< Luke 10 >

1 And, after these things, the Lord appointed seventy two others, and sent them forth, two and two before his face, into every city and place whither, he himself, was about to come.
Baada ya hayo, Bwana aliwachagua wengine sabini na wawili, akawatuma wawiliwawili, wamtangulie katika kila kijiji na mahali ambapo yeye mwenyewe alitaka kwenda.
2 And he was saying unto them—The harvest, indeed, is, great, but, the labourers, few; beg ye, therefore, of the Lord of the harvest, that he would thrust forth, labourers, into his harvest.
Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache. Kwa hivyo, mwombeni mwenye shamba atume wavunaji shambani mwake.
3 Withdraw! Lo! I send you forth as lambs amid wolves.
Sasa nendeni; fahamuni kwamba ninawatuma ninyi kama kondoo wanaokwenda kati ya mbwa mwitu.
4 Be not carrying purse, or satchel, or sandals, and, no one along the road, salute ye;
Msichukue mfuko wa fedha, mkoba, wala viatu; msimsalimu mtu yeyote njiani.
5 And, into whatsoever house ye enter, First, say, Peace to this house!
Mkiingia katika nyumba yoyote, kwanza wasalimuni hivi: Amani iwe katika nyumba hii!
6 And, if the son of peace be, there, your peace, shall rest upon it; but, otherwise, at least, unto you, shall it return.
Kama akiwako mwenye kupenda amani, amani yenu itakaa naye, la sivyo, itawarudieni.
7 And, in the self-same house, abide ye, eating and drinking such things as they have; for, worthy, is the labourer, of his hire: be not removing from house to house.
Kaeni katika nyumba hiyo mkila na kunywa wanavyowapeni, maana mfanyakazi anastahili mshahara wake. Msiende mara nyumba hii mara nyumba ile.
8 And, into whatsoever city ye shall enter, and they bid you welcome, be eating such things as are set before you;
Kama mkifika mji fulani na watu wakiwakaribisha, kuleni wanavyowapeni.
9 And be curing the sick that are, therein, and be saying unto them—The kingdom of God hath drawn nigh upon you.
Ponyeni wagonjwa walioko huko, waambieni watu: Ufalme wa Mungu umekaribia kwenu.
10 But, into whatsoever city ye shall enter, and they do not welcome you, going forth into the broadways thereof, say ye:
Lakini mkiingia katika mji wowote, wasipowakaribisheni, tokeni; nanyi mpitapo katika barabara zao semeni:
11 Even the dust that cleaveth unto us, out of your city, unto our feet, do we wipe off against you; nevertheless, of this, be taking notice—The kingdom of God hath drawn near.
Hata mavumbi ya mji wenu yaliyoshikamana na miguu yetu tunawakung'utieni. Lakini, jueni kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
12 I tell you, for them of Sodom, in that day, more tolerable, will it be, than for that city.
Hakika nawaambieni, siku ile mji huo utapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Sodoma.
13 Alas for thee, Chorazin! Alas for thee, Bethsaida! Because, if, in Tyre and Zidon, had been done the works of power which have been down in you, of old, in sackcloth and ashes sitting, they would have repented.
“Ole wako Korazini! Ole wako Bethsaida! Maana, kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika kule Tiro na Sidoni, watu wake wangalikwishavaa mavazi ya gunia kitambo, na kukaa katika majivu kuonyesha kwamba wametubu.
14 Moreover, for Tyre and Zidon, more tolerable, will it be, in the judgment, than, for you.
Hata hivyo, Siku ya Hukumu ninyi mtapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Tiro na Sidoni.
15 And, thou, Capernaum, —Unto heaven, shalt thou be uplifted? …Unto hades, thou shalt be brought down! (Hadēs g86)
Na wewe Kafarnaumu, unataka kujikweza mpaka mbinguni? La; utaporomoshwa mpaka Kuzimu.” (Hadēs g86)
16 He that hearkeneth unto you, unto me, doth hearken, and, he that setteth you aside, doth set, me, aside; and, he that setteth, me, aside, doth set aside, him that sent me.
Halafu akasema, “Anayewasikiliza ninyi, ananisikiliza mimi; na anayekataa kuwapokea ninyi, anakataa kunipokea mimi. Yeyote anayekataa kunipokea, anakataa kumpokea yule aliyenituma.”
17 And the seventy [-two] returned, with joy, saying—Lord! even the demons, submit themselves unto us, in thy name!
Baadaye, wale sabini na wawili walirudi wamejaa furaha, wakisema, “Bwana, hata pepo wametutii tulipolitaja jina lako.”
18 And he said unto them—I was beholding Satan, when, like lightning, out of heaven, he fell!
Yeye akawaambia, “Nilimwona Shetani jinsi alivyokuwa anaporomoka kama umeme kutoka mbinguni.
19 Lo! I have given you the authority—to be treading upon serpents and scorpions, and over all the power of the enemy, and, nothing, unto you, shall in anywise do harm;
Naam, nimewapeni uwezo wa kukanyaga nyoka na ng'e, na uwezo juu ya nguvu zote za yule adui; hakuna chochote kitakachowadhuru.
20 Notwithstanding, in this, be not rejoicing—that, the spirits, unto you submit themselves; but be rejoicing—that, your names, are inscribed in the heavens!
Hata hivyo, msifurahi kwa sababu pepo wamewatii, bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.”
21 In the self-same hour, exulted he in the Holy Spirit, and said—I openly give praise unto thee, Father! Lord of heaven and earth! in that thou hast hid these things from the wise and discerning, and hast revealed them unto babes, —Yea, O Father! that, so, hath it become, a delight, before thee.
Saa ileile, Yesu akafurahi kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, akasema, “Nakushukuru ee Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa kuwa umewaficha wenye hekima na elimu mambo haya, ukawafumbulia wadogo. Naam, Baba, ndivyo ilivyokupendeza.”
22 All things, unto me, have been delivered up by my Father; and, no one, knoweth, who the Son is, save the Father, —and who the Father is, save the Son, and he to whomsoever the Son may be minded to reveal him.
Kisha akasema, “Baba yangu ameweka yote mikononi mwangu. Hakuna amjuaye Mwana ni nani ila Baba, wala amjuaye Baba ni nani ila Mwana, na yeyote yule ambaye Mwana anataka kumfunulia hayo.”
23 And, turning unto his disciples, privately, he said—Happy, the eyes, that see what ye see!
Halafu akawaelekea wafuasi wake akawaambia, “Heri wanaoona yale mnayoyaona ninyi!
24 For I tell you, Many prophets and kings, have desired to see what, ye, see, and they saw not, and to hear what ye hear, and they heard not.
Hakika, manabii na wafalme walitamani kuona yale mnayoyaona ninyi wasiyaone, na kusikia yale mnayoyasikia wasiyasikie.”
25 And lo! a certain lawyer, arose, putting him to the test, saying—Teacher! by doing what, shall I inherit, life age-abiding? (aiōnios g166)
Baadaye mwalimu mmoja wa Sheria alisimama akamwuliza akitaka kumtega, “Mwalimu, nifanye nini ili nipate uzima wa milele?” (aiōnios g166)
26 And, he, said unto him—In the law, what is written? how dost thou read?
Yesu akamwuliza, “Imeandikwa nini katika Sheria? Unaelewaje?”
27 And, he, answering, said—Thou shalt love the Lord thy God, out of all thy heart, and with all thy soul, and with all thy might, and with all thine intention; and thy neighbour, as thyself?
Akamjibu, “Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote na kwa akili yako yote. Na, mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”
28 And he said unto him—Rightly, hast thou answered: This, do, and thou shalt live.
Yesu akawaambia, “Vema! Fanya hivyo, nawe utaishi.”
29 But, he, wishing to justify himself, said unto Jesus—And, who is, my, neighbour?
Lakini yeye akitaka kujihakikishia kuwa mwema akamwuliza Yesu, “Na jirani yangu ni nani?”
30 And taking up [the question], Jesus said—A certain man, was going down from Jerusalem unto Jericho, and, with robbers, fell in, —who, stripping him, and inflicting, wounds, upon him, departed, leaving him, half dead.
Yesu akamjibu, “Mtu mmoja alikuwa anashuka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko. Alipokuwa njiani, alivamiwa na majambazi, wakamnyang'anya mali yake na kumpiga, wakamwacha amelala pale nusu mfu.
31 And, by chance, a certain priest, was coming down by that road, and, seeing him, passed by, on the opposite side.
Kumbe, kuhani mmoja akawa anapita barabara ileile, akamwona, akapita kando.
32 And, in like manner, a Levite also, coming down to the place, and seeing him, passed by, on the opposite side.
Hali kadhalika na Mlawi mmoja, alipofika mahali akamwona, akapita kando.
33 But, a certain Samaritan, going on his journey, came down to him, and, seeing him, was moved with compassion;
Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa anasafiri, alifika pale yule mtu alipokuwa, naye alipomwona, alimwonea huruma.
34 and, coming near, bound up his bruises, pouring thereon oil and wine, —and, setting him on his own beast, brought him into an inn, and took care of him.
Akamwendea, akamtibu majeraha yake kwa kumtia mafuta na divai; na kuyafunga halafu akampandisha juu ya punda wake akampeleka katika nyumba moja ya wageni akamuuguza.
35 And, on the morrow, throwing out two denaries, he gave them to the inn-keeper, and said—Take care of him, and, whatsoever thou shall further spend, I, when on my way back, will duly pay thee.
Kesho yake akatoa fedha dinari mbili akampa yule mwenye nyumba, akamwambia, Muuguze mtu huyu; na chochote utakachotumia zaidi, nitakulipa nitakaporudi.”
36 Which of these three, seemeth unto thee to have become, neighbour, unto him who fell among the robbers?
Kisha Yesu akauliza, “Kati ya hao watatu, ni yupi aliyeonyesha kuwa jirani yake yule aliyevamiwa na majambazi?”
37 And, he, said—He who dealt mercifully with him. And Jesus said unto him—Be taking thy journey, and, thou, be doing, in like manner.
Yule mwalimu wa Sheria akamjibu, “Ni yule aliyemwonea huruma.” Yesu akamwambia, “Nenda ukafanye vivyo hivyo.”
38 And, as they were journeying, he, entered into a certain village; and, a certain woman, named Martha, welcomed him into her house.
Walipokuwa safarini, waliingia katika kijiji kimoja na mwanamke mmoja, aitwaye Martha, alimkaribisha nyumbani kwake.
39 And, she, had a sister, called Mary, who also, seating herself at the feet of the Lord, was hearing his word.
Martha alikuwa na dada yake aitwaye Maria; huyu aliketi karibu na Yesu akisikiliza mafundisho yake.
40 But, Martha, was distracted about much ministering, and, coming near, said—Lord! carest thou not that, my sister, hath left me to be ministering, alone? Speak to her, then, that she help me.
Lakini Martha alikuwa anashughulika na mambo mengi. Basi, akamwendea Yesu, akamwambia, “Bwana, hivi hujali kwamba dada yangu ameniacha nishughulike peke yangu? Mwambie basi, anisaidie.”
41 But the Lord, answering, said to her—Martha! Martha! thou art anxious and troubled about many things:
Lakini Bwana akamjibu, “Martha, Martha, unahangaika na kusumbuka kwa mambo mengi.
42 Of few things, is there need, or, of one; Mary, in fact, hath chosen, the good part, —one which shall not be taken away from her.
Kitu kimoja tu ni muhimu. Maria amechagua kitu bora zaidi ambacho hakuna mtu atakayemnyag'anya.”

< Luke 10 >