< Luke 5 >

1 And it came to pass, while the multitude was pressing upon him, and was hearing the word of God, that, he, was standing near the lake of Gennesaret;
Basi ilitokea wakati watu walipomkusanyikia na kumzunguka Yesu na kusikiliza neno la Mungu, ambapo alikuwa amesimama kando ya ziwa Genesareti.
2 and he saw two boats placed near the lake, and, the fishers, having gone away, from them, were washing their nets.
Aliona mashua mbili zimetia nanga pembeni mwa ziwa. Wavuvi walikuwa wametoka na walikuwa wakiosha nyavu zao.
3 And, entering into one of the boats, which was Simon’s, he requested him, to put off from the land, a little; and, taking a seat, out of the boat, began he teaching the multitudes.
Yesu akaingia katika mojawapo ya zile mashua, ambayo ilikuwa ya Simoni na kumwomba aipeleke majini mbali kidogo na nchi kavu. Kisha akakaa na kufundisha kutokea kwenye mashua.
4 And, when he ceased speaking, he said unto Simon—Put off into the deep, and let down your nets for a draught.
kuongea, akamwambia Simoni, “Ipeleke mashua yako mpaka kwenye kilindi cha maji nakushusha nyavu zako ili kuvua samaki.”
5 And Simon, answering, said—Master! although through the whole night we toiled, we took, nothing; howbeit, at thy bidding, I will let down the nets.
Simon akajibu na kusema, Bwana, tumefanya kazi usiku wote, na hatukukamata chochote, lakini kwa neno lako, nitazishusha nyavu.
6 And, when this they had done, they enclosed a very large number of fishes, and their nets began to break.
Walipofanya hivyo walikusanya kiasi kikubwa cha samaki na nyavu zao zikaanza kukatika.
7 And they made signs to their partners in the other boat, to come and help them; and they came, and filled both the boats, —so that they began to sink.
Hivyo wakawaashiria washirika wao kwenye mashua nyingine ili waja na kuwasaidia. Walikuja wakazijaza mashua zote, kiasi kwamba zikaanza kuzama.
8 And Simon, beholding, fell down at the knees of Jesus, saying—Depart from me! Because, a sinful man, am I, O Lord!
Lakini Simoni Petro, alipoona hivyo, alianguka magotini pa Yesu akisema,”Ondoka kwangu, kwa sababu mimi ni mtu mwenye dhambi Bwana.”
9 For, amazement, overcame him, and all them who were with him, on account of the draught of the fishes which they had taken;
Kwa sababu alishangazwa, na wote waliokuwa pamoja naye, kwa uvuvi wa samaki waliokuwa wameufanya.
10 likewise also, both James and John, sons of Zebedee, who were partners with Simon. And Jesus said unto Simon—Do not fear! henceforth, shall thou be taking, men, that they may, live.
Hili liliwajumuisha Yakobo na Yohana wana wa Zebedayo, ambao walikuwa washirika wa Simoni. Na Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope, kwa sababu kuanzia sasa na kuendelea utavua watu.”
11 And, bringing the boats down on to the land, they left all, and followed him.
Walipokwishazileta mashua zao nchi kavu, waliacha kila kitu na kumfuata yeye.
12 And it came to pass, while he was in one of the cities, that lo! there was a man full of leprosy; and, seeing Jesus, he fell on his face, and entreated him, saying—Lord! if thou be willing, thou canst cleanse me.
Ilitokea kwamba alipokuwa katika mji mmojawapo, mtu aliyekuwa amejaa ukoma alikuwa huko. Wakati alipomuona Yesu, alianguka akiinamisha uso kwake mpaka chini na kumuomba, akisema, “Bwana, ikiwa unataka, waweza kunitakasa.”
13 And, stretching forth the hand, he touched him, saying—I am willing: Be cleansed! And, straightway, the leprosy departed from him.
Kisha Yesu alinyoosha mkono wake na kumgusa, akisema, “Nataka. Takasika.” Na saa ileile ukoma ukamwacha.
14 And, he, charged him to tell, no one, —but, departing, Show thyself to the priest, and offer for thy cleansing, according as Moses enjoined, for a witness unto them.
“Alimwagiza asimwambie mtu yeyote, lakini alimwambia, “Nenda zako, na ukajionyeshe kwa makuhani na utoe sadaka ya utakaso wako, sawasawa na kile Musa alichokiamuru, kwa ushuhuda kwao.”
15 But the report concerning him the more went abroad, and many multitudes were coming together, to hear, and be getting cured from their infirmities;
Lakini habari kumuhusu yeye zikaenea mbali zaidi, na umati mkubwa wa watu ukaja pamoja kumsikiliza akifundisha na kuponywa magonjwa yao.
16 howbeit, he, was retiring in the deserts, and engaging in prayer.
Lakini mara kwa mara alijitenga faraghani na kuomba.
17 And it came to pass, on one of the days, that, he, was teaching, and there were sitting Pharisees and Teachers of the law, who had come out of every village of Galilee and Judaea and Jerusalem; and, the power of the Lord, was there, that he might heal.
Ilitokea siku moja kati ya hizo siku alikuwa akifundisha, na walikuwapo Mafarisayo na waalimu wa sheria wamekaa hapo ambao walikuja wakitokea vijiji vingi tofauti katika mkoa wa Galilaya na Yudea, na pia kutokea katika mji wa Yerusalemu. Nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye kuponya.
18 And lo! men bearing, upon a couch, one who was paralyzed, and they were seeking to bring him in, and lay him before him.
watu kadhaa walikuja, wamembeba kwenye mkeka mtu aliyepooza, na wakatafuta njia ya kumwingiza ndani ili kumlaza chini mbele ya Yesu.
19 And, not finding by what means they might bring him in, because of the multitude, going up on the house-top, through the tiling, let they him down, with the little-couch, into the midst before Jesus.
Hawakupata njia ya kumwingiza ndani kwa sababu ya umati, hivyo walipanda juu ya paa la nyumba na kumshusha yule mtu chini kupitia kwenye vigae, juu mkeka wake katikati ya watu, mbele kabisa ya Yesu.
20 And, beholding their faith, he said—O man! thy sins are forgiven thee.
Akiangalia imani yao, Yesu alisema, “Rafiki, dhambi zako umesamehewa.”
21 And the Scribes and the Pharisees began to reason, saying—Who is this that speaketh profanities? Who can forgive, sins, save, God alone?
Waandishi na Mafarisayo waliaanza kuhoji hilo, wakisema, “Huyu ni nani anayeongea makufuru? Ni nani anaweza kusamehe dhambi ila Mungu pekee yake?”
22 And Jesus, taking note of their reasonings, answering, said unto them—Why are ye reasoning in your hearts?
Lakini Yesu, akitambua nini walichokuwa wakifikiri, aliwajibu na kuwaambia, “Kwa nini mnaulizana hili mioyoni mwenu?
23 Which is easier, To say—Thy sins are forgiven thee; or to say—Arise and be walking?
Kipi ni rahisi kusema, 'Dhambi zako zimesamehewa' au kusema 'Simama utembee?'
24 But, that ye may know that, the Son of Man, hath, authority, upon the earth to forgive sins—he said to the paralyzed man—To thee, I say, Arise, and, taking up thy couch, be going thy way unto thy house.
Lakini mjue ya kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani ya kusamehe dhambi, Nakwambia wewe, 'Amka, chukua mkeka wako na uende nyumbani kwako.'”
25 And, instantly arising before them, he took up that whereon he had been lying, and departed unto his house, glorifying God.
Wakati huo huo akaamka mbele yao na akachukua mkeka wake aliokuwa ameulalia. Kisha akariudi nyumbani kwake akimtukuza Mungu.
26 And, astonishment, seized one and all, and they began glorifying God, and were filled with fear, saying—We have seen unaccountable things, to-day!
Kila mmoja alishangazwa na wakamtukuza Mungu. Walijawa na hofu, wakisema, “Tumeona mambo yasiyo ya kawaida leo.”
27 And, after these things, he went forth, and looked upon a tax-collector, by name Levi, —presiding over the tax-office; and he said to him—Be following me!
Baada ya mambo haya kutokea, Yesu alitoka huko na akamwona mtoza ushuru aliyeitwa Lawi amekaa eneo la kukusanyia kodi. Akamwambia, “Nifuate.”
28 And, forsaking all, he arose, and was following him.
Hivyo Lawi akanyanyuka na kumfuata, akiacha kila kitu nyuma.
29 And Levi made a great reception for him, in his house, and there was a great multitude of tax-collectors, and others, —who were with them reclining.
Kisha Lawi akaandaa nyumbani kwake karamu kubwa kwa ajili ya Yesu. Walikuwapo watozaushuru wengi kule na watu wengi walioketi mezani wakila pamoja nao.
30 And the Pharisees and their Scribes began murmuring unto his disciples, saying—Wherefore, with the tax-collectors and sinners, are ye eating and drinking?
Lakini Mafarisayo na waandishi wao walikuwa wakiwanung'unikia wanafunzi, wakisema, “Kwa nini mnakula na kunywa na watoza ushuru pamoja na watu wengine wenye dhambi?”
31 And, answering, Jesus said unto them—No need, have, the whole, of a physician, but, they who are sick.
Yesu akawajibu, “Watu walio katika afya njema hawahitaji tabibu, ni wale tu wanaoumwa ndiyo watakao mhitaji mmoja.
32 I have not come to call, righteous, men, but, sinners, unto repentance.
Sikuja kuwaita watu wenye haki haki wapate kutubu, bali kuwaita wenye dhambi wapate kutubu.”
33 But, they, said unto him—The disciples of John, do fast much, and, supplications, do make, —likewise also the disciples of the Pharisees; but, thine, do eat and drink!
Wakamwambia, “Wanafunzi wa Yohana mara nyingi hufunga na kuomba, na wanafunzi wa Mafarisayo nao hufanya vivyo hivyo. Lakini wanafunzi wako hula na kunywa.”
34 Jesus, however, said unto them—Can, ye make, the sons of the bridechamber, fast, while the bridegroom is with them?
Yesu akawaambia, “Inawezekana mtu yeyote akawafanya waliohudhuria harusi ya Bwana Arusi kufunga wakati Bwana Arusi bado yu pamoja nao?
35 But there will come days, even when the bridegroom shall be taken from them, then, will they fast, in those days.
Lakini siku zitakuja wakati Bwana Arusi atakapoondolewa kwao, ndipo katika siku hizo watafunga.”
36 Moreover, he went on to speak, a parable also, unto them—No one, rending a patch from a new mantle, patcheth it upon an old mantle; otherwise, at least, both, the new, he will rend, and, with the old, the patch which is from the new, will not agree.
Kisha Yesu aliongea pia kwao kwa mfano. “Hakuna anayechana kipande cha nguo kutoka kwenye vazi jipya na kukitumia kurekebisha vazi la zamani. Kama akifanya hivyo, ataichana nguo mpya, na kipande cha nguo kutoka vazi jipya kisengefaa kutumika na nguo ya vazi la zamani.
37 And, no one, poureth new wine into old skins; otherwise, at least, the new wine, will burst the skins, and will, itself, be poured out, and the skins be destroyed.
pia, hakuna mtu ambaye huweka divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Kama akifanya hivyo, divai mpya ingepasua kile chombo, na divai ingemwagika, na viriba vingeharibika.
38 But, new wine, into unused skins, must be poured.
Lakini divai mpya lazima iwekwe kwenye viriba vipya.
39 [No one, having drunk old, desireth new; for he saith, The old, is, mellow.]
Na hakuna mtu baada ya kunywa divai ya zamani, hutataka mpya, kwa sababu husema, 'Ya zamani ni bora.”'

< Luke 5 >