< John 21 >

1 After these things, Jesus manifested himself again, unto the disciples, by the sea of Tiberias; and manifested himself, thus: —
Baada ya haya Yesu akawatokea tena wanafunzi wake kando ya Bahari ya Tiberia. Yeye alijionyesha kwao hivi:
2 There were together, Simon Peter, and Thomas, who was called Didymus, and Nathanael, who was from Cana of Galilee, and the sons of Zebedee, and, two other, of his disciples.
Simoni Petro, Tomaso aitwaye Didimasi, yaani Pacha, Nathanaeli wa Kana ya Galilaya, wana wa Zebedayo na wanafunzi wengine wawili walikuwa pamoja.
3 Simon Peter saith unto them—I go a fishing! They say unto him—We also, go with thee! They went out, and got up into the boat, and during that night, they caught nothing.
Simoni Petro akawaambia wenzake, “Mimi naenda kuvua samaki.” Nao wakamwambia, “Tutakwenda pamoja nawe.” Wakatoka, wakaingia ndani ya mashua, lakini usiku ule hawakupata chochote.
4 But, morning by this time drawing on, Jesus stood upon the beach; nevertheless, the disciples knew not that it was, Jesus.
Mara baada ya kupambazuka, Yesu akasimama ufuoni, lakini wanafunzi hawakumtambua kwamba alikuwa Yesu.
5 Jesus, therefore, saith unto them—Children! perhaps ye have nothing to eat? They answered him—No.
Yesu akawaambia, “Wanangu, je, mna samaki wowote?” Wakamjibu, “La.”
6 And, he, said unto them—Cast the net, on the right side of the boat, —and ye shall find. They cast, therefore; and, no longer, were they able, to draw, it, for the multitude of the fishes.
Akawaambia, “Shusheni nyavu upande wa kuume wa mashua yenu nanyi mtapata samaki.” Wakashusha nyavu na tazama wakapata samaki wengi mno hata wakashindwa kuvutia zile nyavu zilizojaa samaki ndani ya mashua.
7 That disciple, therefore, whom Jesus loved, saith unto Peter—It is, the Lord! Simon Peter, therefore, hearing that it was the Lord, girded about him, his upper garment, —for he was naked; and cast himself into the sea;
Yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akamwambia Petro, “Huyu ni Bwana!” Simoni Petro aliposikia haya, akajifunga nguo yake kwa kuwa alikuwa uchi, naye akajitosa baharini.
8 but, the other disciples, came, by the little boat, —for they were not farther from the land than about two hundred cubits off, —dragging the net of fishes.
Wale wanafunzi wengine wakaja kwa ile mashua huku wakikokota ule wavu uliyojaa samaki, maana hawakuwa mbali na nchi kavu, ilikuwa yapata dhiraa 200
9 So, when they got out upon the land, they behold a coal fire lying, and fish lying over, and bread.
Walipofika ufuoni, wakaona moto wa makaa na samaki wakiokwa juu yake na mikate.
10 Jesus saith unto them—Bring of the fish which ye caught just now.
Yesu akawaambia, “Leteni baadhi ya hao samaki mliovua sasa hivi.”
11 Simon Peter, therefore, went on board, and drew the net on to the land, —full of large fishes, a hundred and fifty-three; and, though they were so many, the net was not rent.
Simoni Petro akapanda kwenye mashua na kuukokota ule wavu pwani. Ulikuwa umejaa samaki wakubwa 153. Ingawa samaki walikuwa wengi kiasi hicho, ule wavu haukuchanika.
12 Jesus saith unto them—Come! break your fast. Not one, of the disciples was venturing to ask him, Who art, thou? knowing that it was, the Lord.
Yesu akawaambia, “Njooni mpate kifungua kinywa.” Hakuna hata mmoja wa wanafunzi aliyethubutu kumuuliza, “Wewe ni nani?” Kwa sababu walijua ya kuwa ni Bwana.
13 Jesus cometh, and taketh the bread, and giveth unto them; and the fish, in like manner.
Yesu akaja, akachukua ule mkate, akawapa na vivyo hivyo akawagawia pia wale samaki.
14 This, already, is the third time Jesus was manifested unto the disciples, after he was raised from among the dead.
Hii ilikuwa mara ya tatu Yesu kuwatokea wanafunzi wake baada yake kufufuliwa kutoka kwa wafu.
15 When, therefore, they had broken their fast, Jesus saith unto Simon Peter—Simon, son of John! lovest thou me more than these? He saith unto him—Yea, Lord! thou, knowest that I am fond of thee, he saith unto him—Be feeding my lambs.
Walipokwisha kula, Yesu akamuuliza Simoni Petro, “Je, Simoni mwana wa Yohana, unanipenda kweli kuliko hawa?” Yeye akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha wana-kondoo wangu.”
16 He saith unto him, again, the second time—Simon, son of John! lovest thou me? He saith unto him—Yea, Lord! thou, knowest that I am fond of thee. He saith unto him—Be shepherding my sheep.
Yesu akamwambia tena, “Simoni, mwana wa Yohana, wanipenda?” Petro akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Chunga kondoo zangu.”
17 He saith unto him, the third time—Simon, son of John! art thou fond of me? Peter was grieved, that he said unto him, the third time, Art thou fond of me? and he said unto him—Lord! all things, thou, knowest: thou perceivest that I am fond of thee. Jesus saith unto him—Be feeding my sheep.
Kwa mara ya tatu Yesu akamuuliza Petro, “Simoni mwana wa Yohana, unanipenda?” Petro akahuzunika sana kwa kuwa Yesu alimuuliza mara ya tatu, “Unanipenda?” Akamjibu, “Bwana, wewe unajua yote, unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha kondoo wangu.
18 Verily, verily, I say unto thee—When thou wast younger, thou usedst to gird thyself, and to walk whither thou didst choose; but, when thou shalt become aged, thou shalt stretch out thy hands, and, another, shall gird thee, and bear thee, whither thou dost not choose.
Amin, amin nakuambia, ulipokuwa kijana ulivaa na kwenda unakotaka, lakini utakapokuwa mzee utanyoosha mikono yako na mtu mwingine atakuvika na kukupeleka usipotaka kwenda.”
19 Now, this, he said, signifying, by what manner of death, he should glorify God. And, having said this, he saith unto him—Be following me.
Yesu alisema haya ili kuashiria ni kifo cha aina gani Petro atakachomtukuza nacho Mungu. Kisha Yesu akamwambia Petro, “Nifuate!”
20 Peter, turning about, beholdeth the disciple whom Jesus loved, following, —who also reclined during the supper upon his breast, and said—Lord, who is it that is delivering thee up?
Petro akageuka, akamwona yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akiwafuata. (Huyu ndiye yule mwanafunzi aliyeegama kifuani mwa Yesu walipokula naye chakula cha mwisho na kuuliza, “Bwana, ni nani atakayekusaliti?”)
21 Peter, therefore, seeing, this one, saith unto Jesus—Lord! and, this one, what?
Petro alipomwona huyo mwanafunzi, akamuuliza Yesu, “Bwana na huyu je?”
22 Jesus saith unto him—If I will that, he, remain until I come, what is that to thee? Thou, be following me.
Yesu akamjibu, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini? Wewe inakupasa unifuate!”
23 This word, therefore, went forth unto the brethren, that, that disciple, should not die. Howbeit, Jesus did not tell him, he should not die; but, If I will that, he, remain until I come, what is that to thee?
Kwa sababu ya maneno haya ya Yesu, uvumi ukaenea miongoni mwa ndugu kwamba huyu mwanafunzi hangekufa. Lakini Yesu hakusema kuwa hangekufa. Yeye alisema tu kwamba, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini?”
24 This, is the disciple who beareth witness concerning these things, and who hath written these things; and we know that, true, is, his witness.
Huyu ndiye yule mwanafunzi anayeshuhudia mambo haya na ndiye ambaye ameandika habari hizi. Nasi tunajua ya kuwa ushuhuda wake ni kweli.
25 Now there are many other things also, which Jesus did, which, indeed, if they were to be written one by one, not even the world, itself, I suppose, would contain, the books which must be written.
Lakini kuna mambo mengine mengi ambayo Yesu alifanya. Kama yote yangeliandikwa, nadhani hata ulimwengu wote usingekuwa na nafasi ya kutosha kuweka vitabu vyote ambavyo vingeandikwa. Amen.

< John 21 >