< Luke 8 >

1 And it came to pass, in due course, that he was passing through, city by city and village by village, proclaiming, and delivering the glad-message of the kingdom of God, —and, the twelve, were with him;
Baada ya hayo, Yesu alipitia katika miji na vijiji akitangaza Habari Njema za Ufalme wa Mungu. Wale kumi na wawili waliandamana naye.
2 and certain women, who had been cured from evil spirits and infirmities, —Mary, the one called Magdalene, from whom seven demons had gone forth,
Pia wanawake kadhaa ambao Yesu alikuwa amewatoa pepo wabaya na kuwaponya magonjwa, waliandamana naye. Hao ndio akina Maria (aitwaye Magdalene), ambaye alitolewa pepo wabaya saba;
3 and Joana, wife of Chuza steward of Herod, and Susanna, and many others, —who indeed were ministering unto them out of their possessions.
Yoana, mke wa Kuza, mfanyakazi mkuu wa Herode; Susana na wengine kadhaa. Hao wanawake walikuwa wakiwatumikia kwa mali yao wenyewe.
4 And, seeing that a great multitude were coming together, and they who from every city were journeying forth unto him, he spake through means of a parable: —
Kundi kubwa la watu lilikuwa linakusanyika, na watu walikuwa wanamjia Yesu kutoka kila mji. Naye akawaambia mfano huu:
5 The sower went forth to sow his seed, —and, as he sowed, some, indeed, fell beside the pathway, and was trodden down; and, the birds of heaven, devoured it.
“Mpanzi alikwenda kupanda mbegu zake. Alipokuwa akipanda zile mbegu, nyingine zilianguka njiani, na wapita njia wakazikanyaga, na ndege wakazila.
6 And, other, fell down upon the rock; and, growing, was withered, because it had not moisture.
Nyingine zilianguka penye mawe, na baada ya kuota zikanyauka kwa kukosa maji.
7 And, other, fell and thorns; and, growing together, the thorns, choked it.
Nyingine zilianguka kati ya miti ya miiba. Ile miti ya miiba ilipoota ikazisonga.
8 And, other, fell into good ground; and, growing, brought forth fruit, a hundredfold. These things, saying, he went on to cry aloud—He that hath ears to hear, let him hear.
Nyingine zilianguka katika udongo mzuri, zikaota na kuzaa asilimia mia.” Baada ya kusema hayo, akapaaza sauti, akasema, “Mwenye masikio na asikie!”
9 But his disciples began to question him—What might, this very, parable be?
Wanafunzi wake wakamwuliza Yesu maana ya mfano huo.
10 And, he, said—Unto you, hath it been given, to get to know the sacred secrets of the kingdom of God; but, unto the rest, in parables, —in order that, seeing, they may not see, and, hearing, they may not understand.
Naye akajibu, “Ninyi mmejaliwa kujua siri za Ufalme wa Mungu, lakini hao wengine sivyo; ila hao huambiwa kwa mifano, ili wakitazama wasiweze kuona, na wakisikia wasifahamu.
11 Now the parable, is this—The seed, is, the word of God.
“Basi, maana ya mfano huu ni hii: mbegu ni neno la Mungu.
12 And, those beside the pathway, are they who have heard; afterwards, cometh the adversary, and catcheth away the word from their heart, lest, believing, they should, be saved.
Zile zilizoanguka njiani zinaonyesha watu wale wanaosikia lile neno, halafu Ibilisi akaja na kuliondoa mioyoni mwao wasije wakaamini na hivyo wakaokoka.
13 And, those upon the rock, are they who, as soon as they hear, with joy, welcome the word; and, these, not having, root, are they who, for a season, believe, —and, in a season of testing, draw back.
Zile zilizoanguka penye mawe zinaonyesha watu wale ambao wanaposikia juu ya lile neno hulipokea kwa furaha. Hata hivyo, kama zile mbegu, watu hao hawana mizizi maana husadiki kwa kitambo tu, na wanapojaribiwa hukata tamaa.
14 And, that which in among the thorns fell, these, are they who have heard; and, by anxieties and wealth and pleasures of life being borne along, are choked up, and bear not to perfection.
Zile zilizoanguka kwenye miti ya miiba ni watu wale wanaosikia lile neno, lakini muda si muda, wanapokwenda zao, husongwa na wasiwasi, mali na anasa za maisha, na hawazai matunda yakakomaa.
15 But, that in the good ground, these, are they who, indeed, in a noble and good heart having heard the word, hold fast, and bear fruit with endurance.
Na zile zilizoanguka kwenye udongo mzuri ndio watu wale wanaolisikia lile neno, wakalizingatia kwa moyo mwema na wa utii. Hao huvumilia mpaka wakazaa matunda.
16 And, no one having lit a lamp, covereth it up with a vessel, or, beneath a couch, putteth it; but, upon a lamp-stand, putteth it, that, they who come in, may see the light.
“Watu hawawashi taa na kuifunika kwa chombo au kuiweka mvunguni. Lakini huiweka juu ya kinara ili watu wanapoingia ndani wapate kuona mwanga.
17 For there is no secret, which shall not be made, manifest; neither a hidden thing, which shall in anywise not be made known, or not come, where it can be seen.
“Chochote kilichofichwa kitafichuliwa na siri yoyote itagunduliwa na kujulikana hadharani.
18 Be taking heed therefore how ye hear; for, whosoever shall have, it shall be given unto him; and, whosoever shall not have, even what he seemeth to have, shall be taken from him.
“Kwa hiyo, jihadharini jinsi mnavyosikia; maana aliye na kitu ataongezewa, lakini yule asiye na kitu, hata kile anachodhani kuwa anacho, kitachukuliwa.”
19 And his mother and brethren came near unto him, and were unable to reach him, because of the multitude.
Hapo mama na ndugu zake Yesu wakamjia, lakini hawakuweza kumkaribia kwa sababu ya umati wa watu.
20 And it was reported to him—Thy mother and thy brethren, are standing outside, desiring, to see, thee.
Yesu akapewa habari kwamba mama na ndugu zake walikuwa nje, wanataka kumwona.
21 But, he, answering, said unto them—My mother and my brethren, are, these—they who, the word of God, are hearing and doing.
Lakini Yesu akawaambia watu wote, “Mama yangu na ndugu zangu ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulishika.”
22 And it came to pass, on one of the days, that, he, entered into a boat, and his disciples; and he said unto them—Let us pass over unto the other side of the lake. And they set sail.
Siku moja, Yesu alipanda mashua pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, “Tuvuke ziwa twende mpaka ng'ambo.” Basi, wakaanza safari.
23 Now, as they were sailing, he fell asleep. And there came down a hurricane of wind upon the lake, and they began to be filled, and to be in peril.
Walipokuwa wanasafiri kwa mashua, Yesu alishikwa na usingizi, akalala. Dhoruba kali ikaanza kuvuma, maji yakaanza kuingia ndani ya mashua, wakawa katika hatari.
24 And, coming near, they roused him up, saying—Master! Master! we perish! And, he, roused up, rebuked the wind, and the surging of the water; and they ceased, and it became a calm.
Wale wanafunzi wakamwendea Yesu, wakamwamsha wakisema, “Bwana, Bwana! Tunaangamia!” Yesu akaamka, akaikemea dhoruba na mawimbi, navyo vikatulia, kukawa shwari.
25 And he said unto them—Where was your faith? But, struck with fear, they marvelled, saying one to another—Who then is, this, —that, even unto the winds, he giveth orders, and unto the water, and they hearken unto him.
Kisha akawaambia, “Iko wapi imani yenu?” Lakini wao walishangaa na kuogopa huku wakiambiana, “Huyu ni nani basi, hata anaamuru dhoruba na mawimbi, navyo vinamtii?”
26 And they sailed down into the country of the Gerasenes, the which is over against Galilee.
Wakaendelea na safari, wakafika pwani ya nchi ya Wagerase inayokabiliana na Galilaya, ng'ambo ya ziwa.
27 And, when he went forth upon the land, there met him a certain man, out of the city, having demons; and, for a considerable time, he had put on no garment, and, in a house, would not abide, but among the tombs.
Alipokuwa anashuka pwani, mtu mmoja aliyekuwa amepagawa na pepo alimjia kutoka mjini. Kwa muda mrefu mtu huyo, hakuwa anavaa nguo, wala hakuwa anaishi nyumbani bali makaburini.
28 But, seeing Jesus, he cried out aloud, and fell down before him, and, with a loud voice, said—What have I in common with thee, O Jesus, Son of [God] the Most High? I beg of thee—Do not torment me!—
Alipomwona Yesu, alipiga kelele na kujitupa chini mbele yake, na kusema kwa sauti kubwa “We, Yesu Mwana wa Mungu Aliye Juu una shauri gani nami? Ninakusihi usinitese!”
29 for he was about to charge the impure spirit to come out from the man. For, many times, had it snatched him away; and he used to be bound with chains and fetters, for a safe-guard, and was wont to break in pieces the bonds, and to be driven by the demon into the deserts.
Alisema hivyo kwa kuwa Yesu alikwishamwambia huyo pepo mchafu amtoke mtu huyo. Pepo huyo mchafu alikuwa anamvamia mtu huyo mara nyingi, na ingawa watu walimweka ndani na kumfunga kwa minyororo na pingu, lakini kila mara alivivunja vifungo hivyo, akakimbizwa na pepo huyo mchafu hadi jangwani.
30 And Jesus questioned him—What name hast thou? And, he, said—Legion! because many demons had entered into him.
Basi, Yesu akamwuliza, “Jina lako nani?” Yeye akajibu, “Jina langu ni Jeshi” —kwa sababu pepo wengi walikuwa wamempagaa.
31 And they were beseeching him that he would not order them, into the abyss, to depart. (Abyssos g12)
Hao pepo wakamsihi asiwaamuru wamtoke na kwenda kwenye shimo lisilo na mwisho. (Abyssos g12)
32 Now there was there, a herd of a good many swine, feeding in the mountain; and they besought him, that he would suffer them, into those, to enter; and he suffered them.
Kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe wakilisha mlimani. Basi, hao pepo wakamsihi awaruhusu wawaingie. Naye Yesu akawapa ruhusa.
33 And the demons, going forth from the man entered into the swine; and the herd rushed down the cliff, into the lake, and were choked.
Kwa hiyo pepo hao wakamtoka yule mtu, wakawaingia wale nguruwe, nao wakaporomoka kwenye ule mteremko mkali, wakatumbukia ziwani, wakazama majini.
34 And they who had been feeding them, seeing what had happened, fled, and carried tidings into the city, and into the country-places.
Wale wachungaji walipoona yote yaliyotokea walikimbia, wakaenda kuwapa watu habari, mjini na mashambani.
35 And they went forth to see what had happened; and came unto Jesus, and found the man from whom the demons had gone forth, sitting, clothed, and of sound mind, near the feet of Jesus, —and they were struck with fear.
Watu wakaja kuona yaliyotokea. Wakamwendea Yesu, wakamwona yule mtu aliyetokwa na pepo ameketi karibu na Yesu, amevaa nguo, ana akili zake, wakaogopa.
36 And they who had seen it, reported unto them, how the demonized man was saved.
Wale watu walioshuhudia tukio hilo waliwaeleza hao jinsi yule mtu alivyoponywa.
37 And one and all of the throng of the surrounding country of the Gerasenes, requested him, to depart from them; because, with a great fear, were they oppressed. And, he, entering into a boat, returned.
Wakazi wa nchi ya Gerase walishikwa na hofu kubwa. Kwa hiyo wakamwomba Yesu aondoke, aende zake. Hivyo Yesu alipanda tena mashua, akaondoka.
38 And the man from whom the demons had gone forth, began to beg of him, that he might be with him; but he dismissed him, saying—
Yule mtu aliyetokwa na wale pepo akamsihi aende pamoja naye. Lakini Yesu hakumruhusu, bali akamwambia,
39 Be returning unto thy house, and telling forth what great things, God, for thee, hath done. And he departed, through all the city, proclaiming what great things, Jesus, had done for him.
“Rudi nyumbani ukaeleze yote Mungu aliyokutendea.” Basi, yule mtu akaenda akitangaza kila mahali katika mji ule mambo yote Yesu aliyomtendea.
40 Now, when Jesus returned, the multitude welcomed him back, for they were all expecting him.
Yesu aliporudi upande mwingine wa ziwa, kundi la watu lilimkaribisha, kwa maana wote walikuwa wanamngojea.
41 And lo! there came a man, whose name was Jairus, and, the same, was, a ruler of the synagogue, —and, falling down near the feet of Jesus, he began beseeching him to enter into his house;
Hapo akaja mtu mmoja aitwaye Yairo, ofisa wa sunagogi. Alijitupa miguuni pa Yesu, akamwomba aende nyumbani kwake,
42 because he had, an only-begotten daughter, about twelve years old, and, she, was dying. Now, as he withdrew, the multitudes, were hemming him in.
kwa kuwa binti yake wa pekee, mwana wa pekee mwenye umri wa miaka kumi na miwili, alikuwa mahututi. Yesu alipokuwa akienda, watu wakawa wanamsonga kila upande.
43 And, a woman, with a flow of blood of twelve years standing, who indeed could, from no one, be cured,
Kulikuwa na mwanamke mmoja kati ya lile kundi la watu, ambaye alikuwa na ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili, ingawa alikuwa amekwisha tumia mali yake yote kwa waganga, hakuna aliyefaulu kumponya.
44 coming near behind, touched the fringe of his mantle; and, instantly, was stayed the flow of her blood.
Huyo mwanamke alimfuata Yesu nyuma, akagusa pindo la vazi lake. Papo hapo akaponywa ugonjwa wake wa kutokwa damu.
45 And Jesus said—Who, is it that touched me? And, when all were denying, Peter said—Master! the multitudes, are hemming thee in, and pressing along.
Yesu akasema, “Ni nani aliyenigusa?” Wote wakasema kwamba hapakuwa na mtu aliyemgusa. Naye Petro akasema, “Mwalimu, umati wa watu umekuzunguka na kukusonga!”
46 But, Jesus, said—Some one touched me, for, I, took note of power, gone out from me.
Lakini Yesu akasema, “Kuna mtu aliyenigusa, maana nimehisi nguvu imenitoka.”
47 And, the woman seeing that she had not escaped notice, trembling, came, and, falling down before him, reported before all the people, for what cause she had touched him, and how she was healed instantly!
Yule mwanamke alipoona kwamba hawezi kujificha, akajitokeza akitetemeka kwa hofu, akajitupa mbele ya Yesu. Hapo akaeleza mbele ya wote kisa cha kumgusa Yesu na jinsi alivyoponyeshwa mara moja.
48 And, he, said to her—Daughter! thy faith, hath saved thee: Go thy way into peace.
Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani.”
49 While yet he is speaking, there cometh one from the synagogue ruler’s, saying—Thy daughter, is dead: No further, be troubling the teacher.
Alipokuwa bado akiongea, Yairo akaletewa habari kutoka nyumbani: “Binti yako ameshakufa, ya nini kumsumbua Mwalimu zaidi?”
50 But, Jesus, hearing, answered him—Do not fear! Only believe, and she shall be saved.
Yesu aliposikia hayo akamwambia Yairo, “Usiogope; amini tu, naye atapona.”
51 And, when he came into the house, he suffered no one to enter with him, save Peter and John and James, and the father of the girl, and the mother.
Alipofika nyumbani hakumruhusu mtu kuingia ndani pamoja naye, isipokuwa Petro, Yohane, Yakobo na wazazi wa huyo msichana.
52 And they were all weeping, and beating themselves, for her. And he said—Be not weeping; for she died not, but is sleeping.
Watu wote walikuwa wakilia na kuomboleza kwa ajili yake. Lakini Yesu akawaambia, “Msilie, kwa maana mtoto hajafa, amelala tu!”
53 And they were deriding him, knowing that she died.
Nao wakamcheka kwa sababu walijua kwamba alikuwa amekufa.
54 But, he, grasping her hand, called aloud, saying—O girl! arise!
Lakini Yesu akamshika mkono akasema, “Mtoto amka!”
55 And her spirit returned, and she rose up instantly, and he ordered that something should be given her to eat.
Roho yake ikamrudia, akaamka mara. Yesu akaamuru wampe chakula.
56 And her parents were beside themselves. But, he, charged them to tell, no one, what had happened.
Wazazi wake walishangaa, lakini Yesu akawaamuru wasimwambie mtu yeyote hayo yaliyotendeka.

< Luke 8 >