< John 15 >

1 I, am the real vine, and, my Father, is, the husbandman.
Mimi ni mzabibu wa huu kweli, na baba yangu ni mkulima wa mzabibu.
2 Every branch in me that beareth not fruit, He taketh it away; and, every one that beareth, fruit, He pruneth it, that, more fruit, it may bear.
Kila tawi ndani yangu ambalo halizai tunda, na husafisha kila tawi ambalo huzaa tunda huliondoa ili kwamba liweze kuzaa zaidi.
3 Already, ye, are, pure, because of the word which I have spoken unto you:
Ninyi tayari mmekuwa safi kwa sababu ya ujumbe ambao nimekwisha waambia.
4 Abide in me, and, I, in you. Just as, the branch, cannot be bearing fruit of itself, except it abide in the vine, so, neither, ye, except, in me, ye abide.
Mkae ndani yangu, na mimi ndani yenu. Kama tawi lisivyoweza kuzaa peke yake lisipo kuwa katika mzabibu, kadhalika nayi, msipo kaa ndani yangu.
5 I, am the vine: Ye, are the branches. He that abideth in me and, I, in him, the same, beareth much fruit; because, apart from me, ye can bring forth, nothing.
Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi. Adumuye ndani yangu na mimi ndani yake, mtu huyu huzaa matunda mengi, kwa kuwa pasipo mimi hamuwezi kufanya jambo lolote.
6 If one abide not me, he is cast out as the branch, and withered, and they gather them, —and, into fire, they cast them, and they are burned.
Ikiwa mtu yeyote hatasalia ndani yangu, atatupwa kama tawi na kukauka; watu hukusanya matawi na kuyatupa katika moto, na kuteketea.
7 If ye abide in me, and, my sayings, in you, abide, whatsoever ye may be desiring, ask! and it shall be brought to pass for you.
Ikiwa mtadumu ndani yangu, na kama maneno yangu yakidumu ndani yenu, ombeni lolote mtakalo, nanyi mtafanyiwa.
8 Herein, was my Father glorified, that, much fruit, ye should bear, and become my disciples.
Katika hili baba yangu ametukuzwa, kwamba mnazaa matunda mengi na kwamba ni wanafunzi wangu.
9 Just as the Father loved me, I also, loved you: Abide ye in my love.
Kama baba yangu alivyonipenda mimi, mimi pia nimewapenda ninyi; dumuni katika pendo langu.
10 If, my commandments, ye keep, ye shall abide in my love, —just as, I, the Father’s commandments, have kept, and abide in his love.
Ikiwa mtashika amri zangu, mtadumu katika pendo langu kama nilivyo shika amri za baba yangu na kudumu katika pendo lake.
11 These things, have I spoken unto you, that, my own joy, in you, may be, and, your joy, may be made full.
Nimesema mambo haya kwenu ili kwamba furaha yangu iwe ndani yenu na ili kwamba furaha yenu ifanyike kuwa timilifu.
12 This, is my own commandment, That ye be loving one another, just as I loved you.
Hii ndiyo amri yangu, kwamba mpendane ninyi kwa ninyi kama nilivyo wapenda ninyi.
13 Greater love than this, hath, no one, That, his life, one should lay down in behalf of his friends.
Hakuna mtu aliye na upendo mkuu kuliko huu, kwamba ayatoe maisha yake kwa ajiliya rafiki zake.
14 Ye, are, friends of mine, if ye be doing that which, I, am commanding you.
Ninyi ni rafiki zangu ikiwa mtafanya yale niwaagizayo.
15 No longer, do I call you, servants, for, the servant, knoweth not what, his lord, is doing. But, you, I have called, friends, because, all things which I heard from my Father, made I known unto you.
Siwaiti watumwa, kwa kuwa mtumwa hajui kile afanyacho bwana wake. Nimewaita ninyi marafiki, kwa sababu nimewajulisheni mambo yote ambayo nimesikia kutoka kwa Baba.
16 Not, ye, chose, me, but, I, chose you, and placed you, that ye should go your way and bear, fruit, —and, your fruit, should abide: that, whatsoever ye should ask the Father in my name, he might give unto you.
Hamkunichagua mimi, bali mimi niliwachagua ninyi na kuwaweka mwende mazae matunda, na tunda lenu lipate kukaa. Hii liko hivi ili kwamba chochote muombacho kwa Baba kwa jina langu, atawapeni.
17 These things, I command you, That ye be loving one another.
Mambo haya ninawaagiza, kwamba mpendane kila mtu na mwenzake.
18 If, the world, is hating, you, ye are getting to know that, me, before you, it hath hated.
Kama ulimwengu utawachukia, mjuwe kwamba ulinichukia mimi kabla haujawachukia ninyi.
19 If, of the world, ye had been, the world, of its own, had been fond; but, because, of the world, ye are not, on the contrary, I, chose you out of the world, therefore, the world, doth hate you.
Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda kama wa kwao; Lakini kwa sababau ninyi sio wa ulimwengu na kwa sababu niliwachagua kutoka katika ulimwengu, ni kwa ajili hii ulimwengu huwachukia.
20 Remember the word which, I, spake unto you: A servant is not greater than his lord. If, me, they persecuted, you too, will they persecute, —If, my word, they kept, your own also, will they keep.
Kumbukeni neno ambalo niliwaambia, 'Mtumwa si mkuu kuliko bwana wake.' Ikiwa walinitesa mimi, watawateseni ninyi pia; Kama walishika neno langu, wangelishika la kwenu pia.
21 But, all these things, will they do unto you, on account of my name, because they know not him that sent me.
Watawatendeeni mambo haya yote kwa ajili ya jina langu kwa sababu hawamjui yule aliyenituma.
22 Had I not come and spoken unto them, Sin, had they none; but, now, have they no, excuse, for their sin.
Kama nisingekuja na kuwaambia waambia, wasingalikuwa wamefanya dhambi; lakini sasa hawana udhuru kwa dhambi yao.
23 He that hateth me, hateth, my Father also.
Anichukiaye mimi humchukia Baba pia.
24 Had I not done among them, the works, which, no other, had done, sin, had they none; but, now, have they, both seen and hated both me and my Father.
Ikiwa sijafanya kazi miongoni mwao ambayo hapana mmoja aliyeifanya, wangelikuwa hawana dhambi; lakini sasa wamefanya yote mawili wameona na wamenichukia mimi na Baba yangu.
25 But…that the word which, in their law, is written, might be fulfilled—They hated me without cause.
Hili linatokea ili kwamba neno litimie ambalo limeandikwa katika sheria yao: 'Wananichukia mimi bila sababu.'
26 Whensoever the Advocate shall come, Whom, I, will send unto you from the Father, The Spirit of truth, which, from the Father, cometh forth, He, will bear witness concerning me;
Wakati mfariji amekuja, ambaye nitamtuma kwenu kutoka kwa Baba, huyu ndiye, Roho wa kweli, ambaye anatokea kwa Baba, atanishuhudia.
27 And do, ye also, bear witness, because, from the beginning, ye are, with me,
Ninyi pia mnanishuhudia kwa sababu mmekuwa pamoja nami tangu mwanzo.

< John 15 >