< Luke 10 >

1 And, after these things, the Lord appointed seventy two others, and sent them forth, two and two before his face, into every city and place whither, he himself, was about to come.
Baada ya hayo, Bwana akawachagua wengine sabini na wawili, akawatuma wawili wawili katika kila mji na kila sehemu aliyokusudia kwenda baadaye.
2 And he was saying unto them—The harvest, indeed, is, great, but, the labourers, few; beg ye, therefore, of the Lord of the harvest, that he would thrust forth, labourers, into his harvest.
Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini watendakazi ni wachache. Kwa hiyo mwombeni Bwana wa mavuno, ili apeleke watendakazi katika shamba lake la mavuno.
3 Withdraw! Lo! I send you forth as lambs amid wolves.
Haya! nendeni. Ninawatuma kama wana-kondoo katikati ya mbwa mwitu.
4 Be not carrying purse, or satchel, or sandals, and, no one along the road, salute ye;
Msichukue mkoba, wala mfuko, wala viatu, na msimsalimu mtu yeyote njiani.
5 And, into whatsoever house ye enter, First, say, Peace to this house!
“Mkiingia katika nyumba yoyote, kwanza semeni, ‘Amani iwe kwenu.’
6 And, if the son of peace be, there, your peace, shall rest upon it; but, otherwise, at least, unto you, shall it return.
Kama kuna mtu wa amani humo, basi amani yenu itakuwa juu yake. La sivyo, itawarudia.
7 And, in the self-same house, abide ye, eating and drinking such things as they have; for, worthy, is the labourer, of his hire: be not removing from house to house.
Kaeni katika nyumba hiyo, mkila na kunywa kile watakachowapa, kwa sababu kila mtendakazi anastahili malipo yake. Msihamehame kutoka nyumba hadi nyumba.
8 And, into whatsoever city ye shall enter, and they bid you welcome, be eating such things as are set before you;
“Mkienda katika mji na watu wake wakawakaribisha, kuleni chochote kiwekwacho mbele yenu,
9 And be curing the sick that are, therein, and be saying unto them—The kingdom of God hath drawn nigh upon you.
waponyeni wagonjwa waliomo na waambieni: ‘Ufalme wa Mungu umekaribia.’
10 But, into whatsoever city ye shall enter, and they do not welcome you, going forth into the broadways thereof, say ye:
Lakini mkiingia katika mji, nao hawakuwakaribisha, tokeni mwende katika barabara zake mkaseme:
11 Even the dust that cleaveth unto us, out of your city, unto our feet, do we wipe off against you; nevertheless, of this, be taking notice—The kingdom of God hath drawn near.
‘Hata mavumbi ya mji wenu yaliyoshikamana na miguu yetu, tunayakungʼuta dhidi yenu. Lakini mjue kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.’
12 I tell you, for them of Sodom, in that day, more tolerable, will it be, than for that city.
Ninawaambia, itakuwa rahisi zaidi kwa Sodoma kustahimili katika siku ile kuliko mji ule.
13 Alas for thee, Chorazin! Alas for thee, Bethsaida! Because, if, in Tyre and Zidon, had been done the works of power which have been down in you, of old, in sackcloth and ashes sitting, they would have repented.
“Ole wako Korazini! Ole wako Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwenu ingefanyika Tiro na Sidoni, miji hiyo ingekuwa imetubu zamani, kwa kuvaa magunia na kujipaka majivu.
14 Moreover, for Tyre and Zidon, more tolerable, will it be, in the judgment, than, for you.
Lakini itakuwa rahisi zaidi kwa Tiro na Sidoni kustahimili katika siku ya hukumu, kuliko ninyi.
15 And, thou, Capernaum, —Unto heaven, shalt thou be uplifted? …Unto hades, thou shalt be brought down! (Hadēs g86)
Nawe, Kapernaumu, je, utainuliwa hadi mbinguni? La hasha, utashushwa mpaka kuzimu.” (Hadēs g86)
16 He that hearkeneth unto you, unto me, doth hearken, and, he that setteth you aside, doth set, me, aside; and, he that setteth, me, aside, doth set aside, him that sent me.
“Yeye awasikilizaye ninyi anisikiliza mimi; naye awakataaye ninyi amenikataa mimi. Lakini yeye anikataaye mimi amkataa yeye aliyenituma.”
17 And the seventy [-two] returned, with joy, saying—Lord! even the demons, submit themselves unto us, in thy name!
Wale sabini na wawili wakarudi kwa furaha, na kusema, “Bwana, hata pepo wachafu wanatutii kwa jina lako.”
18 And he said unto them—I was beholding Satan, when, like lightning, out of heaven, he fell!
Yesu akawaambia, “Nilimwona Shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme wa radi.
19 Lo! I have given you the authority—to be treading upon serpents and scorpions, and over all the power of the enemy, and, nothing, unto you, shall in anywise do harm;
Tazama nimewapa mamlaka ya kukanyaga nyoka na nge na juu ya nguvu zote za adui; wala hakuna kitu chochote kitakachowadhuru.
20 Notwithstanding, in this, be not rejoicing—that, the spirits, unto you submit themselves; but be rejoicing—that, your names, are inscribed in the heavens!
Basi, msifurahi kwa kuwa pepo wachafu wanawatii, bali furahini kwa kuwa majina yenu yameandikwa mbinguni.”
21 In the self-same hour, exulted he in the Holy Spirit, and said—I openly give praise unto thee, Father! Lord of heaven and earth! in that thou hast hid these things from the wise and discerning, and hast revealed them unto babes, —Yea, O Father! that, so, hath it become, a delight, before thee.
Wakati huo Yesu akashangilia katika Roho Mtakatifu, akasema, “Nakuhimidi Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa umewaficha mambo haya wenye hekima na wenye elimu, nawe ukawafunulia watoto wadogo. Naam, Baba, kwa kuwa hivyo ndivyo ilivyokupendeza.
22 All things, unto me, have been delivered up by my Father; and, no one, knoweth, who the Son is, save the Father, —and who the Father is, save the Son, and he to whomsoever the Son may be minded to reveal him.
“Nimekabidhiwa vitu vyote na Baba yangu. Hakuna mtu amjuaye Mwana ni nani ila Baba, wala hakuna amjuaye Baba ni nani ila Mwana na yeyote ambaye Mwana anapenda kumfunulia.”
23 And, turning unto his disciples, privately, he said—Happy, the eyes, that see what ye see!
Basi Yesu akawageukia wanafunzi wake akanena nao faraghani, akawaambia, “Heri macho yanayoona yale mambo mnayoyaona.
24 For I tell you, Many prophets and kings, have desired to see what, ye, see, and they saw not, and to hear what ye hear, and they heard not.
Kwa maana nawaambia, manabii wengi na wafalme walitamani kuona yale mnayoyaona lakini hawakuyaona, na walitamani kusikia yale mnayoyasikia lakini hawakuyasikia.”
25 And lo! a certain lawyer, arose, putting him to the test, saying—Teacher! by doing what, shall I inherit, life age-abiding? (aiōnios g166)
Wakati huo mtaalamu mmoja wa sheria alisimama ili kumjaribu Yesu, akamuuliza, “Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?” (aiōnios g166)
26 And, he, said unto him—In the law, what is written? how dost thou read?
Yesu akamjibu, “Imeandikwaje katika Sheria? Kwani unasoma nini humo?”
27 And, he, answering, said—Thou shalt love the Lord thy God, out of all thy heart, and with all thy soul, and with all thy might, and with all thine intention; and thy neighbour, as thyself?
Akajibu, “‘Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote’; tena, ‘Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.’”
28 And he said unto him—Rightly, hast thou answered: This, do, and thou shalt live.
Yesu akamwambia, “Umejibu vyema. Fanya hivyo nawe utaishi.”
29 But, he, wishing to justify himself, said unto Jesus—And, who is, my, neighbour?
Lakini yule mtaalamu wa sheria, akitaka kujionyesha kuwa mwenye haki, akamuuliza Yesu, “Jirani yangu ni nani?”
30 And taking up [the question], Jesus said—A certain man, was going down from Jerusalem unto Jericho, and, with robbers, fell in, —who, stripping him, and inflicting, wounds, upon him, departed, leaving him, half dead.
Yesu akamjibu akasema, “Mtu mmoja alikuwa akiteremka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko, naye akaangukia mikononi mwa wanyangʼanyi. Wakampiga, wakaondoka, wakamwacha akiwa karibu kufa.
31 And, by chance, a certain priest, was coming down by that road, and, seeing him, passed by, on the opposite side.
Kuhani mmoja alikuwa akipitia njia ile, alipomwona huyo mtu, akapita upande mwingine, akamwacha hapo barabarani.
32 And, in like manner, a Levite also, coming down to the place, and seeing him, passed by, on the opposite side.
Vivyo hivyo, Mlawi mmoja naye alipofika mahali pale, alimwona, akapita upande mwingine, akamwacha hapo barabarani
33 But, a certain Samaritan, going on his journey, came down to him, and, seeing him, was moved with compassion;
Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa akisafiri alipomwona, alimhurumia.
34 and, coming near, bound up his bruises, pouring thereon oil and wine, —and, setting him on his own beast, brought him into an inn, and took care of him.
Akaenda alipokuwa na akasafisha majeraha yake kwa divai na mafuta, kisha akayafunga. Ndipo akampandisha kwenye punda wake, akampeleka mpaka kwenye nyumba ya wageni na kumtunza.
35 And, on the morrow, throwing out two denaries, he gave them to the inn-keeper, and said—Take care of him, and, whatsoever thou shall further spend, I, when on my way back, will duly pay thee.
Kesho yake, yule Msamaria akachukua dinari mbiliakampa yule mwenye nyumba ya wageni na kusema, ‘Mtunze, nami nirudipo nitakulipa gharama yoyote ya ziada uliyotumia kwa ajili yake.’
36 Which of these three, seemeth unto thee to have become, neighbour, unto him who fell among the robbers?
“Ni yupi basi miongoni mwa hawa watatu wewe unadhani ni jirani yake yule mtu aliyeangukia mikononi mwa wanyangʼanyi?”
37 And, he, said—He who dealt mercifully with him. And Jesus said unto him—Be taking thy journey, and, thou, be doing, in like manner.
Yule mtaalamu wa sheria akajibu, “Ni yule aliyemhurumia.” Ndipo Yesu akamwambia, “Nenda, ukafanye vivyo hivyo.”
38 And, as they were journeying, he, entered into a certain village; and, a certain woman, named Martha, welcomed him into her house.
Ikawa Yesu na wanafunzi wake walipokuwa wakienda Yerusalemu, akaingia kwenye kijiji kimoja ambapo mwanamke mmoja aliyeitwa Martha alimkaribisha nyumbani kwake.
39 And, she, had a sister, called Mary, who also, seating herself at the feet of the Lord, was hearing his word.
Martha alikuwa na mdogo wake aliyeitwa Maria, ambaye aliketi chini miguuni mwa Bwana akisikiliza yale aliyokuwa akisema.
40 But, Martha, was distracted about much ministering, and, coming near, said—Lord! carest thou not that, my sister, hath left me to be ministering, alone? Speak to her, then, that she help me.
Lakini Martha alikuwa akihangaika na maandalizi yote yaliyokuwa yafanyike. Martha akaja kwa Yesu na kumuuliza, “Bwana, hujali kwamba ndugu yangu ameniachia kazi zote mwenyewe? Basi mwambie anisaidie.”
41 But the Lord, answering, said to her—Martha! Martha! thou art anxious and troubled about many things:
Lakini Bwana akamjibu, “Martha, Martha, mbona unasumbuka na kuhangaika na mengi?
42 Of few things, is there need, or, of one; Mary, in fact, hath chosen, the good part, —one which shall not be taken away from her.
Lakini kunahitajika kitu kimoja tu. Maria amechagua kile kilicho bora, wala hakuna mtu atakayemwondolea.”

< Luke 10 >