< Leviticus 14 >

1 And Yahweh spake unto Moses, saying—
Bwana akamwambia Mose,
2 This, shall be the law of the leper, in the day when he is declared clean, —he shall be brought in unto the priest;
“Haya ndiyo masharti yamhusuyo mtu mgonjwa wakati wa kufanyiwa ibada ya utakaso wakati aletwapo kwa kuhani:
3 then shall the priest go forth unto the outside of the camp, —and the priest shall take a view, and lo! if the plague of leprosy hath been healed out of the leper;
Kuhani atakwenda kumchunguza nje ya kambi. Kama mtu huyo atakuwa amepona ugonjwa wake wa ngozi wa kuambukiza,
4 then shall the priest give command, —and there shall be taken—for him that is to be cleansed—two living clean birds, —and cedar wood, and crimson am hyssop;
kuhani ataagiza vitu vifuatavyo viletwe kwa ajili ya mtu atakayetakaswa: ndege wawili safi walio hai, mti wa mwerezi, kitani nyekundu, na hisopo.
5 and the priest shall give command, and one bird shall be slain, —within an earthen vessel over living water:
Kisha kuhani ataagiza kwamba mmoja wa ndege wale achinjwe kwenye chungu chenye maji safi.
6 as for the living bird, he shall take, it, and the cedar wood and the crimson, and the hyssop, —and shall dip them and the living bird, in the blood of the bird that hath been slain over the living water;
Kisha kuhani atamchukua ndege aliye hai na kumtumbukiza pamoja na mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo ndani ya damu ya yule ndege aliyechinjiwa kwenye maji safi.
7 and shall sprinkle upon him that is to be cleansed from the leprosy, seven times, —and shall pronounce him clean, and shall let go the living bird over the face of the field.
Atamnyunyizia yule mwenye ugonjwa wa kuambukiza maji hayo mara saba, na kumtangaza kuwa safi. Kisha atamwachia yule ndege aliye hai aende zake kwenye mashamba.
8 And he that is to be declared clean shall wash his clothes and shave off all his hair, and bathe in water, and be clean, and, afterwards, shall he come into the camp, —and dwell outside his tent, seven days;
“Huyo mtu atakayetakaswa ni lazima afue nguo zake, anyoe nywele zake zote, na aoge kwa maji; ndipo atakapokuwa safi kwa desturi ya ibada. Baada ya hili anaweza kuingia kambini, lakini ni lazima akae nje ya hema lake kwa siku saba.
9 and it shall be on the seventh day, that he shall shave off all the hair of his head, and his beard, and his eyebrows, even all his hair, shall he shave off, —and shall wash his clothes and bathe his flesh in water so shall he be clean.
Siku ya saba ni lazima anyoe nywele zake zote; yaani anyoe nywele za kichwa, ndevu zake, kope zake na nywele nyingine zote. Ni lazima afue nguo zake, na aoge kwa maji, naye atakuwa safi.
10 And, on the eighth day, he shall take two he-lambs, without defect, and one ewe-lamb, the choice of its year without defect, —and three-tenths of fine meal for a meal-offering, overflowed with oil, and one log of oil.
“Siku ya nane, ni lazima alete kondoo dume wawili na kondoo jike mmoja, wote wa mwaka mmoja na wasio na dosari, pamoja na sehemu tatu za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta, kwa ajili ya sadaka ya nafaka, na logi moja ya mafuta.
11 And the priest that is cleansing him shall cause the man that is to be cleansed, and those things to stand before Yahweh, at the opening of the tent of meeting.
Kuhani atakayemtangaza kuwa safi atahitaji kumkabidhi mgonjwa aliyepona pamoja na sadaka zake zote mbele za Bwana katika ingilio la Hema la Kukutania.
12 And the priest shall take one he-lamb, and bring him near as a guilt-bearer and the log of oil, —and shall wave them as a wave-offering, before Yahweh;
“Kisha kuhani atamchukua mmoja wa wale kondoo dume na kumtoa kuwa sadaka ya hatia, pamoja na ile logi moja ya mafuta; ataviinua mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
13 and shall slay the lamb in the place where the sin-bearer and the ascending-sacrifice are slain, in the holy place, —for like the sin-bearer, the guilt-bearer, is the priest’s, most holy, it is.
Atamchinja huyo kondoo katika mahali patakatifu ambapo sadaka ya dhambi na ile ya kuteketezwa huchinjiwa. Kama ilivyo sadaka ya dhambi, sadaka ya hatia ni ya kuhani; nayo ni takatifu sana.
14 Then shall the priest take of the blood of the guilt-bearer, and the priest shall put it upon the tip of the right ear of him that is to be cleansed, —and upon the thumb of his right hand, and upon the great toe of his right foot;
Kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya hatia na kuitia kwenye ncha ya sikio la kuume la yule atakayetakaswa, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
15 and the priest shall take of the log of oil, —and shall pour it upon the palm of the priest’s left hand,
Kuhani atachukua sehemu ya ile logi ya mafuta, ayamimine kwenye kiganja cha mkono wake mwenyewe wa kushoto,
16 and the priest shall dip his right finger [and take] of the oil that is on the palm of his left hand, —and shall sprinkle of the oil with his finger seven times before Yahweh:
na achovye kidole chake cha shahada cha mkono wake wa kuume kwenye mafuta yaliyoko kwenye kiganja chake, na kwa kidole hicho anyunyize mafuta hayo mara saba mbele za Bwana.
17 and of the remainder of the oil which is on the palm of his hand, shall the priest put upon the tip of the right ear of him that is to be cleansed, and upon the thumb of his right hand, and upon the great toe of his right foot, —upon the blood of the guilt-bearer;
Kuhani atampaka yule anayetakaswa sehemu ya mafuta yaliyobaki kiganjani kwenye ncha ya sikio lake la kuume, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume, mahali palepale alipompaka damu ya sadaka ya kuondoa hatia.
18 and that which remaineth of the oil that is on the palm of the priest’s hand, he shall put upon the head of him that is to be cleansed, —so shall the priest put a propitiatory-covering over him, before Yahweh.
Kuhani atayapaka mafuta yaliyobaki kwenye kiganja chake juu ya kichwa cha yule anayetakaswa, na kufanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana.
19 Then shall the priest offer the sin-bearer, and shall put a propitiatory-covering over him that is to be cleansed because of his uncleanness, —and, afterwards, shall he slay the ascending-sacrifice.
“Kisha kuhani atatoa dhabihu ya sadaka ya dhambi na kufanya upatanisho kwa ajili ya yule atakayetakaswa kutoka unajisi wake. Baada ya hayo, kuhani atachinja sadaka ya kuteketezwa
20 And the priest shall cause the ascending-sacrifice, and the meal-offering to ascend at the altar, —so shall the priest put a propitiatory-covering over him, and he shall be clean.
na kuitoa juu ya madhabahu, pamoja na sadaka ya nafaka ili kumfanyia upatanisho, naye atakuwa safi.
21 But if he be poor and his hand hath not enough, then shall he take one he-lamb as a guilt-bearer to be waved to put a propitiatory-covering over him, —and one-tenth of fine meal, overflowed with oil for a meal-offering, and a log of oil,
“Hata hivyo, kama ni maskini na hawezi kupata vitu hivi, lazima achukue mwana-kondoo mmoja kama sadaka ya hatia ipate kuinuliwa ili kumfanyia upatanisho, pamoja na sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na logi moja ya mafuta kwa ajili ya sadaka ya nafaka,
22 and two turtle-doves or two young pigeons, for which his hand hath enough, —so shall one be a sin-bearer, and the other an ascending-sacrifice.
na hua wawili au makinda mawili ya njiwa, kile atakachoweza kupata, mmoja kwa sadaka ya dhambi, na mwingine kwa sadaka ya kuteketezwa.
23 And he shall bring them in on the eighth day, for his cleansing, unto the priest, —unto the entrance of the tent of meeting, before Yahweh.
“Katika siku ya nane, lazima avilete vitu hivyo kwa kuhani, kwa ajili ya kutakaswa kwake kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana.
24 Then shall the priest take the guilt-bearing lamb and the log of oil, —and the priest shall wave them as a wave-offering, before Yahweh.
Kuhani atamchukua mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya hatia, pamoja na ile logi ya mafuta ya kuinuliwa mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
25 Then shall the guilt-bearing lamb be slain, and the priest shall take of the blood of the guilt-bearer, and put upon the tip of the right ear of him that is to be cleansed, —and upon the thumb of his right hand, and upon the great toe of his right foot;
Atamchinja huyo mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya hatia. Pia ataichukua sehemu ya damu yake na kuipaka kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayetakaswa, na aipake pia kwenye kidole gumba cha mkono wa kuume wa huyo mtu, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
26 also of the oil, shall the priest pour out, —on the palm of his own left hand;
Kuhani atamiminia sehemu ya mafuta kwenye kiganja chake cha mkono wa kushoto,
27 and the priest shall sprinkle with his right finger, of the oil that is on the palm of his left hand, —seven times, before Yahweh;
na kwa kidole chake cha shahada cha mkono wa kuume, atamnyunyizia yule anayetakaswa yale mafuta yaliyo kwenye kiganja chake mara saba mbele za Bwana.
28 then shall the priest put, of the oil that is on the palm of his hand, upon the tip of the right ear of him that is to be cleansed, and upon the thumb of his right hand, and upon the great toe of his right foot, —upon the place of the blood of the guilt-offering;
Atampaka mafuta yaliyobaki kwenye kiganja chake katika sehemu zote, kama alivyompaka damu ya sadaka ya hatia: yaani, kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayetakaswa, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
29 and that which remaineth of the oil which is on the palm of the priest’s hand, shall he put upon the head of him that is to be cleansed, —to put a propitiatory-covering over him before Yahweh.
Kuhani atayapaka mafuta yaliyobaki katika kiganja chake kwenye kichwa cha yule anayetakaswa, na kufanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana.
30 Then shall he offer one of the turtle-doves, or of the young pigeons, —of that for which his hand hath enough;
Kisha atatoa dhabihu wale hua ama yale makinda ya njiwa ambayo mtu ataweza kuwapata,
31 even that for which his hand hath enough, —the one as a sin-bearer and the other as an ascending-sacrifice, upon the meal-offering, —so shall the priest put a propitiatory-covering over him that is to be cleansed before Yahweh.
mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sadaka ya nafaka. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya yule anayetakaswa.”
32 This is the law for him in whom hath been the plague of leprosy, whose hand hath not enough for that which pertaineth to his cleansing.
Haya ndiyo masharti kwa mtu yeyote mwenye ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, na ambaye hana uwezo wa kutoa sadaka za kawaida kwa ajili ya kutakaswa kwake.
33 And Yahweh spake unto Moses and unto Aaron saying:
Bwana akawaambia Mose na Aroni,
34 When ye enter into the land of Canaan which I am about to give you for a possession, —and I put a plague-mark of leprosy in a house, of the land of your possession,
“Mtakapoingia katika nchi ya Kanaani ambayo ninawapa kuwa milki yenu, nami nikaweka upele ueneao kwenye nyumba katika nchi ile,
35 then shall he that owneth the house come in, and tell the priest, saying, —A kind of plague-mark, appeareth to me in the house;
ni lazima mwenye nyumba hiyo akamwambie kuhani, ‘Nimeona kitu fulani kinachofanana na upele kwenye nyumba yangu.’
36 and the priest shall give command, and they shall empty the house, ere yet the priest cometh in to view the mark, so that he do not pronounce unclean all that is in the house, —and, after this, shall the priest come in to view the house:
Kuhani ataagiza vitu vyote vitolewe ndani ya nyumba, kabla hajaenda kuchunguza kama ina ugonjwa huo, ili kitu chochote ndani ya nyumba kisitangazwe kuwa najisi. Baada ya hili, kuhani ataingia ndani na kuikagua hiyo nyumba.
37 then shall he view the mark and lo! if the mark is in the walls of the house, with sunken places greenish yellow or reddish, —and they appear to be lower than the [surface of the] wall,
Atachunguza upele huo katika kuta za nyumba hiyo, nazo kama zina rangi ya kijani kibichi au wekundu, na kuna mibonyeo ndani ya ukuta,
38 then shall the priest come forth out of the house, unto the entrance of the house, —and shall shut up the house seven days;
kuhani atatoka na kufunga mlango wa nyumba hiyo kwa siku saba.
39 and the priest shall return on the seventh day, —and take a view, and lo! if the mark hath spread in the walls of the house,
Siku ya saba, kuhani atarudi kuikagua nyumba. Kama upele umeenea juu ya kuta,
40 then shall the priest give command, and they shall pull out the stones, wherein is the mark, —and cast them forth outside the city, into an unclean place;
ataagiza kwamba mawe yote yaliyoambukizwa yaondolewe na kutupwa katika eneo lililo najisi nje ya mji.
41 and, the house itself, shall he cause to be scraped on the inside round about, —and they shall pour out the mortar which they have scraped off, outside the city, into an unclean place;
Kuta zote za ndani ya nyumba hiyo ni lazima zikwanguliwe, na kifusi chake kitupwe mahali najisi nje ya mji.
42 and shall take other stones, and put in the place of the stones, —and, other mortar, shall he take and plaster the house.
Kisha watachukua mawe mengine na kujenga palipobomolewa kwa udongo mpya wa mfinyanzi, na kuipiga nyumba hiyo lipu mpya.
43 But if the mark again breaketh out in the house, after the taking out of the stones, —and after the scraping of the house and after the plastering;
“Ikiwa upele huo utatokea tena ndani ya ile nyumba baada ya mawe kuondolewa na nyumba kukwanguliwa na kuwekwa lipu mpya,
44 then shall the priest come in, and take a view, and lo! if the mark hath spread in the house, a fretting leprosy, it is in the house unclean, it is,
kuhani atakwenda kuikagua, na kama upele umeenea ndani ya nyumba, basi ni upele uharibuo; nyumba hiyo ni najisi.
45 and he shall pull down the house, —the stones thereof, and the timber thereof and all the mortar of the house, —and shall carry them forth outside the city, into an unclean place.
Ni lazima ibomolewe: mawe yake, mbao na lipu yake, vyote vikatupwe nje ya mji mahali palipo najisi.
46 And as for him that entereth into the house, all the days it is shut up, he shall be unclean until the evening;
“Yeyote atakayeingia katika nyumba hiyo ikiwa imefungwa, atakuwa najisi mpaka jioni.
47 And, he that lieth in the house, shall wash his clothes, and he that eateth in the house shall wash his clothes.
Yeyote atakayelala au kula ndani ya nyumba hiyo ni lazima afue nguo zake.
48 But, though the priest do come, into the house, and take a view, yet lo! if the plague-mark hath not spread in the house after the house was plastered, then shall the priest pronounce the house clean, for, healed, is the plague.
“Lakini ikiwa kuhani atakuja kuikagua na kukuta kuwa upele haujaenea tena baada ya nyumba kupigwa lipu, ataitangaza nyumba ile kuwa safi, kwa sababu upele umekwisha.
49 Then shall he take to cleanse, the house, two birds, —and cedar wood, and crimson, and hyssop;
Ili kuitakasa nyumba hiyo, mwenye nyumba ataleta ndege wawili, mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo.
50 and shall kill one bird, —within an earthen vessel over living water;
Atamchinja mmoja wa wale ndege kwenye chungu chenye maji safi.
51 and take the cedar wood and the hyssop, and the crimson and the living bird, and dip them in the blood of the slain bird, and in the living water, —and sprinkle the house seven times;
Kisha atachukua mti wa mwerezi, hisopo, kitani nyekundu na ndege aliye hai, na kuvitumbukiza ndani ya damu ya ndege aliyechinjwa pamoja na maji safi, na kuinyunyizia nyumba ile mara saba.
52 and so cleanse the house, with the blood of the bird and with the living water, —and with the living bird, and with the cedar wood and with the hyssop, and with the crimson;
Ataitakasa nyumba kwa damu ya yule ndege, maji safi, ndege aliye hai, mti wa mwerezi, hisopo na kitani nyekundu.
53 and shall let go the living bird unto the outside of the city, unto the face of the field, —so shall he put a propitiatory-covering over the house and it shall be clean.
Kisha atamwachia yule ndege aliye hai huru mashambani nje ya mji. Kwa njia hii atafanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ile, nayo itakuwa safi.”
54 This, is the law, —for every plague-mark of leprosy and for scall;
Haya ndiyo masharti kuhusu aina yoyote ya ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, mwasho wowote,
55 and for garment leprosy, and for house [leprosy];
upele ndani ya nguo au ndani ya nyumba,
56 and for rising, and for scab and for a bright spot;
kwa uvimbe, vipele au kipaku kingʼaacho,
57 to give instruction, on the day of declaring unclean, and on the day of declaring clean, —This is the law of leprosy.
kupambanua wakati kitu fulani ni safi au najisi. Haya ndiyo masharti kuhusu magonjwa ya ngozi ya kuambukiza na upele.

< Leviticus 14 >