lipi lililo rahisi zaidi: kusema, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Simama, utembee?
6 But, that ye may know, that the Son of Man hath, authority, upon the earth, to be forgiving sins, then, saith he to the paralytic, —Rise! take up thy couch, and withdraw unto thy house.
Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anao uwezo wa kuwasamehe watu dhambi duniani.” Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza, “Inuka, chukua kitanda chako, uende nyumbani kwako.”
7 And, rising, he departed unto his house.
Huyo mtu aliyekuwa amepooza akainuka, akaenda nyumbani kwake.
8 Now the multitudes, seeing, were struck with fear, and glorified the God who had given authority, such as this, unto men.
Watu wote katika ule umati walipoona hayo, walishangaa na kuogopa; wakamtukuza Mungu aliyewapa binadamu uwezo wa namna hiyo.
9 And Jesus, passing aside from thence, saw a man presiding over the tax-office, called, Matthew, and saith unto him, —Be following me. And, arising, he followed him.
Yesu aliondoka hapo, na alipokuwa anakwenda zake, alimwona mtu mmoja aitwaye Mathayo, ameketi katika ofisi ya ushuru. Basi, Yesu akamwambia, “Nifuate.” Naye Mathayo akainuka, akamfuata.
10 And it came to pass, as he was reclining in the house, that lo! many tax-collectors and sinners, came, and were reclining together with Jesus and his disciples.
Yesu alipokuwa nyumbani ameketi kula chakula, watoza ushuru wengi na wahalifu walikuja wakaketi pamoja naye na wanafunzi wake.
11 And, the Pharisees, observing it, began to say unto his disciples, —Wherefore, with tax-collectors and sinners, doth your Teacher eat?
Mafarisayo walipoona hayo, wakawaambia wanafunzi wake, “Mbona mwalimu wenu anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?”
12 And, he, hearing it, said, —No need have the strong, of a physician, but they who are sick.
Yesu aliwasikia, akasema, “Watu wenye afya hawahitaji daktari; wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa. Sikuja kuwaita watu wema, ila wenye dhambi.
13 But go ye, and learn what this meaneth, —Mercy, I desire, and not, sacrifice; For I came, not to call the righteous, but sinners.
Basi, kajifunzeni maana ya maneno haya: Nataka huruma, wala si dhabihu. Sikuja kuwaita watu wema, bali wenye dhambi.”
14 Then come near unto him the disciples of John, saying, —Wherefore do, we, and the Pharisees, fast, whereas, thy disciples, fast not?
Kisha wanafunzi wa Yohane mbatizaji walimwendea Yesu, wakamwuliza, “Sisi na Mafarisayo hufunga mara nyingi; mbona wanafunzi wako hawafungi?”
15 And Jesus said unto them, —Can, the sons of the bridechamber, mourn, so long as, the bridegroom, is, with them? But days will come, when the bridegroom, shall be taken from them, and, then, will they fast.
Yesu akawajibu, “Je, walioalikwa arusini wanaweza kuomboleza wakati bwana arusi yupo pamoja nao? La hasha! Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kati yao; wakati huo ndipo watakapofunga.
16 Howbeit, no one, layeth on a patch of unshrunk cloth, upon an old garment, —for the shrinking of it teareth away from the garment, and, a worse rent, is made.
“Hakuna mtu atiaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kuukuu. Maana kiraka hicho kitararua hilo vazi kuukuu, na pale palipokuwa pameraruka pataongezeka.
17 Neither pour they new wine into old skins: otherwise at least, the skins are burst, and, the wine, runneth out, and, the skins, are spoiled, —but they pour new wine into unused skins, and, both, are together preserved.
Wala hakuna mtu awekaye divai mpya katika viriba vikuukuu. Akifanya hivyo, viriba hupasuka na divai ikamwagika, navyo viriba vikaharibika. Ila divai mpya hutiwa katika viriba vipya, na vyote viwili, viriba na divai, vikahifadhiwa salama.”
18 While, these things, he was speaking unto them, lo! a [certain] ruler, came, and began bowing down to him, saying, —My daughter, just now died! But come, and lay thy hand upon, her, and she shall live.
Yesu alipokuwa akisema hayo, ofisa mmoja Myahudi alifika, akamwinamia na kusema, “Binti yangu amekufa sasa hivi. Lakini, tafadhali njoo umwekee mkono wako naye ataishi.”
19 And Jesus, arising, was following him, also his disciples.
Yesu akaondoka pamoja na wanafunzi wake, akamfuata.
20 And lo! a woman, having a flow of blood twelve years, coming near behind, touched the fringe of his mantle.
Mama mmoja, mgonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili, alimfuata Yesu nyuma, akagusa pindo la vazi lake.
21 For she kept saying within herself, —If only I touch his mantle, I shall be made well!
Alifanya hivyo kwani alifikiri moyoni: “Nikigusa tu vazi lake, nitapona.”
22 And, Jesus, turning and seeing her, said, —Take courage! daughter, Thy faith, hath made thee well. And the woman was made well, from that hour.
Basi, Yesu akageuka akamwona, akamwambia, “Binti, jipe moyo! Imani yako imekuponya.” Mama huyo akapona saa ileile.
23 And, Jesus, coming, into the house of the ruler, and seeing the flute-players and the multitude in confusion, was saying:
Kisha Yesu akaingia nyumbani kwa yule ofisa. Na alipowaona wapiga filimbi na umati wa watu wanaofanya matanga,
24 Give place! for the maiden died not, but is sleeping. And they began to deride him.
akasema, “Ondokeni hapa! Msichana huyu hakufa, amelala tu.” Nao wakamcheka.
25 But, when the multitude had been put forth, he went in, and grasped her hand, —and the maiden arose.
Basi, umati wa watu ulipoondolewa, Yesu aliingia ndani, akamshika huyo msichana mkono, naye akasimama.
26 And forth went this report, into the whole of that land.
Habari hiyo ikavuma sana katika nchi ile yote.
27 And, as Jesus, was passing aside from thence, there followed him, two blind men, crying aloud and saying, —Have mercy on us, O Son of David!
Yesu aliondoka hapo, na alipokuwa anakwenda, vipofu wawili walimfuata wakipiga kelele, “Mwana wa Daudi, utuhurumie!”
28 And, when he entered the house, the blind men came unto him, —and Jesus saith unto them, Believe ye, that I can, do this? They say unto him, Yea, Lord!
Yesu alipoingia nyumbani, vipofu hao wawili wakamwendea, naye akawauliza, “Je, mnaamini kwamba naweza kuwafanyia jambo hilo?” Nao wakamjibu, “Naam, Mheshimiwa.”
29 Then touched he their eyes, saying, According to your faith, be it done unto you.
Hapo Yesu akayagusa macho yao, akasema, “Na iwe kwenu kama mnavyoamini.”
30 And their eyes were opened. And Jesus, sternly charged them, saying, Mind! let no one know!
Macho yao yakafunguliwa. Naye Yesu akawaonya kwa ukali: “Msimwambie mtu yeyote jambo hili.”
31 They, however, going forth, made him known throughout the whole of that land.
Lakini wao wakaondoka, wakaeneza habari za Yesu katika nchi ile yote.
32 And, as, they, were going forth, lo! there was brought to him, a dumb man, demonized.
Watu walipokuwa wanakwenda zao, wengine walimletea Yesu mtu mmoja aliyekuwa bubu kwa sababu alikuwa amepagawa na pepo.
33 And, the demon being cast out, the dumb man spoke; and the multitudes marvelled, saying, —Never, was it seen thus, in Israel.
Mara tu huyo pepo alipotolewa, mtu huyo aliyekuwa bubu akaanza kuongea tena. Watu wakashangaa na kusema, “Jambo kama hili halijapata kuonekana katika Israeli!”
34 [But, the Pharisees, beg to say, In the ruler of the demons, is he casting out the demons.]
Lakini Mafarisayo wakawa wanasema, “Anawatoa pepo kwa nguvu ya mkuu wa pepo wabaya.”
35 And Jesus was going round all the cities and the villages, teaching in their synagogues, and proclaiming the glad-message of the kingdom, —and curing every disease, and every infirmity.
Yesu alitembelea miji yote na vijiji, akafundisha katika masunagogi yao akihubiri Habari Njema ya Ufalme wa Mungu, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila namna.
36 But, seeing the multitudes, he was moved with compassion concerning them, because they were torn and thrown down, like sheep hating no shepherd.
Basi, alipowaona watu, makundi kwa makundi, aliwaonea huruma kwa sababu walikuwa hoi na wenye wasiwasi kama kondoo wasio na mchungaji.
37 Then, saith he unto his disciples, The harvest, indeed, is great, but, the labourers, few;
Hapo akawaambia wanafunzi wake, “Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache.
38 Beg ye, therefore, of the Lord of the harvest, —That he would thrust forth labourers, into his harvest.
Kwa hivyo mwombeni mwenye shamba atume wavunaji shambani mwake.”

< Matthew 9 >