< Leviticus 10 >

1 Then Aaron’s sons, Nadab and Abihu, took each man his censer and placed therein fire, and put thereon incense, —and brought near before Yahweh strange fire, which he had not commanded them.
Nadabu na Abihu, wana wa Aroni, wakachukua vyetezo vyao, wakaweka moto ndani yake na kuongeza uvumba; kisha wakamtolea Bwana moto usio halali, kinyume na agizo la Mungu.
2 Then came there forth fire from before Yahweh, and consumed them, —and they died before Yahweh.
Hivyo moto ukaja kutoka kwa uwepo wa Bwana na kuwaramba, nao wakafa mbele za Bwana.
3 Then said Moses unto Aaron—The very thing, that Yahweh spake, saying—In them that draw near to me, must I be hallowed, And before the faces of all the people, must I get myself honour, —And Aaron, was dumb.
Kisha Mose akamwambia Aroni, “Hili ndilo alilonena Bwana wakati aliposema: “‘Miongoni mwa wale watakaonikaribia nitajionyesha kuwa mtakatifu; machoni pa watu wote nitaheshimiwa.’” Aroni akanyamaza.
4 Then called Moses unto Mishael, and unto Elzaphan, sons of Uzziel, uncle of Aaron, —and said unto them—Draw near bear away your brethren from before the sanctuary, unto the outside of the camp.
Mose akawaita Mishaeli na Elisafani, wana wa Uzieli mjomba wake Aroni, akawaambia, “Njooni hapa. Ondoeni miili ya binamu zenu mbele ya mahali patakatifu, mkaipeleke nje ya kambi.”
5 So they drew near and bare them away, in their tunics, unto the outside of the camp, —as spake Moses.
Hivyo wakaja na kuwaondoa, wakiwa bado wamevalia makoti yao ya ibada, wakawapeleka nje ya kambi, kama Mose alivyoamuru.
6 Then said Moses unto Aaron and to Eleazar and to Ithamar, his sons—Your heads, ye may not bare and your garments, ye shall not rend so shall ye not die, neither against all the assembly, will he be wroth, —but let, your brethren the whole house of Israel, bewail the consuming fire wherewith Yahweh hath consumed.
Ndipo Mose akamwambia Aroni pamoja na wanawe, Eleazari na Ithamari, “Msifunue vichwa vyenu wala msirarue mavazi yenu, la sivyo mtakufa na Bwana ataikasirikia jumuiya nzima. Lakini ndugu zenu, nyumba yote ya Israeli, wanaweza kuwaombolezea wale ambao Bwana amewaangamiza kwa moto.
7 But, from the entrance of the tent of meeting, shall ye not go forth, lest ye die, for, the anointing oil of Yahweh is upon you. And they did according to the word of Moses.
Msitoke nje ya ingilio la Hema la Kukutania, la sivyo mtakufa, kwa sababu mafuta ya Bwana ya upako yako juu yenu.” Hivyo wakafanya kama vile Mose alivyosema.
8 Then spake Yahweh unto Aaron, saying:
Kisha Bwana akamwambia Aroni,
9 Wine and strong drink, thou mayest not drink, —thou nor thy sons with thee when ye enter into the tent of meeting, so shall ye not die, —an age-abiding statute to your generations;
“Wewe na wanao msinywe mvinyo wala kinywaji kingine kilichochachuka wakati mwingiapo katika Hema la Kukutania, la sivyo mtakufa. Hili litakuwa Agizo la kudumu kwa vizazi vijavyo.
10 That ye may make a difference, between the sacred and the common, —and between the unclean and the clean;
Ni lazima mtenganishe kilicho kitakatifu na kile kilicho cha kawaida, kati ya yaliyo najisi na yaliyo safi,
11 And may teach the sons of Israel, —all the statutes which Yahweh hath spoken unto them, by the mediation of Moses.
na lazima mwafundishe Waisraeli amri zote ambazo Bwana aliwapa kupitia Mose.”
12 Then spake Moses unto Aaron and unto Eleazar and unto Ithamar his sons that were left, Take ye the meal-offering that is left of the altar-flames of Yahweh, and eat it unleavened beside the altar, —for, most holy, it is;
Mose akamwambia Aroni pamoja na wanawe waliosalia, Eleazari na Ithamari, “Chukueni sadaka ya nafaka iliyobaki kutoka sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto, muile hapo kando ya madhabahu ikiwa imeandaliwa bila chachu, kwa sababu ni takatifu sana.
13 therefore shall ye eat it in a holy place, for, thine by statute, and thy sons’ by statute, it is, from among the altar-flames of Yahweh, —for, so, am I commanded.
Mtaila katika mahali patakatifu kwa sababu ni fungu lenu na fungu la wana wenu la sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto, kwa maana hivyo ndivyo nilivyoamriwa.
14 And the wave-breast, and the heave-shoulder, shall ye eat in clean place, thou, and thy sons and thy daughters with thee, —for as thine by statute and thy sons’ by statute, have they been given, from among the peace-offerings of the sons of Israel.
Lakini wewe na wanao na binti zako mwaweza kula kidari kile kilichoinuliwa na paja lile lililotolewa. Mtavila mahali safi pa kawaida ya ibada; mmepewa wewe na watoto wako kuwa fungu lenu la sadaka za amani za Waisraeli.
15 The heave-shoulder and the wave-breast upon the altar-flames of the fat portions, shall they bring in, to wave as a wave-offering, before Yahweh, —so shall they be thine, and thy sons’ with thee, by an age-abiding statute, As Yahweh hath commanded.
Paja lile lililotolewa na kidari kile kilichoinuliwa lazima viletwe pamoja na sehemu za mafuta ya sadaka za kuteketezwa kwa moto, ili kuinuliwa mbele za Bwana kama sadaka ya kuinuliwa. Hili litakuwa fungu lako la kawaida na wanao, kama Bwana alivyoagiza.”
16 Now, as for the sin-bearing goat, Moses diligently sought it but lo! it had been burnt up, —then was he wroth against Eleazar and against Ithamar, the sons of Aaron that were left, saying:
Mose alipouliza kuhusu mbuzi atolewaye kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na kukuta kwamba ameteketezwa, aliwakasirikia Eleazari na Ithamari, wana wa Aroni waliobaki, akawauliza,
17 Wherefore did ye not eat the sin-bearer in the holy place? for most, holy, it is, —and thee same, hath he given you that ye may bear the iniquity of the assembly, to put a propitiatory-covering over them before Yahweh.
“Kwa nini hamkula sadaka ya dhambi katika eneo la mahali patakatifu? Ni takatifu sana. Mlipewa ninyi ili kuondoa hatia ya jumuiya kwa ajili ya kuwafanyia upatanisho mbele za Bwana.
18 Lo! the blood thereof had not been taken into the holy place, within, —ye should have, indeed eaten, it, in a holy place, as I commanded.
Kwa kuwa damu yake haikuletwa ndani ya Mahali Patakatifu, mngemla mbuzi huyo katika sehemu ya mahali patakatifu kama nilivyoagiza.”
19 Then spake Aaron unto Moses—Lo! this very day, when they had brought near their own sin-bearer, and their own ascending-sacrifice, there befell me such things as these, —if, then, I had eaten of the sin-bearer this day, would it have been well-pleasing in the eyes of Yahweh?
Aroni akamjibu Mose, “Leo wanangu wametoa sadaka zao za dhambi na sadaka zao za kuteketezwa mbele za Bwana, lakini mambo kama haya yamenitokea mimi. Je, Bwana angependezwa kama ningekuwa nimekula sadaka ya dhambi leo?”
20 And, when Moses heard that, then was it well-pleasing in his eyes.
Mose aliposikia haya, akaridhika.

< Leviticus 10 >