< Joshua 8 >

1 Then said Yahweh unto Joshua—Do not fear nor be dismayed, take with thee all the army, and arise, go up to Ai, —see! I have given into thy hand, the king of Ai and his people, and his city, and his land;
Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Usiogope, wala usivunjike moyo. Chukua jeshi lote la vita uende pamoja nalo kuishambulia Ai. Kwa kuwa nimeshamweka mikononi mwako mfalme wa Ai, pamoja na watu wake, mji wake na nchi yake.
2 so shalt thou do unto Ai and to her king, as thou didst unto Jericho unto her king, save only, the spoil thereof and the cattle thereof, shall ye take as your own prey, —set thee an ambush for the city, behind it.
Utafanya Ai na mfalme wake kama ulivyofanya kwa mji wa Yeriko na mfalme wake, isipokuwa mnaweza kuchukua mateka wake na mifugo wake, kwa ajili yenu. Weka waviziaji upande wa nyuma ya mji.”
3 So Joshua arose, and all the people of war, to go up to Ai, —and Joshua chose out thirty thousand men, the mighty men of valour, and sent them forth by night.
Basi Yoshua na jeshi lote wakainuka kushambulia Ai. Akachagua watu mashujaa elfu thelathini walio bora miongoni mwa wapiganaji wake, akawapeleka wakati wa usiku
4 And he commanded them, saying—See! ye, shall be lying in ambush against the city, behind the city, do not go very far from the city, —so shall ye all be ready.
akiwaagiza: “Sikilizeni kwa makini. Mtavizia nyuma ya mji. Msiende mbali sana na mji. Wote kuweni macho.
5 But, I, and all the people who are with me, will draw near unto the city, —and it shall be, when they come out to meet us, as at the first, then will we flee before them;
Mimi na watu walio pamoja nami, tutaukabili mji, kisha itakuwa hapo watu watakapotoka nje kupigana nasi, kama walivyofanya hapo kwanza, sisi tutawakimbia.
6 so will they come out after us, until we have drawn them away from the city, for they will say, Fleeing before us, as at the first! therefore will we flee before them.
Watatufuatilia mpaka tutakapokuwa tumewavuta mbali na mji kwa kuwa watasema, ‘Wanatukimbia, kama walivyofanya hapo awali.’ Hivyo tutakapowakimbia,
7 Then, ye, shall rise up out of the ambush, and take possession of the city, —and Yahweh your God will deliver it into your hand.
ninyi inawapasa mwinuke mtoke huko mafichoni na kuuteka mji. Bwana Mungu wenu atautia mkononi mwenu.
8 And it shall be, when ye have seized the city, then shall ye burn the city with fire, according to the word of Yahweh, shall ye do, —see! I have commanded you.
Mtakapokuwa mmeuteka mji, uteketezeni kwa moto. Fanyeni kama vile Bwana alivyoamuru. Angalieni, nimewaagiza.”
9 So Joshua sent them forth, and they went into ambush, and abode between Bethel and Ai, on the west of Ai, —but Joshua lodged that night in the midst of the people.
Ndipo Yoshua akawatuma watu, nao wakaenda mahali pa kujificha, wakawa wanavizia kati ya Betheli na Ai, kuelekea upande wa magharibi wa Ai, lakini Yoshua akalala miongoni mwa watu usiku huo.
10 And Joshua rose up early in the morning, and mustered the people, —and went up—he and the elders of Israel, before the people, to Ai.
Asubuhi na mapema siku iliyofuatia, Yoshua akawakutanisha watu wake, na yeye na viongozi wa Israeli wakawa mbele ya watu kwenda Ai.
11 And, all the people of war who were with him, went up, and drew near, and came in, right before the city, —and pitched on the north of Ai, with, a valley, between them and Ai.
Watu wote wa vita waliokuwa pamoja naye walipanda, wakakaribia na kufika mbele ya mji. Wakapiga kambi kaskazini mwa Ai, pakiwa na bonde kati yao na huo mji.
12 And he took about five thousand men, —and set them in ambush between Bethel and Ai, on the west of the city.
Yoshua alikuwa amewachukua watu wapatao elfu tano, akawaweka katika uavizi kati ya Betheli na Ai, upande wa magharibi wa mji.
13 And, when the people had set all the host that was on the north of the city, with the rear thereof on the west of the city, then went Joshua, during the night, into the midst of the valley.
Wakawaweka askari katika maeneo yao: wale wote waliokuwa kambini wakawa kaskazini ya mji na wale waliokuwa wakivizia wakawa upande wa magharibi. Usiku huo Yoshua akaenda katika lile bonde.
14 And it came to pass, when the king of Ai saw it, that they hasted, and rose up early, and the men of the city came out to meet Israel for battle, he and all his people, at an appointed time, before the waste plain, —he not knowing that there was an ambush lying in wait for him, behind the city.
Mfalme wa Ai alipoona jambo hili, yeye pamoja na watu wote wa mji wakatoka kwa haraka asubuhi na mapema, ili kukutana na Israeli katika vita mahali fulani panapotazamana na Araba. Lakini hakujua kwamba kulikuwa kumewekwa waviziaji dhidi yake nyuma ya mji.
15 So then Joshua and all Israel suffered themselves to be smitten before them, —and fled, by the way of the wilderness;
Yoshua na Israeli wote wakaruhusu kurudishwa nyuma mbele yao, na kuelekea jangwani.
16 and all the people who were in the city were called out to pursue them, —and they pursued Joshua, and so were drawn out away from the city.
Watu wote wa Ai wakaitwa ili kuwafuatia, nao wakavutwa kumfuatia Yoshua mbali na mji.
17 And there remained not a man, in Ai or Bethel, who had not gone out after Israel, —and they left the city, open, and pursued Israel.
Hakuna hata mwanaume mmoja aliyebakia Ai wala Betheli ambaye hakufuatia Israeli. Wakauacha mji wazi na kuwafuatia Israeli.
18 Then said Yahweh unto Joshua—Stretch out with the javelin which is in thy hand, towards Ai, for, into thy hand, will I deliver it. So Joshua stretched out with the javelin which was in his hand, towards the city.
Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Inua huo mkuki ulio mkononi mwako kuuelekeza Ai, kwa kuwa nitautia huo mji mkononi mwako.” Hivyo Yoshua akauelekeza mkuki wake Ai.
19 And, the ambush, rose up quickly, out of their place, and ran, when he stretched out his hand, and entered the city, and captured it, —and hasted, and set the city on fire.
Mara tu alipofanya hivi, wale watu waliokuwa mavizioni wakaondoka upesi kutoka mahali pao na kukimbilia mbele. Wakaingia ndani ya mji, wakauteka na kuutia moto kwa haraka.
20 And the men of Ai turned behind them, and looked, and lo! the smoke of the city had risen up towards the heavens, and there was in them no strength, to flee this way or that way, —moreover, the people that were fleeing to the wilderness, turned back upon the pursuers.
Watu wa Ai wakaangalia nyuma, wakauona moshi wa huo mji ukielekea angani lakini hawakuwa na nafasi ya kutoroka kwa upande wowote, kwa kuwa wale Waisraeli waliokuwa wanawakimbia kuelekea jangwani walikuwa wamegeuka nyuma kuwakabili wakimbizaji wao.
21 Yea, when, Joshua and all Israel, saw that the ambush had captured the city, and that the smoke of the city had risen up, then returned they, and smote the men of Ai.
Basi Yoshua na Israeli wote walipoona kwamba waviziaji wameshauteka mji na moshi ulikuwa unapaa juu kutoka kwenye mji, wakawageukia watu wa Ai na kuwashambulia.
22 And, the others, came forth out of the city to meet them, so they were in the midst of Israel, some on this side, and some on that side, —and they smote them, until there was left them none to remain or to escape.
Wale waviziaji nao pia wakatoka nje ya mji dhidi yao, hivi kwamba wakashikiwa katikati, Waisraeli wakiwa pande zote mbili. Israeli wakawaua, bila kuwaachia yeyote aliyenusurika wala aliyetoroka.
23 And, the king of Ai, they caught alive, —and brought him near unto Joshua.
Lakini wakamchukua mfalme wa Ai akiwa hai na kumleta kwa Yoshua.
24 And it came to pass, when Israel had made an end of slaying all the inhabitants of Ai in the field, in the wilderness whither they had pursued them, and all of them had fallen by the edge of the sword until they were consumed, then all Israel returned to Ai, and smote it with the edge of the sword.
Israeli ilipomaliza kuwaua wanaume wote wa Ai katika mashamba na jangwani walipokuwa wamewafukuzia, na baada ya kila mmoja wao kuuawa kwa upanga, Waisraeli wote wakarudi Ai na kuwaua wale waliokuwa wamebakia mjini.
25 And so it was, that all who fell that day, both of men and of women, were twelve thousand, —all people of Ai.
Watu kumi na mbili elfu, waume kwa wake, waliangamia siku ile, yaani watu wote wa Ai.
26 Now, Joshua, drew not back his hand which he had stretched out with the javelin, —until he had utterly destroyed all the inhabitants of Ai.
Kwa maana Yoshua hakuurudisha ule mkono wake uliokuwa umeuinua mkuki hadi alipomaliza kuwaangamiza wote walioishi Ai.
27 Nevertheless, the cattle and the spoil of that city, Israel took as their own prey, —according to the word of Yahweh, which he commanded Joshua.
Lakini Israeli wakajichukulia mifugo na nyara za mji huu, kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Yoshua.
28 So then Joshua burned Ai, —and made of it an age-abiding heap—a desolation, [as it remaineth] until this day.
Kwa hiyo Yoshua akauchoma moto mji wa Ai na kuufanya kuwa lundo la magofu la kudumu, mahali pa ukiwa hadi leo.
29 And, the king of Ai, hanged he on a tree until eventide, —but, at the going in of the sun, Joshua gave command and they took down his dead body from the tree, and cast it in at the opening of the gate of the city, and raised up over it a great heap of stones—[which remaineth] until this day.
Akamwangika mfalme wa Ai kwenye mti na kumwacha hapo mpaka jioni. Wakati wa jua kutua, Yoshua akawaamuru wautoe mwili wake kwenye mti na kuutupa kwenye ingilio la lango la mji. Kisha wakalundika mawe makubwa mengi juu yake, ambayo yamesalia mpaka leo.
30 Than, built Joshua, an altar, unto Yahweh, God of Israel, —in Mount Ebal:
Kisha Yoshua akajenga madhabahu ya Bwana, Mungu wa Israeli, katika Mlima wa Ebali,
31 as Moses, the servant of Yahweh, commanded the sons of Israel, as it is written in the scroll of the law of Moses, an altar of whole stones, whereon had not been wielded any tool of iron, —and they caused to go up thereon, ascending-sacrifices unto Yahweh, and sacrificed peace-offerings.
kama Mose mtumishi wa Bwana alivyokuwa amewaamuru Waisraeli. Akaijenga sawasawa na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria ya Mose: madhabahu ya mawe yasiyochongwa, ambayo juu yake hakuna chombo cha chuma kilichotumika. Hapo juu yake wakamtolea Bwana sadaka za kuteketezwa na kutoa sadaka za amani.
32 Then wrote he there, upon the stones, a copy of the law of Moses, which he wrote, in the presence of the sons of Israel.
Pale, mbele ya Waisraeli Yoshua akanakili juu ya hayo mawe sheria ya Mose, aliyokuwa ameiandika.
33 And, all Israel, and their elders and officers, and their judges, were standing on this side and on that side of the ark, before the priests the Levites, who were bearing the ark of the covenant of Yahweh, as well the sojourner as the home-born, half of them over against Mount Gerizim, and half of them over against Mount Ebal, —as Moses the servant of Yahweh commanded to bless the sons of Israel, first of all.
Israeli yote, wageni na wazawa sawasawa, wakiwa na wazee wao, maafisa na waamuzi, walikuwa wamesimama pande zote mbili za Sanduku la Agano la Bwana, wakiwaelekea wale waliokuwa wamelichukua, yaani makuhani, ambao ni Walawi. Nusu ya watu ilisimama mbele ya Mlima Gerizimu na nusu hiyo ingine ikasimama mbele ya Mlima Ebali, kama vile Mose mtumishi wa Bwana alivyokuwa ameamuru hapo mwanzo alipotoa maagizo ya kuwabariki watu wa Israeli.
34 And, after that, read he all the words of the law, the blessing and the cursing, —according to all that was written in the scroll of the law.
Hatimaye, Yoshua akasoma maneno yote ya sheria, yaani baraka na laana, kama vile ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria.
35 Them was not a word of all that Moses commanded, —which Joshua read not before all the convocation of Israel, with the women and the little ones, and the sojourner who was going on in their midst.
Hakuna neno lolote katika yale yote ambayo Mose alikuwa ameamuru ambalo Yoshua hakulisomea kusanyiko lote la Israeli, ikiwa ni pamoja na wanawake na watoto, na wageni walioishi miongoni mwao.

< Joshua 8 >