< Joshua 21 >

1 Then came near the ancestral heads of the Levites, unto Eleazar, the priest, and unto Joshua son of Nun, —and unto the ancestral heads of the tribes, of the sons of Israel;
Kisha wakuu wa koo za Walawi walimwendea Eliazari kuhani, na kwa Yoshua mwana wa Nuni, na kwa viongozi wa familia za mababu zao miongoni mwa watu wa Israeli.
2 and spake unto them in Shiloh in the land of Canaan, saying: Yahweh himself, commanded, by the hand of Moses, that there should be given unto us cities to dwell in, —with their pasture-lands for our cattle.
Waliwaambia, “Yahweh aliwaagizeni ninyi kwa mkono wa Musa kwamba mtupatieni miji ya kuishi yenye maeneo kwa ajili ya kuchungia ya mifugo.” waliyasema haya huko Shilo katika nchi ya Kanaani.
3 So the sons of Israel gave unto the Levites, out of their own inheritance, at the bidding of Yahweh, —these cities, with their pasture-lands.
Hivyo, kwa agizo la Yahweh, watu wa Israeli waliwapa Walawi kutoka katika urithi wa wao miji ifuatayo pamoja na maeneo yao ya kuchungia.
4 And, when the lot came out for the families of the Kohathites, then had the sons of Aaron the priest, from among the Levites—out of the tribe of Judah and out of the tribe of the Simeonites and out of the tribe of Benjamin—by lot, thirteen cities.
Upigaji wa kura kwa ajili ya koo za Wakohathi ulileta matokeo haya: makuhani ambao ni wazawa wa Haruni ambao walitokana na Walawi, walipokea miji kumi na mitatu waliopewa kutoka kwa kabila la Yuda, kutoka kabila la Simoni, na kutoka kabila la Benyamini.
5 And, the sons of Kohath that remained, had—out of the families of the tribe of Ephraim and out of the tribe of Dan and out of the half tribe of Manasseh—by lot, ten cities.
Koo zilizobaki za Wakohathi walipokea kwa kupiga kura kwa miji kumi kutoka katika kabila za Efraimu, Dani, na kutoka kwa nusu ya kabila la Manase.
6 And, the sons of Gershon, had—out of families of the tribe of Issachar and out of the tribe of Asher and out of the tribe of Naphtali and out of the half tribe of Manasseh in Bashan—by lot, thirteen cities.
Na watu wazawa wa Gershoni walipewa miji kumi na mitatu kwa kupigiwa kura kutoka kwa koo za kabila la Isakari, Asheri, Nafutali, na nusu ya kabila la Manase katika Bashani.
7 The sons of Merari, by their families, had—out of the tribe of Reuben and out of the tribe of Gad and out of the tribe of Zebulun, twelve cities.
Watu waliokuwa wazawa wa Merari walipokea miji kumi na miwili kutoka katika makabila ya Rubeni, Gadi na Zabuloni.
8 So the sons of Israel gave unto the Levites these cities, with their pasture lands, —as Yahweh commanded, by the hand of Moses, by lot.
Basi, watu wa Israeli waliwapa Walawi miji hii pamoja na maeneo yao ya kuchungia, kwa kupiga kura, kama vile Yahweh alivyokuwa ameagiza kwa mkono wa Musa.
9 Thus then they gave—out of the tribe of the sons of Judah and out of the tribe of the sons of Simeon—these cities which are mentioned by name.
Kutoka kwa makabila la Yuda na Simoni, waliwapa nchi katika miji ifuatayo iliyoorodheshwa kwa majina.
10 And the sons of Aaron, from among the sons of Kohath, from among the sons of Levi, had them, —because, theirs, was the first lot;
Miji hii walipewa wazawa wa Haruni, ambao walikuwa miongoni mwa koo za Wakohathi, ambao walitoka katika kabila la Lawi. Kwa kuwa upigaji wa kura ya kwanza uliwaangukiwa wao.
11 yea there was given unto them, the city of Arba, the father of Anak, the same, is Hebron, in the hill country of Judah, —with the pasture land thereof, round about it;
Waisraeli waliwapatia Kiriathi Arba ( Arba alikuwa ni baba wa Anaki), eneo hilo liliitwa pia Hebroni, katika nchi ya milima ya Yuda, pamoja na maeneo ya kulishia mifugo yaliyouzunguka mji.
12 whereas, the fields of the city, and the villages thereof, gave they unto Caleb son of Jephunneh, as his possession.
Lakini mashamba ya mji na vijiji vyake vilikuwa tayari ameshapewa Kalebu mwana Yefune, kama mali yake.
13 But, unto the sons of Aaron the priest, gave they the city of refuge for the manslayer, even Hebron, with the pasture lands thereof, —Libnah also, with her pasture lands;
Na kwa wana wa Haruni kuhani, waliwapa Hebroni pamoja na eneo lake la kulishia mifugo ambao ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu bila kukusudia na Libna pamoja na maeneo ya kulishia mifugo.
14 and Jattir with her pasture land, and Eshtemoa with her pasture land;
Na Yatiri pamoaja na maeno yake ya kuchungia, na Eshitemoa pamoja na maeneo yake ya malisho.
15 and Holon, with her pasture land, and Debir, with her pasture land;
Lakini pia waliwapa Holoni pamoja na maeneo yake ya malisho, Debiri pamoja na maeneo yake ya malisho,
16 and Ain, with her pasture land, and Juttah, with her pasture land, Beth-shemesh, with her pasture land, —nine cities, out of these two tribes.
Aini pampoja na maeneo yake ya malisho, na Bethi Shemeshi pamoja na maeneo yake ya malisho. Ilikuwa ni miji kumi na tisa ambayo walipewa kutoka katika makabila haya mawilil.
17 And, out of the tribe of Benjamin, Gibeon, with her pasture land, —Geba, with her pasture land;
Kutoka katika kabilala Benyamini walipewa Gibea pamoja na maeneo yake ya malisho, na Geba pamoja na maeneo yake ya malisho,
18 Anathoth, with her pasture land, and Almon, with her pasture land, —four cities.
na Anathothi pamoja na maeneo yake ya malisho, na amoni pamoja na vitongoji vyake vinne.
19 All the cities of the sons of Aaron, the priests, were thirteen cities, with their pasture lands.
Miji waliyopewa makuhani, wana wa Haruni, ilikuwa ni miji kumi na mitatu kwa ujumla, kujumlisha na maeneo yake ya malisho.
20 And, as for the families of the sons of Kohath, the Levites, which remained of the sons of Kohath, the cities of their lot were out of the tribe of Ephraim.
Na kwa ajili ya sehemu ya familia ya Kohathi iliyosalia, wale Walawi walio wa familia ya Kohathi, walipewa miji kutoka katika kabila la Efraimu kwa kupiga kura.
21 So they gave unto them a city of refuge for the manslayer, even Shechem with her pasture land, in the hill country of Ephraim, —also Gezer, with her pasture land;
Walipewa Shekemu pamoja na maeneo yake ya malisho katika nchi ya milima ya Efraimu - mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu bila kukusudia, na Gezeri pamoja na maeneo yake ya malisho,
22 and Kibzaim, with her pasture land, and Beth-horon, with her pasture land, —four cities.
na Kibzaimu pamoja na maeneo yake ya malisho, na Bethi Horoni pamoja na maeneo yake ya malisho, ilikuwa miji minne kwa ujumla wake.
23 And, out of the tribe of Dan, Elteke, with her pasture land, —Gibbethon, with her pasture land;
Kutoka katika kabila la Dani, ukoo wa Kohathi ulipewa Elteke pamoja na maeneo yake ya malisho, na Gibethoni pamoja na maeneo yake ya malisho, na
24 Aijalon, with her pasture land, Gath-rimmon, with her pasture land, —four cities.
Aijaloni pamoja na maeneo yake ya malisho, na Gathrimoni pamoja na maeneo yake ya malisho, ilikuwa ni miji minne kwa ujumla wake.
25 And, out of the half tribe of Manasseh, Taanach, with her pasture land, and Gath-rimmon, with her pasture land, —two cities.
Kutoka katika nusu ya kabila la Manase, ukoo wa Kohathi walipewa miji miwili - Taanaki pamoja na maeneo yake ya malisho na Gathirimoni pamoja na maeneo yake ya malisho.
26 All the cities, were ten, with their pasture lands: for the families of the sons of Kohath which remained.
Kulikuwa na miji kumi kwa ujumla wake kwa ajili ya koo zilizosalia za Wakohathi, pamoja na maeneo yao ya malisho.
27 And, the sons of Gershon, of the families of the Levites, had, out of the half tribe of Manasseh, a city of refuge for the manslayer, even Golan in Bashan, with her pasture land, and Be-eshterah, with her pasture land, —two cities.
Kutoka katika nusu ya kabila la Manase, jamaa za Gershoni, ambazo hizi zilikuwa ni koo zingine za Walawi, zilipewa Golani katika Bashani pamoja na maeneo yao ya malisho, ni mji wa makimbilio kwa ajili ya mtu yeyote aliyeua mtu bila kukusudia, sambamba na Beeshitera pamoja na maeneo yake ya malisho - ilikuwa miji miwili kwa ujumla.
28 And, out of the tribe of Issachar, Kishion, with her pasture land, —Daberath, with her pasture land;
Koo za Gershoni zilipewa pia miji minne kutoka kwa kabila la Isakari - Kishoni sambamba na maeneo yake ya malisho, Daberathi pamoja na maeneo yake ya malisho,
29 Jarmuth, with her pasture land, En-gannim, with her pasture land, —four cities.
Yarmuthi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Engnimu pamoja na maeneo yake ya malisho.
30 And, out of the tribe of Asher, Mishal, with her pasture land, Abdon, with her pasture land;
Kutoka katika kabila la Asheri, walipewa miji minne kwa ujumla - Mishali pamoja na maeneo yake ya malisho, Abdoni pamoja na maeneo yake ya malisho,
31 Helkath, with her pasture land, and Rehob, with her pasture land, —four cities.
Helikathi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Rehobu pamoja na maeneo yake ya malisho.
32 And, out of the tribe of Naphtali, a city of refuge for the manslayer—even Kedesh in Galilee, with her pasture land, and Hammoth-dor, with her pasture land, and Kartan, with her pasture land, —three cities.
Kutoka kwa kabila la Nafutali, nasaba za Gershoni walipewa miji mitatu kwa ujumla - Kedeshi katika Galilaya pamoja na maeneo yake ya malisho, ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu yeyote aliyeua mtu bila kukusudia; na Hamothidori pamoja na maeneo yake ya malisho, na Kartani pamoja na maeneo yake ya malisho.
33 All, the cities of the Gershonites, by their families, were thirteen cities, with their pasture lands.
Kulikuwa na miji kumi na mitatu kwa ujumla, kujumuisha na maeneo yake ya malisho, kwa ajili ya koo za Gershoni.
34 And, unto the families of the sons of Merari, the Levites that remained, out of the tribe of Zebulun, Jokneam, with her pasture land, —Kartah, with her pasture land;
Na kwa Walawi waliosalia, koo za Merari waliokuwa wamepewa kutoka katika kabila la Zabuloni: Yokneamu pamoa na maeneo yake ya marisho, Karta pamoja na maeneo yake ya malisho,
35 Dimnah, with her pasture land, Nahalal, with her pasture land, —four cities.
Dimna pamoja na maeneo yake ya malisho, na Nahalali pamoja na maeneo yake ya malisho- ilikuwa ni miji minne kwa ujumla.
36 And, out of the tribe of Reuben, Bezer, with her pasture land, —and Jahaz, with her pasture land;
Kwa mbari za Merari walipewa miji minne kutoka katika kabila la Rubeni: Bezeri pamoja na maeneo yake ya malisho, Yahazi pamoja na maene yake ya malisho,
37 Kedemoth, with her pasture land and Mephaath, with her pasture land, —four cities.
na Kedemothi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Mefaathi pamoja na maeneo yake ya malisho.
38 And, out of the tribe of Gad, a city of refuge for the manslayer—even Ramoth in Gilead, with her pasture land, —and Mahanaim, with her pasture land;
Kutoka katika kabila la Gadi walipewa miji ya Ramothi katika Gileadi pamoja na sehemu zake za malisho - huu ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu mwenzake bila kukusudia - na Mahanaimu pamoja na sehemu zake za malisho.
39 Heshbon, with her pasture land, Jazer, with her pasture land, —in all, four cities.
Koo za Merari zilipewa pia Heshiboni pamoja na maeneo yake ya malisho, na Yazeri pamoja na malisho yake.
40 All the cities for the sons of Merari, by their families, who remained of the families of the Levites, yea their lot was, twelve, cities.
Hii ilikuwa ni miji minne kwa ujumla wake. Hii yote ilikuwa ni miji ya koo kadhaa za Merari, ambao walitoka katika kabila la Lawi, miji kumi na miwili walipewa wao kwa kupiga kura.
41 All the cities of the Levites, in the midst of the possession of the sons of Israel, were forty-eight cities, with their pasture lands:
Miji waliyopewa Walawi kutoka katikati ya nchi iliyomilikiwa na watu wa Israeli ilikuwa miji arobaini na nane, kujumuisha na sehemu za malisho yao.
42 these cities passed, each severally, with its pasture lands round about it; thus, was it with all these cities.
Miji hii kila mmoja ulikuwa na maeneo yake ya malisho kwa kuuzunguka mji. Miji hii yote ilikuwa hivyo.
43 So Yahweh gave unto Israel, all the land which he had sworn to give unto their fathers, —and they took possession thereof, and dwelt therein.
Basi Yahweh aliwapa Israeli nchi yote ambayo aliwaapia baba zao kuwa atawapa. Waisraeli waliimiliki nchi na wakakaa humo.
44 And Yahweh gave them rest round about, according to all that he had sworn unto their fathers, —and there stood not a man before them, of all their enemies; all their enemies, did Yahweh deliver into their hand.
Kisha Yahweh akawapa pumziko kwa kila upande, kama tu alivyowaahidia baba zao. Hakuna hata adui mmoja atakayeweza kuwashinda. Yawhew aliwatia maadui wao wote mikononi mwao.
45 There failed not a thing, out of all the good things, whereof Yahweh had spoken unto the house of Israel, —the whole, came to pass.
Hakuna hata kitu kimoja miongoni kwa ahadi nzuri ambazo Yahweh alizisema kwa nyumba ya Israeli ambazo hazikutimia. Ahadi zote zilitimia.

< Joshua 21 >