< Matthew 16 >

1 And, the Pharisees and Sadducees coming near, putting him to the test, requested him, a sign out of the heaven, to shew unto them.
Mafarisayo na Masadukayo wakamjia Yesu na kumjaribu kwa kumwomba awaonyeshe ishara kutoka mbinguni.
2 But, he, answering said unto them— When evening cometh ye say, Fair! for fiery is the heaven;
Yesu akawajibu, “Ifikapo jioni, mnasema, ‘Hali ya hewa itakuwa nzuri, kwa kuwa anga ni nyekundu.’
3 And at morn, To-day, a storm! for fiery, and yet sad, is the heaven. The face of the heaven indeed, ye learn to distinguish, —but, the signs of the times, ye cannot.
Nanyi wakati wa asubuhi mnasema, ‘Leo kutakuwa na dhoruba, kwa sababu anga ni nyekundu na mawingu yametanda.’ Mnajua jinsi ya kupambanua kule kuonekana kwa anga, lakini hamwezi kupambanua dalili za nyakati.
4 A wicked and adulterous generation, a sign, doth seek after, and, a sign, will not be given it, —save the sign of Jonah. And, leaving them behind, he departed.
Kizazi kiovu na cha uzinzi kinatafuta ishara, lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ishara ya Yona.” Yesu akawaacha, akaenda zake.
5 And the disciples coming, to the other side, had forgotten to take loaves.
Wanafunzi wake walipofika ngʼambo ya bahari, walikuwa wamesahau kuchukua mikate.
6 And, Jesus, said unto them—Mind! and beware, of the leaven of the Pharisees and Sadducees.
Yesu akawaambia, “Jihadharini. Jilindeni na chachu ya Mafarisayo na ya Masadukayo.”
7 And, they, began to deliberate among themselves, saying—Because, loaves, we took not.
Wakajadiliana wao kwa wao, wakisema, “Ni kwa sababu hatukuleta mikate.”
8 And, observing it, Jesus said—Why are ye deliberating among yourselves, ye little-of-faith! because, loaves, ye have not?
Yesu, akifahamu majadiliano yao, akauliza, “Enyi wa imani haba! Mbona mnajadiliana miongoni mwenu kuhusu kutokuwa na mikate?
9 Not yet, perceive ye, neither remember, —The five loaves of the five thousand, and how many baskets ye received?
Je, bado hamwelewi? Je, hamkumbuki ile mikate mitano iliyolisha watu 5,000 na idadi ya vikapu vingapi vya mabaki mlivyokusanya?
10 Nor the seven loaves of the four thousand, and how many hampers ye received?
Au ile mikate saba iliyolisha watu 4,000 na idadi ya vikapu vingapi vya mabaki mlivyokusanya?
11 How is it ye perceive not, that, not concerning loaves, spake I unto you, —but beware of the leaven, of the Pharisees and Sadducees?
Inakuwaje mnashindwa kuelewa kwamba nilikuwa sisemi nanyi habari za mikate? Jilindeni na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo.”
12 Then, understood they that he did not bid them beware of [the] leaven [of loaves] but of, the teaching, of the Pharisees and Sadducees.
Ndipo wakaelewa kwamba alikuwa hasemi juu ya chachu ya kutengeneza mikate, bali juu ya mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo.
13 And, Jesus coming into the parts of Caesarea of Philip, began questioning his disciples, saying—Who are men saying that, the Son of Man, is?
Basi Yesu alipofika katika eneo la Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake, “Watu husema kwamba mimi Mwana wa Adamu ni nani?”
14 And, they, said—Some, indeed, John the Immerser, and, others, Elijah, —but, others, Jeremiah, or one of the prophets.
Wakamjibu, “Baadhi husema ni Yohana Mbatizaji; wengine husema ni Eliya; na bado wengine husema ni Yeremia au mmojawapo wa manabii.”
15 He saith unto them—But who say, ye, that I am?
Akawauliza, “Je, ninyi mnasema mimi ni nani?”
16 And, Simon Peter, answering, said—Thou, art the Christ, the Son of the Living God.
Simoni Petro akamjibu, “Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.”
17 And Jesus, answering, said to him—Happy, art thou, Simon Bar-yona, —because, flesh and blood, revealed it not unto thee, but my Father who is in the heavens.
Naye Yesu akamwambia, “Heri wewe, Simoni Bar-Yona, kwa maana hili halikufunuliwa kwako na mwanadamu, bali na Baba yangu aliye mbinguni.
18 And, I also, unto thee, say—Thou, art Peter, —and, upon this rock, will I build my assembly, and, the gates of hades, shall not prevail against it. (Hadēs g86)
Nami nakuambia, wewe ndiwe Petro na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu, hata malango ya Kuzimu hayataweza kulishinda. (Hadēs g86)
19 I will give thee, the keys of the kingdom of the heavens, —and, whatsoever thou shalt bind upon the earth, shall be bound in the heavens, and, whatsoever thou shalt loose upon the earth, shall be loosed in the heavens.
Nitakupa funguo za Ufalme wa mbinguni, na lolote utakalolifunga duniani litakuwa limefungwa Mbinguni, nalo lolote utakalofungua duniani litakuwa limefunguliwa mbinguni.”
20 Then, straitly charged he the disciples, lest, to any man, they should say—He, is, the Christ.
Kisha akawakataza wanafunzi wake wasimwambie mtu yeyote kwamba yeye ndiye Kristo.
21 From that time, began Jesus Christ to be pointing out to his disciples that he must needs, into Jerusalem, go away, and, many things, suffer, from the elders and chief priests and scribes, and be slain, —and on, the third day, arise.
Tangu wakati huo, Yesu alianza kuwaeleza wanafunzi wake kwamba hana budi kwenda Yerusalemu na kupata mateso mengi mikononi mwa wazee, viongozi wa makuhani, na walimu wa sheria, na kwamba itampasa auawe lakini siku ya tatu kufufuliwa.
22 And, taking him aside, Peter began to rebuke him, saying—Mercy on thee Lord! In nowise, shall, this, befall thee.
Petro akamchukua kando, akaanza kumkemea akisema, “Haiwezekani, Bwana! Jambo hili kamwe halitakupata!”
23 But, he, turning, said to Peter—Withdraw behind me, Satan! A snare, art thou of mine, because thou art not regarding the things of God, but the things of men.
Lakini Yesu akageuka na kumwambia Petro, “Rudi nyuma yangu, Shetani! Wewe ni kikwazo kwangu. Moyo wako hauwazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.”
24 Then, Jesus said unto his disciples—If any one intendeth, after me, to come, let him deny himself, and take up his cross, and be following me;
Ndipo Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.
25 For, whosoever intendeth, his life, to save, shall lose it, —but, whosoever shall lose his life, for my sake, shall find it.
Kwa maana yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu atayapata.
26 For what shall a man be profited, though, the whole world, he gain, and, his life, he forfeit? Or what shall a man give, in exchange for his life?
Kwa maana, je, itamfaidi nini mtu kuupata ulimwengu wote, lakini akayapoteza maisha yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?
27 For the Son of Man is destined to be coming, in the glory of his Father, with his messengers, —and, then, will he give back unto each one, according to his practice.
Kwa maana Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake, naye ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.
28 Verily, I say unto you—There are some of those, here standing, who, indeed, shall in nowise taste of death, until they see the Son of Man, coming in his kingdom.
Nawaambia kweli, baadhi yenu hapa hawataonja mauti kabla ya kumwona Mwana wa Adamu akija katika Ufalme wake.”

< Matthew 16 >